Mtoto wa ujanani!

wandugu, nilipata mtoto na binti mmoja miaka kadhaa iliyopita, hatukuoana wala kuwahi kuishi pamoja, nilimchukua mtoto akiwa na miaka miwili (pls dont ask why)na nilimlea mwenyewe hadi nilipooa, hii ikiwa ni miaka miwili na nusu baadae, mke wangu alimkubali na kumlea mtoto kwa mapenzi yote kiasi kwamba ni wachache mno ambao wanafahamu kuwa yeye sie mama yake mzazi, hata mtoto na wadogo zake hawalifahamu hilo na baadhi ya ndugu zangu pia. mama mzazi wa mtoto alishaolewa na ana maisha yake kwa mumewe na watoto wao na tuna mawasiliano ya msimu kuhusu mtoto, hajawahi kumuona mwanae kwa zaidi ya miaka nane sasa! tatizo linakuja ni kwamba mtoto amekua na ana shughuli mbeleni ambayo sidhani kama itakuwa jambo la busara mama yake kutohudhuria au kutopata taarifa, je mtoto, wadogo zake, na mama yake(mke wangu) watalipokeaje?!nachelea kufanya lolote litakaloikosesha familia yangu amani, i love my family na siko tayari kuona hili litokee,je nimpotezee tu mama yake bila kumfahamisha? but in otherside ana haki kwani ni mwanae! ni wakati gani muafaka wa kumuweka wazi mtoto kuhusu hili au nalo nilipotezee hadi atakapokuja gundua mwenyewe mbele ya safari??seriosly hili linanitatiza na noamba ushauri wako..tafadhali usinihikumu kwa makosa ya nyuma, nakaribisha ushauri wako..

Ni kweli kabisa huyo mama ana haki kama mama wa mtoto, lakini alikuwa wapi miaka zaidi ya minane bila hata kutamani kumtia machoni mwanae kuona kama anaendelea vizuri au la na pia kujenga uhusiano na mwanae ili wafahamiane kwa karibu!? Muulize Mkeo ili usikilize naye ana maoni gani kuhusu swala hili, lakini kwa maoni yangu hasa ukitilia maanani kwamba miaka yote hii amempa malezi bora binti yenu na yeye na wadogo zake mliojaliwa na mkeo bila wao kugundua kama dada yao ana mama tofauti, basi mpotezee tu huyo mama ila kama mkeo ana mawazo tofauti basi msikilize.
 
kwa umri huo wa 10+ yrs mtoto anakuwa na mihangaiko mingi ya kujitambua. ukiingiza suala la identity tena unaweza kumchanganya na kumfanya apoteze muelekeo. mama yake pia anaweza kutamani kumgombea na kuleta usumbufu mkubwa. kama hakua na interest for all those years why now? binti akimaliza sec,maybe form 6 unaweza ukamuambia hizi habari wakati akipoteza mawazo ya matokeo awaze haya ma-crap.
 
Hadi sasa ni upande mmoja tu unao ongelewa. Swali ninalotaka kumuuliza mleta hoja ni kuwa, wakati anamchukua mtoto akiwa mdogo wa miaka miwili, na kisha mama yake mzazi kuolewa, Je, huyo mzazi mwenzie, alimjulisha mume wake wa sasa kwamba ana mtoto? na kama huyo mume wake wa sasa hajui (alifichwa), naona pia tatizo jingine. Utakapomjulisha huyo mama, hata kama ni harusi atahudhuriaje pasipo mume wake kufahamu?

Kumjulisha mama yake ni vizuri lakini pia huyo mume wake naye anapaswa kufahamu. Je hapo inakuwaje? Vinginevyo, Msikilize mjadili na mkeo ili upate mawazo yake, na zaidi yeye ndiye aamue. Asipoamua yeye itakuwa ni mvurugano ktk familia yake. Mimi nadhani mama yake anaweza kujulishwa tu tukio lakini asihudhurie. Akihudhuria kutakuwa na negative impact kwa sababu itabidi atambulishwe na hiyo itakuwa ni mshituko kwa mtoto na wadogo zake wengine.
 
Hapo ndipo na mie nimejiuliza, hayo mawasiliano ni ya juu ya nini, kuna wanawake wana roho ngumu sana, mtoto umeingia leba mwenyewe usimuone miaka nane? halafu unataka kwenda kwenye sherehe, huyu mama ni mjinga wala hastahili kwenda kwenye hiyo sherehe ata mconfuse tu mtoto keshazoea maisha yake

Nakubaliana na wewe Gaga huyo mama ni wa aina gani? miaka nane hajawahi muona mwanae wa kumzaa? Mi naona mchunie tu na wala mtoto msimueleze hayo mambo sasa hivi kwani yatamkosesha amani na wakati mwingine atakua hata akigombezwa atakua anasema labda kwa sababu mi sio mtoto wake. Muacheni mpaka apate akili ndio mumwambie na kizuri zaidi huyo mama wa mtoto nae anaonekana hana hata mpango na mwanae.
 
wandugu, nilipata mtoto na binti mmoja miaka kadhaa iliyopita, hatukuoana wala kuwahi kuishi pamoja, nilimchukua mtoto akiwa na miaka miwili (pls dont ask why)na nilimlea mwenyewe hadi nilipooa, hii ikiwa ni miaka miwili na nusu baadae, mke wangu alimkubali na kumlea mtoto kwa mapenzi yote kiasi kwamba ni wachache mno ambao wanafahamu kuwa yeye sie mama yake mzazi, hata mtoto na wadogo zake hawalifahamu hilo na baadhi ya ndugu zangu pia. mama mzazi wa mtoto alishaolewa na ana maisha yake kwa mumewe na watoto wao na tuna mawasiliano ya msimu kuhusu mtoto, hajawahi kumuona mwanae kwa zaidi ya miaka nane sasa! tatizo linakuja ni kwamba mtoto amekua na ana shughuli mbeleni ambayo sidhani kama itakuwa jambo la busara mama yake kutohudhuria au kutopata taarifa, je mtoto, wadogo zake, na mama yake(mke wangu) watalipokeaje?!nachelea kufanya lolote litakaloikosesha familia yangu amani, i love my family na siko tayari kuona hili litokee,je nimpotezee tu mama yake bila kumfahamisha? but in otherside ana haki kwani ni mwanae! ni wakati gani muafaka wa kumuweka wazi mtoto kuhusu hili au nalo nilipotezee hadi atakapokuja gundua mwenyewe mbele ya safari??seriosly hili linanitatiza na noamba ushauri wako..tafadhali usinihikumu kwa makosa ya nyuma, nakaribisha ushauri wako..

hili jambo ndugu usilichukulie juu juu .. kwanza nampa mama yake mlezi hongera kumfikisha hadi hapo alipo nawe nakupongeza.... naamini kuna mambo mengi ambayo hutaki kuuliza ambayo yangesaidia sana watu kuujua ukweli maana umesema usiulizwe kwa nini .. ila kawaida utengano wa wazazi huwa uko katika sehemu 3

kwanza baba atakuwa na matatizo pili mama ndo tatizo na la tatu wote ni matatizo..

mtoto anapokuwa na shughuli ni vyema wazazi wote wawepo kwani huyo mtoto hukubeba wewe mimba na kujifungua ila mama yake ndo alikuwa na jukumu hilo na hata malezi ya awali yalikuwa ni ya mama ..

matatizo au ugomvi wa wazazi usipewe nafasi ya kujennga au kupandikiza mbegu za chuki kwa mtoto hilo naomba sana liweke pembeni na isije likawa unalipa nafasi ili mama mlezi awe mama mzazi au kwa wewe kuona kama mama mlezi atakosa haki ya kushiriki ... nakuomba sana tena sana mwite mama mzazi wa mtoto mkae muongee na muweke sawa ushiriki wake katika hito shughuli maana ana nafasi yake tena ya msingi ila kama ataomba udhuru wa kutokuwepo ni sawa lakini husisha na hata ndugu zake mama wa mtoto
 
Duuh nafuta machozi kwakweli, nimeishi na mama wakambo na alikuwa anajifanya ananipenda mzee akiwepo lakini akiwa safarini ilikuwa ni mateso kwakwenda mbele, nakumbuka baadhi ya visa alivokwisha wahi kunifanyia ni pamoja na kunilisha UGALI akati yeye na wanae wakila CHIPSI YAI, aliwahi Kuweka MAVI YA MBWA kwenye kitanda changu kisa eti Sikuyatoa asubuhi wakati nafagia uwanja,

Mie pia nilikaa miaka 4 bila kumwona mama mzazi, siku nilipopata nafasi yakwenda kwake nilifurahi sana, Mama ni mama ndugu zangu hata akiwa masikini, atajibana ili mwanae akufurahishe, basi akati narudi kwa mama wakambo nilipewa mchele debe moja lakini bado nikawa nanyimwa wali ukipikwa, duuh nililia sana na kutoroka mpaka Kwa mama mzazi, lakini nashukuru mungu kwani nimejifunza mengi na siteteleki sasahv japo mama mzazi alishatangulia mbele ya haki miaka 9 iliopita bado nampenda sana

I'm 22 yrs now, naomba tu huyo baba ampeleke mtoto kwa mama yake amuone na hata kwaenye hyo sherehe amwalike mzazi mwenzie, Mama ni mama jamani,

USHAURI: mlio kwenye ndoa muishi kwa upendo na uvumilivu, msiachane kwani watoto mtawapa wakati mgumu, kweli malezi ya pande moja hayajitoshelezi kwa mtoto...
 
Back
Top Bottom