Msaada wa tyre nzuri za gari na bei nafuu

Akili Unazo!

JF-Expert Member
Feb 18, 2009
3,930
4,893
wakuu nisaidieni nahitaji kununua matyre ya gari langu lakini nimezunguka kwenye maduka kila nikiulizia naambiwa hili kiasi fulani ni china mara hili la india mara hili ni Vee Rubber.

jamani nisidie mwenye uzoefu wa hii kitu.
 
Nenda kwa Bin Slum tyre ana duka pale Livingstone karibu na bank ya NMB au anaduka jingine barabara ya Lumumba pale wanauza bei chee.
 
Nenda kwa Bin Slum tyre ana duka pale Livingstone karibu na bank ya NMB au anaduka jingine barabara ya Lumumba pale wanauza bei chee.

ushauri wako mzuri bwana Fidel80, lakini inaonekana jamaa keshapita huko kwenye maduka na akawa anapewa termz za matairi ambazo azifahamu sasa alikuwa anaomba msaada humu kwenye JF kama kuna mtu anajua hizo nterminology za mambo ya matairi na maana yake na tairi zipi ni nzuri na za bei npoa
bwana Chaku na mimi nipo interested kama wewe kwa hiyo ukipata info nzuri kwenye PM yako bac naomba unipe info pia
 
Matairi mazuri ni Michelini ingawa bei yake ni kubwa kidogo. Pia Dunlop ni mazuri ukipata ya kutoka Japan (tumenunua wiki kama 2 zilizopita mtaa wa Lumumba). Bei inategemea na ukubwa wa tairi. Kwa gari ndogo Dunlop ya Japan inauzwa kwa 160,000/=.
 
Baada ya kusoma nenda sasa kwa Bin slum pale Lumumba au Livingstone utapata tyre unayo taka kwa barabara zatu hizi.
 
Baada ya kusoma nenda sasa kwa Bin slum pale Lumumba au Livingstone utapata tyre unayo taka kwa barabara zatu hizi.

Kitu kingine kwa ufafanuzi hapa je ubora w Tyre unaujua kwa jina la mtengenezaji au bei tyre linalouzwa au ni kitu gani mbali na kujua taarifa muhimu hizo
 
Kitu kingine kwa ufafanuzi hapa je ubora w Tyre unaujua kwa jina la mtengenezaji au bei tyre linalouzwa au ni kitu gani mbali na kujua taarifa muhimu hizo

Ubora unauujua kwa jina la mtengenezaji kama Michelini ni tyre bora na bei yake ipo juu lakini ukinunua Ling Long ni la hali ya chini vivyo hivyo na bei yake ipo chini.
 
Jibu la hili linategemea mengi, cha kwanza na cha msingi ni bajeti yako. Chochote kizuri ni ghali mno na ukitaka Premium brands basi sharti uwe tayari kutokwa na fedha nyingi. Cha pili inategemea matumizi yako, je unataka matairi kwa matumizi ya namna gani? Porini, Lami tupu, mchanganyiko wa lami na barabara za pori kidogo etc. Kingine ni durability ila kwa matairi ya premium brands ni kawaida kulast atleast 40,000km ikiwa utayatunza ipasavyo.

Kama mdau wa juu alivyosema bei ya matairi hutegemea pia na size yake. Mwanzilishi wa thread ametoa taarifa chache mno mpaka inakuwa vigumu kumsaidia
 
Jibu la hili linategemea mengi, cha kwanza na cha msingi ni bajeti yako. Chochote kizuri ni ghali mno na ukitaka Premium brands basi sharti uwe tayari kutokwa na fedha nyingi. Cha pili inategemea matumizi yako, je unataka matairi kwa matumizi ya namna gani? Porini, Lami tupu, mchanganyiko wa lami na barabara za pori kidogo etc. Kingine ni durability ila kwa matairi ya premium brands ni kawaida kulast atleast 40,000km ikiwa utayatunza ipasavyo.

Kama mdau wa juu alivyosema bei ya matairi hutegemea pia na size yake. Mwanzilishi wa thread ametoa taarifa chache mno mpaka inakuwa vigumu kumsaidia

Asante kwa kuhitaji taarifa zaidi ya huu msaada niuombao.

Kwanza kabisa matumizi ya gari ni yakawaida tu wala siyo ya biashara na barabara ni mchanganyiko ila muda mwing ni lami huku barabara ndogo kukiwa nikuchache saana labda nikichukuwa vacation end of this year.

Kingine tyre nilikuwa nayo kwenye gari langu ilikuwa P215/85R15 lakini likawa linanisumbuwa wakati wakukata kona hivyo nataka nichukuwe either P215/70-75R15 au P195/70-75R15 au P205/70-75R15pia gari lenyewe ni suzuki escudo.

Kilichonitatizo ni hizi VEE RUBBER nimekuta bei ipo poa sana mpaka naziogopa na muuzaji anasema zimetoka Thailand kwingine nimeenda akaanza kuniambia masuala ya china na india ndo hapo nikazidi kwisha kabisa

Hopefu nimejitahidi kueleza kile kilichokuwa kinahitajika mkuu.
 
Kilichonitatizo ni hizi VEE RUBBER nimekuta bei ipo poa sana mpaka naziogopa na muuzaji anasema zimetoka Thailand kwingine nimeenda akaanza kuniambia masuala ya china na india ndo hapo nikazidi kwisha kabisa

Heheheh yeah hizo mama wahindi wanakupiga mchanga wa macho wanaleta feki wanadai zinatoka Thailand hapo mi naona bora ununue tu GT. Watakuja wataalamu zaidi.
 
Asante kwa kuhitaji taarifa zaidi ya huu msaada niuombao.

Kwanza kabisa matumizi ya gari ni yakawaida tu wala siyo ya biashara na barabara ni mchanganyiko ila muda mwing ni lami huku barabara ndogo kukiwa nikuchache saana labda nikichukuwa vacation end of this year.

Kingine tyre nilikuwa nayo kwenye gari langu ilikuwa P215/85R15 lakini likawa linanisumbuwa wakati wakukata kona hivyo nataka nichukuwe either P215/70-75R15 au P195/70-75R15 au P205/70-75R15pia gari lenyewe ni suzuki escudo.

Kilichonitatizo ni hizi VEE RUBBER nimekuta bei ipo poa sana mpaka naziogopa na muuzaji anasema zimetoka Thailand kwingine nimeenda akaanza kuniambia masuala ya china na india ndo hapo nikazidi kwisha kabisa

Hopefu nimejitahidi kueleza kile kilichokuwa kinahitajika mkuu.

Chaku, umetoa three contrasting tyre sizes ambazo tofauti yake ni kubwa sana kuanzia kwenye section width mpaka height. Jaribu kuangalia sticker katika mlango wa dereva wa gari lako ujue the right tyre size kwa gari lako, alternatively niambie ni la mwaka gani. From my own experiences kama stock size ni 205/70R15 then fitting 215/85R15 will rub the tyres immensely, I know this because a friend of mine got dupped by the dealers and ended up swapping her original 205/70R15 for 215/70 R15 and they rubbed like hell when going through bumps and at corners. Pia its worth noting kwamba your vehicle's drive geometry is calibrated in accordance to the stock size kwa hiyo ukibadilisha size ina maanisha ya kwamba both your speedometer na odometer zitakudanganya at some point.

I know that Michelin don't do size 205/70R15 atleast kwa Tanzania. Pirelli Scorpion ATRs are by far the best kwa size hiyo na unaweza kuapata kwa TSh. 230k per tyre. Goodyear Wrangler ATRs also have a good rep and should be marginally cheaper than the Pirellis.

Katika matairi ya China na India, you will be better off with Indian tyres, Appollo do the sizes quoted and should cost you about TSh 120k a tyre.

In addition either an All Terrain or All Season tyre should suit your use needs.
 
Last edited:
Aisee Chaku hakuna tairi low quality kama Vee rubber! yaan iogope sana, iyo ni tairi ya china. Ingawa kuna brand zingine za china ambazo zinadumu mfano GT Radial, SIAMTYRE na Goodride. Hizi zina uafadhali ukilinganisha na Vee rubber. Pia katika size unayotaka kubaidli mi nakushauri uweke 205 kwani ukiweka 195 na mwanzo ulikuwa umeweka 215 gari utaiona imeshuka chini kwa kiasi kikubwa, so nafkiri 205 itakuwa poa zaidi. kuhusu 70 au 75 unaweza chagua yoyote.
Pia kuhusu hizi tairi zenye majina mazuri kama Michelini, Dunlop na Goodyear, hakikisha unapata zilizotengenzwa katika nchi zenye kiwanda na sio under licence mfano Goodyear halisi zinatoka japan ila kuna zinzotengenezwa South Africa under licence na ubora wake kidogo sio kama za Japan.
 
Pirelli ni mazuri kwa upande wangu. kwa saizi hiyo pia ni bei chini kidogo kuliko michelin. wana wataalam na watakushauri, na kukupimia alignment bure baada ya kufunga. wapo junction ya Nyerere road na Kawawa ukivuka mataa kama unaenda Chang'ombe upande wa kulia unaingia servise road utawaona kushoto
 
Aisee Chaku hakuna tairi low quality kama Vee rubber! yaan iogope sana, iyo ni tairi ya china. Ingawa kuna brand zingine za china ambazo zinadumu mfano GT Radial, SIAMTYRE na Goodride.

Out of all the Chinese mish mash they call tyres, Goodride has been the one which has shown signs resembling a normal tyre. They are more than decent and for the usual prices TSh.80-90k are worth a shout. The ones I have seen have lasted for just over two and a half years (about 20-25,000 km).

Pia katika size unayotaka kubaidli mi nakushauri uweke 205 kwani ukiweka 195 na mwanzo ulikuwa umeweka 215 gari utaiona imeshuka chini kwa kiasi kikubwa, so nafkiri 205 itakuwa poa zaidi. kuhusu 70 au 75 unaweza chagua yoyote.

Tofauti ya 215mm na 195mm ni katika unene wa tairi na ni 20mm, sio kubwa sana. Ile namba ya katikati ni muhimu maana ni asilimia ya unene wa tairi ambayo ndio urefu wake. Kwa hiyo mtu mwenye tairi la 195/80 ana tairi refu kushinda wa 215/70.


Pia kuhusu hizi tairi zenye majina mazuri kama Michelini, Dunlop na Goodyear, hakikisha unapata zilizotengenzwa katika nchi zenye kiwanda na sio under licence mfano Goodyear halisi zinatoka japan ila kuna zinzotengenezwa South Africa under licence na ubora wake kidogo sio kama za Japan.

Hii sio sahihi, Goodyear ni kampuni ya Marekani hivyo by your logic matairi yake ni lazima yatoke Marekani? Nchi za wenzetu zina quality control ya products bwana na hivi ni viwanda ambavyo vinatumia technology za parent tyre companies hivyo kwenye ubora ni lazima uwe wa hali ya juu otherwise kuna legal and business repercussions. Pirelli nyingi hutengezwa Brazil na hupelekwa katika masoko mbalimbali.

Hata hivyo dada Chaku, sio vyote ving'aavyo ni dhahabu. Hizi Premium brands pia zinatofautiana kwa ubora. Mara nyingi top three yao ni Michelin, Pirelli, Goodyear in no order because different sizes perform differently. Firestone/Bridgestone are good too ila the tyre tech matters kwa hawa. Dunflops-- usiguse
 
za kichina, india etc ni nzuri kama si mtu wa safari ndefu (i mean kila mwezi unaenda mbeya au arusha) mh bora uwe na michelin, dunlop,bridgestone etc,tena uende kwa wauzaji ambao ni mawakala, the othrs wajua tena wachina wanaiga everything men.pia utunzaji wa tairi, check upepo kubalance,kagua mara kwa mara,jaza pressure sahihi, so hata three yrs. mimi nimekaa na western tyres(zitakuwa za india hizi) huu ni mwaka wa tatu, natumia nissan safari!!
 
'Old is gold' nimeona nitumie thread hii japo ni ya zamani kidogo lakini bado ina umuhimu. Natafuta ofisi za dealer wa tairi za Good Year kwa hapa Dar es Salaam. Nahisi kama tairi zao ni nzuri na huwa wanauza bei ya chini kidogo japo sina hakika sana na ubora wa tairi zao.
 
Mkuu nenda hapo victoria service station ni mpango mzima!mm naweka tuu chinese made,manake zenye majina siziwezi!
 
Mkuu tafadhali angalia kabla hujanunua tairi yeyote ni lazima ufahamu expiry date yake. Kwa kawaida matairi yeyote hata kama ni mapya na yana umri wa zaidi ya miaka minne (4) hayafai. Na pia unaweza kununua kama hujui matairi ambayo yamebakiza muda mfupi kuishi.
Tafutakwenye tairi nambayenye digit 4. Kwa mfano 3211-ina maana tairi hili limetengenezwa wikiya 32 ya mwaka 2011 n.k.

Vitu vingine vya kuangalia ni kama tairi ina spidi inayolingana na max ya gari yako. Angalia joto n.k.
Kla la heri.
 
'Old is gold' nimeona nitumie thread hii japo ni ya zamani kidogo lakini bado ina umuhimu. Natafuta ofisi za dealer wa tairi za Good Year kwa hapa Dar es Salaam. Nahisi kama tairi zao ni nzuri na huwa wanauza bei ya chini kidogo japo sina hakika sana na ubora wa tairi zao.
Nenda vungunguti opposite na YANA tyres.
Ukikosa, vuka uingie Yana wakupe substitute.
 
Back
Top Bottom