Elitwege
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 5,154
- 10,809
Nimesoma katika Mitandao mbalimbali za Kijamii pamoja na vyombo vya habari kuhusiana maoni ya Mbunge wa Mtama na aliyekuwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa Idara ya itikadi na Uenezi katika serikali ya Awamu ya Nne chini ya Mh. Jakaya Mrisho Kikwete Komred Nape Moses Nnauye kuomba kufanyiwa Auditing mikopo iliyochukuliwa na serikali ya CCM ya awamu ya Tano chini Mh Hayati Dr. John Pombe Joseph Magufuli, mimi kama mwanachama wa Chama Cha Mapinduzi kundi la Watumwa nakubaliana na hoja ya Ndugu Nape Nnauye.
Mimi ni Mjasiriamali najua changamoto ya vyombo vya Fedha kutoa mikopo ya maendeleo.
Iliwezekanaje Awamu ya Tano katika kipindi cha miaka mitano tu wakapewa mikopo ya Dola za Kimarekani Bilioni tisa wakati serikali ya akina Nape ya awamu ya Nne iliwachukua miaka Kumi kupata mikopo ya dola bilioni saba tu? Hapa inahitajika Auditing kujua mbinu waliyotumia aliyekuwa Waziri wa Fedha na Mipango Dr. Philip Mpango na Rais wake Hayati Dr. John Pombe Joseph Magufuli.
Serikali ya Hayati Magufuli iliyotajwa kuwa haipendwi na wakubwa wa Dunia, Hayati Magufuli anatajwa kuwa aliharibu Mahusiano na Mataifa makubwa yenye Ukwasi wa Fedha aliwezaje kupewa dola bilioni tisa ndani ya miaka mitano na watu aliyoharibu nayo mahusiano wakati serikali yao pendwa ya awamu ya Nne ambayo ilikuwa na Mahusiano mazuri na wakubwa mpaka katuletea Rais wa America Barack Obama kuja kucheza Mpira kwenye mitambo wa Umeme Ubungo hawa walipewa usd $7bilioni tu kwa miaka Kumi?
Nasema naunga mkono hoja ya Nape kwasababu mdogo wangu labda hakuwepo bungeni wakati Bajeti ya serikali inawasilishwa na aliyekuwa Waziri wa Fedha na mipango Dr. Philip Mpango kwa kipindi chote cha miaka mitano ndiyo maana anasema mikopo ya awamu ya tano haikuwa ya wazi na wala hajui mikopo hiyo ilitoka wapi na pesa zilifanya kazi gani?
Comred Nape anasema Bilioni tisa za awamu ya tano hajui zilitumikaje au pesa iliyokopwa ni nyingi kuliko miradi inayotajwa.
Nataka nimpe mahesabu tu kidogo ya darasa la saba niliyofundishwa na Mwalimu wangu Hisabati Mr. Obondo aliyenifundisha Darasa la Saba pale Kongo Primary School wilayani Rorya na wengine mkifahamu mtaniongezea kwasababu mimi mahesabu yangu ni Darasa la Saba pale kijijni kwetu Buganjo Rorya.
Tunafahamu kuwa Rufiji hydropower au Bwawa la Umeme la Mwalimu Julius Kambarage Nyerere imechukua Usd $3billion, SGR toka Dar-Morogoro- Makutopora Dodoma imechukua Usd $3Bilioni SGR toka Mwanza- Isaka Usd $500 milioni kuna Ujenzi wa Msalato Airport Usd $200milioni ukarabati wa Bandari ya Dar na Mtwara ni kama USd $400milioni.
Mimi kwa mahesabu yangu nimepata dola za Kimarekani $7.1Bilioni.
Hapa nimeacha Ujenzi wa madaraja yote kuanzia Tanzanite Dar, Kijazi Flyover, Daraja la Busisi Ujenzi wa Barabara zote hapa nchini ambapo karibu kila Jiji na Manispaa mpaka kwa watani zangu Waha Kigoma, watani zangu Wanyaturu Singida, watani zangu Wahaya Bukoba siku hizi kuna taa za barabarani mijini haya mambo yalikuwa kwetu Mara pale Jiji la Musoma, Barabara kama Kimara Kibaha njia nane, Mwendokasi Mbagala, ukarabati wa Reli ya kati kutoka Dar- Mwaza, Tabora- Kigoma -Mpanda, Ruvu-Arusha, Ukarabati wa viwanja vya ndege zote nchini ikiwepo Ujenzi wa kiwanja cha Chato. Ujenzi wa Rada katika viwanja vinne KIA, Songwe, Mwanza na Dar.
Tuseme yote hayo mikopo yake yalichukuliwa kwenye serikali ya Akina Nape ya awamu ya Nne iliyokopa Usd $7bilioni kwa miaka Kumi.
Nimeacha elimu bila malipo, nimeacha vituo vya Afya 400 nchi nzima zenye hadhi ya hospital za wilaya, nimeacha hospital za wilaya 60, nimeacha Ujenzi wa meli na vivuko, nimeacha ununuzi wa ndege 11, nimeacha Ujenzi wa hospital Nne za Kanda nimeacha vifaa tiba katika hospitali zetu, nimeacha Usambazaji Umeme vijiji 5000 kwa kipindi cha miaka mitano tu wakati katika kipindi cha miaka 20 ya awamu ya Tatu ya Hayati Benjamin Mkapa na awamu pendwa ya Nne ya Jakaya Kikwete walisambaza umeme vijiji 2000 tu pamoja na kupewa msaada wa REA kutoka serikali ya America, nimeacha ununuzi wa vifaa vya Ulinzi na Usalama hapa nchini, nimeacha Ujenzi wa Masoko na stand za Kisasa za Mabasi zilizosambaa nchi nzima nakadhalika nakadhalika.
Ndugu zetu waliyokuwa serikali ya awamu ya Nne naona Wamejipanga kuwachafua viongozi wa awamu ya Tano na hasa mlengwa ni Jemadari wetu Hayati Dr.John Pombe Joseph Magufuli na hasa lile kundi lililopitiwa na panga la Hayati Magufuli aidha kwenye Baraza la Mawaziri, Ubunge, watendaji serikalini au maslahi yao mengine kama Biashara, Mihadharati na fedha walizokuwa wanachotaka kutoka serikalini.
Juzi wamemnunua mwanahabari na mmiliki wa Gazeti moja la Kila wiki kumchafua Hayati Magufuli kuwa katika serikali ya awamu ya tano alikopa Tsh 78tirilioni na Leo nimesoma mahala fulani kuwa Hayati Magufuli pekee alikopa shilingi 51Tirilioni Japo Nape anasema Hayati Magufuli alikopa $9billion na deni la Taifa ni Shilingi 64Tirilioni.
Utadhani Hayati Magufuli ndiye aliyekuwa anaenda kufanya Negotiations ya mikopo huko Nje wanasahu aliyekuwa Waziri wa Fedha na Mipango ambaye ndiye Makamu wa Rais JMT wa Sasa ndiyo mhusika mkuu wa mikopo na mipango ya matumizi ya mikopo hiyo.
Nape alitaka aliyekuwa Rais Mh.Magufuli angetoka hadharani kuonyesha fedha za mikopo zilitoka wapi na zilifanyaje kazi kama walivyoandaa sherehe juzi kusherekea mikopo kutoka IMF, ina maana Mh Nape hakuona viongozi wa serika na AfDB, WB, IMF, Standard Charter Bank wakishiriki Utiaji sahini mikataba mbalimbali iliyofanywa hadharani huku zikishuhudiwa na Mh Rais hayati Magufuli au hata bungeni hakushiriki kupitisha Bajeti ya Serikali?
Tumuache Hayati Magufuli apumzike kwa Amani kama ni nchi kawachia mtafune tu Kiroho safi kabisa chokochoko za nini?
Inawezekana mkidhani mnamtukana hayati Magufuli ambaye kimsingi amelala Usingizi asikii hata hayo matusi huku mkisahu aliyekuwa Makamu wa Rais wa Awamu ya Tano Mh Samiah Suluhu Hassan ndiye Rais kwasasa ambaye mnajipendekeza kwake Aliyekuwa Waziri wa Fedha na Mipango Dr. Philip Mpango ndiye Makamu wa Rais wa sasa mnayejipendekeza Waziri Mkuu ni yuleyule Mwalimu Kasimu Majaliwa Majaliwa kwahiyo mnapozodoa awamu ya tano mtarajie na wao mnawazodoa mnaposema pesa ilitumika vibaya ni haohao ndiyo walikuwa wasimamizi wakuu katika serikali ya awamu ya Tano.
Pumzika kwa Amani Mzee wetu Dr.John Pombe Joseph Magufuli sisi wanachama wenzio wanyonge ndani ya CCM tuko tayari kwa mapambano ya aina yoyote kulinda Legacy yako bila Uoga wala aibu.
Kidumu Chama Cha Mapinduzi.
Ni mimi mwanachama wa CCM kundi la watumwa.
Frey Cosseny nikiwa Msanga Kisarawe Pwani.
Mimi ni Mjasiriamali najua changamoto ya vyombo vya Fedha kutoa mikopo ya maendeleo.
Iliwezekanaje Awamu ya Tano katika kipindi cha miaka mitano tu wakapewa mikopo ya Dola za Kimarekani Bilioni tisa wakati serikali ya akina Nape ya awamu ya Nne iliwachukua miaka Kumi kupata mikopo ya dola bilioni saba tu? Hapa inahitajika Auditing kujua mbinu waliyotumia aliyekuwa Waziri wa Fedha na Mipango Dr. Philip Mpango na Rais wake Hayati Dr. John Pombe Joseph Magufuli.
Serikali ya Hayati Magufuli iliyotajwa kuwa haipendwi na wakubwa wa Dunia, Hayati Magufuli anatajwa kuwa aliharibu Mahusiano na Mataifa makubwa yenye Ukwasi wa Fedha aliwezaje kupewa dola bilioni tisa ndani ya miaka mitano na watu aliyoharibu nayo mahusiano wakati serikali yao pendwa ya awamu ya Nne ambayo ilikuwa na Mahusiano mazuri na wakubwa mpaka katuletea Rais wa America Barack Obama kuja kucheza Mpira kwenye mitambo wa Umeme Ubungo hawa walipewa usd $7bilioni tu kwa miaka Kumi?
Nasema naunga mkono hoja ya Nape kwasababu mdogo wangu labda hakuwepo bungeni wakati Bajeti ya serikali inawasilishwa na aliyekuwa Waziri wa Fedha na mipango Dr. Philip Mpango kwa kipindi chote cha miaka mitano ndiyo maana anasema mikopo ya awamu ya tano haikuwa ya wazi na wala hajui mikopo hiyo ilitoka wapi na pesa zilifanya kazi gani?
Comred Nape anasema Bilioni tisa za awamu ya tano hajui zilitumikaje au pesa iliyokopwa ni nyingi kuliko miradi inayotajwa.
Nataka nimpe mahesabu tu kidogo ya darasa la saba niliyofundishwa na Mwalimu wangu Hisabati Mr. Obondo aliyenifundisha Darasa la Saba pale Kongo Primary School wilayani Rorya na wengine mkifahamu mtaniongezea kwasababu mimi mahesabu yangu ni Darasa la Saba pale kijijni kwetu Buganjo Rorya.
Tunafahamu kuwa Rufiji hydropower au Bwawa la Umeme la Mwalimu Julius Kambarage Nyerere imechukua Usd $3billion, SGR toka Dar-Morogoro- Makutopora Dodoma imechukua Usd $3Bilioni SGR toka Mwanza- Isaka Usd $500 milioni kuna Ujenzi wa Msalato Airport Usd $200milioni ukarabati wa Bandari ya Dar na Mtwara ni kama USd $400milioni.
Mimi kwa mahesabu yangu nimepata dola za Kimarekani $7.1Bilioni.
Hapa nimeacha Ujenzi wa madaraja yote kuanzia Tanzanite Dar, Kijazi Flyover, Daraja la Busisi Ujenzi wa Barabara zote hapa nchini ambapo karibu kila Jiji na Manispaa mpaka kwa watani zangu Waha Kigoma, watani zangu Wanyaturu Singida, watani zangu Wahaya Bukoba siku hizi kuna taa za barabarani mijini haya mambo yalikuwa kwetu Mara pale Jiji la Musoma, Barabara kama Kimara Kibaha njia nane, Mwendokasi Mbagala, ukarabati wa Reli ya kati kutoka Dar- Mwaza, Tabora- Kigoma -Mpanda, Ruvu-Arusha, Ukarabati wa viwanja vya ndege zote nchini ikiwepo Ujenzi wa kiwanja cha Chato. Ujenzi wa Rada katika viwanja vinne KIA, Songwe, Mwanza na Dar.
Tuseme yote hayo mikopo yake yalichukuliwa kwenye serikali ya Akina Nape ya awamu ya Nne iliyokopa Usd $7bilioni kwa miaka Kumi.
Nimeacha elimu bila malipo, nimeacha vituo vya Afya 400 nchi nzima zenye hadhi ya hospital za wilaya, nimeacha hospital za wilaya 60, nimeacha Ujenzi wa meli na vivuko, nimeacha ununuzi wa ndege 11, nimeacha Ujenzi wa hospital Nne za Kanda nimeacha vifaa tiba katika hospitali zetu, nimeacha Usambazaji Umeme vijiji 5000 kwa kipindi cha miaka mitano tu wakati katika kipindi cha miaka 20 ya awamu ya Tatu ya Hayati Benjamin Mkapa na awamu pendwa ya Nne ya Jakaya Kikwete walisambaza umeme vijiji 2000 tu pamoja na kupewa msaada wa REA kutoka serikali ya America, nimeacha ununuzi wa vifaa vya Ulinzi na Usalama hapa nchini, nimeacha Ujenzi wa Masoko na stand za Kisasa za Mabasi zilizosambaa nchi nzima nakadhalika nakadhalika.
Ndugu zetu waliyokuwa serikali ya awamu ya Nne naona Wamejipanga kuwachafua viongozi wa awamu ya Tano na hasa mlengwa ni Jemadari wetu Hayati Dr.John Pombe Joseph Magufuli na hasa lile kundi lililopitiwa na panga la Hayati Magufuli aidha kwenye Baraza la Mawaziri, Ubunge, watendaji serikalini au maslahi yao mengine kama Biashara, Mihadharati na fedha walizokuwa wanachotaka kutoka serikalini.
Juzi wamemnunua mwanahabari na mmiliki wa Gazeti moja la Kila wiki kumchafua Hayati Magufuli kuwa katika serikali ya awamu ya tano alikopa Tsh 78tirilioni na Leo nimesoma mahala fulani kuwa Hayati Magufuli pekee alikopa shilingi 51Tirilioni Japo Nape anasema Hayati Magufuli alikopa $9billion na deni la Taifa ni Shilingi 64Tirilioni.
Utadhani Hayati Magufuli ndiye aliyekuwa anaenda kufanya Negotiations ya mikopo huko Nje wanasahu aliyekuwa Waziri wa Fedha na Mipango ambaye ndiye Makamu wa Rais JMT wa Sasa ndiyo mhusika mkuu wa mikopo na mipango ya matumizi ya mikopo hiyo.
Nape alitaka aliyekuwa Rais Mh.Magufuli angetoka hadharani kuonyesha fedha za mikopo zilitoka wapi na zilifanyaje kazi kama walivyoandaa sherehe juzi kusherekea mikopo kutoka IMF, ina maana Mh Nape hakuona viongozi wa serika na AfDB, WB, IMF, Standard Charter Bank wakishiriki Utiaji sahini mikataba mbalimbali iliyofanywa hadharani huku zikishuhudiwa na Mh Rais hayati Magufuli au hata bungeni hakushiriki kupitisha Bajeti ya Serikali?
Tumuache Hayati Magufuli apumzike kwa Amani kama ni nchi kawachia mtafune tu Kiroho safi kabisa chokochoko za nini?
Inawezekana mkidhani mnamtukana hayati Magufuli ambaye kimsingi amelala Usingizi asikii hata hayo matusi huku mkisahu aliyekuwa Makamu wa Rais wa Awamu ya Tano Mh Samiah Suluhu Hassan ndiye Rais kwasasa ambaye mnajipendekeza kwake Aliyekuwa Waziri wa Fedha na Mipango Dr. Philip Mpango ndiye Makamu wa Rais wa sasa mnayejipendekeza Waziri Mkuu ni yuleyule Mwalimu Kasimu Majaliwa Majaliwa kwahiyo mnapozodoa awamu ya tano mtarajie na wao mnawazodoa mnaposema pesa ilitumika vibaya ni haohao ndiyo walikuwa wasimamizi wakuu katika serikali ya awamu ya Tano.
Pumzika kwa Amani Mzee wetu Dr.John Pombe Joseph Magufuli sisi wanachama wenzio wanyonge ndani ya CCM tuko tayari kwa mapambano ya aina yoyote kulinda Legacy yako bila Uoga wala aibu.
Kidumu Chama Cha Mapinduzi.
Ni mimi mwanachama wa CCM kundi la watumwa.
Frey Cosseny nikiwa Msanga Kisarawe Pwani.