Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,484
- 30,160
Kwa kuwa imekuwa kawaida yake, Rais wetu Jakaya Kikwete, kulihutubia Taifa, kwa njia ya Televisheni na Redio, kila mwisho wa mwezi, kwa lengo la kutolea ufafanuzi masuala mazito yaliyolikumba Taifa katika kipindi cha mwezi mzima.
Natabiri kuwa hotuba ya mwisho wa mwezi huu, inaweza kuwa na wasikilizaji na watazamaji wengi, kuliko hotuba yoyote aliyowahi kuitoa Rais, tokea aina hiyo ya kuwasiliana na wananchi, alipoianza mwaka 2006! Nasema hotuba hiyo inasubiriwa kwa hamu na mamilioni ya wananchi kutokana na matukio makubwa yaliyojitokeza mwezi huu.
Ingawa yapo mambo mengi yaliyotokea, mimi nitayataja mawili ambayo nayaona yametawala vyombo vya habari mwezi huu. Suala la kwanza, ni kuuawa na polisi, kwa mwanahabari wa channel ten, mkoani Iringa. Ingawa suala hilo limetikisa vyombo vya habari vya ndani na nje ya nchi, na pamoja na Rais wetu huwa anakuwa mwepesi sana wa kutuma salaam za rambirambi, kwa misiba mbalimbali, lakini kilichowashangaza wananchi, ni namna alivyokaa kimya kabisa, bila kusema chochote, kwa jambo hilo zito, lillotokea.
Siamini kuwa katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi, ataamua kutoliongelea, hasa tukitilia maanani kuwa, kwa mazngira ya kifo cha Mwangosi kilivyotokea, kuna shinikizo kubwa kwa kutakiwa kuwajibishwa baadhi ya vigogo wa Polisi.
Suala la pili linahusu ripoti ambayo ilitolewa mwezi wa 6 mwaka huu na Benki kuu ya Uswisi kuwa wapo vigogo kadhaa, ambao wameficha kwenye nchi hiyo, pesa zinazofikia shilingi bilioni 315, kwa kuwa tokea itolewe taarifa hiyo, tulisikia kauli ya mkurugenzi wa Takukuru, akiahidi kulifuatilia suala hilo, na ikithibitika ni kweli wawafichue watu hao na kuwafikisha kwenye, vyombo vya sheria.
Tokea kipindi hicho, hatujasikia lolote, hadi majuzi, majina ya wale wanaosadikika kuficha mabilioni hayo, kuwekwa mtandaoni, na kwa kuwa miongoni ya hayo majina 30 yaliyotajwa, limo la JK na mwanae Ridhiwani, naamini Rais, ataona umuhimu wa kutoa ufafanuzi wa suala kubwa kama hilo.
Vile vile, kwa kuwa inafahamika hotuba za Rais, huwa zinaandaliwa na Mkurugenzi wa mawasiliano wa Ikulu, Salva Rweyemamu, ambaye naamini, anapita sana humu jamvini JF.
Naamini katika uandishi wa hotuba ya Rais, ya mwisho wa mwezi, hawezi kuacha kutolea ufafanuzi, masuala hayo mazito sana, yaliyolikumba Taifa letu, katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita. Wananchi tunaisubiri kwa hamu sana, hotuba ya mwisho wa mwezi
Natabiri kuwa hotuba ya mwisho wa mwezi huu, inaweza kuwa na wasikilizaji na watazamaji wengi, kuliko hotuba yoyote aliyowahi kuitoa Rais, tokea aina hiyo ya kuwasiliana na wananchi, alipoianza mwaka 2006! Nasema hotuba hiyo inasubiriwa kwa hamu na mamilioni ya wananchi kutokana na matukio makubwa yaliyojitokeza mwezi huu.
Ingawa yapo mambo mengi yaliyotokea, mimi nitayataja mawili ambayo nayaona yametawala vyombo vya habari mwezi huu. Suala la kwanza, ni kuuawa na polisi, kwa mwanahabari wa channel ten, mkoani Iringa. Ingawa suala hilo limetikisa vyombo vya habari vya ndani na nje ya nchi, na pamoja na Rais wetu huwa anakuwa mwepesi sana wa kutuma salaam za rambirambi, kwa misiba mbalimbali, lakini kilichowashangaza wananchi, ni namna alivyokaa kimya kabisa, bila kusema chochote, kwa jambo hilo zito, lillotokea.
Siamini kuwa katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi, ataamua kutoliongelea, hasa tukitilia maanani kuwa, kwa mazngira ya kifo cha Mwangosi kilivyotokea, kuna shinikizo kubwa kwa kutakiwa kuwajibishwa baadhi ya vigogo wa Polisi.
Suala la pili linahusu ripoti ambayo ilitolewa mwezi wa 6 mwaka huu na Benki kuu ya Uswisi kuwa wapo vigogo kadhaa, ambao wameficha kwenye nchi hiyo, pesa zinazofikia shilingi bilioni 315, kwa kuwa tokea itolewe taarifa hiyo, tulisikia kauli ya mkurugenzi wa Takukuru, akiahidi kulifuatilia suala hilo, na ikithibitika ni kweli wawafichue watu hao na kuwafikisha kwenye, vyombo vya sheria.
Tokea kipindi hicho, hatujasikia lolote, hadi majuzi, majina ya wale wanaosadikika kuficha mabilioni hayo, kuwekwa mtandaoni, na kwa kuwa miongoni ya hayo majina 30 yaliyotajwa, limo la JK na mwanae Ridhiwani, naamini Rais, ataona umuhimu wa kutoa ufafanuzi wa suala kubwa kama hilo.
Vile vile, kwa kuwa inafahamika hotuba za Rais, huwa zinaandaliwa na Mkurugenzi wa mawasiliano wa Ikulu, Salva Rweyemamu, ambaye naamini, anapita sana humu jamvini JF.
Naamini katika uandishi wa hotuba ya Rais, ya mwisho wa mwezi, hawezi kuacha kutolea ufafanuzi, masuala hayo mazito sana, yaliyolikumba Taifa letu, katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita. Wananchi tunaisubiri kwa hamu sana, hotuba ya mwisho wa mwezi