Ushauri: Mwaka umepita toka mzazi mwenzangu achukuliwe na mama yake kwa nguvu, nimechoka nataka kuanza safari mpya

INSPECTOR JOE

Member
Apr 14, 2014
26
12
Habari wanajamii naomba msaada wenu, miaka takribani mitano nyuma nilikuwa kwenye mahusiano ambayo yalipelekea kuwa mzazi wa mtoto mmoja wa kiume.

Kiuhalisia maisha hayakuwa mazuri sana ila tulikuwa na furaha na tuliishi kwa kupendana sana. Safari yetu ilikuwa nzuri kiujumla, lakini ikatiwa doa na mama mzazi wa mzazi mwenzangu kwa kumchukua mwanae kinguvu huku akinisema kwa ubaya jambo ambalo lilinikereketa vibaya kila kukicha.

Ni mwaka sasa umetamatika baada ya mimi na mzazi mwenzangu kutengana lakini imefika mahali upendo umepungua sana. Nilikuwa nimezoea kumpigia simu kujua hali ya mtoto na yeye lakini mama yake amekuwa mtu wa kuvuruga hadi mawasiliano yetu.

Imefika mahali natamani kuanza safari mpya maana nimechoka kiuhalisia maana nimejikuta namchukia sana mama mzazi wa mke wangu kutokana na tabia alizozionyesha za kumchukua mwanae kwa nguvu akiambatanisha na vitisho huku pia akidai namtesa mwanae wakati toka nimenza kuishi nae sijawahi kufanya, kuelezea kila kitu siwezi kwa haraka haraka.

Maana niliyofanyiwa mpaka naomba ushauri wenu ni mengi na yanumiza. Nimwache abaki na mama yake au nirudiane naye?
 
IMG_0058.jpeg
 
Maybe haukumchukua kwao kwa utaratibu... Hakuna mzazi anafurahishwa binti yake achukuliwe tu kienyeji azalishwe na aishi na mwanaume bila wao kuhusishwa na kufata taratibu za kimila au za kidini
 
Habari wanajamii naomba msaada wenu, miaka takribani mitano nyuma nilikuwa kwenye mahusiano ambayo yalipelekea kuwa mzazi wa mtoto mmoja wa kiume.

Kiuhalisia maisha hayakuwa mazuri sana ila tulikuwa na furaha na tuliishi kwa kupendana sana. Safari yetu ilikuwa nzuri kiujumla, lakini ikatiwa doa na mama mzazi wa mzazi mwenzangu kwa kumchukua mwanae kinguvu huku akinisema kwa ubaya jambo ambalo lilinikereketa vibaya kila kukicha.

Ni mwaka sasa umetamatika baada ya mimi na mzazi mwenzangu kutengana lakini imefika mahali upendo umepungua sana. Nilikuwa nimezoea kumpigia simu kujua hali ya mtoto na yeye lakini mama yake amekuwa mtu wa kuvuruga hadi mawasiliano yetu.

Imefika mahali natamani kuanza safari mpya maana nimechoka kiuhalisia maana nimejikuta namchukia sana mama mzazi wa mke wangu kutokana na tabia alizozionyesha za kumchukua mwanae kwa nguvu akiambatanisha na vitisho huku pia akidai namtesa mwanae wakati toka nimenza kuishi nae sijawahi kufanya, kuelezea kila kitu siwezi kwa haraka haraka.

Maana niliyofanyiwa mpaka naomba ushauri wenu ni mengi na yanumiza. Nimwache abaki na mama yake au nirudiane naye?
Mkuu
Kuna vitu vingine ni vigumu sana wanaume tunapitia.

Kikubwa be a man. Fanya uamuzi sahihi na songa mbele. Hakikisha mwanao anakuwa begi lako yaani kuwa naye karibu sana na umkuze bila kuzingatia huyo aliyeondoka
 
Polee sana maybe huna pesa mzazi anaona mwanae atapata shida, ila usivunjike moyo endelea na maisha yako.
 
Maybe haukumchukua kwao kwa utaratibu... Hakuna mzazi anafurahishwa binti yake achukuliwe tu kienyeji azalishwe na aishi na mwanaume bila wao kuhusishwa na kufata taratibu za kimila au za kidini
Hata kama.
Mtoto ameshazalishwa na ana mtoto mmoja. Mtoto anatakiwa alelewe na baba yake na mama yake. Kukaa na mtoto (mjukuu) ni kudhulumu haki ya mjukuu
Wazazi huvuruga sana mahusiano ya watu na mara nyingi familia za hivyo ni zile mama ndiyo anasauti.
Ukikuta nyumba, mama anasauti kuliko baba, usioe hapo
 
Mwanamke wako hana misimamo. Kwann mzazi aseme yeye anateseka wakati muhusika hana tatizo? Au labda ni kweli unamtesa mtoto wa watu.
 
Taratibu zote zilifuatwa
Unamtesaje sasa? Wewe haujatupa maelezo yaliyonyooka umelezea nusu au robo.

Mama mkweo anasemaje kwa kauli zake ziseme hapa tujue anakutamkia maneno gani?

Mkeo anasemaje kuhusu hili swala?

Kabla ya mama mkwe kuwaingilia ulikuwa na changamoto gani na mtoto wa watu hapo kwako?

Una kazi ya maana ya kukupa kipato cha kumudu maisha na huyo mwanamke?

Hebu nyoosha maelezo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom