Nahisi mwiba ulikuwa wataka leta ajenda ingine kupitia hii.
Sioni kosa la Mwakyembe apo.
Isipokuwa ni yule mzenji kupewa kaazabu kumrudisha kwenye utimama na ajijue kuwa chochote asemacho anaongea kama nani na kina impact gani kwa jamii.
 
Ndugu MWIBA, kama wewe si yule mmoja wao au mfaidika kutoka kwao basi nahofu kuna fisadi kakununua. Tutajie umelipwa ngapi kama ujira wa kuwasafisha mafisadi ili hapa JF tuweze kufanya harambee tukurudishie fedha ukawarudishie uwe huru kwani ulichoongea kina harufu ya kutumwa / kununuliwa! Samahhani kama nimekukwaza, ila twakuhitaji sana ukiwa na mawazo huru tusaidie kupambana. Nawasilisha
 
Ndugu yangu Mwiba, wakati mwingine huwa unanichekesha sana unapoamua kumwaga pumba kavu kavu.

Utaona pumba ikiwa unaufinyu wa kuelewa kilichokusudiwa na utabakia kupiga makofi wakati hujui hata kinachojadiliwa.
 
mi nadhani Mwiba anajikomba apewe ajira ya uandishi wa habari kwenye magazeti mapya yaliyoanzishawa hivi karibuni.otherwise akapime.
 
Nahisi mwiba ulikuwa wataka leta ajenda ingine kupitia hii.
Sioni kosa la Mwakyembe apo.
Isipokuwa ni yule mzenji kupewa kaazabu kumrudisha kwenye utimama na ajijue kuwa chochote asemacho anaongea kama nani na kina impact gani kwa jamii.
Kosa jingine la Mwakiyembe kama bado mna matatizo ya kufahamu, ni lini alizungumza Shamhuna ? Ni lini Spika Sitta alisimamisha mambo hayo kuzungumzwa Bungeni ? Ni Lini Mwakiyembe alizungumza ,Je haoni kama alimdharau Spika kwa kuleta ushambenga wake wakati ulikwisha kupigwa stop ? Au ndio anapeleka ujumbe kuwa kuna vikao vya siri vinalifuatia suala hilo chini kwa chini maana Mwakiyembe ni CCM na Pinda mwenyewe alipoona maji makubwa alikwisha sema analirudisha kwa CCM ,hivyo akina Mwakiyembe wanaonyesha misuli yao ndani ya Chama ,hawa ni watu wa kigeugeu utawaona wanasema mpaka kipovu kinawatoka lakini hawana maana hata ya senti tano ,hawa ndio wanaotulizwa na mafisadi bungeni usione hoja siku hizi hazizungumzwi na badala yake wamerukia suala la Zanzibar si Nchi ,hivi hamshangai na kuwahoji akina Mwakiyembe yako wapi makali yao ya kuwabana mafisadi na Chama chake kinawawajibisha mafisadi ,yupo Lowasa na wengine asimamie waondoshwe kwenye Chama kwani wamekitia aibu na yeye si ndie aliekusanya ushahidi na mengine akayaficha atumie ushahidi huo kuwawajibisha waliohusika.Anaogopa kukosa adabu au sio?
Shamhuna na wengine huko Zenji walikwisha kukaa kimya kitambo na sasa hoja imepelekwa kwa Wananchi ambao wanaandaa maanadamano makubwa ,kwa nini Mwakiyembe amezusha tena Bungeni haoni kama anafufua malumbano ,huku si ndio kukosa adabu kwenyewe ,wakati spika anakaribia kuzimisha hoja wewe unaenda kuifufua upya na kutoa hukumu ?
 
Matokeo ya makosa ya Mwakyembe ndio kama ilivyo hapa chini, kazi kwako mwiba mi simo.

Richmond: Vigogo wahaha upyaa...!



Kuna habari kuwa baadhi ya vigogo waliotajwa kuhusika katika kuingiwa kwa mkataba tata baina ya Serikali kupitia TANESCO na Kampuni ya Kuzalisha umeme ya Richmond wameanza kuhaha upya baada ya kutolewa taarifa kuwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda yuko tayari kuanika hatua kadhaa ambazo Serikali imeamua kuzichukua dhidi ya wote waliohusika.

Taarifa ambazo Alasiri imezipata kutoka kwa chanzo kimoja kilicho karibu na vigogo hao, zinasema hofu iliyopo sasa ni kubwa na kwamba wanahaha katika kuhakikisha kuwa wanajua kile kilichokubaliwa na Serikali kuwa kitekelezwe, kati ya mapendekezo 23 yaliyoainishwa na Kamati ya Bunge iliyoibua kwa umahiri mkubwa uozo wote wa mkataba huo, huku ikiongozwa na Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe.

``Kama kuna wakati mgumu zaidi kwa hawa vigogo waliotajwa ni huu... mmoja aliye bosi wangu amekuwa na hofu kubwa kwa sababu hajajua ni uamuzi upi hasa ambao Serikali imekubali kuutekeleza. Anahofia kuwa hatua yoyote dhidi yake inaweza kummaliza,`` kikasema chanzo chetu hicho.

Hivi akribuni, katika moja ya maelezo yake bungeni, Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye ndiye anayesubiriwa kulieleza Bunge juu ya hatua zilizochukuliwa na Serikiali katika kutekeleza mapendekezo ya Kamati ya Mwakyembe, alisema yeye yuko tayari kutangaza yale yaliyoafikiwa na Serikali wakati wowote ule.

``...ninachosubiri sasa ni kupangiwa ratiba na Spika,`` alisema Mhe. Pinda, wakati akitoa maelezo hayo.

Hata hivyo, sasa zimebaki siku 14 tu kabla ya kuahirishwa kwa Mkutano wa sasa wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano, hivyo hatma ya vigogo hao kuendelea kuwa mikononi mwa Spika Sitta ambaye anasubiriwa kumpangia wasaa muafaka Mheshimiwa Waziri Mkuu ili naye aanike kile ambacho Serikali imeamua kukitekeleza.

Wakati wa kuwasilishwa kwa mapendekezo ya Kamati ya Bunge iliyochunguza Mkataba wa Richmond, Mwenyekiti wa Kamti hiyo Dk. Mwakyembe, alitaja mapendekezo 23, baadhi yake ikiwa ni pamoja na kuondolewa katika nafasi zao baadhi ya watendaji wa Serikali, mapendekezo ambayo yalioungwa mkono na wabunge wote.

* SOURCE: Alasiri [Accessed 1800 EAT]
 
Nahisi mwiba ulikuwa wataka leta ajenda ingine kupitia hii.
Sioni kosa la Mwakyembe apo.
Isipokuwa ni yule mzenji kupewa kaazabu kumrudisha kwenye utimama na ajijue kuwa chochote asemacho anaongea kama nani na kina impact gani kwa jamii.
Ngoja uyo Shamhuna apate habari halafu usikie vitu vyake,mimi sipo na akina Shamhuna wala Mwakiyembe ,maana wote hao ni ndugu ila nashangaa kwa upande wangu kwa nini CCM Wahafidhina wamelivalia njuga suala hili nilitegemea CUF ndio wawe mstari wa mbele lakini kinyume chake,ndio saa ingine naona timu ya Butiama na Timu ya Wafidhina Kisiwa ndui bado zinapimana nguvu.
Kwa vile najiweka upande wa upinzani naona haya madai na mdaiwa si bure ila kuna game inachezwa, stay tuning.
 
Habari wana jamiiforums. Nami ningependa kutoa maoni yangu kidogo kuhusu issue ya zanzibar. Mimi kwa upande wangu naona kuna vitu vya kuwekwa sawa. Kwanza kipindi kile cha kuunganisha hakuna mwananchi yeyote aliyeshirikishwa katika kuunganisha nchi hizi hivyo kuna watu especially Zanzibar ambao hawakuridhika na hiyo dhana na kwa mazingira yalivyouwa walikuwa hawaweza kusema kama wafanyavyo sasa. So cha kwanza uwekwe mchakato kama watu wanataka muungano ama la.
Pili ubinafsi ukiangalia kwa undani sana utaona ni kwa jinsi gani zanizibar inainyonya tanganyika maana tanganyika yenyewe ina kila kitu lakini imekaa kimya. Kuna mangapi ambayo wazanzibari walikuwa wanapata lakini watanganyika hawapati umeme, maji etc tena bure hapo kabla! Je huku bara watu wamewahi kupata umeme au maji bure? Acha huduma.
Tatu wanaona kuwa nguvu nyingi iko bara hivyo ili kuizuia hiyo watambulike wenyewe. Mfano mdogo hawa jamaa wa mpira ZFA na TFF nafikiri kila mtu alisikia ZFA inatakwa gawio lake la kutoka FIFA. Hiyo ni baada ya kujaribu kujiunga wakakataliwa kuwa wao si nchi haiwezekani nchi moja iwe na vyama viwili. Wanataka nusu kwa nusu. Je basis yao ni wapi? Maana haiwezekani zanzibar na tanganyika ziwe sawa.

Hivyo mimi kwa upande wangu kama kawaida ya wabara huwa hawarush kwenye maamuzi hivyo tuite kura ya maoni nani anataka muungano na kama unatakiwa then uwe wa aina gani ili kuondoa hivi vijineno vya hapa na pale.

Nawakilisha
 
SOVEREIGNTY AS RIGHT AND POWER

Sovereignty does not signify merely a certain degree or quantity of power, as if the extent to which a state is sovereign can be measured simply by calculating its relative military and economic power. Sovereignty signifies simultaneously a right to act and a power to act. There are cases where the power of a state to act is so confined and limited LIKE THE ISSUE OF FIFA AND OIC ZANZIBAR DONT HAVE THAT ONE ...that its sovereign right to act is rendered largely meaningless. Equally, there are times when the actual power of a state is so great that, although its sovereign right to use this power has not been formally acknowledged by others, it is tacitly recognized. These are extreme cases, however. Normally sovereignty means the possession of a right and power, and disputes about sovereignty are disputes about right and power.

Sovereignty manifests itself in different forms, and this largely accounts for the varying definitions that are given of it. Seen from one angle, the right and power of sovereignty is exercised over territory, and is akin to the right and power of possession or ownership of a potion of the Earth's surface. This ownership of territory includes in turn a right and power over all that exists, whether static or mobile, human or non-human, within the territory concerned, and extends to so-called territorial waters and airspace. Great Britain's claim to sovereignty over the Falkland Islands (Islas Malvinas) is a claim of ownership of this kind. Argentina denies Great Britain's right, claiming a prior right of her own. Argentina has attempted to give her right substance by challenging Great Britain's power in the Falklands War, but without success.
 
Hata akitangaza huo utakuwa ni mwanzo labda utumike udikteta nasema kama mpinzani sipo tayari kuunga hatua yeyote ya Serikali au Chama kilichopo madarakani natumai tumeelewana.
Maana hawa hawa wote ni CCM ,sasa kama wameharibu ni wote ,hawa ndio waliokuwa wakipita mitaani na kutangaza sera leo ni miaka mitatu wanabadilisha mawaziri na mawizara miaka inakatika,sasa kufanya hivyo wanategemea kununua miaka mingine mitano au sio ?
Kuondolewa kwenye nafasi zao hivi mmepaona hapo ? Na kwa nini isiwe kufukuzwa kwenye nafasi zao ! Wanaogopa watakosa adabu.Kama viongozi hawakukosolewa na kutolewa nishai wataendelea kutuburuza mpaka mwisho wa kiama.Ni lazima watolewe uvivu.
Kuna yule mwanafunzi wa dalasa la saba aliemuuliza Lowasa kuwa mnatuambia tusome ili tuje kupata nafasi za kazi,kazi zenyewe zipo wapi wakati kiongozi mmoja tu wa CCM anamadaraka na vyeo kibao nafasi hizo zitatoka wapi ?(Sina uhakika na hilo suala lakini ni muelekeo kama lilivyoulizwa) Mpaka leo suala lile halijajibiwa na yule kijana nusura avamiwe kwa fikra za akina Mwakyembe amemdharau mkuu hana heshima hana adabu,sijui mna kumbukumbu ?
 
Naona wachangiaji wengi wamejikita katika kuujadili Muungano kwa bias kwenye upande hasa wa kiuchumi na kisiasa.Nahoji hivi,ni kweli kuwa hakuna vitu vingine kama kijamii au/na kiusalama ambapo muungano huu una manufaa?Au ni kuwa the cons overweigh the pros.Sijaisoma thread yote,hivyo kama haya niliyoandka ni duplicate ya yaliyokwisha andikwa basi mtaniwia radhi.
 
Naona wachangiaji wengi wamejikita katika kuujadili Muungano kwa bias kwenye upande hasa wa kiuchumi na kisiasa.Nahoji hivi,ni kweli kuwa hakuna vitu vingine kama kijamii au/na kiusalama ambapo muungano huu una manufaa?Au ni kuwa the cons overweigh the pros.Sijaisoma thread yote,hivyo kama haya niliyoandka ni duplicate ya yaliyokwisha andikwa basi mtaniwia radhi.

Muungano mzima hauna hata sehemu moja utakayoigusa ukaikuta salama ,mafisadi wameteka kila kona na utawasikia wakiapa kuwa wataulinda Muungano na wengine hula viapo japo hawaendi makanisani wala misikitini.
 
This is ridiculous. Zanzibar is semi autonomous, Tanzania is soverein and Tanganyika is non existent or impotent. I feel sick when i hear people ask this kind of question which has obvious answer.
 
Kila kitu kiko wazi juu ya hili.Katiba ya muungano iko juu ya katiba ya zanzibar, kwa hiyo kama kuna mkanganyo upo kwenye hiyo ya zanzibar, ya Muungano ndio muamuzi. Hawa akina Shamhuna si kwamba hawajui hilo bali wanataka iwe nchi sasa. Nadhani ni wakati mwafaka huu muungano kuletwa kwa wananchi waupigie kura ya maoni, maana wazee wale walijifanyia tu mambo yao bila kuhusisha watu kikamilifu.
Kuhusu mafuta kuwepo zanzibar, hiyo ni ndoto ya mchana au kutokujua kitu juu ya utafutaji wa mafuta. Dalili za kuwepo mafuta, si kuwa tayari kuna reserve ya mafuta. Katika taratibu za utafutaji mafuta, huwezi kutangaza umepata mafuta mpaka uchimbe kisima na ku flow out the oil(of economical value) ndio useme.Kama mafuta ndio basis ya mgogoro basi kuna tatizo kubwa la upeo wa mambo huko Zanzibar.
 
SOVEREIGNTY AS RIGHT AND POWER

Sovereignty does not signify merely a certain degree or quantity of power, as if the extent to which a state is sovereign can be measured simply by calculating its relative military and economic power. Sovereignty signifies simultaneously a right to act and a power to act. There are cases where the power of a state to act is so confined and limited LIKE THE ISSUE OF FIFA AND OIC ZANZIBAR DONT HAVE THAT ONE ...that its sovereign right to act is rendered largely meaningless. Equally, there are times when the actual power of a state is so great that, although its sovereign right to use this power has not been formally acknowledged by others, it is tacitly recognized. These are extreme cases, however. Normally sovereignty means the possession of a right and power, and disputes about sovereignty are disputes about right and power.

Sovereignty manifests itself in different forms, and this largely accounts for the varying definitions that are given of it. Seen from one angle, the right and power of sovereignty is exercised over territory, and is akin to the right and power of possession or ownership of a potion of the Earth's surface. This ownership of territory includes in turn a right and power over all that exists, whether static or mobile, human or non-human, within the territory concerned, and extends to so-called territorial waters and airspace. Great Britain's claim to sovereignty over the Falkland Islands (Islas Malvinas) is a claim of ownership of this kind. Argentina denies Great Britain's right, claiming a prior right of her own. Argentina has attempted to give her right substance by challenging Great Britain's power in the Falklands War, but without success.

Ingawa hiyo lugha mimi sieelewi vizuri. Nafikiri umeielezea vizuri sana sovereignity. Hivyo naamini utakubaliana nami kuwa Zanzibar ni Nchi yenye sovereiginty yake ya asili. Imeungana na Tanganyika kwa hiari yake, na hivyo kuikabidhi sovereignity hiyo kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Haikufa wala kupotea. Inachodai Zanzibar(kama nchi) ni kuwa inawekewa mikwala kuitumia sovereignity(milki yake ya asili) kama inavyopendelea kupitia Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hakuna malumbano hapa, mikwala na iondoshwe. Kama imo katika Katiba- vipengele na vibadilishwe -Twende na wakati.
 
This is ridiculous. Zanzibar is semi autonomous, Tanzania is soverein and Tanganyika is non existent or impotent. I feel sick when i hear people ask this kind of question which has obvious answer.

Nani kakwambia kuwa Zanzibar ni Semi-Autonomous. Nenda katafute uzuri ni nini Semi Autonomous, na ivishe Zanzibar hapo -Jee inastahili kuitwa hivyo?
 
Ana kesi ya kujibu mbele ya WaTanganyika iweje waTanganyika ? na Sio WaTanzania hivi unaelewa ya kwamba Tanganyika imezirai na Zanzibar bado inatuta ? Unaweza kukariri mstari ambao wewe unauona kuwa ni kweli tupu,halafu tuone kama Mwakyembe hakuvunja Katiba kwa kuzuia haki na kutaka Shamhuna asulubiwe ,maana ndivyo ilivyozoeleka ndani ya CCM ukisema ukweli unaitwa mhaini,unaitwa mpinzani unaonekana si mwenzetu ,unaekewa kikao na wafuata upepo wote wanakuzamisha kwa kuwa tu umepinga kauli,jamani mambo ya Ndio Mkuu yamepitwa na wakati wakuu wenyewe sasa hawajui hata dira ya Tanzania ilipoekea wanahitaji msaada wa hali ya juu na sio kila wanakotuongoza tuseme ndio huko huko mbele kwa mbele ,huu ni wakati wa kuekana sawa awe Raisi,Waziri Mkuu,au Waziri yeyote au kiongozi yeyote yule Jeshi au Polisi si wakati wa kunyamaziana na anapopingwa mtu wengine wakaruka na kusema unakosa adabu ,huna nidhamu ,kila mtu tapewa heshima yake na kuheshimiwa lakini linapokuja suala la kujadiliana hapo hapatakiwi usawa nani Mkuu nani mtawala nani mtawaliwa panatakiwa hoja kujadiliwa kupingwa kukosolewa isiwe akipingwa mtu aseme fulani inafaa adhibitiwe,inafaa achuliwe hatua ,inafaa aadhibiwe, ukisikia mtu anasema hivyo basi huyo ni adui wa haki tena ni mtu ambae inaonyesha ubaya wake upo ndani kwa ndani.
Shamhuna hana uhusiano na serikali ya Muungano wala CCM kama sikosei,ni kiongozi katika serikali ya Zanzibar ,hivyo alikuwa anawajibika kusema lolote iwe amesema alivyosema Pinda ni sahihi au alivyosema Pinda si sahihi ,natumai anayo haki hiyo ,sasa kilichowatonesha akina Mwakiyembe ni kwa nini Shamhuna amesema au ameipinga kauli ya Pinda hata kama kauli hiyo ilikwishatolewa maelezo lakini ifahamike ni wapi ilipotolewa maelezo ni Bungeni kwenye chombo cha Muungano na Shamhuna nae ametolea maelezo kwenye Baraza la wawakilishi Chombo chao huko Zanzibar ,kosa lipo wapi ? Bahati mbaya Shamhuna amesimamia Uzalendo wa Taifa lake na Katiba ya Zanzibar ambayo inatamka wazi Zanzibar ni nchi ,na yeye yupo sahihi zaidi kuliko Pinda kwani hakuna sehemu katika Katiba ya Muungano palipoandikwa Zanzibar si Nchi.
Jaribuni mnaposoma na kutoa hoja msiwe na jazba aidha kama wewe ni CCM hapo nitakuwa sina la kukufanya ,vilevile ukiwa ni Mtanganyika pia nitakuwa nakuangalia tu.Ila Kama unajihesabu ni Mtanzania basi itabidi uwe katika njia inayotakiwa kuwepo ,japo upo na Chama usijaribu kukilinda chama kinapokosea ni lazima ukiulize,ukihoji ili kupata maelezo na kama yanahitajika kupingwa basi usisite kupinga ,kuliko kuogopa kuambiwa unadharau au huna adabu ni aibu kwa DR>Mwakiyembe kusema maneno alisema ya fulani adhibitiwe au sijui atiwe adabu na wengine mnarukia na kumuona ni shujaa sijui kwa kigezo kipi.

Ustadh Mwiba mata nyingi hupinga mawazo yako. Kumradhi yakhe (Ndo demokrasia). Lakini kwa haya mengine nakuunga mkono uelezayo ni sahihi. Hiyo kunyamaza na kupiga makofi tu japo yanaenda mrama imewakosesha mengi Wazanzibari. Endelea na msimamo wako Mwiba elezea uelezayo. Mwakyembe amefurunda -yeye.
 
Nani kakwambia kuwa Zanzibar ni Semi-Autonomous. Nenda katafute uzuri ni nini Semi Autonomous, na ivishe Zanzibar hapo -Jee inastahili kuitwa hivyo?

Pakacha,
Baada ya kuungana na Tanganyika Zanzibar ilipoteza sovereignty yake. Ndio maana kiti chake katika UN kiliangukia chini ya Tanzania. Ndio maana ilipojiunga na OIC kinyemelea ililazimika kujiondoa baada ya jambo hilo kufahamika hadharani. Tatizo liko wapi?
 
Habari wana jamiiforums. Nami ningependa kutoa maoni yangu kidogo kuhusu issue ya zanzibar. Mimi kwa upande wangu naona kuna vitu vya kuwekwa sawa. Kwanza kipindi kile cha kuunganisha hakuna mwananchi yeyote aliyeshirikishwa katika kuunganisha nchi hizi hivyo kuna watu especially Zanzibar ambao hawakuridhika na hiyo dhana na kwa mazingira yalivyouwa walikuwa hawaweza kusema kama wafanyavyo sasa. So cha kwanza uwekwe mchakato kama watu wanataka muungano ama la.
Pili ubinafsi ukiangalia kwa undani sana utaona ni kwa jinsi gani zanizibar inainyonya tanganyika maana tanganyika yenyewe ina kila kitu lakini imekaa kimya. Kuna mangapi ambayo wazanzibari walikuwa wanapata lakini watanganyika hawapati umeme, maji etc tena bure hapo kabla! Je huku bara watu wamewahi kupata umeme au maji bure? Acha huduma.
Tatu wanaona kuwa nguvu nyingi iko bara hivyo ili kuizuia hiyo watambulike wenyewe. Mfano mdogo hawa jamaa wa mpira ZFA na TFF nafikiri kila mtu alisikia ZFA inatakwa gawio lake la kutoka FIFA. Hiyo ni baada ya kujaribu kujiunga wakakataliwa kuwa wao si nchi haiwezekani nchi moja iwe na vyama viwili. Wanataka nusu kwa nusu. Je basis yao ni wapi? Maana haiwezekani zanzibar na tanganyika ziwe sawa.

Hivyo mimi kwa upande wangu kama kawaida ya wabara huwa hawarush kwenye maamuzi hivyo tuite kura ya maoni nani anataka muungano na kama unatakiwa then uwe wa aina gani ili kuondoa hivi vijineno vya hapa na pale.
Nawakilisha
Na ni bora ulivyojitokeza ili upate msasa kidogo,tatizo mlilonalo Tanganyika mashuleni hamsomeshwi somo la historia ya Zanzibar na hata mkosomeshwa inakuwa kama mnapigwa burushi tu na meno yanaendelea kuoza.
Hebu tafuteni Zanzibar Empire muone na nyie mlioko pwani mnaweza kujigamba ,kama ni ukiristu au uislamu wote ulipitia Zanzibar ndio ukaenea kwengineko ,jaribuni kuijua Zanzibar kwanza ili mupate muongozo kwa yale mnayoyasema.
Nikipitia mistari yako kwa haraka Zanzibar hawataki Muungano unaoongozwa na mafisadi ,hakuna kiongozi wa CCM asie kuwa fisadi ila wamezidiana mbinu za kujificha.Kiasi ya kwamba huwezi kuwafikiria kabisa ,hivi ni nani aliejua kama Chenge ana mijihela hajui aifanye nini kaiweka benki inazaliana tu.Hivyo ujue wako wengi kama Chenge. weka kando hilo.
Kusema zamani Wazanzibar walikuwa hawawezi kusema kama wasemavyo sasa hilo nataka ulifahamu sio Zanzibar pekee hata Tanganyika kuna visa na mikasa ,na kwa ufupi tawala zote za ulimwenguni wananchi wake walikuwa hawawezi kusema kama wasemavyo leo ,upo ! hilo halina mshiko.
Wewe unaonekana umefukuka maana unaposema Zanzibar wakipata maji bure na umeme bure ,hayo hayakutoka Tanganyika ,tokea zama Zanzibar maji ni bure ,umeme ukilipwa ,mashule bure madaftari kabakaba,balaa la kulipia mashule na kuadimika vifaa anavyohitaji mwanafunzi limezuka kwa utawala wa Tanganyika kujivalisha ndani ya Tanzania na kuikaba koo Zanzibar kupitia udhibiti wa njia za uchumi na serikali ya Zanzibar kushindwa kutimiza malengo yake nakuhakikishia hata umeme ungelifikia kuwa bure ,lakini leo maji yanaanza kulipiwa ,mashule ndio hivyo usiseme umeme bwanamkubwa mara kazima switch,Zanzibar imegandamizwa na haiwezi hata kufurukuta kwa jamaa waTanganyika roho zilivyowabadilika ,kuna jamaa huko bara wanafikiri Zanzibar ni sawa na Ulaya, this is too macha.
Fedha ikiletwa Tanzania inabidi igawiwe 50 / 50 ,,zimeungana nchi mbili na hapo pia napo pana kero ,vipi utaipa Zanzibar fedha kama unaigawia Wilaya ,hapo ndipo Mawaziri wa Tanzania wanaposhindwa kuwajibika ndani ya Serikali ya Muungano uzalendo unawajaa na kumega sehemu kubwa ya msaada kwa ajili ya kwa Tanganyika ,hivyo sivyo kabisa angalau msaada ungewekwa 2/3 tukafahamiana ,na ndio Muungano lakini mnabinya na mwisho au misaada mingine hata Zanzibar haioni ndani inagawiwa juu kwa juu.
 
Pakacha,
Baada ya kuungana na Tanganyika Zanzibar ilipoteza sovereignty yake. Ndio maana kiti chake katika UN kiliangukia chini ya Tanzania. Ndio maana ilipojiunga na OIC kinyemelea ililazimika kujiondoa baada ya jambo hilo kufahamika hadharani. Tatizo liko wapi?
Naona mmeshikilia sovereignty hivi hakuna neno la kiswahili ? Au mnaliepuka maana huenda tafsiri yake ikawagonganisha vichwa.
Zanzibar inakuja zake na itarudi tu,sasa kama nyinyi mmeng'ang'ania kuulinda Muungano endeleeni hivyo hivyo ila msije kukubali nchi yenu kuitwa Tanzania hilo nawaomba mlikatae na kulipinga kwa kila kitu,lakini pia mna hiari zenu kama mtabaki na Tanzania au Tanganyika.
 
Back
Top Bottom