Mpiga debe wa Kichina stendi ya Ubungo

jamani kama mtu anajua bei ya nauli ya mbeya ya hilo basi naomba maana natamani nijaribu kulipanda nione service zao
 
Hakuna ubaya mgeni yeyote kufanya biashara TZ kama amefuata sheria za nji hii, na analipa kodi, hata kama wanauza mchicha, wachina wako safi kuliko hata jirani zetu wababaishaji. Ni changamoto na kichocheo kwa sisi wabongo ambao bado tumelala fofofo.

Wabongo kazi yetu ni kukwepa kodi na uvivu tu,na kualalamika kila kukicha, uharibifu unaofanywa na waTZ ni mkubwa kuliko wanaofanya wageni.
 
Kama mlidhani Globalization lelemama basi mlikosea, Cha msingi ni kutafuta namna ya kusurvive na kujiletea maendeleo popote duniani. Mipaka ya kisiasa huko mbeleni itabaki kwenye ramani tu ila wanadamu watajichanganya tu. kwa sababu alichokifanya mchina huyo mpiga debe kinaweza kufanywa na Mzambia, Mganda, Mrundi na tusione ajabu sana lakini kwa sababu Mchina anaonekana na rangi kidogo tofauti na sisi basi tunaona ajabu kweli kweli.

Kiufupi ni kwamba Mchina kupiga debe ni kwa sababu amekuta Watanzania wanapiga debe na biashara zao zinatoka, angekuta Watanzania wanafanya booking online naye bila shaka angeanzia hapo kwa huduma zake. sasa iweje Mtanzania kupiga debe iwe sawa lakini mchina kupiga debe si sawa wakati wote wanagombania wateja walewale?.
 
Kama mlidhani Globalization lelemama basi mlikosea, Cha msingi ni kutafuta namna ya kusurvive na kujiletea maendeleo popote duniani. Mipaka ya kisiasa huko mbeleni itabaki kwenye ramani tu ila wanadamu watajichanganya tu. kwa sababu alichokifanya mchina huyo mpiga debe kinaweza kufanywa na Mzambia, Mganda, Mrundi na tusione ajabu sana lakini kwa sababu Mchina anaonekana na rangi kidogo tofauti na sisi basi tunaona ajabu kweli kweli.

Kiufupi ni kwamba Mchina kupiga debe ni kwa sababu amekuta Watanzania wanapiga debe na biashara zao zinatoka, angekuta Watanzania wanafanya booking online naye bila shaka angeanzia hapo kwa huduma zake. sasa iweje Mtanzania kupiga debe iwe sawa lakini mchina kupiga debe si sawa wakati wote wanagombania wateja walewale?.
Gamba,
Globalization maana yake siyo kufanya mambo kiholela tu. Ubaya wa Tanzania, hasa wizara ya mambo ya ndani ni ufisadi na hongo. Kuna watu wengi tu waliongia nchini kinyume cha sheria lakini kwa sababu ya hongo basi wanaongezewa muda na wengine visa zao kubadilishwa na kupewa haki ya kufanya kazi na biashara nchini.

Kuna jamaa wa Kilebanon aliniambia mdogo wake amenunua uraia na pasipoti ya Tanzania kwa dola alfu mbili. Hongo na ufisadi ndivyo vitakavyotuangamiza na wala si globalization.
 
Kiukweli huduma yao iko poa sana, mwendo c mbaya, na nauli mpaka mbeya nakumbuka kwa mara ya mwisho nilivyopanda ilikuwa sh 30,000 lakini ukiwabembeleza mpaka 25,000 wanakubali, na tunduma ni 32,000.
 
Kama alivyosema Gamba la Nyoka, yote haya ni globalisation, hata kama kuna makosa yanafanyika katika kutekeleza baadhi ya sheria.


Mtoa hoja kuna mambo matatu ya kufanya.

1. Aidha tufunge mipaka na kuwa hakuna kuingia wala kutoka au

2. tukubali kuwa dunia ni kama kijiji, kama umeidharau TZ kuna watu wanaona kuna opportunity, hivyo tuamke. au

3. Tukubali, waingie na tubadilike kuwa watumwa kama karne iliyopita!

Mind you, ili kuthibitisha kuwa wabongo bado tunafanya mambo holela, hawa wachina watapata wateja kuliko basi lolote lile, baadaye wataongeza mabasi na watatawala biashara, simply they care. si mambo ya kukata tiketi kiti kimoja watu wawili.

sio hapo tu kila sehemu na taasisi mbalimbali, if they do well, no problem, acha tutengeneze mfano wa USA maskini afrika, wanakuja kila kutoka kila kona. SISI HATUNA UZALENDO, VIONGOZI WATOTO WAO WAKO ULAYA, LA KAMA WAKO TZ, THEY STILL QUALIFYING TO WORK ANYWHERE IN THE WORLD.

Huku mna shule za kiswahili tupu, huku shule zingine kiingereza kitupu ndani ya taifa moja!

we have a lots to discuss kuhusu ishu ya utaifa au uzalendo, haipo no one care for the next generation!

this is matokeo kaka NA HILI TRAILER TU SUBIRI PICHA

yaani kama mwanamke, basi Tanzania ni bikra bado! kila mtu anaitolea mimacho huamini?? angalia;

madini, utalii, mapori ya rutuba, wafanyakazi cheap,viongozi wenye mawazo ya kitumwa na woga wa kijinga, umaskini, maji mengi, amani ya uongo iliyopo, wananchi hawana silaha mikononi, hali nzuri ya hewa,bahari, maziwa, samaki, sheria duni na za kikoloni, elimu ya kikoloni isiyowabadilisha watu, do i need to say more??? nchi zingine hutakuta opportunity kama hizi, mkuu hujajiuliza tu , Europe walikuja miaka ya 1800 kwa ajili ya kutafuta malighafi, mpaka leo hawajafa wanaishi na wako juu!

Kenya tu hapo wanatubembeleza tuoane, tunajiumauma tu
 
Last edited:
sioni shida kwa wanaokaa marekani kazi za kupiga box(sorry wenyewe wanaita"factory") na Nursing homes(sitaingia kwa undani) ni za kawaida kwa wabongo ndio Globalization hiyo tukilala usingizi watachukua mpaka Urais
 
Leo asubuhi nilikuwa nasindikiza wageni kuelekea bara (mkoani). Nikiwa ndani ya stendi ya mabasi ya Ubungo kiasi cha saa 11:15 (kumi na moja na robo alfajiri) nilikumbana na mpiga debe wa kichina akiniaambia 'lipo basi la Obama hapa linakwenda Mbeya hadi Tunduma" (lafudhi ya kihuuhii). Sikuamini ilibidi nisimame nihakikishe anayoyasema. Baada ya kudadisi nikaambia hao wachina (walikuwa watatu) unaowaona wanamiliki hilo basi (pembeni yetu) lenye rangi za bendera ya USA linalofanya safari zake Dar-Tunduma.

Jamani, hivi kweli mchina ananunua basi na anaajiri mpiga debe mchina, mkata tiketi mchina, vibari vya kufanya uhuni huu wanapata wapi?

Kweli mtanzania unaweza kwenda nchi za watu ukafanya hivi?

Tuwacheni fikra za kikoloni zilizokwisha pitwa na wakati wake hao wachina ikiwa wameruhusiwa kufanya kazi hapa nchinikihalali kwa nini wasifanye hivyo na kama baadhi yetu tunahisi kuwa jamaa wanapata basi tufanye hizo kazi wezetu wanangalia hatma ya maisha sisi wengi tunafikira starehe wapi nitapata beer na nyama choma jioni yaleo malengo hatuna starehe tumeweka mbele hata kazi zakipato cha chini wakifanya wageni tunakuwa haraka kulalamika sisi wenyewe hatupo tayari kuhangaikia kazi za aina hiyo Niliwahi kusoma katika Gazeti moja kati ya magazeti makubwa ya UK wakimnuku aliyekuwa kiongozi mmoja wa TZ kwa sasa amesha fariki Alitembelea shule moja hapa TZ na kumuliza mmoja kati ya wanafunzi atapenda kufanya kazi gani akimaliza masomo yule mtoto akasema kuwa atapenda kuwa awe muhudumu katika hoteli waiter yule kiongozi akawa hakufurahia
 
Hawa wako Ubungo, si muda mrefu tutawaona kwenye ofisi za ATCL, manake wako katika mazungumzo na Serikali ili wawekeze, watamiliki hisa 49% na Serikali 51%.

Tatizo si hawa jamaa kufanya biashara ya basi lao. Lakini jee tuna sera gani kulinda ajira za wazawa?, tunapoangalia Utandawazi (Globalization) lazima pia tuwe na sheria za kumlinda raia wa kawaida, ikumbukwe kama hatutakuwa na sheria za kutulinda, wenzetu wana mitaji hivyo wanaweza kuja kufanya ama kuchukua kila kitu.
 
Hawa wako Ubungo, si muda mrefu tutawaona kwenye ofisi za ATCL, manake wako katika mazungumzo na Serikali ili wawekeze, watamiliki hisa 49% na Serikali 51%.
Tatizo si hawa jamaa kufanya biashara ya basi lao. Lakini jee tuna sera gani kulinda ajira za wazawa?, tunapoangalia Utandawazi (Globalization) lazima pia tuwe na sheria za kumlinda raia wa kawaida, ikumbukwe kama hatutakuwa na sheria za kutulinda, wenzetu wana mitaji hivyo wanaweza kuja kufanya ama kuchukua kila kitu.

Naunga mkono, tatizo si kuwekeza kwenye mabasi ama ATCL. Lakini serikali ya CCM walivyolewa MADARAKA, ninaamini wanasubiri kupewa msaada wa wataalam kutoka China kutufundisha mafanikio ya China katika kulinda ajira za raia wao tokana na GLOBALISATION.

Halafu CCM hawana haja ya kuumiza kichwa sana ili kufanya kila kitu kiwe sawa TZ, maana wanauhakika wa kuunda serikali hata kama NEC YAO wangetuchagulia PAKA kua mgombea wa uraisi.
 
Hakuna ubaya mgeni yeyote kufanya biashara TZ kama amefuata sheria za nji hii, na analipa kodi, hata kama wanauza mchicha, wachina wako safi kuliko hata jirani zetu wababaishaji. Ni changamoto na kichocheo kwa sisi wabongo ambao bado tumelala fofofo. Wabongo kazi yetu ni kukwepa kodi na uvivu tu,na kualalamika kila kukicha, uharibifu unaofanywa na waTZ ni mkubwa kuliko wanaofanya wageni.

I salute you,

...Wabongo kazi yetu ni kukwepa kodi na uvivu tu ninaongezea na wizi...hebu angalia vibao vinavyoonesha alama za barabrani, wanakwiba...mapaa ya vituo vya basi, wanakwiba...mifuniko ya maji machafu, wanakwiba...wakipiga debe kwenye mabasi...wanaibia abiria. Wacha wachina wawaoneshe ni jinsi gani ya kufanya kazi.

Sioni sababu ya sisi wabongo kulalamika, kwani wachina wapo siku nyingi tu, mbona hatuhoji wakifungua Chinese Restaurants? Tunahitaji kujjifunza kutoka kwao ni namna gani tunaweza kufanya kazi kwa bidii, maarifa na UBUNIFU.
 
Tuache uoga wabongo huo ushindani utatufanya tufanye kazi kwa bidii na kwa makini,kama wamefikia kuwa na mabasi ya full AC na ni wasafi na madereva wao wako makini hakutakuwa na ajali za kizembe na makampuni ya wasauzi wanakuja tugangamale wabongo,leteni mabasi ya kisasa nk.tutawasapoti.
 
Chief naomba utufahamishe yafuatayo maana wewe umesha onja hiyo huduma yao:--
1. Nauli (kutoka DAR -MBY-TND) ukilinganisha na mabasi mengine (ya kiswahili - aka wazawa)
2. Mwendo wa Mabasi haya (ya wachina - aka wawekezaji)
3. Huduma (kuanzia, kupiga debe, kukata ticket, ndani ya basi, mizigo, kusimamisha abiria nk nk)
4. Vp yakifika kwenye mizani kuna abiria wanashushwa?
5. Je wanafuata ratiba waliyopangiwa ya kusafiri? (mda uliopangwa DAR-TDM unatumika vilivyo)
6. Vp kuhusu wateja....wanapata au wanapelaka basi tupu?



Baada ya kuyafahamu hayo basi tufanye kulinganisha na huduma za mabasi ya wawekezaji wazawa ambayo tunayajua vizuri. Baada ya hapo sasa tuendelee na kudiscuss je uwepo wao una manufaa?

Asante.

1. Nauli = Nililipa Shs 30,000
2. Mwendo = Yako fast kwa kweli ingawaje huwezi ku-feel. Nilikaa mbele na maximum speed as per the speedometer ni kms 140 kwa saa na jamaa alikuwa anafikisha hapo. Scania bus hazifui dafu kwenye tambarare. Engine: Ni Cummins kutoka USA. Drawback: Zina air suspension hivyo kwenye mashimo kidogo inabidi aende mwendo wa wastani kwani zinanepa sana.
3. Huduma = Nzuri. Reclining seats. Wanatoa free soft drinks. Hakuna kusimama. Kuna toilet ndani. Nilimtuma mtu kukata tiketi hivyo sijui huko kituoni.
4. Kuna kushushwa kwenye mizani/abiria kuletwa mbele ya basi kwani ina engine nyuma. Nafikiri huchukua mizigo mingi kweye buti.
5. Siwezi kusema kuhusu ratiba kwani sijui wanatakiwa kufika saaa ngapi.
6. Wateja = Nadhani wanapata ingawaje competition ni kubwa sana kwa mabasi ya Mbeya/Tunduma na ndio kwanza wameingia kwenye biashara. Angalau tulikuwa tumejaa kwenye basi.
 
Sasa kama sisi Watz tumelala- je wao wafanyeje?

Hapana aisee, hatujalala. Tumekuwa sidelined na serikali yetu tuliyoiweka madarakani kulinda maslahi yetu. Jambo hilo limeendelea siku nyingi na wasiwasi wangu ni kuwa linaweza kutufanya siku zijazo tugeuke kuwa kama Somalia.
 
Hapana aisee, hatujalala. Tumekuwa sidelined na serikali yetu tuliyoiweka madarakani kulinda maslahi yetu. Jambo hilo limeendelea siku nyingi na wasiwasi wangu ni kuwa linaweza kutufanya siku zijazo tugeuke kuwa kama Somalia.

I beg to differ with you, kwanini wakati wote tunajenga mawazo ya kuwa tegemezi kwa serikali? au sisi wenye mawazo ya utegemezi ndiyo kichocheo cha kuwafanya viongozi wetu na wenyewe wakati wote wafikirie misaada kutoka nje?

Hata hivyo ukweli itabidi tuusema mchana kweupe, wabongo hatufanyi kazi, tuko wavivu sana. hatuwezi kujenga nchi kwa kutegemea serikali ifanye kila kitu. Watu inabidi wawe wabunifu kuna mambo hayahitaji hata mkono wa serikali. Hivi tunahitaji mkono wa serikali katika kutoa huduma bora kwa wateja?

Tunahitaji mkono wa serikali kuwaondoa kiburi wanaotoa huduma? tunahitaji mkono wa serikali wa kutuambia tufanye kazi gani ya kujiingizia kipato?

Tuwe wa kweli, tuache maneno mengi, kuzunguka bila ya kutoa majibu, tujali muda na juu ya yote tuwe wabunifu.
 
Leo asubuhi nilikuwa nasindikiza wageni kuelekea bara (mkoani). Nikiwa ndani ya stendi ya mabasi ya Ubungo kiasi cha saa 11:15 (kumi na moja na robo alfajiri) nilikumbana na mpiga debe wa kichina akiniaambia 'lipo basi la Obama hapa linakwenda Mbeya hadi Tunduma" (lafudhi ya kihuuhii). Sikuamini ilibidi nisimame nihakikishe anayoyasema. Baada ya kudadisi nikaambia hao wachina (walikuwa watatu) unaowaona wanamiliki hilo basi (pembeni yetu) lenye rangi za bendera ya USA linalofanya safari zake Dar-Tunduma.

Jamani, hivi kweli mchina ananunua basi na anaajiri mpiga debe mchina, mkata tiketi mchina, vibari vya kufanya uhuni huu wanapata wapi?

Kweli mtanzania unaweza kwenda nchi za watu ukafanya hivi?

Mkuu ndo raha ya utandawazi hiyo.Wabongo wangapi wapo south wanapiga kiwi?
Wabongo wangapi wapo USA wanabeba box?Mbona wao hawalalamiki waache waje tu imradi hawavunji sheria za nchi tena mabus yao very luxury mazuri sana.
 
Mkuu ndo raha ya utandawazi hiyo.Wabongo wangapi wapo south wanapiga kiwi?
Wabongo wangapi wapo USA wanabeba box?Mbona wao hawalalamiki waache waje tu imradi hawavunji sheria za nchi tena mabus yao very luxury mazuri sana.


Kwa kuongezea...na ATCL wanachukua Wachina...hebu ngoja nianze kujifunza kichina mie!
 
Basi hilo ni zuri sana. Nilipanda kwenda Mbeya majuzi. Ni fully airconditioned (inafanya kazi), reclining seats (2X2) na toilet ndani.

If that is the case let them do kwani tumechoka kupanda maroli. Tujifunze kazi na kuheshimu kazi. Wachina wako kote Duniani wanafanya kazi sio utapeli.
 
1. Nauli = Nililipa Shs 30,000
2. Mwendo = Yako fast kwa kweli ingawaje huwezi ku-feel. Nilikaa mbele na maximum speed as per the speedometer ni kms 140 kwa saa na jamaa alikuwa anafikisha hapo. Scania bus hazifui dafu kwenye tambarare. Engine: Ni Cummins kutoka USA. Drawback: Zina air suspension hivyo kwenye mashimo kidogo inabidi aende mwendo wa wastani kwani zinanepa sana.
3. Huduma = Nzuri. Reclining seats. Wanatoa free soft drinks. Hakuna kusimama. Kuna toilet ndani. Nilimtuma mtu kukata tiketi hivyo sijui huko kituoni.
4. Kuna kushushwa kwenye mizani/abiria kuletwa mbele ya basi kwani ina engine nyuma. Nafikiri huchukua mizigo mingi kweye buti.5. Siwezi kusema kuhusu ratiba kwani sijui wanatakiwa kufika saaa ngapi.
6. Wateja = Nadhani wanapata ingawaje competition ni kubwa sana kwa mabasi ya Mbeya/Tunduma na ndio kwanza wameingia kwenye biashara. Angalau tulikuwa tumejaa kwenye basi.


1) Kms 140/hr against 80kms/hr for buses in TZ

2) Kushushwa kny mizani, why? basi linatakiwa litengenezwa kwa uwiano mzuri wa uzito hata kama engine itakuwa nyuma!

So hawa nao wanavunja sheria za barabarani!
 
Back
Top Bottom