Facts1
JF-Expert Member
- Dec 23, 2009
- 307
- 28
Imeandikwa na John Nditi, Morogoro;
Tarehe: 30th December 2009
MKUTANO Mkuu wa Uchaguzi wa Chipukizi taifa umemchagua kwa kishindo mtoto wa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Jakaya Kikwete, Khalfani Kikwete (11) kuwa Mjumbe wa Baraza Kuu la Chipukizi Taifa Tanzania Bara.
Khalfani alipata kura 301 na kuwashinda wagombea wenzake 11. Kwa Tanzania Zanzibar, mshindi alikuwa Abdallah Haji Mgeni. Kutokana na ushindi huo Khalfani ataliwakilisha Baraza Kuu la Umoja wa Vijana (UVCCM).
Mtoto wa Katibu wa Fedha na Uchumi wa Taifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Amos Makala, Gabriel Makala (12), amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Chipukizi Taifa.
Gabriel alishinda kwa kupata kura 300 kati ya kura 357, aliwashinda wagombea wanane,kura saba ziliharibika.
Uchaguzi Mkuu huo wa Chipukizi Taifa uliofanyika mjini Morogoro ni wa vijana wadogo wa CCM kutoka katika mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar.
Nafasi ya Mkutano Mkuu wa UVCCM Taifa upande wa Tanzania Bara ilichukuliwa na Gladness Urassa na Ramadhani Guruwe,Tanzania Zanzibar ilichukuliwa na Elias Cassion.
Katika nafasi ya Kamati ya Uendeshaji Taifa Tanzania Bara, ilichukuliwa na Glory Mwambeleko na Asnail King, wakati upande wa Zanzibar, ilikwenda kwa Abdalah Haji Mgeni na Abdulatif Ramadhan Abdullah.
Source: Gazeti la Habari Leo
Tarehe: 30th December 2009
MKUTANO Mkuu wa Uchaguzi wa Chipukizi taifa umemchagua kwa kishindo mtoto wa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Jakaya Kikwete, Khalfani Kikwete (11) kuwa Mjumbe wa Baraza Kuu la Chipukizi Taifa Tanzania Bara.
Khalfani alipata kura 301 na kuwashinda wagombea wenzake 11. Kwa Tanzania Zanzibar, mshindi alikuwa Abdallah Haji Mgeni. Kutokana na ushindi huo Khalfani ataliwakilisha Baraza Kuu la Umoja wa Vijana (UVCCM).
Mtoto wa Katibu wa Fedha na Uchumi wa Taifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Amos Makala, Gabriel Makala (12), amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Chipukizi Taifa.
Gabriel alishinda kwa kupata kura 300 kati ya kura 357, aliwashinda wagombea wanane,kura saba ziliharibika.
Uchaguzi Mkuu huo wa Chipukizi Taifa uliofanyika mjini Morogoro ni wa vijana wadogo wa CCM kutoka katika mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar.
Nafasi ya Mkutano Mkuu wa UVCCM Taifa upande wa Tanzania Bara ilichukuliwa na Gladness Urassa na Ramadhani Guruwe,Tanzania Zanzibar ilichukuliwa na Elias Cassion.
Katika nafasi ya Kamati ya Uendeshaji Taifa Tanzania Bara, ilichukuliwa na Glory Mwambeleko na Asnail King, wakati upande wa Zanzibar, ilikwenda kwa Abdalah Haji Mgeni na Abdulatif Ramadhan Abdullah.
Source: Gazeti la Habari Leo