Sildenafil Citrate
JF-Expert Member
- Jan 29, 2021
- 573
- 2,553
Baba aitwaye Amani Malekela Madumba na watoto wake watatu wa kiume wamefariki dunia kwa kuteketea na moto baada ya nyumba waliyokuwa wakiishi kuwaka moto katika Kijiji cha Malolo B, Kata ya Malolo, Tarafa ya Mikumi wilayani Kilosa mkoani Morogoro.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Malolo B, Sufiani Ramadhani Ndagama, amesema tukio hilo limetokea majira ya saa 7:00 usiku wa kuamkia Mei 5, 2023.
UPDATE;
Imeelezwa Mzee Amani Madumba aliyekuwa akiishi Kata ya Ruaha Mbuyuni wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro aliyefariki dunia yeye pamoja na watoto wake watatu usiku wa kuamkia leo Mei 5, kwa kuteketea kwa moto, kwamba yeye ndiye aliyeichoma nyumba hiyo kisa ugumu wa maisha.
Ndugu wa marehemu aitwaye Rajab Madumba, amesema ndugu yao huyo wakati wa uhai wake alikuwa akilalamika kwamba endapo yeye akifariki basi watoto wake watabaki wakiteseka na pengine ndiyo sababu ya kuamua kuiteketeza familia yake hiyo.
Chanzo: EATV
Mwenyekiti wa Kijiji cha Malolo B, Sufiani Ramadhani Ndagama, amesema tukio hilo limetokea majira ya saa 7:00 usiku wa kuamkia Mei 5, 2023.
UPDATE;
Imeelezwa Mzee Amani Madumba aliyekuwa akiishi Kata ya Ruaha Mbuyuni wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro aliyefariki dunia yeye pamoja na watoto wake watatu usiku wa kuamkia leo Mei 5, kwa kuteketea kwa moto, kwamba yeye ndiye aliyeichoma nyumba hiyo kisa ugumu wa maisha.
Ndugu wa marehemu aitwaye Rajab Madumba, amesema ndugu yao huyo wakati wa uhai wake alikuwa akilalamika kwamba endapo yeye akifariki basi watoto wake watabaki wakiteseka na pengine ndiyo sababu ya kuamua kuiteketeza familia yake hiyo.
Chanzo: EATV