Semilong
JF-Expert Member
- Mar 5, 2009
- 1,712
- 219
classic! kuna watu wanataka tuamini tu bila hata kuhoji kuwa endapo tungefanya kila kitu ambacho IMF imetushauri kufanya tusingekuwa hapa tulipo. Well.. miaka 25 iliyopita tumefanya kila kitu ambacho WB, IMF, UNDP, UNICEF, ADB na wenzake wanayotaka tufanye je tunaweza kusema kweli hali yetu ni bora zaidi? Kufanya yote ambayo Mtei alishauri isingekuwa a panacea ya matatizo yetu kama taifa. Ingekuwa just that - tumefanya tuliyoambiwa na wakubwa kufanya hata kama hayakubaliani na misingi yetu kama taifa. Pamoja na heshima yangu yote niliyonayo kwa Mzee Mtei leo hii mapendekezo yake yamefanyiwa kazi kuanzia Mwinyi hadi Kikwete, ameridhika?
Moja ya mambo mtei aliyo mshauri Nyerere ni kuacha kusubsidize haya mashirika kama NMC. Kuyaacha haya mashirika yaendeshwe na watu binafsi.
Mifano ya leo ni kuwa baharesa na wauza chakula wengine wanafanya kazi vizuri tu..
Leo hii TZ breweries wamefungua kiwanda kingine mbeya, wakati wa enzi zile usambazaji wa bia tu ulikuwa unawashinda...
Kama hii sera ingetekelezwa kipindi kile viwanda vyetu vingi vingekuwa hai na vinauza mpaka nchi jirani, sasa hivi viwanda vyetu vingi vinapiagana market ya ndani.
Mabadiliko ni makubwa sana yaliyoletwa na hii sera ya ubinafsishaji sio kwa viwanda tu hata kwa bank zetu, productivity imeongezeka.