hilo tatizo je ulikuwa wakati anatumia antibiotic unamsafisha hilo sikio kwa kutumia zile pamba za masikio inasaidia sana huku anatumia dawa nawewe unamfanyia usafi asubuhi mchana na jioni na hico kipamba unatubukiza kwenye maji ya vuguvugu kabla hujamsafisha nacho
Kuna mtoto ana miaka mitano sasa, mtoto alikuwa mbunifu, mwenye maswali sana, sasa amepata tatizo!
mwanzo alikuwa anasikia vizuri, lakini ametokea kuwa anapoteza uwezo wa kusikia vizuri, ili akusikie lazima awe karibu yako, akiwa mbali hasikii, ingawa masikio hayana usaha.
Nilimpeleka hospitali zetu za kiswahili, akapimwa na akaandikiwa dawa, tena za bei ghali nilizinunua akazitumia wala hazikumpa nafuu yoyote.
Wasamalia wema waliponisikia nikilalama juu ya tatizo hilo walinishauri kumpa amoxiline na dawa ya matone ya kudondoshea, (ingawa siikumbuki jina) ile dawa ilimsaidia akawa anasikia kwa kiasi fulani, lakini baada ya muda mfupi hali ile inarudi.
Naomba msaada wadau, ni dawa gani anatakiwa kupewa mtoto huyo?
Pole sana kwa tatizo hilo.
Kwa vile upo dodoma, tafuta ofisi ya labor (kazi), uwaulize ofisi ya wakala wa afya na usalama kazini. Utakayemkuta muambie tatizo lako. Nina wasiwasi tatizo lako linahusiana na kazi unayofanya, haswa kelele. Endapo utatokea kuwa dar, ni-pm nikuelekeze ofisi ambayo utapewa msaada wa kutambua tatizo na kuelekezwa marekebisho/rehabilitation.
Pole sana kwa tatizo hilo.
Kwa vile upo dodoma, tafuta ofisi ya labor (kazi), uwaulize ofisi ya wakala wa afya na usalama kazini. Utakayemkuta muambie tatizo lako. Nina wasiwasi tatizo lako linahusiana na kazi unayofanya, haswa kelele. Endapo utatokea kuwa dar, ni-pm nikuelekeze ofisi ambayo utapewa msaada wa kutambua tatizo na kuelekezwa marekebisho/rehabilitation.
Siku hizi kuna tiba/tiba mbadala hata mabubu, ambao naturally huwa ni viziwi, wanasikia.
Usikate tamaa, hakuna ugonjwa usio na tiba nenda India. Hao wanaokwambia hakuna tiba ndio madaktari uchwara, watu wamesha "break through" kwenye matatizo ya masikio.
Tafuta pesa uende India, yaliyoshindikana hapa mengi wao huyaweza, kajaribu na huko. Usione watu wanakimbilia huko burebure kuna manufaa huko.
FF utaratibu gani mtu anaweza pelekwa India kwa ufadhili wa serikali?