Elections 2010 Mteketa mbunge Kilombero

Regina,

Ngangamala hasa na hawa Vibaka wa Demokrasia maana Wenje angelala, ingekula kwake.

Nategemea Lisu atakuwa huko kwako maana nimepata habari kuwa Marando atatua Kigoma muda wowote.

Wanasheria wa Chadema na wengine watakaotaka kusaidia Demokrasia, kazi kwenu.

NGO zinazotetea wanawake, msimtupe mwenzenu jamani. Pia NGO za kila aina, msaada wenu wahitajika.

Atetewe au asaidiwe? kama mwanamke au kama mgombea. Kama issue ni uanamke hata viti maalum vipo!
 
Chagua unaloona linafaa kumsaidia na LIFANYE.

Kama una wazo jingine pia linakaribishwa. Lengo hapa si kushindana Lugha.

Atetewe, asaidiwe, ahurumiwe etc yote kwangu sawa tu. La muhimi ni HAKI ya dada yetu na Mtani wangu ISIPOTEE.

Wengine unafahamu tunaishi shamba huku Sikonge na Kiswahili kimetupigaga chenga Mwana wane.
Atetewe au asaidiwe? kama mwanamke au kama mgombea. Kama issue ni uanamke hata viti maalum vipo!
 
idadi ya wapiga kura walioandikishwa ilikuwa 211276 na idadi halisi ya waliopiga kura 88834 na kura halali zilikuwa 86574 na kura zilizokataliwa ni 2260.

Kikwete (ccm) 53386, rungwe hashim (nccr-mageuzi) 162, peter mziray (appt-maendeleo) 869, wilbroad slaa (chadema) 27721 , yahmi dovutwa (updp), ibrahim lipumba (cuf) 4200, mutamwega mgwaya(tlp) 117.

Matokeo ya ubunge

abdul mteketa(ccm)43459 regia mtema (chadema)38550, zainabu himili(4469), abdu mnola(updp)299.

Idadi ya walioandikishwa ilikuwa 211276,idadi halisi ya wapiga kura 88942,kura halali ni 86777 na kura zilizokataliwa ni 2165.

Hakukuwa na fujo ya aina yoyote ila regia mtema wa chadema amegoma kusaini fomu za matokeo.
mkuu atasainije wakati anauhakika ni mshindi?
 
Mimi bado sijaelewa ni nini kimechakachuliwa, upande wa makaratasi yakupigia kura - mabox, au figures katika fomu? je kila mgombea anazo fomu original?
 
Idadi ya wapiga kura walioandikishwa ilikuwa 211276 na idadi halisi ya waliopiga kura 88834 na kura halali zilikuwa 86574 na kura zilizokataliwa ni 2260.

KIKWETE (CCM) 53386, RUNGWE HASHIM (NCCR-MAGEUZI) 162, PETER MZIRAY (APPT-MAENDELEO) 869, WILBROAD SLAA (CHADEMA) 27721 , Yahmi Dovutwa (UPDP), Ibrahim Lipumba (CUF) 4200, Mutamwega Mgwaya(TLP) 117.

Matokeo ya Ubunge

Abdul Mteketa(CCM)43459 REGIA MTEMA (Chadema)38550, Zainabu Himili(4469), Abdu Mnola(UPDP)299.

Idadi ya walioandikishwa ilikuwa 211276,idadi halisi ya wapiga kura 88942,kura halali ni 86777 na kura zilizokataliwa ni 2165.

Hakukuwa na fujo ya aina yoyote ila REGIA MTEMA wa Chadema amegoma kusaini fomu za matokeo.

Kuna kitu sielewi hapa. Equation gani inatumika? Mbona havi-tally? Regia hesabu zimewapiga chenga nyie wote hapo kituoni?

Uwiano Maalum,
Hapo ndio ujue kwamba matokeo hayo yamechakachuliwa, tena na watu ambao sio smart kabisa. Katika hali ya kawaida unategemea idadi ya waliopiga kura za urais, ubunge na udiwani iwe sawa maana unapoingia kwenye election booth unapewa form zote tatu, tofauti itakuwa katika kura halali na zilizoharibika. Lakini hicho ulichohighlight hapo juu ni kwamba idadi ya watu waliopiga kura za urais ilikuwa ndogo kulinganisha na wale waliopiga za ubunge, which is VERY DOUBTFUL.....it can only explain the theory that there's additional of non-existing votes to make up the numbers.
 
Kifupi ni kwamba matokeo yamechakachuliwa.Matokeo halisi yalikuwa Abdu Mteketa-CCM Kura 42,000,Regia Mtema-CHADEMA Kura 43,200 CUF na UPDP Kura zao kwa pamoja hazizidi 3000.Kuna mambo mengi yaliyojitokeza lakini mwisho wa siku msimamizi wa uchaguzi amemtangaza bwana Mteketa kuwa mshindi kwa kura 43459,Mtema kura 38,550,CUF 4469 na UPDP 299.Sijakubali matokeo na sasa ndio tunafanya utaratibu ili kufungua kesi.

Ukiyakubali matokeo hayo, utakuwa msaliti wa jamii yako na wewe mwenyewe. USIKUBALI. Anzisha kesi na kesi yako itakuwa bonge la kampeini dhidi ya ufisadi wa CCM. Simama kidete kupigania haki na Mungu atasimama pamoja na wewe. Pole dada.

Wa Tanzania wenzangu, sasa nchi yetu imepotea mwelekeo, tangu watu walipoanza kujipa u-Dr wa bure, sasa wanataka kujipa u-Dictator na kuburuza nchi yetu. Naamini tunaweza kukataa, kwasababu kinachoendelea hakikubaliki kamwe.
 
Kifupi ni kwamba matokeo yamechakachuliwa.Matokeo halisi yalikuwa Abdu Mteketa-CCM Kura 42,000,Regia Mtema-CHADEMA Kura 43,200 CUF na UPDP Kura zao kwa pamoja hazizidi 3000.Kuna mambo mengi yaliyojitokeza lakini mwisho wa siku msimamizi wa uchaguzi amemtangaza bwana Mteketa kuwa mshindi kwa kura 43459,Mtema kura 38,550,CUF 4469 na UPDP 299.Sijakubali matokeo na sasa ndio tunafanya utaratibu ili kufungua kesi.

Naomba unishirikishe katika kesi hiyo nitatoa msaada wa kisheria kadiri nitakavyoweza. Nadhani unaweza ukaanza na Lissu kwani aliendesha kesi ya Dr. Slaa vizuri.Vilevile unaweze kumtumia Mzee Marando. Kwa mujibu wa sheria nadhani sasa una siku 30 si kama 14 za zamani kufungua kesi. Mimi nitasaidia pindi nitakapokuja na kuwa nyumbani. Tutawasiliane!
 
Kifupi ni kwamba matokeo yamechakachuliwa. Matokeo halisi yalikuwa Abdu Mteketa-CCM Kura 42,000; Regia Mtema-CHADEMA Kura 43,200 CUF na UPDP Kura zao kwa pamoja hazizidi 3,000.

Kuna mambo mengi yaliyojitokeza lakini mwisho wa siku msimamizi wa uchaguzi amemtangaza bwana Mteketa kuwa mshindi kwa kura 43,459, Mtema kura 38,550, CUF 4,469 na UPDP 299.

Sijakubali matokeo na sasa ndio tunafanya utaratibu ili kufungua kesi.
Pole sana kwa yanayokukuta, Mungu anaona. Hata hivyo, pamoja na kuchakachua, pamoja na kuonyesha kuwa umeshindwa, lakini mimi naona umeshinda kwa sababu kazi uliyoifanya ni kubwa na jasho ulilowatoa wenyewe wanajua kuwa wamekutana na chuma cha pua. Hongera sana
 
CCM 43159 NA CHADEMA 38550 AS AT 20:42HRS
ITV wameomba radhi kwa mkanganyiko uliotokea kupitia ITV na TBC nao wakaludia kuwa ITV wameomba radhi hasa baada ya msimizi wa uchaguzi kuwapigia ITV kutokana nafujo zilizoanza uko Kilombero
 
Back
Top Bottom