Elections 2010 Mtei amwonya Kikwete

- Wakuu samahani sana naomba kuuliza swali kidogo tu na linaweza kua nje ya mada, hivi kwa standard za ufisadi sasa hivi katika nchi yetu Tanzania, Mzee Mtei binafsi, hawi fisadi pia?

- I mean mali yote aliyonayo ambayo aliikusanya akiwa katika uongozi mbali mbali wa taifa letu, ni kweli haina ufisadi kabisaaa? Kama inayo anapata wapi moral authority ya kum-lecture rais wetu wa sasa kuhusu ufisadi wakati yeye ni mmoja wa waanzilishi wa ufisadi, kama sikosei katika taifa letu, au?

- Ninafahamu kwamba aliwahi kufanya kazi nje, lakini hivi mbona hata wakina Dk. Salim, waliwahi kufanya kazi nje lakini hawana mali za ajabu kama za huyu Mzee wetu muhasisi wa upinzani nchini?

- Ahsanteni Ndugu Zangu na Pasaka njema Sana.

William.

Hapana sio kila mtu mwenye mali ni fisadi; huyu ni shujaa, na ana-tofauti kubwa sana na wengine, kama hao ambao huganga njaa kama mzee wetu wa Glasgow.
1. Mtei-Pamoja na cheo chake kikubwa bila ya kujipendekeza kwa Mwalimu alitofautiana na siasa zake (za mwalimu) akaachia ngazi.
2. We understand that others have chosen "to sleep with the devil"; meaning; even if they hated that devil; kwao kuganga njaa ndiyo muhimu zaidi.
3. Huyu jamaa alichagua kuacha cheo na kufanya shughuli zake tangu mwaka 1979; and he was a high profile guy; another example was Justinian Rweyemamu who also diiffered.

We fikiria hawa wazee wetu wangepangana vizuri wawe wanatoa hekima zao kama huyu mzee wangekuwa wapi? Chukulia Mtei, Salim, Mwinyi, Mzee Wa Glasgow, Msuya, na wengine kama wangepangana na kuona "country first" hao mafisadi si wangeogopa?
 
nyerere si angemtafuna kama angekuwa na mali ya ufisadi
na wala hajawahi kukimbia nchi kama wakina cheyo
ameacha kazi sikunyingi na ameamua kuwa mjarisimali
acheni mawazo mgando na kudhania hela zinapatikana kwa njia za kifisadi tuuu...
 
- Mkuu mmoja huko juu unayedai Mtei ni shujaa vipi Balali naye au naye ni shujaa? Maana huyo mzee wako wa glas je ni fisadi naye kama Balali? si ungesema ukweli kwanza kuhusu Balali halafu ndio uzungumzie wanaolala na devil jinsi walivyoliibia taifa kama Balali au?

- Mnaotaka ushahidi vipi mkitoa ushahidi wa mafisadi mnaowadai ndani ya CCM?

- Eti Mtei ni shujaa?
 
W. J. Malecela,
Mkuu wangu, mbona unataka kutuchanganya akili hapa.. iweje Mzee Mtei awe ktk kundi la Mafisadi wakati mtu huyu aliacha hata madaraka ya kuitumikia serikali kwa sababu ambazo unaweza kusema ni Uchungu wa maslahi ya Taifa...madaraka ambayo ni wachache sana wangeweza kufikia maamuzi kama hayo kwani upo sehemu nyeti (ya fedha), unapata huduma zote bure pamoja na heshima kubwa ya Uheshimiwa..Wangapi wameweza kufanya hivyo ktk historia ya nchi yetu..

Hakika leo hii mimi naweza kumwita Mzee Mtei shujaa kwani aliweza kusimama kupinga Ujamaa wakati sisi sote tulimwona mchawi na angeweza kabisa kukaa kimya na kuendelea kuvuta mshahara mnono ktk mfumo usioweza kuendeleza nchi kiuchumi... At the end of all that - He was RIGHT!, leo hii tunambeza tena jamani!

Naweza kumwita Shujaa kwa sababu pamoja na upinzani wake wa mfumo wa Ujamaa ktk maswala ya Uchumi, Mtei hakuwa mpinzani wa itikadi nzima ya Ujamaa na hakuthubutu kutafuta njia za mkato kupata Umaarufu kama vile kujaribu kuipindua nchi..badala yake alikuwa mmoja kati ya waasisi wa vyama vya Upinzani nchini..

Mkuu, mafisadi ni watu wanaoliibia Taifa letu, Wahujumu wa Uchumi wetu, watu ambao wanatumia madaraka au mali za Taifa kwa faida zao binafsi..Ni waharibifu wa mipango yote ya maendeleo ya nchi yetu kwa faida zao binafsi au familia zao..

Mkuu, nadhani kati ya watu ambao wanastahiri heshima kubwa nchini huyu babu ni mmoja kati yao..Kuchuma fedha au utajiri wowote ambao hautokani na kuliibia Taifa letu hauwezi kuwekwa ktk fungu la Ufisadi..
 
Mwiba,
Acha uongo. At the time of his death Jamal hakuwa na mke. Alitunzwa na binti yake Canada alikofia. Acha uwongo ndugu yangu.
 
W. J. Malecela,
Mkuu wangu, mbona unataka kutuchanganya akili hapa.. iweje Mzee Mtei awe ktk kundi la Mafisadi wakati mtu huyu aliacha hata madaraka ya kuitumikia serikali kwa sababu ambazo unaweza kusema ni Uchungu wa maslahi ya Taifa...madaraka ambayo ni wachache sana wangeweza kufikia maamuzi kama hayo kwani upo sehemu nyeti (ya fedha), unapata huduma zote bure pamoja na heshima kubwa ya Uheshimiwa..Wangapi wameweza kufanya hivyo ktk historia ya nchi yetu..

Hakika leo hii mimi naweza kumwita Mzee Mtei shujaa kwani aliweza kusimama kupinga Ujamaa wakati sisi sote tulimwona mchawi na angeweza kabisa kukaa kimya na kuendelea kuvuta mshahara mnono ktk mfumo usioweza kuendeleza nchi kiuchumi... At the end of all that - He was RIGHT!, leo hii tunambeza tena jamani!

Naweza kumwita Shujaa kwa sababu pamoja na upinzani wake wa mfumo wa Ujamaa ktk maswala ya Uchumi, Mtei hakuwa mpinzani wa itikadi nzima ya Ujamaa na hakuthubutu kutafuta njia za mkato kupata Umaarufu kama vile kujaribu kuipindua nchi..badala yake alikuwa mmoja kati ya waasisi wa vyama vya Upinzani nchini..

Mkuu, mafisadi ni watu wanaoliibia Taifa letu, Wahujumu wa Uchumi wetu, watu ambao wanatumia madaraka au mali za Taifa kwa faida zao binafsi..Ni waharibifu wa mipango yote ya maendeleo ya nchi yetu kwa faida zao binafsi au familia zao..

Mkuu, nadhani kati ya watu ambao wanastahiri heshima kubwa nchini huyu babu ni mmoja kati yao..Kuchuma fedha au utajiri wowote ambao hautokani na kuliibia Taifa letu hauwezi kuwekwa ktk fungu la Ufisadi..


Kupinga Ujamaa. Mtei is my hero. Ujamaa sucks.
 
- Swali nililouliza ni very simple, amepata mali yaote aliyonayo? Kwani alipokuwa kiongozi wa serikali si alikuwa akifanya kazi na viongozi wengine ambao alistaafu nao na sasa ni masikini wa kutupwa?

- Wakuu naomba kusema hivi, jana nilipata bahati ya kuongea na Mkurugenzi mmoja ambaye hujadiliwa sana hapa JF, (niliongea naye off the record):- aliniuliza vipi Jamiiforums wanasemaje? Nikamjibu kama kawaida wanakata ishus, akasema kwamba ninawaheshimu sana wale maana hawana mchezo na pia hawamuonei mtu wale, hata iwe vipi watakupa haki yako tu lakini hawatakuhukumu kama huna makosa, na ukiona wote wanakubaliana kuwa wewe hufai, ujue basi wewe hufai, lakini ninawaheshimu sana kwa fairness.

- Ninasema hivi kwa wale ambao tuko serious na kujaribu kuyafichua maovu ya viongozi wetu ili yarekebishwe, ni lazima tuwe wakweli, tuache hii tabia ya kuangalia sura kwa sababu haiwezi kutusaidia lolote kwa taifa letu, hakuna atakayekubali kufa kwa uovu ambao anajua kua wenziwe wengi pia wanashiriki au waliwahi kushiriki, na hata huyo rais tunayemtaka asafishe uovu na yeye ataishia kuangalia sura ni ya nani kwanza kama sisi, matokeo hakitafanyika kitu.

- Unapotaka kuongelea kulala na devil, basi labda uanze na awamu ya kwanza kwa sababu sio siri tena kwamba hawa devils wametokea huko, sasa kufikiria kwamba unaweza kumchafua kiongozi asiyekuhusu bila ushahidi lakini ukamficha anayekuhusu na huku ushahidi wa wazi upo tele ni kujaribu kujidanganya na hata hapa JF huwezi kumdanganya mtu, ndio maana vita vya ufisadi ni vigumu sana kwa sababu kila mmoja wetu anajaribu kuangalia sura kwanza, mpaka siku atakapotokea kiongozi jasiri asiyeangalia sura ndio tutajisafisha na huu ufisadi ambao sasa umegeuka kuwa wimbo usio na ladha tena, maana sasa fisadi mmoja anampigia kengele mwingine kumbe na yeye ni fisadi kuliko hata yule mwingine.

Ni hayo tu ahsanteni.

William.
 
- Wakuu samahani sana naomba kuuliza swali kidogo tu na linaweza kua nje ya mada, hivi kwa standard za ufisadi sasa hivi katika nchi yetu Tanzania, Mzee Mtei binafsi, hawi fisadi pia?

- I mean mali yote aliyonayo ambayo aliikusanya akiwa katika uongozi mbali mbali wa taifa letu, ni kweli haina ufisadi kabisaaa? Kama inayo anapata wapi moral authority ya kum-lecture rais wetu wa sasa kuhusu ufisadi wakati yeye ni mmoja wa waanzilishi wa ufisadi, kama sikosei katika taifa letu, au?

- Ninafahamu kwamba aliwahi kufanya kazi nje, lakini hivi mbona hata wakina Dk. Salim, waliwahi kufanya kazi nje lakini hawana mali za ajabu kama za huyu Mzee wetu muhasisi wa upinzani nchini?

- Ahsanteni Ndugu Zangu na Pasaka njema Sana.

William.

Bwana William,

1) Ifuatilie historia ya Mzee Mtei, alianzia na kupitia wapi kufikia sasa.
2)Mwalimu angeweza kumkabithi usimamizi wa BOT au Wizara ya fedha, wakati Mzee Mtei mwenyewe hakuwa na uwezo hata wa kutunza kipato chake?
3)Aliyekudanganya kuwa SAS hana fedha ni nani. Kwa sababu hajichani kama wazee wengine mtaani haina maana ni masikini.
 
Bwana William,

1) Ifuatilie historia ya Mzee Mtei, alianzia na kupitia wapi kufikia sasa.
2)Mwalimu angeweza kumkabithi usimamizi wa BOT au Wizara ya fedha, wakati Mzee Mtei mwenyewe hakuwa na uwezo hata wa kutunza kipato chake?
3)Aliyekudanganya kuwa SAS hana fedha ni nani. Kwa sababu hajichani kama wazee wengine mtaani haina maana ni masikini.

- Mkuu hebu jaribu kuangalia sana na kwa makini swali langu kama linafanana na jibu lako, mbona unazunguka sana mimi sikuzunguka mkuu, wewe sema kwamba Mzee Mtei ni msafi na hana doa la ufisadi wala harufu, hayo mengine yote hayana sababu kama unaamini unachosema ni ukweli.

- Ninarudia hivi tukiendelea kuangalaiana usoni, basi tutaimba ufisadi mpaka mwisho wa dunia, DK. Salim angekwua na hela unzosema angeshinda urais 2005, moja ya sababu kubwa iliyomkosesha urais ni umasikini uliza wapambe wake Mzee Warioba, Butiku na Ndejembi watakuelimisha sana mkuu kuhusu hili.

Anyways, nimemaliza mkuu kila siku ninajaribu kua open, fair, na objective, kujali facts zaidi kuliko uwingi wa watu, kwa sababu mara ya mwisho Tanzania tulipolilia uwingi wa wengi, tuliishia kuchagua serikali ya sasa, kwa hiyo wingi sio sababu, ila ukweli tu ndio siku zote husimama, sasa tunapoona rais wetu ana sua sua na mafisadi, tusishangae maana history ya hapa JF iko wazi kwamba hata sisi pia tuna matatizo ya kujali sura kwanza, kabla ya kuangalia ufisadi, lakini tunategema viongozi wetu wawe tofauti.

Ahsante Sana Mkuu.

William.
 
Zakumi,
Mzee Mtei hakupinga Ujamaa waliopinga ni kina Kambona, he worked under Ujamaa (1977 -1979) kabla ya hapo gavana wa Benki kuu (1965 -1974)..Kujiuzuru kwake hakuhusiani kabisa na Siasa....it was a non political issue, hilo kwanza.

William J. Malecela,
Mkuu wangu vipi tena wewe unaelewa kabisa kuwa mkulu alikuwa Executive Director wa IMF kwa miaka minne akilipwa dollar ambayo ilikuwa dhahabu kwa kila mtu, unataka kulinganisha na viongozi wetu..Kuna mtu mwingine alokuwa naye huko majuu tena wakati ule ambaye leo ni maskini?..

Zaidi ya hapo wewe na mimi si tulikuwa wote tukisota enzi hizo imekuaje wewe ulianza makamuzi kabla yetu, wewe pia ulikuwa fisadi?.. maisha tu mkuu wangu umaskini wangu sii lazima uwe wako hata kama tunafanya kazi moja...Enzi zile ujanja kuwahi au sio!

Mzee Mtei ana kila sababu ya kufika hapo alipofika ukichukulia miaka ile alofanya kazi.. 4Yrs IMF tena wakati ambao nchi zote duniani zilikuwa ktk Depression, lazima utavuta kichizi na dollar ilivyokuwa ikithaminiwa Bongo, siwezi kabisa kumwondoa katika hesabu ya watu waliotajirika kwa nguvu zao...
Mkuu tafuta mwingine lakini sii mzee huyu!
 
- Then kila kiongozi bongo alitajirikia kwa nguvu zake, kwani Mh. Rostam hakuwa na hela kabla kuwa kiongozi wa CCM? Kwani Balali hakuwahi kuwa Director huko World Bank?

- Mkuu wangu si unaona tunaowapenda huwa tuna sababu nyingi sana za kuwakingia kifua, isipokuwa wale tu tusiowapenda ndio hawakuwahi kufanya kazi IMF na World Bank.

- Anyways, nimemamliza mkuu.

William.
 
W.J.Malecela,
Mkuu labda hatuelewani.. ni wewe uliyezungumzia Utajiri, ni wewe uliyeanza na kuuliza hizo fedha kazipata vipi?..Hivyo jibu lanfgu halihusiani na utajiri wowote ule isipokuwa Mtei alizipata vipi fedha zake, na kuwa nazo fedha hakuwezi kuondoa sababu ya Ufisadi kwani Mtei anaweza kuwa fisadi leo hii akiwa tajiri..
Mkuu ni vizuri tukaelewana hapo kwanza ili tusitoke nje ya mada..
 
W.J.Malecela,
Mkuu labda hatuelewani.. ni wewe uliyezungumzia Utajiri, ni wewe uliyeanza na kuuliza hizo fedha kazipata vipi?..Hivyo jibu lanfgu halihusiani na utajiri wowote ule isipokuwa Mtei alizipata vipi fedha zake, na kuwa nazo fedha hakuwezi kuondoa sababu ya Ufisadi kwani Mtei anaweza kuwa fisadi leo hii akiwa tajiri..
Mkuu ni vizuri tukaelewana hapo kwanza ili tusitoke nje ya mada..

Mkandara,
Kama ni utajiri Mtei si tajiri hata kidogo. He is well to do kwa standards za Tanzania na labda hapa Marekani tungesema ni "middle class." Nimefika nyumbani kwake pale nje ya Arusha. Ana shamba la kahawa, anafuga nguruwe na nyumba yake ni ya kawaida kabisa huwezi kumweka kwenye ligi ya akina Lowassa na Rostam hata siku moja. Kama anazo mali basi amezificha vizuri sana na katika age yake kama hawezi kufaidi mali basi kuna faida gani ya kuwa na mali?
 
- Mkuu mmoja huko juu unayedai Mtei ni shujaa vipi Balali naye au naye ni shujaa? Maana huyo mzee wako wa glas je ni fisadi naye kama Balali? si ungesema ukweli kwanza kuhusu Balali halafu ndio uzungumzie wanaolala na devil jinsi walivyoliibia taifa kama Balali au?

- Mnaotaka ushahidi vipi mkitoa ushahidi wa mafisadi mnaowadai ndani ya CCM?

- Eti Mtei ni shujaa?
Bahati mbaya Balali kafariki wakati wote hatujui what happened with the BOT money; hivi sielewi hata the cause of his death; you may guess! Lakini kitu kibaya kuliko vyote duniani is "to sleep with a devil"; meaning, unajua kabisa unasema uongo, lakini wewe unataka watu waelewe kuwa ni ukweli. Kama hawa wazee wetu tunaowaita Waasisi wangepangana vizuri hata ufisadi wa Balali tungejua ulitokanaje. Mjomba; kitu kibaya and vanity is why we sleep with the devils"; halafu unajua mtu ukisoma kama mzee wetu wa Glas inabidi uwe "country first"; siyo unakuwa haueleweki; je uko "country au upo kwa "mafisadi first" unajua hata uongo ukisemwa mara mia, wanaosikiliza mara mia watasema huu ni ukweli. Believe me mzee wetu lazima naye yumo kwenye "payroll".
 
Bahati mbaya Balali kafariki wakati wote hatujui what happened with the BOT money; hivi sielewi hata the cause of his death; you may guess! Lakini kitu kibaya kuliko vyote duniani is "to sleep with a devil"; meaning, unajua kabisa unasema uongo, lakini wewe unataka watu waelewe kuwa ni ukweli. Kama hawa wazee wetu tunaowaita Waasisi wangepangana vizuri hata ufisadi wa Balali tungejua ulitokanaje. Mjomba; kitu kibaya and vanity is why we sleep with the devils"; halafu unajua mtu ukisoma kama mzee wetu wa Glas inabidi uwe "country first"; siyo unakuwa haueleweki; je uko "country au upo kwa "mafisadi first" unajua hata uongo ukisemwa mara mia, wanaosikiliza mara mia watasema huu ni ukweli. Believe me mzee wetu lazima naye yumo kwenye "payroll".

- Tizama ulivyoikwepesha habari ya Balali, eti hujui kama aliiba au hakuiba, haya endelea kuwadanganya wananchi hapa,

- Waliolala na devil ni awamu ya kwanza ndugu yangu kina .......... hawa devils tulionao leo walianzia wapi? Sema ukweli mkuu kwa sababu wabongo sio mabwege tena!

FMES!
 
Ni Kingunge Mwizi

Asha

Kingunge, Ninavyokumbuka alisoma nchi za Eastern Europe

EDUCATIONS
School
- University Degree - - GRADUATE
- Philosophy Politics, History, Economics - - CERTIFICATE
- Sociology and Psychology - - CERTIFICATE
- Security Training - - CERTIFICATE

Nimetafuta kwenye mtandao Mtei naye amesoma Makelele BA....
 
au unakuta mzee anajenga haraka haraka wakati akiwa anataka kustaafu unashindwa kuwelewa kwa nini hakufanya hivyo siku zote

wazee wengi wamekufa sana baada ya kustaafu
jamani hii inasababishwa na kipato au watu kuwa boored na kutokujuwa wafanye nini ili mda uwende
au ni shock to the system ndio inawauwa
embu nisaidieni kimawazo kwa hili...

Hii nikutokana na life uncertainty kuwa kubwa, kwa maoni yangu hata watu wengine wasiopenda rushwa wanapokea au kutoa ili wapate certainty za maisha na hasa wakiangalia mifano ya wenzao maisha yalikuaje baada ya kutoka kwenye mfumo ambao unaweza kusaidia maisha ya from hands to mouth. Angalia wasomi wetu wengi kutokana na kupoteza muda mwingi kwenye masomo wengi walichelewa kuanzisha family na hivyo mtu anastaafu wakati watoto wako primary na ndo maana wanaendelea kuwa waoga kutoa maoni ya kujenga nchi hata pale ambapo wanakuwa guilty kwakufanya tofauti na taaluma zao. Wanajua wakifanya hivyo mwisho wasiku hawatopata contracts za kuendelea kusaidia familia zao. Its realy sad and paining, at the end of the day we all end up being helpless. Mfumo wa life after office ni moja ya vitu vya lazima kutazamwa upya katika ku ensure watu wanaopenda kutumikia taifa lao kwa moyo na pia ni prevention ya rushwa disease.

Hata wanasiasa bado uncertainty ni kubwa kwani kutokana na kukosekana kwa free competition kwenye uchaguzi average cost ya kuingia kwenye mchakato ni juu so hiyo tu inapunguza kwa kiasi kikubwa accumulation ambayo itamsaidia mtu kama akiamua kuachana na siasa kwa hiyo mimi nadhani ndo maana hata hao wanashindwa kuwa huru kutoa maoni kwani mwisho wa siku ataenda wapi? Therefore he/she ends up in the caught of prisoners dilemma even if they collectively decide to urgue against something kwa maslahi ya taifa. Zaidi ya hapo inakuwa mbaya kwani hata wenye power wanatumia kama fimbo ya kuwaadhibu wale wanaothubutu.

Hatuna sababu ya kushindwa kuhudumia wastaafu wetu kama tutaamua kutumia positively human resource yetu kwakuzingatia levels za education, un educated to provide manual labour under the good supervision ya learned. Nikosa watu kuwa judge vijana wanao kaa vijiweni eti kuwa ni wavivu wakati kazi ya job creation ni ya policy/government na si ya individual and that is the resource left un utilised. Well wachumi wanasema dependency ratio yetu nikubwa lakini bado hata ile iliyo available haijawa fully utilised and if it would life could have been better than it is now tuache tu ku cut na kupaste model za weupe ambao culture na setting zao ni quite different from what we have.
 
Back
Top Bottom