Mtoto wa Kikwete ashinda kwa kishindo

Nini maana yake?
Soma hapa chini...

Chipukizi ni form ya grooming too, enzi za TANU wakiitwa 'Young Pioneer', Mwalimu alitokanayo China alikolitoa Azimio La Arusha na siasa yake ya Ujamaa na Kujitegemea iliyobakia jina tuu kwenye katiba yetu ya Mwaka 1977.

Grooming always ni kitu kizuri, imekuwa ikifanyika for time immemorial kwenye royal families tangu ndoa inajulikana mtoto wa kwanza wa kiume kuzaliwa kuzaliwa ndio mrithi wa kiti cha ufalme wa babaye, hivyo tagu mimba, inakuwa groomed as the heir to the throne.

Mtoto huyo hulelewa kwa makuzi ya anticipated king, heavily mind indoctrination of not who is realy is, but who ought to be, 'king'.

Sasa kuna ubaya gani kuwagroom hawa vijana wadogo chpukizi wa CCM kuhusu chama chao na baadae kinatoa viongozi wazuri tuu, Nape ametokea Chipukizi, yule mwenyekiti wa zamani, Frank Uhahula ambaye sasa ni mkuu wa wilaya, ametokea chipukizi, the logic is to see the potential in them, groom them to make that potential a reality.

Huu msemo wa 'like father like son' unafanywa practical zaidi kwa kumgroom mwanao afuate nyayo zako ndio maana baada ta Karume Baba, sasa Karume ni rais wa Zanzibar, tumeona kwa Kabila, kwa Bush, Ghadhi, Kenyata, Oginga, Kenedies etc sometime baada ya mume ni mke, kama Sonia Ghadhi, Imelda Marcos, Mama Acquino, Winie Mandela etc, hakuna ubaya wowote, zamu za kina, Makongoro, Dr. Mwinyi, Nikolas, Ridhiwan etc zinafuatia with time.

Angalizo:Baba anaweza kuwa kiongozi bora na mwana asiwe, vile vile baba aweza kuwa kiongozi bomu, mwana akaja kuwa kiongozi bora. Issue isiwe kwa vile ni mtoto wa nani, bali iwe ni uwezo binafsi wa mtoto, ability na capability, kazi ya mzazi ni kumjengea tuu interest, ndicho wanachofanyiwa chipukizi hawa.
 
Hivi Dogo Khalfani atakuwa akilipwa kiasi gani kwa kuwa Chipukizi Mkuu?

Mchungaji.Kishoka

Huu nao ni Ufisadi?

Hapa Kanisani kwetu Kyela kuna Mzee Mchungaji juu ,Kamati zote za maana zinaongozwa na Mama Mchungaji,kiongozi wa kwaya ni Mtoto wa Mchungaji,Sunday School kabinti ka mchungaji ,hii ndo Tanzania Mwanawane.
 
JK mwennyekiti,
Mama Salma (mke) mjumbe
Ridhiwani (mtoto) UVCCM
Khalfani (mtoto) mjumbe wa Baraza la Chipukizi na UVCCM

Sasa chama cha kifamilia na kikabila ni CHADEMA au CCM?

List ni ndefu zaidi..

Kawambwa plus nduguze na Jk wawili
 
JK mwennyekiti,
Mama Salma (mke) mjumbe
Ridhiwani (mtoto) UVCCM
Khalfani (mtoto) mjumbe wa Baraza la Chipukizi na UVCCM

Sasa chama cha kifamilia na kikabila ni CHADEMA au CCM?

Teh teh Mpwaaaaa hii ndio SIASA YA BONGO!

NO COMMENT

 
  • Kibunango, hivi kwa nini kuna sheria inayosema huwezi kujiandikisha kupiga kura hadi ufikishe miaka fulani ?
  • Hawa watoto wanasafiri peke yao ama wanaongozana na ama wazazi wao au guardians wao ?
  • Je, nani anawagharamia kwenye safari na malazi ama wanajilipia ? Kama wanagharamiwa je, ni chombo gani hicho na kinapataje pesa?
  • Kama ni chama cha siasa (CCM) hiyo inaruhusiwa kisheria hivi vikinda kujishughulisha ama kutumiwa kisiasa ?
  • Je, inakuwaje kama mtoto wa miaka kumi hakipendi chama cha baba yake na kwa mtindo huu tunawafundisha nini hawa kinda - kuwa wana tofauti na wenzao ?
  • Je lengo hapa ni kama lile la Al Qaida la kuwasokomezea itikadi tangu utotoni - adui wao hapa ni nani ?
  • Je, ni kweli kuwa CCM hawaoni hatari ya kuwapandikiza watoto wadogo hii tabia ya kubaguana ?
Mababu wa CCM, Wazazi wa CCM, wake wa CCM, Wamama wa CCM, Vijana wa CCM , Chipukizi wa CCM, Wajukuu wa CCM hadi Watukuu wa CCM - jamani tunajenga Taifa gani au ndio mwanzo wa kutanguliza maslahi ya CCM kabla ya taifa.

  • Kitaifa/kiserikali umri wa kuanza kupiga kura ni miaka 18. Hata hivyo hii aizui jumuiya za kichama kuwa na chaguzi zao za ndani kutokana na mfumo wake. Ama ni kwanini umri huo umewekwa natumai unajua fika maana yake, kwamba ndio umri uliofikiliwa kuwa ndio muafaka kwa kijana kuweza kuchagua viongozi wake kitaifa/kiserikali . Ni umri ambao unasadikika kuwa kijana anaweza kuanza kujitegemea na kuwa na maamuzi yake binafsi.

  • Kusafiri peke yao ama kusindikizwa inategemea na mahala wanapokwenda. Kwa kuwa mkutano huo ulifanyika mkoani Morogoro hapana shaka wajumbe wake toka mikoa mbalimbali, washiriki wake walisafiri kwa pamoja chini ya wasimamizi wawili ama mmoja na sio kwa kila chipukizi kupelekwa na mzazi wake. Hii ni jumuiya/kitengo cha chama hivyo kuna taratibu nzuri za kuwasafirisha wajumbe wake.

    Aidha gharama za usafiri, malazi na mahitaji mengine ya mkutano yanagharamiwa na chama, pamoja na waandaaji wake(kichama).

  • Kimsingi kuingia chipukizi ya CCM sio jambo la lazima. Hivyo sio haki kwa mzazi kumshurutisha mtoto wake kujiunga. Mtoto anaweza kupenda kuwa chipukizi kutokana na kupenda shughuli zake nae kutamani kujiunga nao. Mikutano mingi mikubwa ya Chama(CCM) hufunguliwa na gwaride la chipukizi, haraiki ya chipukizi na mambo kadha wa kadha ya watoto hao. Hii pekee inaweza kumvutia mtoto yoyote kujiunga pasipo ushawishi wa mzazi wake.

    Miaka ya chama kimoja hali ilikuwa tofauti kidogo, kwani ilikuwa ni suala la kitaifa zaidi kuliko la kichama.

  • Lengo kubwa sio kujenga itikadi ya kubaguana, zaidi ni kujenga umoja miongoni mwao, kujua kazi za chama chao pamoja na madhumuni yake. Vitu ambavyo vilikuwa vikifundishwa kwa watoto wote(shuleni) kabla ya kurudi kwa vyama vingi.

    Hata baadhi ya vyama vingine naona taratibu wanaanza kuwa na utaratibu kama huu. Nimeona baadhi ya vyama kwenye mikutano yao, viongozi wao wa kitaifa wakivishwa mashada na skafu na watoto(chipukizi). Sidhani kama huko wanafundishwa itikadi mbaya! Ingawa maneno ya viongozi na wafuasi wao yana kila dalili ya itikadi mbaya dhidi ya CCM.

Mengine unaweza kuyafahamu vizuri kwa kupitia nukuu hizi...

Kwangu mimi naona si vibaya kuwashirikisha watoto kama hawa(wenye miaka 10 na kuendelea) kwenye siasa,watakulia(huko) CCM baadae wataamua ama kuendelea na hiyo CCM ama kujiunga na vyama vingine(viongozi na wanachama wengi wa vyama vya siasa Tanzania walipitia CCM ama kwa kuwa Chipukizi ama UVCCM) kabla ya mfumo wa vyama vingi kuanza..CCM wanajiandalia mtaji/hazina ya kisiasa miaka ijayo..Si vibaya kwa vyama vingine wakaanza kuwaandaa wanachama/viongozi wa kizazi kijacho kwa kupitia Chipukizi...Ni mtazamo tu wakuu..Pamoja

Sasa kuna ubaya gani kuwagroom hawa vijana wadogo chpukizi wa CCM kuhusu chama chao na baadae kinatoa viongozi wazuri tuu, Nape ametokea Chipukizi, yule mwenyekiti wa zamani, Frank Uhahula ambaye sasa ni mkuu wa wilaya, ametokea chipukizi, the logic is to see the potential in them, groom them to make that potential a reality.
 
JK mwennyekiti,
Mama Salma (mke) mjumbe
Ridhiwani (mtoto) UVCCM
Khalfani (mtoto) mjumbe wa Baraza la Chipukizi na UVCCM

Sasa chama cha kifamilia na kikabila ni CHADEMA au CCM?
...Nimeipenda hii...
 
Please guys, let us give a kid a break!
Amegombea, watu wamempigia kura.. ndio utamu wa demokrasia!
Hail to The Great Thinker Nyani Ngabu bin Julius.. Miafrika ndivyo tulivyo!

Hebu anaglia hii ripoti ya Mwananchi..

" Mtoto wa Kikwete aula UVCCM"
By Samuel Msuya - Morogoro.

".......Wajumbe wa chipukizi wa nchini kote wakiongozwaa Makatibu wa Mkoa wa UVCCM walimchagua Halfani huku wengi wao wakiwa hawajawahi kumuona na hata kumsikia akiwaomba kura. Wagombea wengine waliokuwako walijieleza na kuomba kura, lakini wakaambulia patupu...."

Jee inamaana alichaguliwa in absentia?

 
Ingekuwa wameshinda kwa kishindo shule hata mimi ningewapongeza. Kweli hili inaonyesha tu jinsi our priorities zilivyokuwa warped!

Amandla....
 
Nchi hii atari sana,kwa nini baba yangu akuchagua siasa,kwani ata kama uwezo wako mdogo aijalishi utawaongoza tu,na kama kilaza lakini baba ndio hivyo kama JK ndio basi utapewa vyeo ambavyo ata majukumu yake uyajui.

Uwezo wa ridhiwani ni wakuungaunga sana sijui uyo mtoto,ata maksi zilikua za kudesa lakini ana vyeo ambavyo ata details zake afahamu.

SISI MACHO LAKINI IPO SIKU TUTACHOKA.
 
JK mwennyekiti,
Mama Salma (mke) mjumbe
Ridhiwani (mtoto) UVCCM
Khalfani (mtoto) mjumbe wa Baraza la Chipukizi na UVCCM

Sasa chama cha kifamilia na kikabila ni CHADEMA au CCM?

Ndugu yangu kamende ulikuwa hujui kuwa CCM wana siasa za kifamilia zaidi kuliko vyama vingine? ndani ya CCM kuna vimungu mtu vya kiukoo ndivyo vinavyoendesha chama havitaki familia zingine ziingie humo havionekani kwa sababu chama ni kikubwa ukoo mmoja uko toka ngazi ya mtaa, kijiji, wilayani, mkoani wizarani hadi Taifa utadhani wengine hawafai.
Watajifanya wanandaa chipukizi lakini wako mstari wa mbele kulaumu CHADEMA kuwa ni chama cha ukoo. Kwa kuanzia nitawaleteeni ukoo wa Kingunge muone picha halisi walio ndani ya chama hadi serikalini. Wanaposema CCM ina wenyewe usifiri propaganda tu za chama ni kweli wengine washika vibendera.
 
Hongereni Chipukizi wote mlioshinda na kupata nafasi ya kuwakilisha chipukizi wengine!
ZZZZIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIII,
kwani nyie sisiemu hamna watoto wengine hadi mnachagua watoto wa viongozi kina kikwete, kina makala, majina hayo hayo kila siku, aaarrrrgggghhh
 
yaleyale ya kina Omar Bongo, tusipoangalia hawa watu wataingiza ufalme! Nyerere, Mwinyi, Mkapa wangeweza fanya hivyo ila walijua kutenganisha uongozi na familia! sasa hako katoto kameshinda through merit au through father influence?
 
Kuna watu humu JF sitaki kuwataja kwa majina wapo mstari wa mbele kukikosoa CHADEMA kuwa ni cha ukoo lakini sasa wamekuja na gia eti CCM wao wana-groom tu hawoni kuwa hiyo pia ni sababu tosha ya ubinafsi ukoonaism wanataka wawe wao tuuuu jamani.
 
  • Kibunango, hivi kwa nini kuna sheria inayosema huwezi kujiandikisha kupiga kura hadi ufikishe miaka fulani ?
  • Hawa watoto wanasafiri peke yao ama wanaongozana na ama wazazi wao au guardians wao ?
  • Je, nani anawagharamia kwenye safari na malazi ama wanajilipia ? Kama wanagharamiwa je, ni chombo gani hicho na kinapataje pesa?
  • Kama ni chama cha siasa (CCM) hiyo inaruhusiwa kisheria hivi vikinda kujishughulisha ama kutumiwa kisiasa ?
  • Je, inakuwaje kama mtoto wa miaka kumi hakipendi chama cha baba yake na kwa mtindo huu tunawafundisha nini hawa kinda - kuwa wana tofauti na wenzao ?
  • Je lengo hapa ni kama lile la Al Qaida la kuwasokomezea itikadi tangu utotoni - adui wao hapa ni nani ?
  • Je, ni kweli kuwa CCM hawaoni hatari ya kuwapandikiza watoto wadogo hii tabia ya kubaguana ?
Mababu wa CCM, Wazazi wa CCM, wake wa CCM, Wamama wa CCM, Vijana wa CCM , Chipukizi wa CCM, Wajukuu wa CCM hadi Watukuu wa CCM - jamani tunajenga Taifa gani au ndio mwanzo wa kutanguliza maslahi ya CCM kabla ya taifa.

Jamani mbona tunakuwa wasahaulifu?

Vyama vyote vikuu vya siasa vina idara zao za vijana,na hii yote ni mipango kamambe ya kuzalisha viongozi wa baadae ambao watakua chachu ya kueneza itikadi za vyama husika.

John myika,ZZ,msafiri mtemelwa,kafulila,Danda etc ni mifano ya wanasiasa ambao wameanza ngazi za chini sana kwenye vyama vyao.

Ukiondoa udhaifu wa mtu binafsi pamoja na kipaji,kiongozi bora ni yule alieanza kupewa uongozi utotoni.msome huyu bwana mdogo http://en.wikipedia.org/wiki/David_Miliband#Early_life
 
Hebu anaglia hii ripoti ya Mwananchi..

" Mtoto wa Kikwete aula UVCCM"
By Samuel Msuya - Morogoro.

".......Wajumbe wa chipukizi wa nchini kote wakiongozwaa Makatibu wa Mkoa wa UVCCM walimchagua Halfani huku wengi wao wakiwa hawajawahi kumuona na hata kumsikia akiwaomba kura. Wagombea wengine waliokuwako walijieleza na kuomba kura, lakini wakaambulia patupu...."

Jee inamaana alichaguliwa in absentia?


........Ghafla, Pamekuwa kimya!
 
JK mwennyekiti,
Mama Salma (mke) mjumbe
Ridhiwani (mtoto) UVCCM
Khalfani (mtoto) mjumbe wa Baraza la Chipukizi na UVCCM

Sasa chama cha kifamilia na kikabila ni CHADEMA au CCM?
Hivi Miraji(mtoto) ni nani tenaa,aah nimekumbuka,huyu ni msela tuu!!
 
Ndugu yangu kamende ulikuwa hujui kuwa CCM wana siasa za kifamilia zaidi kuliko vyama vingine? ndani ya CCM kuna vimungu mtu vya kiukoo ndivyo vinavyoendesha chama havitaki familia zingine ziingie humo havionekani kwa sababu chama ni kikubwa ukoo mmoja uko toka ngazi ya mtaa, kijiji, wilayani, mkoani wizarani hadi Taifa utadhani wengine hawafai.
Watajifanya wanandaa chipukizi lakini wako mstari wa mbele kulaumu CHADEMA kuwa ni chama cha ukoo. Kwa kuanzia nitawaleteeni ukoo wa Kingunge muone picha halisi walio ndani ya chama hadi serikalini. Wanaposema CCM ina wenyewe usifiri propaganda tu za chama ni kweli wengine washika vibendera.
Sasa wewe ukienda usalama wa taifa na wizara ya mambo ya ndani si ndio utalia kabisa ni undugunaizeshen theory,we acha tuu,soma alama za nyakati chukua kilicho chako then take a new move!!
 
Imeandikwa na John Nditi, Morogoro;
Tarehe: 30th December 2009


MKUTANO Mkuu wa Uchaguzi wa Chipukizi taifa umemchagua kwa kishindo mtoto wa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Jakaya Kikwete, Khalfani Kikwete (11) kuwa Mjumbe wa Baraza Kuu la Chipukizi Taifa Tanzania Bara.

Khalfani alipata kura 301 na kuwashinda wagombea wenzake 11. Kwa Tanzania Zanzibar, mshindi alikuwa Abdallah Haji Mgeni. Kutokana na ushindi huo Khalfani ataliwakilisha Baraza Kuu la Umoja wa Vijana (UVCCM).

Mtoto wa Katibu wa Fedha na Uchumi wa Taifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Amos Makala, Gabriel Makala (12), amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Chipukizi Taifa.

Gabriel alishinda kwa kupata kura 300 kati ya kura 357, aliwashinda wagombea wanane,kura saba ziliharibika.

Uchaguzi Mkuu huo wa Chipukizi Taifa uliofanyika mjini Morogoro ni wa vijana wadogo wa CCM kutoka katika mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar.

Nafasi ya Mkutano Mkuu wa UVCCM Taifa upande wa Tanzania Bara ilichukuliwa na Gladness Urassa na Ramadhani Guruwe,Tanzania Zanzibar ilichukuliwa na Elias Cassion.

Katika nafasi ya Kamati ya Uendeshaji Taifa Tanzania Bara, ilichukuliwa na Glory Mwambeleko na Asnail King, wakati upande wa Zanzibar, ilikwenda kwa Abdalah Haji Mgeni na Abdulatif Ramadhan Abdullah.

Source: Gazeti la Habari Leo

Wakati wa watu kupata madaraka na nafasi za kuongoza kutokana na uwezo hizooooooooooo zinaondoka. Matabaka hayooooooooooooooo yanagawika. Tupende tusipende Mlalahoi, "GO TO HELL". Wakati wa kupata elimu, kupata madaraka kutokana na uwezo wako kiakili kwa kuanzia chini na kupanda kidogo kidogo kama walivyopanda wao hawa MAFISADI umekwisha. Only the elite group that will own everything and you and me will deserve nothing.

MAFISADI watazidi kukusanya kila kilichopo, watakalia kila nafasi na kumiliki kila kitu na kiburi chao kuongezeka.

MWENYEZI MUNGU AWALAANI KWA KUWAONGEZEA MARADHI YA KUENDELEA KUTOTOSHEKA KILA WANACHOKIPATA, AWAONGEZEE VIBURI NA JEURI, NA AWAONDOSHEE KABISA UFAHAMU WA KUELEWA MAKUSUDI YA KUUMBWA KWAO, WASIJUE LIPI BAYA/OVU NA LIPI ZURI/JEMA, WAO WACHANGANYE TUU ILI ISAFIKE NJIA YAO YA KUELEKEA MOTONI, NAJISI HAWA.

NA SISI MUNGU ATUJAALIE SHUJAA MIONGONI MWETU AMBAE SIKU MOJA ATAWASGHULIKIA VILIVYO MAFISADI WATAKAOBAKIA KUWEPO WAKATI HUO. ATUONDOSHEE NA AISAFISHE NCHI YEU NA NAJISI HII NA UVUNDO WA MAISHA YA MAFISADI HAWA. MAISHA YA MAFISADI HAWA NI BALAA KWA WANYONGE

LAANATULLAAHI ALAL MUFSIDIIN.
 
Back
Top Bottom