Mpangaji mwenzangu amehama kisa shughuli zangu za kiuchumi zinamkera

Mlundilwa Jr

JF-Expert Member
Dec 11, 2019
2,897
4,314
Wakuu habari,

Mpangaji mwenzangu amehama kisa shughuli zangu zinazoniingizia kipato zinamkera.

Nikawaida kukuta kwenye hizi nyumba za kupanga kukuta watu wakifanya shughuli mbalimbali za kuwaingizia kipato ili maisha yaendelee na kuweza kulipa kodi.

kuna wengine ktk hizi nyumba za kupanga huwa wanakaanga samaki, wengine wanachoma vitumbua, wengine chapati wengine huuza ice cream ivyo yaani.

Sasa mimi kazi ninayofanya ninacheza na moto kwamaana hiyo kivyovyote moshi lazima uwepo sasa huu moshi ndiyo umekua tatizo kwa mpangaji mwenzangu na kupelekea kuhama nyumba.

Alipeleka malalamiko kwa mwenye nyumba ili nipewe notes nihame nakweli mama mwenye nyumba kwakua haishi pale aliamuru kodi ikiisha basi nifungashe virago niondoke.

Ila kuna kibanda najenga na sijakimaliza hivyo nikamuomba anivumilie hadi mwakani ili nikiondoka basi niende kwangu ingawa aligoma kupokea ombi langu, mimi nilichofanya nikamlipa kodi nyingine kwa kufosi ingawa alitaka kunirudishia ila walikaa kama familia wakakubaliana nikae hadi apo muda utakapo fika nihame.

Sasa mpangaji mwenzangu alivyosikia nimeongeza kodi, aisee leo naamka nakuta chumba kipo wazi hata kuniaga hajaniaga. Huyu kijana yeye ni mwalimu na anamke ukimuona ni Mpole ila ndani ni simba.

Hiyo ndiyo hali halisi wakuu, tujitahidi kupambana ili tuwe na kwetu lasivyo unaweza kuta unatolewa vyombo nje mchana kweupe kisa fulani ktk hiyo nyumba unamuharibia mazingira.
 
Kwanini usitafute aehemu maalum kwa ajili ya kufanyia shughuli zako? Maana hyo kero sidhani kama ungekuwa wewe ungeweza kuvumilia

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobil
Kuna ile busara unaweza kutumia kumwambia mpangaji mwenzio na sikwenda kwa mwenye nyumba kutoa malalamiko eti nipewe notes nihame na ukiangalia umenikuta ktk hiyo nyumba, mkuu maisha hayapo hivyo
 
Kwenye nyumba za kupanga hasa uswahilini huku, hakuna ambayo haina kero. Kikubwa ni kuchagua aina ya kero unayotaka kuishi nayo au tafuta pesa kapange Apartment.

Nimewahi kupanga nyumba, mpangaji mwenzangu hataki kuona mgeni anaingia kwangu. Akiingia tu ataanza vituko, visa ugomvi, maneno nyimbo na mapambio. Kiwango cha uswahili kwenye Nyumba kinapanda sana hadi mgeni ataondoka tu. Vikao kila siku. Cha ajabu alikuwa ni mlokole kongozi na mke wake masterminder wa fitna Muimbaji.

Ila hadi leo ni washkaji zangu.
 
Moshi tena dah nachuki mno.. tokea enzi zile za jiko la mchina la mafuta ya taa likizimwa kua mamoshi kanatokea kananuka hadi kifua kinauma... kuna vijalala vinachomwa moto mnaenda zenu shule ule moshi unawafuata nguo zote zinakuwa zinanuka moshi huku perfume ya cobra harufu yake yote inaisha dah kero mno
 
Huenda anafanya kazi serikalini, halafu mkuu unadhani moshi wenyewe moshi basi ila ndiyo hivyo walimwengu wakifanikiwa kuwa na level fulani ya maisha basi hujiona amefika wakati ukute huko kijijini kwao alikua analala kwenye zizi la ng'ombe
Hawa ndo wale kijijini kwao nyumba za miti zinaanguka na hawana choo wanalala kwa majirani....huku dar wanavaa nguo zao dada zao zinawabana mapaja....
 
Kuna ile busara unaweza kutumia kumwambia mpangaji mwenzio na sikwenda kwa mwenye nyumba kutoa malalamiko eti nipewe notes nihame na ukiangalia umenikuta ktk hiyo nyumba, mkuu maisha hayapo hivyo
Yeye hana mkataba na mpangaji ana mkataba na mwenye nyumba.

Wakati anataka kupanga hapo kuna makubaliano alikubaliana na mwenye nyumba na wewe huenda huyajui, sasa kakutana na mimoshi inayoua mapafu yake, hajui makubaliano yako wewe mzalisha mimoshi na mwenye nyumba ni yapi ila ana makubaliano yake na mwenye nyumba, Lazima amfate mwenye nyumba kujadili hilo si wewe, mwenye nyumba ndo akutafute wewe kama kuna ulazima, kama hakuna ulazima basi wataingia makubalino mapya ikiwemo kuondoka.
 
Wakuu habari
Mpangaji mwenzangu amehama kisa shughuli zangu zinazoniingizia kipato zinamkera

Nikawaida kukuta kwenye hizi nyumba za kupanga kukuta watu wakifanya shughuli mbalimbali za kuwaingizia kipato ili maisha yaendelee na kuweza kulipa kodi

kuna wengine ktk hizi nyumba za kupanga huwa wanakaanga samaki, wengine wanachoma vitumbua, wengine chapati wengine huuza ice cream ivyo yaani.

Sasa mimi kazi ninayofanya ninacheza na moto kwamaana hiyo kivyovyote moshi lazima uwepo sasa huu moshi ndiyo umekua tatizo kwa mpangaji mwenzangu na kupelekea kuhama nyumba.

Alipeleka malalamiko kwa mwenye nyumba ili nipewe notes nihame nakweli mama mwenye nyumba kwakua haishi pale aliamuru kodi ikiisha basi nifungashe virago niondoke

Ila kuna kibanda najenga na sijakimaliza hivyo nikamuomba anivumilie hadi mwakani ili nikiondoka basi niende kwangu ingawa aligoma kupokea ombi langu, mimi nilichofanya nikamlipa kodi nyingine kwa kufosi ingawa alitaka kunirudishia ila walikaa kama familia wakakubaliana nikae hadi apo muda utakapo fika nihame

Sasa mpangaji mwenzangu alivyosikia nimeongeza kodi, aisee leo naamka nakuta chumba kipo wazi hata kuniaga hajaniaga. Huyu kijana yeye ni mwalimu na anamke ukimuona ni Mpole ila ndani ni simba.

Hiyo ndiyo hali halisi wakuu, tujitahidi kupambana ili tuwe na kwetu lasivyo unaweza kuta unatolewa vyombo nje mchana kweupe kisa fulani ktk hiyo nyumba unamuharibia mazingira.
Kwa hiyo umekuja kumshtakia?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom