Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Keil

JF-Expert Member
Jul 2, 2007
2,214
803
Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Na Ummy Muya

BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) limesema kutokana na serikali kutupilia mbali ombi la kunzisha Mahakama ya Kadhi, Waislamu hawataipigia kura CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.

Katika taarifa yake, Bakwata ilifikia hatua ya kusema Waislamu wasimchague Rais Jakaya Kikwete iwapo atasimamishwa na CCM kugombea urais, ikiwa ni pamoja na wabunge na madiwani watakaosimamishwa na chama hicho tawala kutokana na kitendo cha serikali kutupilia mbali hoja ya Mahakama ya Kadhi.

Kauli hiyo imetolewa jana wakati Mufti Issa bin Shaaban Simba alipokuwa akitoa tamko kupinga uamuzi wa serikali kutaka kutumia sheria za dini ya Kiislamu katika mahakama za kawaida badala ya kuanzisha Mahakama ya Kadhi, kitu ambacho alisema anaamini kitawanyima haki Waislamu.

Alisema serikali imedhihirisha kuwa inaendeshwa na Wakristo na si kweli kama serikali haina dini na akamtaka Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe kubatilisha kauli hiyo kwa kuwa inamchafua Rais Jakaya Kikwete mbele ya umma wa Waislamu.

Waziri ametuthibitishia kama Rais Kikwete alikuwa akitulaghai ili tumpigie kura kwa kigezo kuwa suala hilo litashughulikiwa na kupatiwa ufumbuzi na sio kuchanganywa kama ilivyokuwa mwaka 1970 katika Sheria ya Ndoa na kuwanyima haki Waislamu,alisema.

Alisema kwa muda mrefu sana Waislamu wamekuwa kimya wakitumia hekima na busara kudai haki zao, lakini katika hatua hii ambayo serikali imefikia hawapo tayari kuendelea kudhalilishwa na kuwa kitendo hicho ni dhalimu.

Mufti alisema wamekuwa wakiiomba Mahakama ya Kadhi kwa zaidi ya miaka 20 na hivyo hawezi kuendelea kuwa kimya na kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa kwa kuwa mahakama hiyo ni haki yao.

Alisema kauli ya Waziri Chikawe imedhihirisha kuwa serikali ina wenyewe na Waislamu wamewekwa katika tabaka la pili pamoja na Rais Jakaya Kikwete kuwatuliza kwa ahadi kuwa watalipatia ufumbuzi suala hilo.

Natoa wito kwa Masheikh wote nchini na Waislamu wa madhehebu yote kupinga vikali kauli iliyotolewa na Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe na kwamba Waislamu waige mfano wa Waislamu wa Afrika Kusini,alisema Mufti na kuhoji:

Kwa nini iwe Afrika ya Kusini na isiwe Zanzibar, Uganda na Kenya ambazo zipo ndani ya Afrika Mashariki? Kwa niaba ya Waislamu nasema serikali haikututendea haki na imetuchukiza sana,alisema.

Alisema lengo la kuomba mahakama hiyo ni kuhakikisha Waislamu wanashughulikia masuala yao ya ndoa na mirathi na si vinginevyo, hivyo waziri asipotoshe jamii kwa kutumia mifano ambayo haiko sahihi.

Mahakama hii haitawakata wezi mikono kwa kuwa nchi hii ina katiba na sheria na sisi tutazirudisha kesi zote za jinai mikononi mwa serikali. Sifahamu hiyo kamati ambayo waziri alisema alikuwa amekaa na kutoa tamko hilo ilikuwa na watu gani,alihoji.
Aliongeza kuwa kutokana na mapungufu hayo waziri arudi tena na kukutana na masheikh ili apate muongozo wa nini Waislamu wanahitaji na sio kuzungumza bila kuwa na usahihi wa kile anachosema.

Wakizungumza na waandishi wa habari baada ya tamko la Bakwata, masheikh walikuwa na mitazamo tofauti. Sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Salum Mussa alisema wapo baadhi ya Waislamu ambao watakubali kutokana na ufinyu wao wa elimu ya dini.
Mussa alisema haoni sababu ya serikali kufanya njia ya mkato katika suala hilo kwani Waislamu wanahitaji Mahakama ya Kadhi kama ilivyo kwa wafanyabiashara ambao wana mahakama yao.

Hukumu inayotolewa katika Mahakama ya Kadhi ni ibada kwa mujibu wa mafundisho ya Mtume Muhammad (S.A.W) hivyo ni lazima kwa atakayetoa hukumu hiyo awe Muislamu na si vinginevyo,alisema.

Namshanga waziri anapotaka sheria hizi zitumiwe katika mahakama za kawaida. Aliona wapi John akawa imamu,alihoji sheikh huyo wa mkoa wa Dar es Salaam.

Naye katibu wa Bakwata wilayani Ilala, Sheikh Issa Ausi alisema historia iko wazi. Waasisi na wanaharakati ambao waliitoa Tanganyika mikononi mwa wakoloni walikuwa Waislamu, na akahoji sababu za serikali kuwa mstari wa mbele kuwafunga midomo leo.
Bakwata imezinduka sasa Waislamu wote tumeungana katika kupigania haki zetu na kutetea maslahi yetu na serikali itambue kuwa Bakwata iko hai hao Wakristo walikuwa wapi wakati sisi tukipigania uhuru,alihoji.

Wakati huohuo, Sheikh Salum Rwambo alisema anawashangaa wabunge Waislamu ambao baadhi ni mahajat na malhaj wanakaa kimya na kushindwa kutetea hoja za msingi na kudai kuwa huo sasa ndio mwisho wao wa kuwaita masheikh na kutaka waombewe dua ili wasipate wepesi katika kampeni zao.

Sheikh Rwambo pia alimsifia mbunge wa Nzega Lucas Selelii kwamba ni miongoni mwa wabunge katika Bunge hilo wanaozungumza ukweli na kwa kujiamini tofauti na wengine ambao wanaenda kukaa bila kufanya kazi zilizowapeleka.


Source: Mwananchi


CCM watajuta kuweka swala la Mahakama ya Kadhi kwenye Ilani yao uchaguzi ya 2005.
 
watagawanyika tuu hivi, jamaa wanatafuta bei zao. serikali iwaweke lupango waache kelele.
 
Nao wakristo waungane kuanzisha "mahakama zao kiroho ndani ya katiba"?Nchi hii itakuwaje?anyway siwalaumu ndugu zangu Waislam maana CCM na serikali yake iliwahaidi jambo hili na hata ikawekwa kwenye ilani yao ya uchaguzi,maskini haweakujua kama wanatapeliwa ili watoe kura kama ambavyo ahadi nyingi hewa zilizotolewa!
Bytheway lkn Waislam hawajachambua wazi wanakosa kitu gani kwenye sheria mama zilizopo tz hivi sasa hadi wanapigania mahakama ya kadhi?watapata ni ni ikianzishwa mahakama ya kadhi ambacho sasa hawapati?
 
Nao wakristo waungane kuanzisha "mahakama zao kiroho ndani ya katiba"?Nchi hii itakuwaje?anyway siwalaumu ndugu zangu Waislam maana CCM na serikali yake iliwahaidi jambo hili na hata ikawekwa kwenye ilani yao ya uchaguzi,maskini haweakujua kama wanatapeliwa ili watoe kura kama ambavyo ahadi nyingi hewa zilizotolewa!
Bytheway lkn Waislam hawajachambua wazi wanakosa kitu gani kwenye sheria mama zilizopo tz hivi sasa hadi wanapigania mahakama ya kadhi?watapata ni ni ikianzishwa mahakama ya kadhi ambacho sasa hawapati?

Ni sehemu ya ibaada
 
..Kikwete alishachomoa kuhusu ahadi ya Mahakama ya Kadhi.

..alidai waliotumbukiza suala hilo kwenye ilani ni Philip Mangula[mkristo] na Ngombale Mwiru[hana dini].
 
Nao wakristo waungane kuanzisha "mahakama zao kiroho ndani ya katiba"?Nchi hii itakuwaje?anyway siwalaumu ndugu zangu Waislam maana CCM na serikali yake iliwahaidi jambo hili na hata ikawekwa kwenye ilani yao ya uchaguzi,maskini haweakujua kama wanatapeliwa ili watoe kura kama ambavyo ahadi nyingi hewa zilizotolewa!
Bytheway lkn Waislam hawajachambua wazi wanakosa kitu gani kwenye sheria mama zilizopo tz hivi sasa hadi wanapigania mahakama ya kadhi?watapata ni ni ikianzishwa mahakama ya kadhi ambacho sasa hawapati?
wewe mkristo inakuhusu nini?
Unajuaje walichokosa kwenye mahakama mama?
wapeni haki zao what is the issue here?
 
Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

mufti2.jpg

Mufti Issa bin Shaaban Simba, amekasilishwa na uamuzi wa serikali kuhusu Mahakama ya Kadhi.

Na Ummy Muya

BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) limesema kutokana na serikali kutupilia mbali ombi la kunzisha Mahakama ya Kadhi, Waislamu hawataipigia kura CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.

Katika taarifa yake, Bakwata ilifikia hatua ya kusema Waislamu wasimchague Rais Jakaya Kikwete iwapo atasimamishwa na CCM kugombea urais, ikiwa ni pamoja na wabunge na madiwani watakaosimamishwa na chama hicho tawala kutokana na kitendo cha serikali kutupilia mbali hoja ya Mahakama ya Kadhi.

Kauli hiyo imetolewa jana wakati Mufti Issa bin Shaaban Simba alipokuwa akitoa tamko kupinga uamuzi wa serikali kutaka kutumia sheria za dini ya Kiislamu katika mahakama za kawaida badala ya kuanzisha Mahakama ya Kadhi, kitu ambacho alisema anaamini kitawanyima haki Waislamu.

Alisema serikali imedhihirisha kuwa inaendeshwa na Wakristo na si kweli kama serikali haina dini na akamtaka Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe kubatilisha kauli hiyo kwa kuwa inamchafua Rais Jakaya Kikwete mbele ya umma wa Waislamu.

Waziri ametuthibitishia kama Rais Kikwete alikuwa akitulaghai ili tumpigie kura kwa kigezo kuwa suala hilo litashughulikiwa na kupatiwa ufumbuzi na sio kuchanganywa kama ilivyokuwa mwaka 1970 katika Sheria ya Ndoa na kuwanyima haki Waislamu,alisema.

Alisema kwa muda mrefu sana Waislamu wamekuwa kimya wakitumia hekima na busara kudai haki zao, lakini katika hatua hii ambayo serikali imefikia hawapo tayari kuendelea kudhalilishwa na kuwa kitendo hicho ni dhalimu.

Mufti alisema wamekuwa wakiiomba Mahakama ya Kadhi kwa zaidi ya miaka 20 na hivyo hawezi kuendelea kuwa kimya na kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa kwa kuwa mahakama hiyo ni haki yao.

Alisema kauli ya Waziri Chikawe imedhihirisha kuwa serikali ina wenyewe na Waislamu wamewekwa katika tabaka la pili pamoja na Rais Jakaya Kikwete kuwatuliza kwa ahadi kuwa watalipatia ufumbuzi suala hilo.

Natoa wito kwa Masheikh wote nchini na Waislamu wa madhehebu yote kupinga vikali kauli iliyotolewa na Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe na kwamba Waislamu waige mfano wa Waislamu wa Afrika Kusini,alisema Mufti na kuhoji:

Kwa nini iwe Afrika ya Kusini na isiwe Zanzibar, Uganda na Kenya ambazo zipo ndani ya Afrika Mashariki? Kwa niaba ya Waislamu nasema serikali haikututendea haki na imetuchukiza sana,alisema.

Alisema lengo la kuomba mahakama hiyo ni kuhakikisha Waislamu wanashughulikia masuala yao ya ndoa na mirathi na si vinginevyo, hivyo waziri asipotoshe jamii kwa kutumia mifano ambayo haiko sahihi.

Mahakama hii haitawakata wezi mikono kwa kuwa nchi hii ina katiba na sheria na sisi tutazirudisha kesi zote za jinai mikononi mwa serikali. Sifahamu hiyo kamati ambayo waziri alisema alikuwa amekaa na kutoa tamko hilo ilikuwa na watu gani,alihoji.

Aliongeza kuwa kutokana na mapungufu hayo waziri arudi tena na kukutana na masheikh ili apate muongozo wa nini Waislamu wanahitaji na sio kuzungumza bila kuwa na usahihi wa kile anachosema.

Wakizungumza na waandishi wa habari baada ya tamko la Bakwata, masheikh walikuwa na mitazamo tofauti. Sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Salum Mussa alisema wapo baadhi ya Waislamu ambao watakubali kutokana na ufinyu wao wa elimu ya dini.

Mussa alisema haoni sababu ya serikali kufanya njia ya mkato katika suala hilo kwani Waislamu wanahitaji Mahakama ya Kadhi kama ilivyo kwa wafanyabiashara ambao wana mahakama yao.

Hukumu inayotolewa katika Mahakama ya Kadhi ni ibada kwa mujibu wa mafundisho ya Mtume Muhammad (S.A.W) hivyo ni lazima kwa atakayetoa hukumu hiyo awe Muislamu na si vinginevyo,alisema.

Namshanga waziri anapotaka sheria hizi zitumiwe katika mahakama za kawaida. Aliona wapi John akawa imamu,alihoji sheikh huyo wa mkoa wa Dar es Salaam.

Naye katibu wa Bakwata wilayani Ilala, Sheikh Issa Ausi alisema historia iko wazi. Waasisi na wanaharakati ambao waliitoa Tanganyika mikononi mwa wakoloni walikuwa Waislamu, na akahoji sababu za serikali kuwa mstari wa mbele kuwafunga midomo leo.

Bakwata imezinduka sasa Waislamu wote tumeungana katika kupigania haki zetu na kutetea maslahi yetu na serikali itambue kuwa Bakwata iko hai hao Wakristo walikuwa wapi wakati sisi tukipigania uhuru,alihoji.

Wakati huohuo, Sheikh Salum Rwambo alisema anawashangaa wabunge Waislamu ambao baadhi ni mahajat na malhaj wanakaa kimya na kushindwa kutetea hoja za msingi na kudai kuwa huo sasa ndio mwisho wao wa kuwaita masheikh na kutaka waombewe dua ili wasipate wepesi katika kampeni zao. Sheikh Rwambo pia alimsifia mbunge wa Nzega Lucas Selelii kwamba ni miongoni mwa wabunge katika Bunge hilo wanaozungumza ukweli na kwa kujiamini tofauti na wengine ambao wanaenda kukaa bila kufanya kazi zilizowapeleka.
http://www.mwananchi.co.tz/contactmwana.asp
 
Bakwata hawana ubavu huo wanabwaka tu, wao wenyewe credibility yao ni questionable wasafishe nyumba yao kwanza.

Hawana jipya zaidi ya kutafuta njia ya kutokea na kuficha madudu yao. Ni ukweli usio na shaka uislam haupo kitaasisi kama ukristo na madhehebu yake catholics, Lutheran, Anglican nk. Bakwata ni kikundi cha wajanja wachache wasio na mandate yeyote kwa waislam ndio maana no body is taking them serious.
 
Mambo yote mengine ambayo sisi tunayapigia kelele hayawafanyi wao kuichukia CCM; yaani yote yaliyofanyika dhidi ya nchi yetu na utajiri wetu wao hayawagusi wala kuwataka waumini wao kuyafanya ya kisiasa na kuiadhibu CCM; yaani yote hayo hayajafikia kiwango cha kuwakera.. isipokuwa hili moja tu?
 
Ngoma ndio inaanza kupigwa anayeweza aingie na acheze...suala hilo zito sana sana waangalie lisije likaleta machafuko na mpasuko...haya amani yetu tu tusije kuipoteza
 
Naye katibu wa Bakwata wilayani Ilala, Sheikh Issa Ausi alisema historia iko wazi. Waasisi na wanaharakati ambao waliitoa Tanganyika mikononi mwa wakoloni walikuwa Waislamu, na akahoji sababu za serikali kuwa mstari wa mbele kuwafunga midomo leo.

Duh, hapa kazi ipo....!
 
I'll believe it when I see it. Siyo wanaongea hapa wakati wakupiga kura wanafanya vingine. History shows kwenye kuiongea tunaongoza lakini kwenye vitendo sifuri.
 
Mambo yote mengine ambayo sisi tunayapigia kelele hayawafanyi wao kuichukia CCM; yaani yote yaliyofanyika dhidi ya nchi yetu na utajiri wetu wao hayawagusi wala kuwataka waumini wao kuyafanya ya kisiasa na kuiadhibu CCM; yaani yote hayo hayajafikia kiwango cha kuwakera.. isipokuwa hili moja tu?

Mwanakijiji wacha hiyo,maana wakijihusisha mtakuja na rangi nyengine hapa ,hawa ni wananchi walioipigia kura CCM na waliipigia kwa kuahidiwa kupatiwa dai hilo wanalolidai ni sawa sawa kabisa na mwanaCCM alieahidiwa kujengewa hospitali,daraja,njia ya lami na mambo kabakaba yakiwemo maisha bora sasa ni wakati wa wale wote walioahidiwa na hadi leo hawajapelekewa hata kokoto au matofali kuanza kubadili muelekeo kama hao Waislamu walioipigia kura CCM hivyo kuanza safari ya kuipeleka CCM kaburini. Hao waislamu walioipigia kura CCM wameanza kuonyesha njia sasa huko kwenye wakiristu walioipigia kura CCM na madai yao hayakutekelezwa nao wapige mbiu ya mgambu ile kufanikisha maziko.

Mambo ya utajiri hayawashughulishi wanaCCM hayo ni ya vyama vya upinzani au hulielewi hilo ? Ila inaonyesha viongozi wa CCM wamewadanganya wenzao waliomo kwenye mrengo wa uislamu, hivyo wanajitayarisha kutoa pigo kwa viongozi wao,sasa tatizo upande wetu wapinzani lipo wapi, hivi ukisikia vita vya panzi furaha ya kunguru unakuwa hufahamu maana ?

Hao sidhani wanazungumza na wanachama wa Chadema CUF au vyama vingine vya kambi ya upinzani ,si waislamu wote waliipigia kura CCM,bali wanazungumza na wanachama wa CCM ambao ni Waislamu kubadili muelekeo wa kuhamisha kura zao na kuzipeleka wanakoona madai yao yatatekelezwa ,hivyo Chama chochote kile kinaweza kuchukua dai hilo na kusema kuwa endapo wao watapewa kura hizo watalitekeleza dai hilo,sioni tatizo la kidini hapa.

Ila ngoma ni nzito sana ukiangalia jamaa alivyopiga mahesabu tokea kudai uhuru.Inaonyesha uvumilivu umeanza kugonga ukomo.
 
Sasa itakuwaje wakristo wa madhehebu yote nao wakisema hawatakipigia kura chama cha mapinduzi kama wataruhusu mahakama ya kadhi?.
 
Back
Top Bottom