Kaka yangu anaoa tarehe 24 April, bado wiki 1 ndoa ianze kutangazwa, wiki 1 moja iliyopita kapigiwa simu na binti 1 akajitambulisha kwake wanajuana waliwahi kuwa na uhusiano mwaka 2004 wakaachana alimfumania msichana, kumbe wakati wanaachana msichana alikuwa na mimba hajijui wakapoteana msichana amezaa sasa hv mtoto ana miaka 6, kamtafuta kaka yangu kwa marafiki hadi kampata. wakaenda kupima DNA kweli mtot ni wa kaka na amemkubali kulipa gharama na matunzo yote na pia atampeleka shule boarding atakuwa anamuhudumia. Ila msichana hatakia anasema yeye anataka kuolewa waleee mtoto wao, mwanaume hataki kumuoa anamwambia sikupendi, masichana ametishia kwenda kupinga ndoa kanisan, la sivyoa aolewe yeye. na msichana anayeolewa alivyosiskia amekasirika amemwambia mwanume nakuacha mlee mtoto wenu, kaka yangu amechanganyikiwa ni mwanume lakini kwa mara ya kwanza nimemuona akilia kama mtoto,kwanza ameachwa ndoa inakaribia, pili hamtaki huyo aliyezaa naye. kama huyo mchumba wake atamrudia huyo mama mtoto akienda kupinga ndoa itavunjika ua kuna taratibu zitafuatwa, maana kamuambia mama mtoto kwamba nikikuoa nitakutesa sana mimi sikupendi kuzaa siyo kigezo, mimi nimekosa cha kumshauri maana ni mwanamke na wote nawaonea huruma.