John Haramba
JF-Expert Member
- Feb 4, 2022
- 365
- 1,373
Anasema "Watu wengi wamekuwa na matatizo ya kupata fangasi kwenye masikio, natoa wito kwa Wananchi kuwa wakati wa kuoga wasiingize maji kwenye masikio na pia wasitumie pamba stick kusafisha masikio.
“Sikio huwa linajisafisha lenyewe, halitakiwi kuingiza kitu chochote kule ndani.
“Unapotumia pamba unaondoa nta kwenye sikio, na watu wengi wanajua ile nta wanayoitoa ni uchafu kutokana na rangi yake ya brown, ule si uchafu una kazi yake ya kulinda sikio na ina njia zake za kutoka, wasiiitoe kwa kuwa inalinda sikio.”
“Kuna wazazi ambao wanatumia pamba kusafisha watoto wanaamini wanawasafisha lakini kumbe wanapunguza ile nta na wakati mwingine inawezana kumbe nyingine inaingia ndani kidogokidogo, mwisho wake inaweza kujaa kwenye sikio na kuziba.