Mume mmoja, wake Saba, umejiandaaje na ujio wa SHERIA hiyo ijayo duniani?

Rabbon

JF-Expert Member
Apr 16, 2022
15,099
22,538
Salaam, Shalom!!!

(Isaya 4:1)

NA SIKU HIYO, WANAWAKE SABA WATAMSHIKA MTU MUME MMOJA WAKISEMA, TUTAKULA CHAKULA CHETU, NA KUVAA NGUO ZETU WENYEWE, LAKINI TUITWE TU KWA JINA LAKO, UTUONDOLEE AIBU YETU.

Maneno ya unabii huo yanakwenda kutimia, inakwenda kutungwa SHERIA kabisa kuruhusu wanawake wengi Kuolewa na mwanamume mmoja.

Tangu 2021, Dunia iliingia msimu mpya, yapo mengi sana yanakwenda kubadilika, hivyo kuleta mgawanyiko wa watu katika makundi mawili makubwa,

Kundi moja, litakuwa wanaomcha Mungu, na kundi la pili, kundi la waovu.


KWANINI WAKE SABA MUME MMOJA?

1. Idadi ya wanaume waoaji imepungua na ITAENDELEA kupungua sana. Maisha magumu na misongo ya mawazo inakwenda kupunguza sana wanaume na uzao wa watoto wa kiume.

2. Mifumo ya kidunia inazidi kuwainua wanawake na kiwashusha chini wanaume Ili kuipindua juu chini Dunia iende kinyume na mapenzi ya Mungu. Mungu aliagiza mume mmoja aoe mke mmoja. Mwanaume awe KICHWA, kiongozi, nw MAPINDUZI yameendekea kukua na kumwachia Mwanaume akitaabika.

3. USHOGA, usagaji na vitendo vya kubadili JINSIA,ni mambo ambayo ya akwenda kupunguza sana idadi ya wanaume duniani.

4. Magonjwa, vita na vifo vitapunguza sana idadi ya wanaume duniani na kuwafanya wawe bidhaa adimu.

5. Nchi nyingi walitunga sera za kupanga uzazi ambazo zimeondoa nguvu KAZI Kwa kiasi kikubwa, na tunakoelekea, Africa itastawi sana kiuchumi sababu ya kutofuata sera hizo.

Yote hayo hapo juu, yanakwenda kutimiza unabii huo.

Wanaume, watakosa nguvu ya kiuchumi na kutawaliwa na wanawake, Nchi zilizoendelea, Hadi tunavyoongea Mwanaume tayari ni mtumwa wa mwanamke.


LINI UNABII HUO UTATIMIA?

Kwa kuanza, mwaka huu 2024- 2030, zitatungwa SHERIA za kuruhusu wanawake kuruhusiwa Kuolewa na mwanamume mmoja, na itakuwa SHERIA kabisa.

HITIMISHO.

Imeandikwa, mwovu na azidi kuwa mwovu, na mtakatifu na azidi kujitakasa. Tunaelekea katika nyakati ngumu na za taabu sana ULIMWENGUNI.

Uyaonapo haya Kutokea, jua kuwa Yesu Yu karibu kurudi. Chagua kuwa moto au baridi.

Ikiwa hujaokoka, fuatisha Sala hii;

EE MUNGU KATIKA JINA LA YESU KRISTO, NINAKUKIRI WEWE KUWA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE, NINAOMBA UNISAMEHE, ULIFUTE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKUMU, ULIANDIKE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA UZIMA, NIPE UWEZO WA KUISHI MAISHA MATAKATIFU, DHAMBI ISINISHINDE, UOVU USINISHINDE, NINAOMBA HAYO KUPITIA JINA LA YESU KRISTO ALIYE BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU. AMEN
 
Back
Top Bottom