Mukama awakana akina Nnauye; Hakuna atakayeshughulikiwa ndani ya siku 90!

Kimbunga

Platinum Member
Oct 4, 2007
14,941
9,947
Jamani nimesikiliza taarifa ya Habari ya TBC1 wakimnukuu Katibu Mkuu wa CCM akisema kuwa hakukuwa na maazimio ya kuwatosa mafisadi baada ya siku tisini. Au sikusikia vizuri!! Mbona Nnauye anasema hivyo kila siku na kuwataja majina, amepata wapi hayo sasa? Makubwa
 
Mkuu kimbunga umesikia vyema kabisa,hawa jamaa wanajiuliza ni nani amvishe paka kengele,yaani hawana ubavu wa kufanya wanayotaka jamii iamini
 
Nape Nnauye ambaye ni msemaji wa Chama amesikika akisema Chama kiliamua na kutoa azimio la kuwafukuza mafisadi ndani ya siku tisini!! Anakuja Katibu Mkuu wa Chama ambaye ni Mtendaji Mkuu wa Chama anasema hakukuwa na azimio kama hilo!! Itabidi sasa Mwenyekiti atoe tamko na wakiendelea kutofautiana inabidi warudi white house wajivue gamba kwa mara nyingine tena.

Cha kushangaza ni kwamba mbona Nape Nnauye amekuwa akitamba kwamba mafisadi wanatakiwa waondolewe ndani ya chama kwa muda mrefu lakini hakuna kiongozi aliyejitosa kumnyamazisha? Imekuwa baada ya takribani mwezi mzima sasa ndio katibu mkuu anajitokeza na kumkana Nape? Kuna nini hapa?
 
Nadhani akina Nnauye wanapotoka.

Kuwasingizia akina EL, RA, EC, kwamba wao ndio walisababisha CCM kupata ushindi kidogo siyo sawa, kwa sababu katika majimbo yote matatu CCM kwa ngazi zote ilishinda kwa zaidi ya asilimia 80, labda wangetafuta sababu nyingine kama ya ufisadi, hata hiyo kisheria lazima uwe na ushahidi vinginevyo inakuwa ni defarmation ambapo mtu anaweza akadai remedies.
 
Lakini mbona 'mzee wa kaya' alimtetea Nape kwamba anayosema ndio maamuzi ya chama.... sasa nimeamini hiki chama kinaelekea kufa!!!:evil:
 
Hawa wapo kwenye ile hali kwa kiingereza inaitwa ' What you do when you cannot do anything'! yaani bonge la confusion. Muda si muda utasikia Nape kamgeukia Mukama! Cinema inaendelea
 
Si waliamua kumtoa mzee wetu Makamba , watakoma sasa maana kila mmoja na lake kwani tumeshawasomea hawa .....
 
Wanakwepesha movie hawa, tulitaka kuona baada ya hizo siku 90 wangefanya nini!. Natamani Mukama awe amekosea ili wachukuwe hatua baada ya hizo siku, yaani movie itakuwa tamu kweli kweli. Du, wanataka kuikwepesha!.
 
Haaa!!! haaa!!!! haaaaaa, CCM bana!!!

Willisoni hiyo ripoti ya kuokotwa mitaani wala haikua Scientific Research, itupe mbali sana kwa kuwa itakisambaratisha CCM kwa haraka zaidi kuliko wengine tunavyotarajia leo hii.


CCM imara zaidi ya KANU ya Kenya ndani ya kambi ya upinzani ni muhimu sana kwa utawala murua kwa CHADEMA na wananchi kwa ujumla tangu hapo 2015.


Masikini CCM, mlivyoingia kiulaini ndani ya huu mtego ya OPERESHENI VUA GAMBA!!! Katika hili mnalooo; nyuma hakurudiki na wala mbele hakuendeki katika vita vyenu dhidi ya UFISADI nchini.

Nasema CCM mnaloooo mwaka huu sijui sasa wananchi tutaelezwa kiswahili gani baada ya siku 90 za kujivua gamba???????????


Jamani nimesikiliza taarifa ya Habari ya TBC1 wakimnukuu Katibu Mkuu wa CCM akisema kuwa hakukuwa na maazimio ya kuwatosa mafisadi baada ya siku tisini. Au sikusikia vizuri!! Mbona Nnauye anasema hivyo kila siku na kuwataja majina, amepata wapi hayo sasa? Makubwa
 
Wanakwepesha movie hawa, tulitaka kuona baada ya hizo siku 90 wangefanya nini!. Natamani Mukama awe amekosea ili wachukuwe hatua baada ya hizo siku, yaani movie itakuwa tamu kweli kweli. Du, wanataka kuikwepesha!.

Kweli CCM imechanganyikiwa, inakuwaje watu wazima wanaoisimamia serikali wanapingana kila kukicha tena hadharani? Naanza kuamini kuwa CCM sasa iko harijojo!! Wamekuja kwa mbwembwe kubwa kwamba wamejivua gamba kumbe hakuna gamba lolote ambalo wamevua!
 
Haaa!!! haaa!!!! haaaaaa, CCM bana!!!

Willisoni hiyo ripoti ya kuokotwa mitaani wala haikua Scientific Research, itupe mbali sana kwa kuwa itakisambaratisha CCM kwa haraka zaidi kuliko wengine tunavyotarajia leo hii.


CCM imara zaidi ya KANU ya Kenya ndani ya kambi ya upinzani ni muhimu sana kwa utawala murua kwa CHADEMA na wananchi kwa ujumla tangu hapo 2015.


Masikini CCM, mlivyoingia kiulaini ndani ya huu mtego ya OPERESHENI VUA GAMBA!!! Katika hili mnalooo; nyuma hakurudiki na wala mbele hakuendeki katika vita vyenu dhidi ya UFISADI nchini.

Nasema CCM mnaloooo mwaka huu sijui sasa wananchi tutaelezwa kiswahili gani baada ya siku 90 za kujivua gamba???????????
Hapo sasa!
Wasitake kukwepesha, na mbwembwe zote za kuzunguka mikoani leo wanataka kukwepa!.
 
Nape Nnauye ambaye ni msemaji wa Chama amesikika akisema Chama kiliamua na kutoa azimio la kuwafukuza mafisadi ndani ya siku tisini!! Anakuja Katibu Mkuu wa Chama ambaye ni Mtendaji Mkuu wa Chama anasema hakukuwa na azimio kama hilo!! Itabidi sasa Mwenyekiti atoe tamko na wakiendelea kutofautiana inabidi warudi white house wajivue gamba kwa mara nyingine tena.

Cha kushangaza ni kwamba mbona Nape Nnauye amekuwa akitamba kwamba mafisadi wanatakiwa waondolewe ndani ya chama kwa muda mrefu lakini hakuna kiongozi aliyejitosa kumnyamazisha? Imekuwa baada ya takribani mwezi mzima sasa ndio katibu mkuu anajitokeza na kumkana Nape? Kuna nini hapa?
Huu wote ni usanii wa CCM hakuna lolote hayo maneno ya akina Nnauye, Mukama JK na CCM kujivua gamba na kuwatosa mafisadi-ingawa wao wenyewe ndio mafisadi -Ni mbinu zao za kutupa turufu na kupima upepo unavyokwenda au kupunguza pressure ya wananchi.

Wanabadiri kauli zao kutokana na hali ya upepo ni mbinu zao za kuvuta muda kwa mategemeo ya kua wananchi watasahau,tusije tukashangaa kuambiwa hata kikao cha kujadili kujivua gamba hakikufanyika"ulikua mkutano wa kawaida wa kuabadil viongozi!" HADAGANYIKI MTU WANANCHI WAMEISHA TAMBUA USANII WENU.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Nakumbuka kama Mwanakijiji alisema haya.

Operation Chaos: Lowassa, Chenge, Rostam et al; Don't Quit CCM!
So far there is no evidence whatsoever put forth by the ruling party that you are the most corrupt members of the part. No one has accused you publicly or has even claimed that there is enough evidence to warrant your removal from the party. At least the Mwakyembe's report had some resemblance of credible allegations especially againt EL and RA but not this so called "skin shedding".

For this reason, I believe you will do your part and your supporters a huge favor and justice by not resigning from any party position and as a matter of fact any measure that will be taken against you should be met with a forceful and precise response.

They have failed to even name you in their public report of the party, they failed to level any credible allegation beside saying "these people have been named by a number of citizen and media that they are involved in corruption".

If you agree to resign you will infact prove without any doubt that you are the most corrupt CCM members ever! By resigning or quitting the party the allegations that have been on your tails for sometimes now will need no further proof. You will go down in history as the most corrupt public officials ever to have hold power.

Are you? Well CCM believes that you are to warrant the resignation of both the Central Committee and the Secretariat. If you resign or quit within the 90 days the answer will be in the affirmative.

I know for sure one thing after 90 days CCM will not do anything against you and still remain credible. They can't fire you, they can't just take your party membership without due quasi judicial course within the part as outlined in the CCM's own constitution or the Principles of Ethics guideline.

So.. stay put, enjoy your position, work like ever before and don't mind the new CCM leadership. They can't do a damn thing.
 
Jamani tusiwalaumu CCM. Walichofanya ni kupima upepo kwamba tukivunja CC na kuwafukuza mapacha wananchi wangeitikiaje? Walipoaona kuwa hata wakiwatosa mapacha wananchi bado hawaonyeshi imani kwa CCM wakaona wasije wakauana bure kumbe hawawezi kukiokoa chama chao. Kwa hiyo CCM sasa hivi wanaishi tu kwa matumaini huku wakisubiri CDM wavurugike kwa mikakati na maintelijensia zao walizoweka zizae matunda. Na wanapotegemea CDM ivurugike matumaini yao ni kama yale ya fisi kumfuata mwanadamu kwa nyuma akidhani kuwa mkono wake utadondoka
 
Back
Top Bottom