Mwanafunzi afariki katika ghasia Chuo Kikuu

jamani ni ngumu sana kubalance vipindi na kufkiria kutafuta maji.hali ya vyoo na mabafu ya mlimani ni mbaya sana hata kipindi ambacho maji yanatoka muda wote, sasa yakikatika ndio balaa.kwa kifupi kama umewahi kusoma pale utaona hali ilivyo mbaya.miundo mbinu ni tangu majengo yalipojengwa, pesa za maintanance watu wanapeleka puani.sasa mtu hajaoga siku tatu afu unataka awe na 'hekima' ya kutofanya fujo, si unafiki huo! shida ya maji inajulikana lakini si kigezo cha kuwanyanyasa wanafunzi kwamba watulie kama makinda ya kuku yaliyopigwa mdondo.kama uongozi wa shule haufany jitihada za ziada kuwapatia maji na walishalalamika kuhusu hili suala, we unategemea watafanya nini zaidi ili wasikilizwe? wamefanya walichofanywa kwa sababu wamelazimika.hayo magari ya maji yanakuja wakati watu wapo kwenye vipindi na pia, si magari ya kutosha na mengi huanza kupeleka maji kwenye nyumba za staffs yakibaki ndo madent wanahudumiwa.ile dhana kwamba mwanafunzi ili ajifunze vizuri ni lazma apitie shida haipo siku hizi, denti anahitaji kusoma katika conducive environment ili afaulu vizuri.na anayesema kua maji hayapo kwa mukandala, ye ndio mkuu wa chuo(baba), ni lazma ahakikisha wanawe(wanafunzi) hawanyanyasiki.suala la mwisho, kuhusu kiwango cha elimu, mlimani kwa stats za 2006, ilikua ya 11 katika vyuo vyote africa, kumi vikiwa south africa.poleni sana familia ya mwanafunzi aliyefariki!
 
Majengo ya kisasa (kizungu) yanahitaji huduma za maji/umeme ili maisha yawe kama kwetu ambapo maji ni ya kisima na vyoo vya shimo. Hivyo uongozi wa chuo waige kile kilichofanywa na Wajapani katika wodi za watoto (A na B) pale Muhimbili hospital kwa kuchimba kisima kirefu ambacho kiliondoa adha ya ukosefu wa maji kwenye wodi hizo. Hii ni local solution wala haihitaji wataalam toka nje, FOE si wapo. Gharama ya deepwell pump na uchimbaji wa kisima kimoja hauzidi $ 3000. Vinginevyo wafanyie ukarabati mfumo wa mabomba, mmoja kwa maji ya kunywa na mwingine kwa maji yasio salama kunywa(industrial water)ambao utatumia maji ya kutoka bwawa karibu ya S/Msingi ikiwa ni long term solution.


Msavila:

Unatoka nje. Suala ya maji ni la infrastructure za nchi kama vile umeme na uongozi wa chuo kikuu unachoweza kufanya ni kulipia gharama hizo. Na matatizo yanapotokea ni tuwashike mashati wanaoongoza infrastructure hizo.

Hizi solution za kushimba visima ndizo zinazofanya nchi isiendelee na inafafana na solutions za mambo mengi yanayoendelea sasa. Mtu anaona shule za serikali zina matatizo anachofanya ni kumpeleka mtoto wake katika shule zinazoitwa St. Kinyogori.

Swali la kujiuliza kwanini tushimbe visima wakati tuna infrastructure na watu wa kuziongoza? Kwanini umpeleke mtoto wako Kenya au Uganda kusoma primary school wakati tulitakiwa kuweka effort zetu kujenga ubora wa shule za kuwasaidia watoto wetu?

Swali jingine, kuna matatizo ya drainage system na vyoo je taasisi zinatakiwa kuchimba vyoo na kununua sewage trucks?
 
Nakumbuka pale bia kulikuwa na matatizo ya uzalishaji, kila mara kiwanda kinasimama shauri ya maji. Akaja Kaburu, akachimba visima na nafikiri mpaka sasa maji sio tatizo tena.

Chuo kikuu, chenye idara kubwa ya Engineering na pale karibu yao kuna chuo cha maji, wanashindwa kuja na solution mpya ya maji kwenye vyuo vyao? Hii ni aibu kubwa sana kwa wasomi.

Chukulieni DAWASCO kama provider ambaye ameshindwa kutoa services zinazoridhisha, je dawa ni kuendelea kupigiana naye kelele au kutatufa solution nyingine?

Kwa suala la chuo mimi naona wangetumia elimu zao na ubunifu kuja na visima vya maji na maji kuvutwa kwa kutumia wind turbine au solar energy.

Kuendelea kutegemea mashirika kama DAWASCO ni kudumaza fikra zetu hasa kwa sehemu kama mlimani. Hivi hata Mkuu wa chuo jamani, kweli anashindwa kuwaita wakuu wa FOE na kuwaambia mates! we have a problem and we need a solution ASAP.

Nafikiri wasomi tuanze kupambana na matatizo na sio kila siku kulaumu tu serikali. Njia nzuri ya kuiumbua serikali ni kwasisi kuwaonyesha yale wanayoona hayawezekani, in fact yanaweza kufanyika tena kwa gharama nafuu sana.
 
Nakumbuka pale bia kulikuwa na matatizo ya uzalishaji, kila mara kiwanda kinasimama shauri ya maji. Akaja Kaburu, akachimba visima na nafikiri mpaka sasa maji sio tatizo tena.

Chuo kikuu, chenye idara kubwa ya Engineering na pale karibu yao kuna chuo cha maji, wanashindwa kuja na solution mpya ya maji kwenye vyuo vyao? Hii ni aibu kubwa sana kwa wasomi.

Chukulieni DAWASCO kama provider ambaye ameshindwa kutoa services zinazoridhisha, je dawa ni kuendelea kupigiana naye kelele au kutatufa solution nyingine?

Kwa suala la chuo mimi naona wangetumia elimu zao na ubunifu kuja na visima vya maji na maji kuvutwa kwa kutumia wind turbine au solar energy.

Kuendelea kutegemea mashirika kama DAWASCO ni kudumaza fikra zetu hasa kwa sehemu kama mlimani. Hivi hata Mkuu wa chuo jamani, kweli anashindwa kuwaita wakuu wa FOE na kuwaambia mates! we have a problem and we need a solution ASAP.

Nafikiri wasomi tuanze kupambana na matatizo na sio kila siku kulaumu tu serikali. Njia nzuri ya kuiumbua serikali ni kwasisi kuwaonyesha yale wanayoona hayawezekani, in fact yanaweza kufanyika tena kwa gharama nafuu sana.

Wewe mtanzania
Nani alikuambia msomi wa tanzania husoma ili awe mbunifu ili aje ayapatie solution matatizo yanayomzunguka????

Msomi wa tz anasoma ili ajue kutumia vitu yani kama OSI Layer basi hua tunajikita zaidi ktk hiyo leya ya 7 na kuzitupilia mbali hizi zingine ,ndio maana matatizo kama yanpokuja hua hatuna ujanja.
 
Mimi naomba nitofautiane kidogo na wenzangu. Kama alivyosema Bin Maryam, suala la maji ni la infrastructure, kitu ambacho jamii yetu imekiponda. Hizo adhoc solutions kama visima katika mzangira ya chuo kikuu hayawezi kusaidia hasa ukiangalia jinsi chuo chenyewe kilivyosambaa. Na hatuwezi katika karne hii kwenye majengo kama yale kutegemea septic tanks. Hawa wasomi hawana haja ya kuwa creative kama tunavyodai maana majibu yanajulikana. Inabidi shirika lenye jukumu la kupeleka maji chuoni kuwekeza kwenye hiyo infrastructure. Inabidi utawala wa chuo kuangalia network ya maji safi na machafu yaliyo ndani ya eneo lake na kuhakikisha inaendana sawa na mahitaji yake ya sasa hivi. Mipango hii ifanywe na iwekwe wazi kwa wanafunzi na jamii nzima ya hapo chuoni. Tatizo ni hiyo lack of political will. Miaka nenda rudi tunasikia chuo kikuu wana matatizo ya maji na tunashindwa kweli kutatua? Nakumbuka ilifika wakati walichimba vyoo vya shimo hapo chuoni! Pit latrines kweli katika our premier university! Tatizo hili si la wanafunzi kutatua bali ni la hao wanaokiendesha chuo hicho pamoja na wale wanaoendesha miji yetu. Wakati umefika ambapo maji safi yawe haki ya kila mmoja wetu.

Imefika wakati ambapo wale waliokuwa tasked kutoa huduma hizo wawajibike na wasiruhusiwe kukwepa kwa kuwatupia mzigo consumers. Dawasco ni lazima wawajibishwe kwenye hili. Tunawadekeza kwa kutafuta njia mbadala ambazo mara nyingi hazituhakikishii maji safi na salama. Kama wanashindwa kudiliva wawapishe wale ambao wataweza. Tusiendekeze uzembe. Mji wowote wa karne ya sasa hauwezi kuendeshwa kwa kutegemea visima, maboza na vyoo vya kuchimba!

Ingawa hili la kufanya fujo haliwezi kutetewa na mtu yeyote, ningeomba tuangalie mazingira tunayolelea wanafunzi wetu kuanzia huko mashuleni. Jamii yetu imeshindwa kuwatambua kuwa hawa wanafunzi ni watu wazima na kuhakikisha kuwa wanapokuwa na matatizo wanasikilizwa. Watawala bado wanakazania ile mifumo ya kizamani ya kukataa kumuona aliye na umri mdogo kwako kuwa ana haki sawa na wewe. Mara nyingi tunatumia bureaucracy na vitisho kuwafunga midomo. Hii imepelekea kujenga dhana kwa hawa vijana kuona njia pekee ambayo itakayotufanya sisi tulio wakubwa wao kuwasikiliza ni fujo. Inabidi tubadilike kijamii na kuheshimu haki ya kila mmoja wetu kuchangia mawazo, kutoa dukuduku zake bila kujali umri au nafasi yake. Naamini kuwa tukianza kuwa'treat' kama watu wenye haki sawa na sisi itasaidia kupunguza hii migongano isiyo na maana.

Tusisahau vile vile kuwa katika jamii yeyote kuna wale ambao maadili yao hayaendani na ya jamii yote. Kwenye vyuo vikuu kuna wabakaji, wezi, waongo, wavuta bangi kama vile walivyokuwepo katika jamii. Tusikihukumu chuo kwa vitendo vya hawa wachache. Hatutakuwa tunawatendea haki.
 
Nakumbuka pale bia kulikuwa na matatizo ya uzalishaji, kila mara kiwanda kinasimama shauri ya maji. Akaja Kaburu, akachimba visima na nafikiri mpaka sasa maji sio tatizo tena.

Chuo kikuu, chenye idara kubwa ya Engineering na pale karibu yao kuna chuo cha maji, wanashindwa kuja na solution mpya ya maji kwenye vyuo vyao? Hii ni aibu kubwa sana kwa wasomi.

Chukulieni DAWASCO kama provider ambaye ameshindwa kutoa services zinazoridhisha, je dawa ni kuendelea kupigiana naye kelele au kutatufa solution nyingine?

Kwa suala la chuo mimi naona wangetumia elimu zao na ubunifu kuja na visima vya maji na maji kuvutwa kwa kutumia wind turbine au solar energy.

Kuendelea kutegemea mashirika kama DAWASCO ni kudumaza fikra zetu hasa kwa sehemu kama mlimani. Hivi hata Mkuu wa chuo jamani, kweli anashindwa kuwaita wakuu wa FOE na kuwaambia mates! we have a problem and we need a solution ASAP.

Nafikiri wasomi tuanze kupambana na matatizo na sio kila siku kulaumu tu serikali. Njia nzuri ya kuiumbua serikali ni kwasisi kuwaonyesha yale wanayoona hayawezekani, in fact yanaweza kufanyika tena kwa gharama nafuu sana.

Nakubaliana na mawazo ya wasomi kuwa wabunifu na kutoitegemea au kulaumu serikali.

Lakini tukumbuke ni sisi watanzania tunaotafuta wawekezaji nje ya nchi. Na wengi wa wawekezaji wa nje wanategemea sana infrastructure zinazoendeshwa mashirika kama DAWASCO au TANESCO. Ni wawekezaji wachache wanaokubali kuja na pump za maji na majenereta ya umeme. Na wanaokuja nazo inabidi tuwape unafuu wa mikataba kitu ambacho kinatuingizia hasara kubwa kuliko hasara ya kuendesha infrastucture.

Na tukiondoa wawekezaji kutoka nje kuna watanzania wengi ambao wangeweza kuwa wawekezaji katika nchi yao wenyewe kama huduma za maji, umeme zingekuwa zinafanya kazi sawasawa. Je mwenye mgahawa wa chai naye anatakiwa awe na kisima chake cha maji au jenereta yake?
 
Nakumbuka pale bia kulikuwa na matatizo ya uzalishaji, kila mara kiwanda kinasimama shauri ya maji. Akaja Kaburu, akachimba visima na nafikiri mpaka sasa maji sio tatizo tena.

Chuo kikuu, chenye idara kubwa ya Engineering na pale karibu yao kuna chuo cha maji, wanashindwa kuja na solution mpya ya maji kwenye vyuo vyao? Hii ni aibu kubwa sana kwa wasomi.

Chukulieni DAWASCO kama provider ambaye ameshindwa kutoa services zinazoridhisha, je dawa ni kuendelea kupigiana naye kelele au kutatufa solution nyingine?


Kuendelea kutegemea mashirika kama DAWASCO ni kudumaza fikra zetu hasa kwa sehemu kama mlimani. Hivi hata Mkuu wa chuo jamani, kweli anashindwa kuwaita wakuu wa FOE na kuwaambia mates! we have a problem and we need a solution ASAP.

Nafikiri wasomi tuanze kupambana na matatizo na sio kila siku kulaumu tu serikali. Njia nzuri ya kuiumbua serikali ni kwasisi kuwaonyesha yale wanayoona hayawezekani, in fact yanaweza kufanyika tena kwa gharama nafuu sana.


Mkuu naungana na wewe kama uliyoyaainisha hapo juu.

Mfumo wa maji TZ unategemea mvua, kama hali haitarekebishwa au kuboreshwa, uhakika wa kupata maji throughout bado ni ndoto.

Kinachotakiwa ni kuwa na solution mbadala (si kwa vyuoni tu bali hata majumbani) kama Dawasco wameshindwa kutoa huduma.

[
Kwa suala la chuo mimi naona wangetumia elimu zao na ubunifu kuja na visima vya maji na maji kuvutwa kwa kutumia wind turbine au solar energy.
Ukiweza kuwa na chanzo chako mwenyewe cha maji, unapunguza matatizo mengi,moja ikiwa ni gharama za kulipia huduma ambayo hauipati.

Mwalimu alisema: It can be done, play your part.

Tatizo watu hawajui 'their/which - parts to play'
 
Mkuu naungana na wewe kama uliyoyaainisha hapo juu.

Mfumo wa maji TZ unategemea mvua, kama hali haitarekebishwa au kuboreshwa, uhakika wa kupata maji throughout bado ni ndoto.

Kinachotakiwa ni kuwa na solution mbadala (si kwa vyuoni tu bali hata majumbani) kama Dawasco wameshindwa kutoa huduma.

[
Ukiweza kuwa na chanzo chako mwenyewe cha maji, unapunguza matatizo mengi,moja ikiwa ni gharama za kulipia huduma ambayo hauipati.

Mwalimu alisema: It can be done, play your part.

Tatizo watu hawajui 'their/which - parts to play'

Hatuwezi kila mmoja wetu awe na chanzo chake cha maji, nishati n.k. Haya ndiyo mambo yanayofanya polisi wetu wakae kwenye polisi post na kuwatupia wananchi mzigo wa kulinda usalama wao. Unapokuwa na mji wenye watu takriban milioni tatu ni lazima pawe na mgawanyo wa majukumu. Ndio maana tunakuwa na serikali za miji ambazo zitatuhakikishia sisi tuishio humo upatikanaji wa hudumakwa bei nafuu, uhakika na zaidi ya yote uslama wa afya zetu. Kwa mfano tumeondoa wajibu wa kushughulika maji taka (maji yatokayo majikoni, mabafuni na vyooni) katika maeneo letu kutoka Dawasco na kupeleka kwa wakazi wa jiji. Hii imefanya njia inayotumika katika maeneo mengi ni septic tanks na soak-pits. Soak pits zinapokea maji kutoka kwenye septic tanks na haya maji yana percolate kwenye udongo unaozunguka. Kutokana na concentration ya hizi soak pits, mabomba ya maji safi mara nyingi yanapita kwenye maeneo ambamo zimejengwa. Hii inasababisha maji mengi yanayotoka katika mabomba yetu kuwa na punjepunje za kinyesi (fecal matter) na kuhatarisha afya za wale wanaotumia. Kwenye sehemu chache zenye sewers, maji haya yanamwagwa kama yalivyo baharini (ushahidi ni harufu inayotoka maeneo ya Ocean Road) na kuhatarisha afya za maharusi ambao imekuwa jadi kwenda kulowesha miguu yao baharini. Ilitakiwa badala ya ku'opt out' kushikia bango mamlaka ya jiji na Dawasco kuwalazimisha wajenge infrastructure ya maji machafu ikijumuisha treatment plants! Hii ni kweli vile vile kwenye maji safi. Tukumbuke kuwa tuna'centralise' huduma hizi kuhakikisha kuwa standards zinalindwa. Maji yanatakiwa yawe salama na si hayo matope tunayoletewa. Visima vitumike kama back up na sio primary source. Hatuwezi kutegemea rain water harvesting kutosheleza mahitaji ya maji ya sehemu kama chuo kikuu. Tatizo ni kwamba wahusika wakishaona hizi juhudi zinafanyika hawakawii kunawa mikono. Tukumbuke kuwa mahitaji ya maji na nishati ya chuo kikuu si kwa ajili ya matumizi ya wakazi tuu bali vilevile zinahitajika sana katika tafiti zinazofanyika. Wakati umefika wa wanachi (wasomi wakiwemo) kudai kupatiwa huduma kutoka hao waliopewa majukumu hayo.
 
Mimi naomba nitofautiane kidogo na wenzangu. Kama alivyosema Bin Maryam, suala la maji ni la infrastructure, kitu ambacho jamii yetu imekiponda. Hizo adhoc solutions kama visima katika mzangira ya chuo kikuu hayawezi kusaidia hasa ukiangalia jinsi chuo chenyewe kilivyosambaa. Na hatuwezi katika karne hii kwenye majengo kama yale kutegemea septic tanks. Hawa wasomi hawana haja ya kuwa creative kama tunavyodai maana majibu yanajulikana. Inabidi shirika lenye jukumu la kupeleka maji chuoni kuwekeza kwenye hiyo infrastructure. Inabidi utawala wa chuo kuangalia network ya maji safi na machafu yaliyo ndani ya eneo lake na kuhakikisha inaendana sawa na mahitaji yake ya sasa hivi. Mipango hii ifanywe na iwekwe wazi kwa wanafunzi na jamii nzima ya hapo chuoni. Tatizo ni hiyo lack of political will. Miaka nenda rudi tunasikia chuo kikuu wana matatizo ya maji na tunashindwa kweli kutatua? Nakumbuka ilifika wakati walichimba vyoo vya shimo hapo chuoni! Pit latrines kweli katika our premier university! Tatizo hili si la wanafunzi kutatua bali ni la hao wanaokiendesha chuo hicho pamoja na wale wanaoendesha miji yetu. Wakati umefika ambapo maji safi yawe haki ya kila mmoja wetu.

Imefika wakati ambapo wale waliokuwa tasked kutoa huduma hizo wawajibike na wasiruhusiwe kukwepa kwa kuwatupia mzigo consumers. Dawasco ni lazima wawajibishwe kwenye hili. Tunawadekeza kwa kutafuta njia mbadala ambazo mara nyingi hazituhakikishii maji safi na salama. Kama wanashindwa kudiliva wawapishe wale ambao wataweza. Tusiendekeze uzembe. Mji wowote wa karne ya sasa hauwezi kuendeshwa kwa kutegemea visima, maboza na vyoo vya kuchimba!

Ingawa hili la kufanya fujo haliwezi kutetewa na mtu yeyote, ningeomba tuangalie mazingira tunayolelea wanafunzi wetu kuanzia huko mashuleni. Jamii yetu imeshindwa kuwatambua kuwa hawa wanafunzi ni watu wazima na kuhakikisha kuwa wanapokuwa na matatizo wanasikilizwa. Watawala bado wanakazania ile mifumo ya kizamani ya kukataa kumuona aliye na umri mdogo kwako kuwa ana haki sawa na wewe. Mara nyingi tunatumia bureaucracy na vitisho kuwafunga midomo. Hii imepelekea kujenga dhana kwa hawa vijana kuona njia pekee ambayo itakayotufanya sisi tulio wakubwa wao kuwasikiliza ni fujo. Inabidi tubadilike kijamii na kuheshimu haki ya kila mmoja wetu kuchangia mawazo, kutoa dukuduku zake bila kujali umri au nafasi yake. Naamini kuwa tukianza kuwa'treat' kama watu wenye haki sawa na sisi itasaidia kupunguza hii migongano isiyo na maana.

Tusisahau vile vile kuwa katika jamii yeyote kuna wale ambao maadili yao hayaendani na ya jamii yote. Kwenye vyuo vikuu kuna wabakaji, wezi, waongo, wavuta bangi kama vile walivyokuwepo katika jamii. Tusikihukumu chuo kwa vitendo vya hawa wachache. Hatutakuwa tunawatendea haki.

Fundi Mchundo:

Ulichoeleza hapa ni sawa lectures nilizochukua katika masuala ya uchumi na uongozi kwa engineers katika shule niliyosoma.

Kuna substitute na innovation. Hivi vitu vinaweza kutoa tafsiri sawa lakini vina tofauti kubwa sana.

Kwa mfano: Chibuku aina tofauti sana na pombe zingine za kienyeji lakini standard ya chibuku ni kubwa kuliko pombe za kienyeji. Kwenye chibuku kuna kwa quality control, kuna usafi na mambo mengine muhimu katika afya za wanywaji. Mnywaji wa chibuku kwa ukosefu wa pesa akihamua kuacha chibuku na kurudi kwenye mataputapu huo sio ubunifu, hiyo ni substitute. Na mtu wa namna hii hapati maendeleo siku zote.

Baada ya vita pili vya dunia. Watu wengi wa Ulaya walirudi katika matumizi ya substitutes. Watu walitumia visima lakini siku zilivyoendelea waliweza kurudi katika ubora wa maisha yao kabla ya vita na kuweza kuendelea. Hata baada ya kuvunjika kuwa ukomunisti nchi nyingi za Ulaya Mashariki zilirudi kwenye substitutes lakini wengi wameachana nazo.

Sisi tuliozaliwa mijini huduma za maji Tanzania zilikuwepo. Kama wakazi wa NY wanavyoelewa kuwa kuna siku magari ya kuzoa taka yanakuja, wakazi wa miji yote Tanzania nao walikuwa wanaelewa kuweka takataka nje na magari ya halmashauri za miji yalikuja kuzoa.

Matatizo yetu ya kiuchumi na uongozi yametufanya tutumie substitutes lakini hii ilikuwa inatakiwa kuwa solutions za muda mfupi na sio za kudumu. Na sifa kubwa ya substitutes ni ku-settle na vitu inferior kuliko vile ulivyotumia mwanzo. Na kuondoka na tatizo hili ni lazima jamii ijue umuhimu wa ku-set standards na usikubali hata siku moja kuwa chini ya standards zako kwa muda mrefu bila kuwa na sababu zisizoeleweka. Na ukikubali kuwa chini ya standards ulizoziweka utajenga tabia ya kukubali kuwa subsitutes na innovation ni kitu kimoja.
 
Kwa wafiwa, Poleni sana.

Mtanzania, Fundi Mchundo na Bin Maryam, mawazo yenu naafikiana nayo. Jambo ambalo najiuliza pamoja na utetezi wako Fundi Mchundo ni huu, Chuo kikuu ni mahali ambapo elimu ya juu na utafiti hufanyika (hasa huku nje ya nchi), Je Chuo Kikuu pale IPI, chuo cha maji na Chuo cha ardhi, wanafanya nini kuleta msukumo wa kubadilisha mfumo mzima wa miundo mbinu ya nchi yetu?

Ndio ni wajibu wa Tanesco, Dawasco, TTCL na vyombo vingine vya miuondombinu, lakini inakuwaje mahali ambapo ndipo chimbuko la wataalamu wetu, panakosekana mwamko wa kimapinduzi wa elimu ya vitendo ili kurutubisha mifumo ya uzalishaji mali kwa kutumia teknolojia?

Ndio yawezekana UDSM hawana pesa za kulipia Maji au kutokana na mitambo midogo, hakuna uwezo wa kusukuma maji kutoka Kimara Kibo kwenda Chuo. Je kwa miaka yote karibu 40 tangu chuo kianzishwe, hapajawa na msukumo kutoka utawala na wanafunzi kutafuta hitimisho kutatua haya matatizo?

Je Chuo hiki kilipojengwa, kilijengwa kwa ajili ya wanafunzi wangapi na familia ngapi? Je ni sahihih kusema kuna overload kutokana na kukosekana kwa vyuo vingine, hivyo azma ya kuwa na wataalamu wengi inasababisha kuongeza idadi ya wanafunzi bila kuongeza miundombinu?

This should be a classic case study of Tanzania as a society and country. The obvious lack of planning which runs parallel with complete dependency of handouts creating inefficiency and complete paralysis of imagination!

I will agree with Bin Maryam for once that Azimio lilidumaza mawazo, kwa kujenga jamii tegemezi isiyo na nguvu za kutumia nadharia na kuwa vitendo!
 
Kwa wafiwa, Poleni sana.

Mtanzania, Fundi Mchundo na Bin Maryam, mawazo yenu naafikiana nayo. Jambo ambalo najiuliza pamoja na utetezi wako Fundi Mchundo ni huu, Chuo kikuu ni mahali ambapo elimu ya juu na utafiti hufanyika (hasa huku nje ya nchi), Je Chuo Kikuu pale IPI, chuo cha maji na Chuo cha ardhi, wanafanya nini kuleta msukumo wa kubadilisha mfumo mzima wa miundo mbinu ya nchi yetu?

Ndio ni wajibu wa Tanesco, Dawasco, TTCL na vyombo vingine vya miuondombinu, lakini inakuwaje mahali ambapo ndipo chimbuko la wataalamu wetu, panakosekana mwamko wa kimapinduzi wa elimu ya vitendo ili kurutubisha mifumo ya uzalishaji mali kwa kutumia teknolojia?

Ndio yawezekana UDSM hawana pesa za kulipia Maji au kutokana na mitambo midogo, hakuna uwezo wa kusukuma maji kutoka Kimara Kibo kwenda Chuo. Je kwa miaka yote karibu 40 tangu chuo kianzishwe, hapajawa na msukumo kutoka utawala na wanafunzi kutafuta hitimisho kutatua haya matatizo?

Je Chuo hiki kilipojengwa, kilijengwa kwa ajili ya wanafunzi wangapi na familia ngapi? Je ni sahihih kusema kuna overload kutokana na kukosekana kwa vyuo vingine, hivyo azma ya kuwa na wataalamu wengi inasababisha kuongeza idadi ya wanafunzi bila kuongeza miundombinu?

This should be a classic case study of Tanzania as a society and country. The obvious lack of planning which runs parallel with complete dependency of handouts creating inefficiency and complete paralysis of imagination!

I will agree with Bin Maryam for once that Azimio lilidumaza mawazo, kwa kujenga jamii tegemezi isiyo na nguvu za kutumia nadharia na kuwa vitendo!

Mkuu, hii huwezi kuiangalia in isolation. Chuo Kikuu ni mahali pa kufundisha na kufanya utafiti. Kazi ya design ya infrastructure inaweza kufanywa na mtaalamu yeyote aliyesomea fani hiyo. Kwa Chuo kama chetu haiwezi kutatuliwa kama class exercise. Hii itakuwa ni kujidanganya tuu. Cha muhimu zaidi ni kuwa na nia ya ku'implement' hizo designs.

Hili tatizo si la chuo kikuu peke yake. Ni la mfumo mzima wa uwajibikaji. Uko sahihi kabisa unaposema kuwa ni mfano halisi wa lack of planning katika jamii yetu. Mimi ningeongezea; na kutokukubali kuwa kuna limits katika kila kitu. Kuanzia tunavyojazana kwenye daladala hadi hapo tunapoongeza majengo, wakazi na matumizi mengine bila kuwekeza kwenye infrastructure. Hatutaki kusikia ushauri wa kitaalamu hadi hapo matatizo yanapotukuta.

Hatuoni kuwa mazingira mazuri ni sehemu muhimu ya elimu tunayotoa. Hivi tunataka hawa wanafunzi waje na njia gani mbadala ya kutoa huduma za vyoo na mabafu katika maghorofa tuliyowajengea? Tunategemea wafanye nini kama tunawajengea hayo maghorofa na kutohudumia lift zinazotakiwa kuwemo? Huduma za maji, nishati na hii ya siku hizi ya communication ni wajibu wa wenye chuo na si wanafunzi. Wanafunzi waachwe wasome na ku'maximise' potential ya muda watakaokuwa pale chuoni. sisi kama wazazi tuhakikishe kuwa hakuna kinachowazuia kutimiza azma hiyo. Hatuwezi kuwategemea watumie choo cha shimo kwenye ghorofa ya 12!
 
Poleni wafiwa.

For years sasa tumeshuhudia UDSM students chaos, from mgomo wa calculators mpaka kuvunja nyumba za wakuu wa chuo. It doesn't click in my mind why educated people can be iresponsible like that.University is core center of sharpen people minds, the place that people get trained how to better them selves. However,in UDSM the case is different, those students shows selfishness for years without knowing they're lucky to be where they are.

Mfumo wa Ujamaa ndio matunda yake haya, UDSM students believes that they diserv everything on time. However, they forgot it is our taxes sponsor they're education. To be educated doesn't mean you knows calculas or nuclear physics inside and outside, but how you make decisions and judgements on your day to day life.

UDSM students has victimise Tanzanian for years kwa kisingizio kwamba "we're smart and we diserv everything we need". I know kukosa maji kwenye puclic place kama high learning institution is not good, however kuvamia nyumba ya mkufunzi wa chuo for that reason is stupidy.

Two or three years ago serikali iliamua kukata full scholarship kwa wanafunzi wa Mlimani, majority of students waliandamana wakidai kwamba it is not fair, sisi ni watoto wa wakulima and so forth. What i can't understand is how watoto wa wakulima can act that way. How many places in Tanzania doesn't have water for years? Does UDSM students have double standard with other Tanzania?

I know majority ya chuo hawakuhusika na jambo hili, however few people who participates on that non sense movement wameikikost chuo kizima, wame disrespect the whole meaning of High learning institutions. Tanzania needs strong rules against this kind of stupid actions.
 
Kwa wafiwa, Poleni sana.

Mtanzania, Fundi Mchundo na Bin Maryam, mawazo yenu naafikiana nayo. Jambo ambalo najiuliza pamoja na utetezi wako Fundi Mchundo ni huu, Chuo kikuu ni mahali ambapo elimu ya juu na utafiti hufanyika (hasa huku nje ya nchi), Je Chuo Kikuu pale IPI, chuo cha maji na Chuo cha ardhi, wanafanya nini kuleta msukumo wa kubadilisha mfumo mzima wa miundo mbinu ya nchi yetu?

Ndio ni wajibu wa Tanesco, Dawasco, TTCL na vyombo vingine vya miuondombinu, lakini inakuwaje mahali ambapo ndipo chimbuko la wataalamu wetu, panakosekana mwamko wa kimapinduzi wa elimu ya vitendo ili kurutubisha mifumo ya uzalishaji mali kwa kutumia teknolojia?

Ndio yawezekana UDSM hawana pesa za kulipia Maji au kutokana na mitambo midogo, hakuna uwezo wa kusukuma maji kutoka Kimara Kibo kwenda Chuo. Je kwa miaka yote karibu 40 tangu chuo kianzishwe, hapajawa na msukumo kutoka utawala na wanafunzi kutafuta hitimisho kutatua haya matatizo?

Je Chuo hiki kilipojengwa, kilijengwa kwa ajili ya wanafunzi wangapi na familia ngapi? Je ni sahihih kusema kuna overload kutokana na kukosekana kwa vyuo vingine, hivyo azma ya kuwa na wataalamu wengi inasababisha kuongeza idadi ya wanafunzi bila kuongeza miundombinu?

This should be a classic case study of Tanzania as a society and country. The obvious lack of planning which runs parallel with complete dependency of handouts creating inefficiency and complete paralysis of imagination!

I will agree with Bin Maryam for once that Azimio lilidumaza mawazo, kwa kujenga jamii tegemezi isiyo na nguvu za kutumia nadharia na kuwa vitendo!


Hapa kuna mada nyingi. Mada kuu mbili zilizojitokeza ni ukosefu wa maji kwa jiji la DSM na kusababisha matatizo UDSM. Na kuna mada ya ubunifu kwa jumuia ya chuo kikuu.

Kuhusiana na suala la maji ukweli ni kuwa jumuia ya UDSM isipate special treatment kuliko jumuia nyingine (period). UDSM isiwe ni kisiwa chenye unafuu wa maisha. Na kama kuna maandamano au juhudi za kushinikiza basi yawe kwa faida ya Tanzania na sio wao wenyewe. Ni muda mfupi wanafunzi wanahutumia wakiwa vyuoni lakini muda uliobakia wa maisha yao wataishi kwenye sehemu wanazoishi watanzania wengine.

Suala la wao kuwa wabunifu linawezekana kabisa lakini ubunifu wao usipimwe kwa kuangalia wao wanaweza kutatua vipi matatizo yao ya maji shuleni. Sijuhi wenzangu mmechukua taaluma gani, katika taaluma za engineer, miaka miwili ya mwanzo mwanafunzi anajifunza kanuni za taaluma yake na kipindi mwanafunzi anajisikia kuwa taaluma yake inaanza kuingia damuni tayari muda wa kumaliza shule umefika na anakabidhiwa digrii au diploma yake. Hivyo ubunifu mkubwa mwanafunzi anauonyesha akiwa amemaliza masomo yake kwa kutumia zile kanuni alizojifunza akiwa chuoni.

Na kwa mtaji huu, taasisi mbalimbali za Tanzania zinaendeshwa na watanzania wenye taaluma mbalimbali. Kama wataalamu hawa watakuwa wabunifu katika fani zao za uongozi, uhasibu, uhandisi na fani zingine basi tunaweza kukabiliana vizuri na matatizo haya.
 
Wanafunzi wa O level walikuwa wakigomea chakula kibaya na kufanya uharibifu mali na miundombinu, kupiga walimu na wapitanjia, Wanafunzi wa A level walikuwa hawajihusishi na fujo hizo. Sasa U-O level ule umeingia chuo kikuu!

Could JKT help?
 
Vijana wa sasa wamekosa mbinu za kudai haki zao. Hii pia imechangiwa na kuondolewa kwa JKT vijana wa vyuo vikuu sasa wanaelekea kuwa kama secondary. Kuna haja ya vyuo vikuu kueleza hawa wasomi wa siku hizi maana ya vyuo vikuu. Sikutegemea wanafunzi wa vyuo vikuu kushiriki katika maandamano ya kuvunja milango, kurusha mawe, kuvunja mafriji na kunywa soda madukani.


Hii ni aibu kubwa kwa wasomi.

Lakini nimesikia hoja zao za msingi hazikuwa maji hila maji walichukuliwa kufikisha ujumbe Hoja zao zilikuwa Kupanda kwa ada ambapo kale ka mkopo wanakopewa na serikali wanakarudisha serikalini kwa kulipia ada. Wengi sana nasikia hata matokeo yao yamezuiliwa baada ya kushindwa kulipa gharama hizi.

Pia la pili lilikuwa maji ambayo sikuona mantiki yake.

Hila kuna umuhimu wakati wanafunzi wanaingia vyuo vikuu waelimishwe namna ya kutatua matatizo yao. Tatizo kubwa lililopo katka vyuo wanafunzi wengi ni wadogo sana. Hivyo hata mawazo yao bado kabisa. Wanahitaji kuelekezwa.
 
Wanafunzi UD sasa wanakosa hekima mbele ya Watz..sasa uharibifu wa mali na kupiga watu ndo watapata maji?

Mbona Dar pia kuna watu miaka mingi tuu hawana maji?

Wanaweza kuandamana..ila kuharibu mali ni aibu kwa wasomi!


Na unaweza mwingine kwao hawanaa maji ila akifika chuo ndo mwanzilishi wa hizo vurugu. Kitu nisichojua ni je maji yalikatika sehemu zote za chuo? ila swala la kukatika kwa maji Dar sio issue.
 
Na unaweza mwingine kwao hawanaa maji ila akifika chuo ndo mwanzilishi wa hizo vurugu. Kitu nisichojua ni je maji yalikatika sehemu zote za chuo? ila swala la kukatika kwa maji Dar sio issue.

Haya ndiyo nisiyoyapenda. Kama kwao anakaa katika nyumba ya nyasi na anateka maji kutoka mtoni basi hana haki ya kulalamika kubebeba ndoo za maji ghorofa 10? Ukikatikiwa maji Manzese au masaki ambapo nyumba nyingi hazina ghorofa zaidi ya moja si sawa na kutokuwa na maji katika maghorofa ya Chuo Kikuu. Tusiendekeze chuki iliyojengeka dhidi ya wasomi katika jamii hii. Tukemee fujo walizofanya lakini tusiwabeze kuhusu matatizo halali waliyokuwa nayo!
 
matatizo halali kweli wanayo......lakini they were way out of line kufanya fujo na kuvamia nyumba ya professor hasa wakati wa usiku.
wameshindwa kutofautisha baina ya wahalifu na wasomi! kwa elimu yao wanayopewa, kuvamia au kuvunja vitu kunaonyesha kuwa labda elimu wanayopewa ni below standard au labda ni wagumu wa kuelewa.

ni aibu kwa kweli.....what a mess !
 
Back
Top Bottom