Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 22,732
- 29,988
Umofia kwenu nyote,
Nimefuatilia kwa jicho la uchambuzi nimengundua Kuna kani (nguvu) isiyo ya kawaida inatendakazi kwa namna ya ajabu sana.
Niliwahi kuandika kuwa Mungu ameondoa kauli kwenye midomo ya watawala kuanzia juu hadi ngazi za chini.
Mungu amesikia kilio chq Watanzania. Mungu ameshuka kuona madhila.ya waja wake na hakika anashusha ghadhabu yake kwa chama kinachojimilikisha nchi kwa usadidizi wa kuzimu. Nani asiyefahamu kwamba teuzi za CCM kwa asilimia kubwa zinahusisha nguvu za giza?
Mwenge wa uhuru ni cover tu, bali ni ziara ya kumuadhimisha shetani kwa sababu historia ya mwenge huo imetokana na kikao cha wachawi wanaptumia nguvu za giza.
Chama cha Mapinduzi (CCM) kinaamini kuwa mrundikano wa wanajeshi wetu lwenye nafasi za juu za chama na nafasi mbalimbali za maamuzi ni kinga inayoweza kukiokoa na gharika yeyote ile. Katika kujisshau huko kimekuwa kikiwaaminisha Watanzania kuwa tatizo la kiuongozi, uadilifu na utawala siyo la chama bali ni viongozi binafsi. Hivyo cover ya kubadilisha uongozi ndani ya chama na serikali ni mkakati makini wa Deep State kuhakikisha thinktank ya nchi irubunike na kushiriki karamu ya uporaji wa haki na rasilimali za nchi kwa faida ya wachache waliomo ndani zaidi ya chama.
Pamoja na kuondoa kauli thabiti na za hekima zenye kuonesha uongozi na mamlaka kwenye vinywa vya viongozi wetu, Mungu ameondoa imani ama uaminifu baina ya wamiliki wa chama.
Kiutani utani, chama kinasimamia kampeni ya kuchafuana wenyewe kwa wenyewe. Mkakati huu ulianzia nyakati za awamu ya tatu kuelekea ya nne na awamu zinazofuatia hali inakuwa mbaya zaidi. Makada wanachafuana kwa kutengenezeana kashfa na taarifa za kuudanganya umma. Mfano mzuri tulianza kumnyang'anya uraia Jenerali Ulimwengu, na wengine walioonesha kukosoa uongozi wa juu. Ingawa dhambi ya kumfix aliyekuwa Katibu wake Mkuu Horace Kolimba inaendelea kuitafuna.
Eneo la kuchafuana sasa limekuwa rasmi na timu zinaundwa na kupewa baraka zote na wakuu wa chama kwa minajoli ya kuwafitini wanachama wanaoonekana tishio ndani ya chama. Makundi haya yamepewa majina kadha wa kadha kukingana na nyakati. Tulianza Mtandao, wakaja MATAGA, sasa tunao CHAWA. Haya yote ni mfano wa makundi yanayotumika kushughulikia wanachama wenzao wanaoonekana tishio kwa wanakula nchi kimya kimya.
Wakuu, inawezekana ni jambo dogo mbele ya macho ya watu lakini hii karma ya kujimaliza ya CCM inaenda kukiua chama kabisa. Inawezekana kufikia 2030 tukawa na mfumo mpya na mzuri wa maongozi ya nchi yetu.
Watu kama Lucas mwashambwa , ChoiceVariable , CM 1774858 na wenzao wanaofanya spin mitandaoni ni sehemu ya anguko taradadi. Ikumbukwe Musiba ni alama ya matumizi mabaya ya madaraka ya juu kwa sababu alitoa vitisho na tuhuma nzito nzito tena zenye viashiria vya uhaini lakini hakukemewa kwa sababu alijitapa kuwa anamtetea mkuu wa mhimili.
Kimsingi hakuna anayeweza kuzuia ghadhabu ya Mungu zaidi ya toba ya kweli na ya kumaanisha. Lakini CCM hii inayoamini nguvu za giza haina pa kuponea.
watanzania wenye mapenzi mema na Nchi wasikate tamaa, CCM inaenda kuporomoka kama jiwe ndani ya maji katika nyakati hizi kwa sababu them sucking the blood of the sufferer.
Pascal Mayalla raraa reree Burapaa Erythrocyte Extrovert Mshana Jr Paw Retired kigogo hood Da vincci Bujibuji Simba Nyamaume figganigga
So to say
Nimefuatilia kwa jicho la uchambuzi nimengundua Kuna kani (nguvu) isiyo ya kawaida inatendakazi kwa namna ya ajabu sana.
Niliwahi kuandika kuwa Mungu ameondoa kauli kwenye midomo ya watawala kuanzia juu hadi ngazi za chini.
Mungu amesikia kilio chq Watanzania. Mungu ameshuka kuona madhila.ya waja wake na hakika anashusha ghadhabu yake kwa chama kinachojimilikisha nchi kwa usadidizi wa kuzimu. Nani asiyefahamu kwamba teuzi za CCM kwa asilimia kubwa zinahusisha nguvu za giza?
Mwenge wa uhuru ni cover tu, bali ni ziara ya kumuadhimisha shetani kwa sababu historia ya mwenge huo imetokana na kikao cha wachawi wanaptumia nguvu za giza.
Chama cha Mapinduzi (CCM) kinaamini kuwa mrundikano wa wanajeshi wetu lwenye nafasi za juu za chama na nafasi mbalimbali za maamuzi ni kinga inayoweza kukiokoa na gharika yeyote ile. Katika kujisshau huko kimekuwa kikiwaaminisha Watanzania kuwa tatizo la kiuongozi, uadilifu na utawala siyo la chama bali ni viongozi binafsi. Hivyo cover ya kubadilisha uongozi ndani ya chama na serikali ni mkakati makini wa Deep State kuhakikisha thinktank ya nchi irubunike na kushiriki karamu ya uporaji wa haki na rasilimali za nchi kwa faida ya wachache waliomo ndani zaidi ya chama.
Pamoja na kuondoa kauli thabiti na za hekima zenye kuonesha uongozi na mamlaka kwenye vinywa vya viongozi wetu, Mungu ameondoa imani ama uaminifu baina ya wamiliki wa chama.
Kiutani utani, chama kinasimamia kampeni ya kuchafuana wenyewe kwa wenyewe. Mkakati huu ulianzia nyakati za awamu ya tatu kuelekea ya nne na awamu zinazofuatia hali inakuwa mbaya zaidi. Makada wanachafuana kwa kutengenezeana kashfa na taarifa za kuudanganya umma. Mfano mzuri tulianza kumnyang'anya uraia Jenerali Ulimwengu, na wengine walioonesha kukosoa uongozi wa juu. Ingawa dhambi ya kumfix aliyekuwa Katibu wake Mkuu Horace Kolimba inaendelea kuitafuna.
Eneo la kuchafuana sasa limekuwa rasmi na timu zinaundwa na kupewa baraka zote na wakuu wa chama kwa minajoli ya kuwafitini wanachama wanaoonekana tishio ndani ya chama. Makundi haya yamepewa majina kadha wa kadha kukingana na nyakati. Tulianza Mtandao, wakaja MATAGA, sasa tunao CHAWA. Haya yote ni mfano wa makundi yanayotumika kushughulikia wanachama wenzao wanaoonekana tishio kwa wanakula nchi kimya kimya.
Wakuu, inawezekana ni jambo dogo mbele ya macho ya watu lakini hii karma ya kujimaliza ya CCM inaenda kukiua chama kabisa. Inawezekana kufikia 2030 tukawa na mfumo mpya na mzuri wa maongozi ya nchi yetu.
Watu kama Lucas mwashambwa , ChoiceVariable , CM 1774858 na wenzao wanaofanya spin mitandaoni ni sehemu ya anguko taradadi. Ikumbukwe Musiba ni alama ya matumizi mabaya ya madaraka ya juu kwa sababu alitoa vitisho na tuhuma nzito nzito tena zenye viashiria vya uhaini lakini hakukemewa kwa sababu alijitapa kuwa anamtetea mkuu wa mhimili.
Kimsingi hakuna anayeweza kuzuia ghadhabu ya Mungu zaidi ya toba ya kweli na ya kumaanisha. Lakini CCM hii inayoamini nguvu za giza haina pa kuponea.
watanzania wenye mapenzi mema na Nchi wasikate tamaa, CCM inaenda kuporomoka kama jiwe ndani ya maji katika nyakati hizi kwa sababu them sucking the blood of the sufferer.
Pascal Mayalla raraa reree Burapaa Erythrocyte Extrovert Mshana Jr Paw Retired kigogo hood Da vincci Bujibuji Simba Nyamaume figganigga
So to say