Bando la wiki
JF-Expert Member
- May 23, 2023
- 315
- 888
Kuna wizi mkubwa ulifumbuliwa na report ya CIG, lakini wizi ule haujachukuliwa hatua yoyote.
Kuna wizi mkubwa unaendelea huko mawizarani na kwenye taasisi za umma lakini hakuna mbinyo wowote.
Kuna malipo makubwa (ya kufuru) kwa wastaafu na wake zao, pasipo kuzingatia hali ya uchumi.
Kuna malipo makubwa kwa viongozi na wabunge pasipo kuzingatia hali ya uchumi hili nalo litaleta anguko la ccm.
Kanuni za kiuchumi zinataka Mapato yawe makubwa kuliko Matumizi ili kupata ustawi uliyo bora.
Lakini jambo hilo kwa serikali ya ccm limeshindikana, ambapo kila mtu anajipigia kwa urefu wa kamba yake na hakuna wa kumfanya kitu chochote.
Anguko la CCM litatokea wapi?
1. Wana CCM kwa CCM watauana wenyewe kwa wenyewe ili kujimilikisha ukwasi ulioko serikalini (unapiga madili machafu halafu hakuna wa kukugusa)
2. Kutokana na ugumu wa maisha wanayoyapitia wananchi bila serikali kujali maumivu hayo, ndipo anguko la CCM lingine litatokea hapo.
3. Katiba sio hitaji la CCM ila kufikia 2026, CCM wenyewe ndo watakuwa wanaitaka na kuililia katiba mpya maana watakuwa nyuma ya wakati.
Kuna wizi mkubwa unaendelea huko mawizarani na kwenye taasisi za umma lakini hakuna mbinyo wowote.
Kuna malipo makubwa (ya kufuru) kwa wastaafu na wake zao, pasipo kuzingatia hali ya uchumi.
Kuna malipo makubwa kwa viongozi na wabunge pasipo kuzingatia hali ya uchumi hili nalo litaleta anguko la ccm.
Kanuni za kiuchumi zinataka Mapato yawe makubwa kuliko Matumizi ili kupata ustawi uliyo bora.
Lakini jambo hilo kwa serikali ya ccm limeshindikana, ambapo kila mtu anajipigia kwa urefu wa kamba yake na hakuna wa kumfanya kitu chochote.
Anguko la CCM litatokea wapi?
1. Wana CCM kwa CCM watauana wenyewe kwa wenyewe ili kujimilikisha ukwasi ulioko serikalini (unapiga madili machafu halafu hakuna wa kukugusa)
2. Kutokana na ugumu wa maisha wanayoyapitia wananchi bila serikali kujali maumivu hayo, ndipo anguko la CCM lingine litatokea hapo.
3. Katiba sio hitaji la CCM ila kufikia 2026, CCM wenyewe ndo watakuwa wanaitaka na kuililia katiba mpya maana watakuwa nyuma ya wakati.