Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
Ni sehemu ya ibaada
Tupatie kamstari toka kwenye Quran kwa msaada tafadhali.
Ni sehemu ya ibaada
wewe mkristo inakuhusu nini?
Unajuaje walichokosa kwenye mahakama mama?
wapeni haki zao what is the issue here?
Sidhani kuwa kauli ya Sheikh Mkuu (Muft) inaashiria nia ya kutoipigia CCM kura. Nadhania anachotaka kukifanya ni kuonyesha hasira zake kuwa muda unakwisha na hakuna jitihada za wazi za kutekeleza ahadi anayodhani walipewa kuhusu kuanzishwa kwa Kadhi Mkuu.Wajameni.... Sintojiingiza kwenye uchambuzi wa kidini, siwezi na sina upeo
Swali ni moja tu, JE WASIPOWAPA CCM WATAWAPA NANI WENGINE? CUF? CHADEMA? TADEA?
...i think its just a move to score some points kwa waumini wake now that anajongelea upinzani wa kiti chake
Mwanakijiji wacha hiyo,maana wakijihusisha mtakuja na rangi nyengine hapa ,hawa ni wananchi walioipigia kura CCM na waliipigia kwa kuahidiwa kupatiwa dai hilo wanalolidai ni sawa sawa kabisa na mwanaCCM alieahidiwa kujengewa hospitali,daraja,njia ya lami na mambo kabakaba yakiwemo maisha bora sasa ni wakati wa wale wote walioahidiwa na hadi leo hawajapelekewa hata kokoto au matofali kuanza kubadili muelekeo kama hao Waislamu walioipigia kura CCM hivyo kuanza safari ya kuipeleka CCM kaburini. Hao waislamu walioipigia kura CCM wameanza kuonyesha njia sasa huko kwenye wakiristu walioipigia kura CCM na madai yao hayakutekelezwa nao wapige mbiu ya mgambu ile kufanikisha maziko.
Mambo ya utajiri hayawashughulishi wanaCCM hayo ni ya vyama vya upinzani au hulielewi hilo ? Ila inaonyesha viongozi wa CCM wamewadanganya wenzao waliomo kwenye mrengo wa uislamu, hivyo wanajitayarisha kutoa pigo kwa viongozi wao,sasa tatizo upande wetu wapinzani lipo wapi, hivi ukisikia vita vya panzi furaha ya kunguru unakuwa hufahamu maana ?
Hao sidhani wanazungumza na wanachama wa Chadema CUF au vyama vingine vya kambi ya upinzani ,si waislamu wote waliipigia kura CCM,bali wanazungumza na wanachama wa CCM ambao ni Waislamu kubadili muelekeo wa kuhamisha kura zao na kuzipeleka wanakoona madai yao yatatekelezwa ,hivyo Chama chochote kile kinaweza kuchukua dai hilo na kusema kuwa endapo wao watapewa kura hizo watalitekeleza dai hilo,sioni tatizo la kidini hapa.
Ila ngoma ni nzito sana ukiangalia jamaa alivyopiga mahesabu tokea kudai uhuru.Inaonyesha uvumilivu umeanza kugonga ukomo.
Masikini CCM inakufa polepole kama muasisi wake Nyerere.
CCM itashinda kwa kishindo kikuu.
Haa haa haaa!! Kwamba serikali itumie busara kwa kuwa waislamu huwa na hasira na jazba za haraka!!! Sasa kwa nini waislamu nao wasiwe na busara kama serikali inavyotakiwa iwe?...
Kimsingi mahakama ya kadhi ni sticky issue na serikali isipotumia busara nafahamu waislamu ni watu huwa na hasira na jazba za haraka.
Kama ilivyo kwa wakatoliki period!!Waislamu hawajakatazwa kuwa na mahakama zao kwa ajili yao, ila wakitaka wazianzishe kwa utaratibu wao ndani ya misikiti yao kwa ajili yao na kwa gharama zao wenyewe, sio kuchangiwa na wananchi wote.
Wasilazimishe mahakama za kiislamu zianzishwe na Serikali ili zilipiwe kodi na watu wote (waislamu, Wakristo na wasio na dini), na ili ziajiri waislamu tu.
Wenzetu hawa huwa wanaweka kando mabaya yote wakishupalia dini, ndiyo maana ukiwaambia mbona hamsemi mtaikacha CCM kwa ajili ya EPA, RICHMOND/DOWANS, DEEP GREEN, TANGOLD, MWANANCHI GOLD, MEREMETA, IPTL, KIWIRA wanabaki mhhh...
Anyway, wakiiacha CCM itakuwa poa tu, watarudi kwao CUF...
Hiyo ahadi haikuwa absolute, ila ccm ilikuwa inaangalia uwezekano wa kuanzisha mahakama ya kadhi!
Hoja ya msingi ni kwamba Waislamu wamekosa demokrasia ndani ya taasisi zao kwa kile tunaita kimombo co-option of few islamic leaders by Government.Taasisi za kikristu kama vile Tanzania Episcopol Council na nyinginezo huwa haziingiliwi na serikali, lakini inapokuja swala zima la uchaguzi ndani ya taasisi za kiislam, serikali ina ingilia(influence) na ndio maana Wapo wanao mkubal sheikh Mkuu na wasiomkubali ndani ya sheikh mkuu. Kwa hiyo hoja ya msingi nikuangalia demokrasia ndani ya taasis za kiislam. Kwa mfano ndani ya kanisa la lutherani (KKT) kumekuwa kunafukuta sehemu mbali mbali kama vile upareni, meru n.k, sababu kubwa utafiti ulibainisha kuwa ni mgawanyo wa rasilimali. Fukuto kubwa ndani ya uisilamu husababishwa na ukosefu wa demokrasia ndani ya taasisi hizo because for some reasons the government does not want the muslims to collectivelly pick the leadership they want. Kwa hiyo hili swala ni lazima litizamwe upya ili lipatiwe ufumbuzi. Wakati civil war inaanza watu huwa hawatangazi ila ilalipuka tu. utasikia tu , fujo mwembe chai, fujo za kkt upareni, vijana wakiislamu wakizuia wazee kuingia misikitini, wakulima wakichinjana na wafugaji, chuo kikuu hakukaliki n.k.