Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,817
- 4,566
Jeshi la Polisi mkoani Mtwara linafanya uchunguzi wa tukio la mwanaume mmoja kujinyonga katika kijiji cha Majengo kata ya Ziwani Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara.
Mwanaume huyo amekutwa amejinyonga jirani ya nyumba ya mkewe ambaye walikorofishana.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo Jumatatu Februari 19,2024, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, ACP-Mtaki Kurwijila amesema mwili ulikutwa jana Jumapili Februari 18, 2024 saa 12 asubuhi ukining’inia kwenye mti wa mkorosho.
Amesema kwa mujibu wa mkewe, mumewe alitoka nyumbani kwake Februari 12 na kwenda kusikojulikana baada ya kutoelewana.
Mwanaume huyo amekutwa amejinyonga jirani ya nyumba ya mkewe ambaye walikorofishana.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo Jumatatu Februari 19,2024, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, ACP-Mtaki Kurwijila amesema mwili ulikutwa jana Jumapili Februari 18, 2024 saa 12 asubuhi ukining’inia kwenye mti wa mkorosho.
Amesema kwa mujibu wa mkewe, mumewe alitoka nyumbani kwake Februari 12 na kwenda kusikojulikana baada ya kutoelewana.