Mwanadamu na matumizi ya uwezo wake!!!!

Hili swali ni tricky...kwani kama Ukristu si Dini kama dini nyingine.Yesu hakuhubiri dini, ila Injili.Na ndio panapowachanganya waislam na wakristu.

Baadaya kuamua jinsi ya ku approach hizo dini then ndio unaingia katika theology za hayo makundi bila kuwa biased ndipo utajua kundi gani utafuata mafundisho yao.Halafu katik hilo kundi ndipo utaangalia ni jinsi gani utafuata hayo mafundisho kufikia malengo yako.Kama ni ukombozi na kuiona mbingu au kama ni kuweza yaishi haya maisha ya dunia kwa kuwa na identity fulani.

Ni vizuri kujua kwanza na lengo la wewe kuamini.Halafu tafuta univeral values ambazo mwanadamu anahitaji kuzishika ili mahusiano yake na dunia, na wengine na yake binafsi yawe mazuri.Jaribu ziangalia zitatumikaje kufanikisha wokovu wako.Then angalia dini gani ina zitekeleza vyema.then zitumie kama vipimo vya kupima mafundisho yao,utekelezaji wake, kwani katika dini nyingine mambo hayatekelezeki kiasi cha kuchanganya waumini wao katika mambo ya msingi.Pia angalia staha, wasifu binafsi wa nabii husika.Kama nabii anakupa shida sana kumwelezea kukupata karaha, kama sifa zake zinatosha mpatia nafasi katika maisha yako na ungependa ufanyake kama yeye bila kuvunja universal principles ulizoziandika.Pia huyo nabii awe na sifa za kiroho asiwe tuu just kiongozi.Nadhani utakuwa katika sehmu nzuri ya kuifuata hiyo dini.

Haya mambo ya dini wakati mwingine yanakuja pale binadamu anaposhindwa kuwa na majawabu ya sintofahamu ya mambo mbalimbali kuhusu yeye na mazingira yanayomzunguuka
 
Inaonekana binadamu ana uwezo mkubwa sana lakini bado hajautumia.Niliwahi kusoma utafiti mmoja na ikagundulika kwenye utafiti ule kuwa mwanadamu anatumia uwezo wake wa akili au kufikiri kwa asilimia 10 tu!Yaani pamoja na vituko vyote hatujaweza hata kutumia asilimia 50!Kumbe inawezekana ikawa sababu ya upofu wetu wa kujijua na kujua kuhusu nguvu zinazotuzunguka kama Mungu n.k,au ndo maana tunaamini katika hizo nguvu,yaani huenda hazipo na tunashindwa kujua hazipo kwa sababu hatufikiri vyema!

Ndio maana kuna watu wanaamini kwamba MUNGU HAJAMUUMBA MWANADAMU bali MWANADAMU NDIO AMEMUUMBA MUNGU kutokana na hofu ya kuelezea baadhi ya mambo ambayo yapo nje ya uwezo wake (yanaweza kuwa kuhusu mwanadamu mwenyewe au mazingira yanayomzunguuka)
 
Ndiyo maana nilitangula kusema uumbaji ni complex concept.
Mtu akivamia na kuanza kuielezea akiwa amesimamia msingi fulani bila evidence atakwama tu.

hapana mi siamin ni complex concept ila kulingana na uvivu wa kufikiri ndo mana hatufikii sehem tunayotaka kufika na pia kuna idea flan flan tushazijenga vichwan mwetu
 
Mkuu, tofauti ya udogo na manii ni ya msingi sana kiasi kwamba hatutakiwi ku-group hizo idea mbili katika kundi moja ili kwa pamoja viwe v/s science.
Manii is more scientific than udogo.
May be we need to elimenate either udogo idea or manii before moving on.

nakuelewa ila hapa mimi nilikuwa namaanisha kuwa "wote wanaongelea uumbaji", yaani kutengeneza binadamu kama binadamu, mwembe kama mwembe, etc .wakati sayansi inasema "chance+evolution".

sasa litakapokuja suala la huo uumbaji ndio kila mtu atahitaji elezea kivyake na hapo ndipo watatofautiana.haina tofauti na mmasai na mhaya wakitete uafrica wao katik kundi la wazungu na wahindi.Ila wakija pamoja ndipo wataanza ona tofauti zao.Ni kama mwl alipotumia mfano wazenj wakiwa pamoja ndipo wataona tofauti zao.Hapa uuambaji ndio core za dini za Mungu mmoja.

Na wale jamaa wa maabara ya ulaya inayotafuta particle waliyoiita "GOD", ni kwamba wakipata tuu na kujaribu iangalia muda itakayokaa basi watakuja na ushahidi wa kupinga dini zote na si sijui ipi yenye maelzo mazuri ya UUmbaji.

Sasa baada ya hao jamaa kushindwa basi watu watapenda jua katika hizo njia za uumbaji zilizo tofauti ni ipi ya kweli, au zote ni uongo na kuna njia nyingine viumbe walifika duniani.Pengine kwa kuletwa toka sayari nyingine ambayo ndio ina siri kubwa ya uhai.
 
Nimekupata unalenga nini ila dini ngumu sana mkuu,
hivi ni nani aliye-approve vitumike vitabu 72 au pungufu katika bible.
Hapo hapo tunaambiwa kuna vitabu vingi tu havimo kwenye hivyo 72(injili ya Thomas, Barnaba...)
nani alivitoa na kwanini?
Mi sioni ugumu, kwani kama unatka visoma hivyo 72 unanyimwa?Hata Quran ktik uandishi mwanzoni kuna copy kibao zilipigwa chini ikachukuliwa iliyokubaliwa kuwa ndio sahihi kuliko nyingine.manabii hawakuandika hivyo vitabu.Kama katik Biblia vitabu vimeandika mika mingi kabla ya Yesu kuja, na vikatolea kwa vipindi tofauti , vingine ni baada ya Yesu .Yesu hakulazimisha watu waandike ila aliwaambia washuhudie na baadaye waende wakahubiri dunia nzima.Biblia ni Library ya vitabu vilivyoandikwa na watu wengi kwa miaka tofauti.Inashangaza vinafuatana kama mwendelezo na kuendana kwa mambo mengi sana.

Cha msingi inabidi ukasome sababu za VItabu fulani kuchaguliwa na vingine kuachwa,halafu pia tofauti iliyopo katika 66 na hivyo 72.Hao akina Barnaba nika kama watu wengine wanaoibuka na kusema kuwa wan amaono ya Yesu na hivyo kutoa maandiko yao wanayotaka nayo Yawe Injili.Hawa wapo wengi,kuanzia kwenye movie, hadi, sayansi. wanakuja na ubunifu wao wa haraka wakiambiwa waandike concepts zikipitiwa wanajikuta hakuna kitu.
kwa haraka ili upate majibu ya barnabas check y-jesus.com.Ila ni bogus Book ambayo kuna baadhi ya waislam wameishikia bango kama suala la sensa.Ila waislam wengine wamejiepusha na hayo masuala kwani kwa kiasi fulani husoma Biblia kama walivyoagizwa wasibague vitabu,ili kupata mambo ya mitume wengine ambayo hayapatikani katik Quran.Na wengine husoma kwa ajili ya kubishana na hivyo kujiweka katika mazingira ya kuitumia katik njia ya Ibada.

Yaani katik dunia kuna vichaa wengi pasipokuwa na control basi kila mtu atafanya chake akiamini kuwa anajua.hembu nenda UD uone watu pale wasipoweka hata tahadhari katik midomo yao wanapojisifu kuwa ni intelectuals.Hadi wanapokutana na watu wasio na hizo degree ila wanawashuka mambo hadi wananywea.

Otherwise dini si ngumu kwa mwelewa na ugumu ukiuona baada ya kusoma vitabu na kujaribu fuata kila kitu then ukaona vingine vinapingana basi ujue hiyo dini haikuwafai.Y-jesus.com
 
Ndiyo maana nilitangula kusema uumbaji ni complex concept.
Mtu akivamia na kuanza kuielezea akiwa amesimamia msingi fulani bila evidence atakwama tu.

Kwani hata evolution ni simple?Au hata theory ya life kuanzia baharini ni rahisi?Watu wanamsoma bacteria na wadudu wengine ambao ni wadogo kam vile wana cell moja.Ila bado hawajamaliza mambo. DNA yenyewe bado watu waakesha isoma ndio itakuwa kiumbe kama Binadamu na wengine?

Creation bado ilaleta sense big time.Kila mahali wanasayansi wanagundua kuwa kuna set ya rules inayoongoza na pakibadilika kitu tuu panatoke uharibifu mkubwa.Kasome kinga ya mwili ya mwili achilia tuu utaona hakuna kitu rahisi.Wanasayansi makini huwa wanajiuliza hizo rules kaweka nani?hayo maswali walijiuliza akina Eistein, wakajikuta wana kiu ya kutafuta formula moja ya kuelezea yote.Kwani kila kitu kinaonekana kuhusian na kingine kwa karibu sana.Eistein aliishia kujaa na formular E=MxCXC.Na bado alikuwa akiamini hiyo formular itakuwa ni GOD mwenyewe.

Si rahisi kuona mapungufu ya sayansi, ya dini fulani na mahusiano ya dini na sayansi.Sasa wanasayansi wanapiga Kelele za mijusi ya Kale ila tamaduni na hat Biblia inazungumzia hao viumbe na jinsi walivyokuwa wakitishia uhai wa Binadamu.panga na mikuki haikuweza ingia katik ngozi zao.Huu ni ushuhuda kuwa hao viumbe waliihsi na binadamu na walipotea katika mafuriko makuu ya Nuhu,hawa inaelekea Nuhu aliwaacha wengi.Na ndipo walipozamishwa katika matope na kugifadhiwa vizuri.Waliobaki walikufa kwa kupata mazingira magumu ,walipoanza shindana na binadamu.Hayo mabaki ya safina yameonekana maeneo ya Uturuki na iran katika safu ya vilima. So kuwepo kwa dinosours na binadamu kunaonyesha mapungufu ya evolution.Kuwa sijui miaka milioni ngapi ni makosa ya vifaa vyao, na uongo wa evolution
 
Mungu amuumbe shetani ye mwenye halafu sisi turithi dhambi?
Sijui.

Ndio hapo theologia inapokuwa muhimu.Kwanza soam universal values+uje katika Sifa za Mungu.Then unaweza pata sense katik tfsiri ya Mungu.

Kwanza Mungu kawapa viumbe wake "freedom" freedom ni issue by itself.Uliza kwa nini serikali nyingi zin asheria kandamizi, au hata wazazi.Hata wewe mwenyewe unaweza kuwa karibu kila siku unailiia serikali iwafungie sijui gazeti gani, cenema gani, sijui uvaaji gani etc. Nadhani umeona shinda.Freedom ni "sacred". Then Mungu kaweka rules, ila pia ili "kuheshimu" uhuru wako na lazima akupe njia ya kuzikataa, hata kama amekuumba yeye na dunia ani yake.Nadhani hilo pi aunadai kwa baba yako(kakuzaa na unakaa katika nyumba yake ila unalilia san auhuu wako)?Shetani alikuwa na huo uhuru akaupiga chini ili akajitegemee kivyake kwa staili ya kuchagua kuwa muasi.Uasi ni kosa.Linahitaji adhabu.Shetani ni mwasi number moja,na ndiye mkazi wa kwanza Jehanum.Hakuna doubt kuwa huyu jamaa yupo.Waafrica wanajua hilo(tunawaona matajiri wa hayo mambo na wana mwisho illussional, tunaona albino wanavyopotezwa).

Halafu katik uhuru wetu tunaanzisha mahusiano na shetani.Nadhani umeona vijana waliotoka home na kuishi gheto na kufanya matendo ya ajabu ajabu huku wakipata hela, wakifanya anasa nyingi, wakipiga miziki na kula unga.Vijana wangapi huyatamani hayo maisha na kujaribu kuwafuata?Na baada ya kuwafuta hukukaribisha katik hiyo life na baadaye kukolea na mwisho kuhama nyumbani?Hivyo ndivyo nasi tumuhasivyo Mungu na kuingia katik mikataba ya bila jijua na shetani.Na kwa vile tulikuwa na mcheche tuliingia mikataba mikubwa sana na hatuwezi lipa.Hapo ndipo Mungu inabidi aonyeshe upendo kam sifa yake ingine, atafute njia ya kututoa.Ila lazima atende haki kwa shetani bila hivyo shetani atamnyooshea vidole na kumlalamiki kwa haki .Kwanini achukue kilicho chake kama keshamfukuza Mbinguni?Kama ni baba inabidi kumtoa mtoto lazima alipe bill za unga na madeni mengine achukue mzigo wake.hapo shetani au hata hao gheto boys lazima wadai zaidi toka kwa kibopa mzee.Kwa issue ya Shetani, Damu ya kondoo haitoshi kwani mara nyingi Binadamu huwa waliahidi dunia na Mbingu(damu za kwao wenyewe, na watoto wao), so hapa patahitaji damu ya binadamu.Imagine mfalme anamwambia mwanaume mroho mwache huyo binti masikini, ila chagua binti mwingine yoyote,halafu mfalme ana mabinti?Halafu fikiria mfalme anakuja gundua kuwa kuna mabinti wengi wapo katik hatari hiyo ya kujikuta wakidaiwa na mwanamme mroho na hivyo kuamua kuweka dili na huyu mroho kuwa atahitaji bei gani kulipwa kwa wote.

Baada ya hapo fikiri atena kuwa pamoja na Mungu kulipa deni la kila mtu bado anahitajika kuhakikisha hawi dicator na hivyo lazima aheshimu uhuru wa watu.Na hivyo katik walillipiwa kuna wengine wanaamua kukataa na kusema watajilipia wenyewe.Na hawa wanafanya kazi maisha yao yote ili kulipa deni kubwa (mwishowe wanashindwa ,wengine wanaamua ingia katik program ya msaada iliyolipiwa).

Kuhusu kurithi shida .hembu fikiria wazee wanavyokula viapo kirahisi kuwa anaapa kwa maisha yake na ya watoto wake?hembu fikiria watu wanavyotakwia lipa madeni ya kidunia aliyokuwa akidaiwa baba yao au hata babu yao.Hembu fikiria binadamu walivyokuwa wakiiuzwa kwa mikataba iliyoweka wazi kuwa kuwa na mtoto ni mali ya mnunuzi,na aliyetumboni akizaliwa ni wa mnunuzi.Sijui kama ulishwahi nunua mbuzi akazaa ukamrudisha mtoto uliponunu mamake?

Well, sitaki uamue kutokana na niliyoandika ila ni njia rahisi ya kukupa picture jinsi gani hayo mambo yanaleta sense zaidi ya unavyofikira.Hapo Mungu anapaswa fiti katika sifa anazostahili ili awe Mkuu kuliko(yaani aweze kila Kitu).Yaani aweze kuwa sehemu zaidi ya Moja kwa muda mmoja, aweze kuwa na maumbile tofauti, awe mwema, awe na huruma, atende haki,aweze sikiliza na kumtendea kil mmoja.aweze umba, aweze angamiza kila kitu(matter and soul),awe mkweli,awe mwaminifu, aweze kujua future, awe na nguvu zote,..vyote hivi vinamfanya asienee katik fikra zetu,na awe msafi kwa kiwango cha juu sana.Na hivyo kumwachia jukumu lingine la kututafuta na kutupa namna ya kumfuata kwa vile hatupo popote na ni dhaifu sana.Na ukisoma Bible utaona Dhambi kubwa ilikuja baada ya Adamu kudai "uhuru wa kuamua na kutumia akili yake mwenyewe kw auelewa wake mwenyewe" wa kufanya mambo yake katik dunia aiyoijua.Huko ndiko alikojikuta ameabudu mungu mwingine zaidi ya MUNGU .Fikiria mtoto anavyolilia kuhama ili kajitegmee ila kichwani anataka uhuru wa kwenda kununua machangu...

Mara nyingi waru wanaodai uhuru kwa nguvu bila kujiandaa hujikuta katika taabu kabla ya kutengamaa na baadaye hizo taabu kuja wasumbua hata wakitengamaa.

Ukritu umechangia sana ukuaji wa maadili ya kimang`aribi katik kutenda haki,kusaidia, kuwa na uimara wa misimamo, na kujismamia, sayansi na mengineyo.
 
Nahisi hayo mengine tumetunga wanadamu kisha tunamsingizia mungu wa watu. Mungu tumuitaye mwenyezi halipizi visasi.
Visasi vimekaa kibinadamu zaidi.

Teh teh..katik philosophy kuna mazingira mengine matendo yameunganishwa na adhabu. Mfano ukifanya ngono zembe ukapata HIV, ukipanda iba wire wa umeme ukiwa na voltage nyingi na bila vitendea kazi,umekimbiza gari kwa kasi kubwa bila mkand na ni kinyume cha sheria,utakapofikia kusababisha ajali iliyokuwa ikizuia na sheria utasababisha madhara kwa wengine na wewe pia utapata kipimo hichohicho.Umachia mifugo ikala mazao ya mwenzio yenye sumu.Hayo makosa huwa hayana rushwa wala nini, na hii haina sheria inayosema kipimo gani kinatosha.

Halafu kuna makosa yanayosubiri ushahidi na maamuzi kabla ya kuhukumiwa kama inavyoelekezwa na sheria.

katika haya makundi hapa mara nyingi watu hufananisha na visasi.Pia watu wanahitaji jua kuwa visasi pia huweza tumika kwa haki.mfano mwtu kamuua baba yako, mkasuluhisha, halafu katoka hapo kaenda mua mama yako.Sidhani ukibahatika mkuta kabla hajamalizia utamwacha.na hapo patakuwa na hasir aya tukio la kwanza n ahivyo zoezi zima kuwa nusu kisasi, nusu reaction ya eneo husika.SO mungu nae anafanya Visasi, kwani pia anayo haki ya kuadhibi, kwa makosa yanayoudhi ambayo hayajasamehewa.
 
hapana mi siamin ni complex concept ila kulingana na uvivu wa kufikiri ndo mana hatufikii sehem tunayotaka kufika na pia kuna idea flan flan tushazijenga vichwan mwetu

Umiza kichwa basi utusadie na sisi.
 
nakuelewa ila hapa mimi nilikuwa namaanisha kuwa "wote wanaongelea uumbaji", yaani kutengeneza binadamu kama binadamu, mwembe kama mwembe, etc .wakati sayansi inasema "chance+evolution".

sasa litakapokuja suala la huo uumbaji ndio kila mtu atahitaji elezea kivyake na hapo ndipo watatofautiana.haina tofauti na mmasai na mhaya wakitete uafrica wao katik kundi la wazungu na wahindi.Ila wakija pamoja ndipo wataanza ona tofauti zao.Ni kama mwl alipotumia mfano wazenj wakiwa pamoja ndipo wataona tofauti zao.Hapa uuambaji ndio core za dini za Mungu mmoja.

Na wale jamaa wa maabara ya ulaya inayotafuta particle waliyoiita "GOD", ni kwamba wakipata tuu na kujaribu iangalia muda itakayokaa basi watakuja na ushahidi wa kupinga dini zote na si sijui ipi yenye maelzo mazuri ya UUmbaji.

Sasa baada ya hao jamaa kushindwa basi watu watapenda jua katika hizo njia za uumbaji zilizo tofauti ni ipi ya kweli, au zote ni uongo na kuna njia nyingine viumbe walifika duniani.Pengine kwa kuletwa toka sayari nyingine ambayo ndio ina siri kubwa ya uhai.

Kwa mtazamo wangu hata theory ya evolution nayo naichukulia kama inazumgumzia uumbaji, wha if mungu mwenye ndiye aliyetengeneza hizo amino acids?
Nani anaweza kusema ndiyo au hapana katika hili?
Mmsai, mchina na muhindi wanaweza wekwa kundi moja la human civilization kama tukiangalia vitu fulani kama family authorities etc.
 
Mi sioni ugumu, kwani kama unatka visoma hivyo 72 unanyimwa?Hata Quran ktik uandishi mwanzoni kuna copy kibao zilipigwa chini ikachukuliwa iliyokubaliwa kuwa ndio sahihi kuliko nyingine.manabii hawakuandika hivyo vitabu.Kama katik Biblia vitabu vimeandika mika mingi kabla ya Yesu kuja, na vikatolea kwa vipindi tofauti , vingine ni baada ya Yesu .Yesu hakulazimisha watu waandike ila aliwaambia washuhudie na baadaye waende wakahubiri dunia nzima.Biblia ni Library ya vitabu vilivyoandikwa na watu wengi kwa miaka tofauti.Inashangaza vinafuatana kama mwendelezo na kuendana kwa mambo mengi sana.

Cha msingi inabidi ukasome sababu za VItabu fulani kuchaguliwa na vingine kuachwa,halafu pia tofauti iliyopo katika 66 na hivyo 72.Hao akina Barnaba nika kama watu wengine wanaoibuka na kusema kuwa wan amaono ya Yesu na hivyo kutoa maandiko yao wanayotaka nayo Yawe Injili.Hawa wapo wengi,kuanzia kwenye movie, hadi, sayansi. wanakuja na ubunifu wao wa haraka wakiambiwa waandike concepts zikipitiwa wanajikuta hakuna kitu.
kwa haraka ili upate majibu ya barnabas check y-jesus.com.Ila ni bogus Book ambayo kuna baadhi ya waislam wameishikia bango kama suala la sensa.Ila waislam wengine wamejiepusha na hayo masuala kwani kwa kiasi fulani husoma Biblia kama walivyoagizwa wasibague vitabu,ili kupata mambo ya mitume wengine ambayo hayapatikani katik Quran.Na wengine husoma kwa ajili ya kubishana na hivyo kujiweka katika mazingira ya kuitumia katik njia ya Ibada.

Yaani katik dunia kuna vichaa wengi pasipokuwa na control basi kila mtu atafanya chake akiamini kuwa anajua.hembu nenda UD uone watu pale wasipoweka hata tahadhari katik midomo yao wanapojisifu kuwa ni intelectuals.Hadi wanapokutana na watu wasio na hizo degree ila wanawashuka mambo hadi wananywea.

Otherwise dini si ngumu kwa mwelewa na ugumu ukiuona baada ya kusoma vitabu na kujaribu fuata kila kitu then ukaona vingine vinapingana basi ujue hiyo dini haikuwafai.Y-jesus.com

Kwanini vitabu 72/66 wakati mungu ni mmoja?
 
Kwani hata evolution ni simple?Au hata theory ya life kuanzia baharini ni rahisi?Watu wanamsoma bacteria na wadudu wengine ambao ni wadogo kam vile wana cell moja.Ila bado hawajamaliza mambo. DNA yenyewe bado watu waakesha isoma ndio itakuwa kiumbe kama Binadamu na wengine?

Creation bado ilaleta sense big time.Kila mahali wanasayansi wanagundua kuwa kuna set ya rules inayoongoza na pakibadilika kitu tuu panatoke uharibifu mkubwa.Kasome kinga ya mwili ya mwili achilia tuu utaona hakuna kitu rahisi.Wanasayansi makini huwa wanajiuliza hizo rules kaweka nani?hayo maswali walijiuliza akina Eistein, wakajikuta wana kiu ya kutafuta formula moja ya kuelezea yote.Kwani kila kitu kinaonekana kuhusian na kingine kwa karibu sana.Eistein aliishia kujaa na formular E=MxCXC.Na bado alikuwa akiamini hiyo formular itakuwa ni GOD mwenyewe.

Si rahisi kuona mapungufu ya sayansi, ya dini fulani na mahusiano ya dini na sayansi.Sasa wanasayansi wanapiga Kelele za mijusi ya Kale ila tamaduni na hat Biblia inazungumzia hao viumbe na jinsi walivyokuwa wakitishia uhai wa Binadamu.panga na mikuki haikuweza ingia katik ngozi zao.Huu ni ushuhuda kuwa hao viumbe waliihsi na binadamu na walipotea katika mafuriko makuu ya Nuhu,hawa inaelekea Nuhu aliwaacha wengi.Na ndipo walipozamishwa katika matope na kugifadhiwa vizuri.Waliobaki walikufa kwa kupata mazingira magumu ,walipoanza shindana na binadamu.Hayo mabaki ya safina yameonekana maeneo ya Uturuki na iran katika safu ya vilima. So kuwepo kwa dinosours na binadamu kunaonyesha mapungufu ya evolution.Kuwa sijui miaka milioni ngapi ni makosa ya vifaa vyao, na uongo wa evolution

Hakuna uthibitisho kuwa kile kipande cha mbao kilichoonekana huko kilikuwa sehemu ya safina.
Pamoja na hilo, unaweza kufafanua ni namna gani nuhu alizunguka dunia nzima na ku-collect species zote?
 
Ndio hapo theologia inapokuwa muhimu.Kwanza soam universal values+uje katika Sifa za Mungu.Then unaweza pata sense katik tfsiri ya Mungu.

Kwanza Mungu kawapa viumbe wake "freedom" freedom ni issue by itself.Uliza kwa nini serikali nyingi zin asheria kandamizi, au hata wazazi.Hata wewe mwenyewe unaweza kuwa karibu kila siku unailiia serikali iwafungie sijui gazeti gani, cenema gani, sijui uvaaji gani etc. Nadhani umeona shinda.Freedom ni "sacred". Then Mungu kaweka rules, ila pia ili "kuheshimu" uhuru wako na lazima akupe njia ya kuzikataa, hata kama amekuumba yeye na dunia ani yake.Nadhani hilo pi aunadai kwa baba yako(kakuzaa na unakaa katika nyumba yake ila unalilia san auhuu wako)?Shetani alikuwa na huo uhuru akaupiga chini ili akajitegemee kivyake kwa staili ya kuchagua kuwa muasi.Uasi ni kosa.Linahitaji adhabu.Shetani ni mwasi number moja,na ndiye mkazi wa kwanza Jehanum.Hakuna doubt kuwa huyu jamaa yupo.Waafrica wanajua hilo(tunawaona matajiri wa hayo mambo na wana mwisho illussional, tunaona albino wanavyopotezwa).

Halafu katik uhuru wetu tunaanzisha mahusiano na shetani.Nadhani umeona vijana waliotoka home na kuishi gheto na kufanya matendo ya ajabu ajabu huku wakipata hela, wakifanya anasa nyingi, wakipiga miziki na kula unga.Vijana wangapi huyatamani hayo maisha na kujaribu kuwafuata?Na baada ya kuwafuta hukukaribisha katik hiyo life na baadaye kukolea na mwisho kuhama nyumbani?Hivyo ndivyo nasi tumuhasivyo Mungu na kuingia katik mikataba ya bila jijua na shetani.Na kwa vile tulikuwa na mcheche tuliingia mikataba mikubwa sana na hatuwezi lipa.Hapo ndipo Mungu inabidi aonyeshe upendo kam sifa yake ingine, atafute njia ya kututoa.Ila lazima atende haki kwa shetani bila hivyo shetani atamnyooshea vidole na kumlalamiki kwa haki .Kwanini achukue kilicho chake kama keshamfukuza Mbinguni?Kama ni baba inabidi kumtoa mtoto lazima alipe bill za unga na madeni mengine achukue mzigo wake.hapo shetani au hata hao gheto boys lazima wadai zaidi toka kwa kibopa mzee.Kwa issue ya Shetani, Damu ya kondoo haitoshi kwani mara nyingi Binadamu huwa waliahidi dunia na Mbingu(damu za kwao wenyewe, na watoto wao), so hapa patahitaji damu ya binadamu.Imagine mfalme anamwambia mwanaume mroho mwache huyo binti masikini, ila chagua binti mwingine yoyote,halafu mfalme ana mabinti?Halafu fikiria mfalme anakuja gundua kuwa kuna mabinti wengi wapo katik hatari hiyo ya kujikuta wakidaiwa na mwanamme mroho na hivyo kuamua kuweka dili na huyu mroho kuwa atahitaji bei gani kulipwa kwa wote.

Baada ya hapo fikiri atena kuwa pamoja na Mungu kulipa deni la kila mtu bado anahitajika kuhakikisha hawi dicator na hivyo lazima aheshimu uhuru wa watu.Na hivyo katik walillipiwa kuna wengine wanaamua kukataa na kusema watajilipia wenyewe.Na hawa wanafanya kazi maisha yao yote ili kulipa deni kubwa (mwishowe wanashindwa ,wengine wanaamua ingia katik program ya msaada iliyolipiwa).

Kuhusu kurithi shida .hembu fikiria wazee wanavyokula viapo kirahisi kuwa anaapa kwa maisha yake na ya watoto wake?hembu fikiria watu wanavyotakwia lipa madeni ya kidunia aliyokuwa akidaiwa baba yao au hata babu yao.Hembu fikiria binadamu walivyokuwa wakiiuzwa kwa mikataba iliyoweka wazi kuwa kuwa na mtoto ni mali ya mnunuzi,na aliyetumboni akizaliwa ni wa mnunuzi.Sijui kama ulishwahi nunua mbuzi akazaa ukamrudisha mtoto uliponunu mamake?

Well, sitaki uamue kutokana na niliyoandika ila ni njia rahisi ya kukupa picture jinsi gani hayo mambo yanaleta sense zaidi ya unavyofikira.Hapo Mungu anapaswa fiti katika sifa anazostahili ili awe Mkuu kuliko(yaani aweze kila Kitu).Yaani aweze kuwa sehemu zaidi ya Moja kwa muda mmoja, aweze kuwa na maumbile tofauti, awe mwema, awe na huruma, atende haki,aweze sikiliza na kumtendea kil mmoja.aweze umba, aweze angamiza kila kitu(matter and soul),awe mkweli,awe mwaminifu, aweze kujua future, awe na nguvu zote,..vyote hivi vinamfanya asienee katik fikra zetu,na awe msafi kwa kiwango cha juu sana.Na hivyo kumwachia jukumu lingine la kututafuta na kutupa namna ya kumfuata kwa vile hatupo popote na ni dhaifu sana.Na ukisoma Bible utaona Dhambi kubwa ilikuja baada ya Adamu kudai "uhuru wa kuamua na kutumia akili yake mwenyewe kw auelewa wake mwenyewe" wa kufanya mambo yake katik dunia aiyoijua.Huko ndiko alikojikuta ameabudu mungu mwingine zaidi ya MUNGU .Fikiria mtoto anavyolilia kuhama ili kajitegmee ila kichwani anataka uhuru wa kwenda kununua machangu...

Mara nyingi waru wanaodai uhuru kwa nguvu bila kujiandaa hujikuta katika taabu kabla ya kutengamaa na baadaye hizo taabu kuja wasumbua hata wakitengamaa.

Ukritu umechangia sana ukuaji wa maadili ya kimang`aribi katik kutenda haki,kusaidia, kuwa na uimara wa misimamo, na kujismamia, sayansi na mengineyo.

Kama mungu anajua yote, hata yale yajayo logically maana yake mungu ndiye anayepanga kila kitu.
Kwahiyo wakati anamuumba shetani alijua matokeo yake na akaona ni sawa, ikawa jioni ikawa asubuhi siku nyingine akaumba jehanamu akijua atakuja mchoma mwanadamu.
Hivi mungu anayetupenda anaweza kuumba jehanamu kabla hata ya mwanadamu.
Mi naogopa kumsingizia mungu.
 
Teh teh..katik philosophy kuna mazingira mengine matendo yameunganishwa na adhabu. Mfano ukifanya ngono zembe ukapata HIV, ukipanda iba wire wa umeme ukiwa na voltage nyingi na bila vitendea kazi,umekimbiza gari kwa kasi kubwa bila mkand na ni kinyume cha sheria,utakapofikia kusababisha ajali iliyokuwa ikizuia na sheria utasababisha madhara kwa wengine na wewe pia utapata kipimo hichohicho.Umachia mifugo ikala mazao ya mwenzio yenye sumu.Hayo makosa huwa hayana rushwa wala nini, na hii haina sheria inayosema kipimo gani kinatosha.

Halafu kuna makosa yanayosubiri ushahidi na maamuzi kabla ya kuhukumiwa kama inavyoelekezwa na sheria.

katika haya makundi hapa mara nyingi watu hufananisha na visasi.Pia watu wanahitaji jua kuwa visasi pia huweza tumika kwa haki.mfano mwtu kamuua baba yako, mkasuluhisha, halafu katoka hapo kaenda mua mama yako.Sidhani ukibahatika mkuta kabla hajamalizia utamwacha.na hapo patakuwa na hasir aya tukio la kwanza n ahivyo zoezi zima kuwa nusu kisasi, nusu reaction ya eneo husika.SO mungu nae anafanya Visasi, kwani pia anayo haki ya kuadhibi, kwa makosa yanayoudhi ambayo hayajasamehewa.

Adhabu za hapa duniani nazikubali bila sida ila sina hakika kama zinatoka kwa mungu.
Kuhusu visasi:
Sifa kuu ya mungu ambayo mi nategemea awenayo ni perfection, sasa ukianza kuniambia mungu anakasirika, anawivu, analipa visasi n.k, naona sisi wanadamu na mapungufu yetu tunaanza kujifananishanaye na kumpunguzia mungu sifa zake.
To me if GOD is perfect then every thing to him/her is ok & follows his/her plans, hakuna kujuta wala kukasirika.
 
Nashukuru sana kwakuelewa point yangu na kuwa open minded.
I like this kind of discussion.
Nakubaliana na wewe kuwa bible ilitangulia na kuna similarities kati ya vitabu hivyo viwili.
Ila wakati bible inazungumzia uumbaji wa mwanadamu kwa udongo, quran inazungumzia tone la manii(kama sijakosea).
Hapo tayari kunatofauti na kila moja kati ya dini hizo mbili zinaamini ziko sahihi.

Pia Quran inasema kuwa Adam aliumbwa kwa udongo, kizazi kilichofuatia cha Adam ndio kimeumbwa kwa tone la manii.
 
Kwanini vitabu 72/66 wakati mungu ni mmoja?

Historia ya Mungu wa Abrahamu na binadamu inachukua uzao fulani toka kwa Adamu hadi Nuhu.Pakapotea hadi kuja endelea kuanzia kwa Abahamu hapa path iliyochukuliwa ilifuata ujuo wa wayahudi na mahusiano yao na Mungu na mwishowe.Kutokea Yesu na wafuasi wake.

Wayahudi kama kabila walikuwa na tamaduni zao ambazo si lazima Wakristu wazichukue.Biblia Ni jina Jipya,mwanzo palikuwa na vitabu vitu vingi kama vile waislam walivyo na hadith Nyingi +vitabu vya Sirat na Quran. Waislam kuna hadith hazijapitishwa na wanazuoni, na hizi nazo kunaweza kuwa na watu wanaoweza endelea hoji kwanini hazipo katika list ya hadith sahihi.

Sasa kama baraza la wasomi wangeamua zikusanya hizo Hadith zilizokubalika + weka na Sirat+Qurani kwa mpangilio mzuri wangekipa kitabu kipya jina lake.Pia pasingekosekana watu wengine ambao wangetamani na hizo hadith nyingine ambazo kwa sasa si sahihi ziwekwe.


Biblia ndio hivyo hivyo, baraza lilikaa na kukubaliana kuna haja ya kuweka vitabu vyote katik binding moja na kukiita hicho kitabu Biblia.Sasa ktk kuchagua kitabu gani kinastahili kukaa na kipi hakistahili kutokana na vigezo walivyojiwekea na kuapa kuna ,watu walikuja na kuona kuwa katik ya 72 vitabu 6 hajikuwa na ulazima sana wa kuwepo.Kwa hiyo makanisa mapya yakavitoa na kubaki na 66.Kanisa katoliki lina 72.Kwa anayehitaji anaweza visoma.
 
Hakuna uthibitisho kuwa kile kipande cha mbao kilichoonekana huko kilikuwa sehemu ya safina.
Pamoja na hilo, unaweza kufafanua ni namna gani nuhu alizunguka dunia nzima na ku-collect species zote?

Ni vipande sio kipande, na jina la huo mlima linaendana sana vilele vilivyopo maeneo hayo na hivyo sayansi ndio inakimbizana kupata majibu hayo.Unaweza ona jinsi watu wanavyoanzia katik biblia halagu wanakuja na majibu baadaye.Ama wanaanza kwa kupinga ama wanaanza kama kutack hayao maeneo.wenzetu huwa wanasoma sana historia kabla ya kutengeza mpango wa kufanya upelelezi.Hata olduvai gorge,hawakuenda chimba tuu porini hadi wakapata hayo mafuvu.

Nuhu aliwaita wanyama wengine, wengine aliwakusanya na kama ilivyo kwa binadamu pia wanyama wengine waliachwa wateketeketee kwa sababu zilizoonekan ana Mungu kuwa sahihi.wengine kama walilaaniwa vile.Imagine kunguru alivyoachiwa hakurudi kwani tamaa ya mizogo ilimfanya asirudi tena.
 
Adhabu za hapa duniani nazikubali bila sida ila sina hakika kama zinatoka kwa mungu.
Kuhusu visasi:
Sifa kuu ya mungu ambayo mi nategemea awenayo ni perfection, sasa ukianza kuniambia mungu anakasirika, anawivu, analipa visasi n.k, naona sisi wanadamu na mapungufu yetu tunaanza kujifananishanaye na kumpunguzia mungu sifa zake.
To me if GOD is perfect then every thing to him/her is ok & follows his/her plans, hakuna kujuta wala kukasirika.

haha..nadhani hujanielewa kwa vile nimeweka mambo mengi.Labda tuu nikuulize perfection ya Mungu inahusiana vipi na mapungufu ya binadamu,mwenye uhuru na kiburi?(mojawapo za roots of evil ni greed, pride,).Huko kuwa perfect ndioko kunamfanta ashindwe ishi na evil.Na kama ni huruma Mungu kafanya Huruma sana kwa binadamu, kafanya maaganao mengi sana nao,ila binadamu kayavunja,bado yeye ndiye anayekuja kututafuta na kuanza tena mengine.

Kukasirika kwa haki si kosa ila ni ukamilifu.Nadhani mara nyingi umeshaona watoto wakililia haki ya kupewa urithi wao, na uhuru wa kutumia wapendavyo, wazai wanaona kabisa mwanao hawezi kutumia hizo mali kwa busara ila hawawezi vunja sheria na kumnyima au hata kumyima uhuru.Ila baadaya wanasikia mwano kawekwa ndani kwa kupigana baa, kaleta hasara na pengine kaua mkewe.Sidhani kama hutokuwa na hasara.Je unadhani hata kama unajua kuwa mwanao hawezi yatazama maisha,nin utafanya kwa haki wakati mwanao mwenyewe hajui kuwa baada ya hapo mambo yatakwenda mwaribikia kabisa?Na hata kama anajua ila kayapenda hayo maisha, na akakuambia kwanini unamhukumu na hujaona akikosea utamjibu nini?Huwezi mhukumumu mtu kabla hajatenda ,hata kama unajua akitenda atasababisha hasara kubwa.Watu wana abuse sheria makusudi, hujaona watu hawaheshimu sheria ikiwabana,ila wanaitumia ikiwa inawasaidia?mahakama haiwezi sema sikupi sheria kwa vile huitambui.
 
Back
Top Bottom