Msaada: Dozi ya Mseto imenikataa, nifanye nini kupunguza maudhi na kuzuia athari zaidi?

Melki the Storyteller

JF-Expert Member
May 3, 2022
5,701
9,779
Usiku ule ulikuwa ni wa kutisha sana. Binafsi niliwaza sana na kumwambia mke wangu, sijui kama patakucha nikiwa hai.

Basi bhana, maumivu ya kichwa yasiyo na kifani, maumivu ya misuli na mifupa, njaa kali, kichefu chefu, sensitivity ya ngozi kuongezeka, kukosa nguvu kabisa viliutawala mwili wangu. Palipokucha tu nikazama duka la dawa kuchukua Dawa tatu. Hadi kufikia saa kumi na mbili jioni, hali ilikuwa imetaradadi. Nikaona wacha nikapate vipimo. Baada ya kumuelezea yule daktari wa kike mwenye kihospitali chake cha mchongo, akanijibu eti tupime Malaria.

Nikajaribu kumfafanulia kuwa siku tatu zilizopita nilitumia dozi ya Malafin lakini aliishia kuniuliza "Unabishana na daktari?"

Basi bhana, akapima malaria, majibu yakatoka kuwa nina malaria wadudu watatu, kisha akatoa ushauri kuwa kwa kiwango cha malaria nilichonacho itabidi nitumie Mseto na Panadol nyingi zaidi iwezekanavyo. "Ndugu mgonjwa, kula chuma hicho," ni maneno ya mwisho ya yule daktari.

Usiku wa juzi nilianza rasmi matumizi ya vidonge hivyo vya mseto. Ngozi yote ilikufa ganzi, kichwa kikawaka kuliko maelezo, nikajihisi kutapika na nisitapike, maumivu ya misuli ya macho na homa juu, kushindwa kutembea, kuona mazigazi n.k

Nimesitisha dozi kwa kweli. Nifanye nini kuondokana na hizi reactions? Msaada tafadhari!
 
Kunywa maji mengi sana, Kula chakula, juice na pain killer Kila usikiapo vibaya utapona ndugu...

Pole sanaa
 
Ngozi yote ilikufa ganzi, kichwa kikawaka kuliko maelezo, nikajihisi kutapika na nisitapike, maumivu ya misuli ya macho na homa juu, kushindwa kutembea, kuona mazigazi n.k

Nimesitisha dozi kwa kweli. Nifanye nini kuondokana na hizi reactions? Msaada tafadhari!

Hizo ni side effects za mseto, ulivyoacha ndio umeharibu kabisa. Niliwahi meza mwaka 2008 mpaka leo sijarudia.

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Niliwahi kumeza Mseto, badala ya kupata nafuu nikashangaa naumwa zaidi, nikasitisha Dozi yake nikaamua kutumia Duo-cotexin..
 
Nikiumwa malaria huwa napona kwa Artesnate Injection. Madawa mengine yote yalishanikataa.
Enzi za utoto wangu niliwahi dungwa sindano ya Quinin. Sitosahau kwa kweli. Mguu wa kushoto ulicheza karibatano mferejini, almanusura nisombwe na maji

Hiyo Artesnate iko vipi? Unadungwa ngapi? Haina side effects?
 
dawa zote za sp ,malafin,oroda n.k ni supesho kwa kuwa kinga wamama wajawazito na maralia, kama allu imezingua nenda wakuchome allu ya sindano,quinine au artesunate for injection.

Pole kwa mgonjwa,

Asichome sindano:
Kwani hatujajua nadhira ni ya nini hasa.

A: Kama kweli madhira anayosema ni ya mseto(ALU). Maana hatujui kama kinachompatia shida ni A-Artemether au Lu- Lumefantrine.

Kama tatizo ni A-Artemeter, kuchoma hizo sindano (Artemether au Artesunate) ni kukaribisha madhira zaidi mwilini. Kama tatizo ni dawa inatakiwa asitumie tena jamii ya hiyo dawa.

B: Au tatizo ni malaria kali
Ukiwa na malaria kali, kitendo cha kuua malaria parasites/kutumia dawa huleta sumu zaidi mwilini kutokana na kupasuka/kufa kwa viumbe husika, mwili pia hutoa askari zaidi na hivyo hali kuwa tafrani.

Ndo maana wakati mwingine tunahitaji supportive measures kama rehydration/kuwekewa drip, dawa za kuchoma za maumivu, oksijeni nk.

Hii hutokana na Malaria huathiri karibu kila kiungo mwilini hivyo uangalifu huitajika sana hasa inapokuwa kali.

Hapo ndo uangalizi wa karibu kwani malaria hudhuru karibu kila kiungo mwilini hivo tiba hailengi kuondoa mdudu husika tu, bali kulinda viungo vya mwili pia dhidi ya athari hasi.

C: Anachotibu sicho
Kuna dengue in inazunguka na virusi vingine strong pia.

NB: Cha msingi ni kufika kituo cha afya ngazi ya juu zaidi afanyiwe vipimo zaidi na tafakuri njema.
 
Back
Top Bottom