Moshi: Yanayojiri katika Kongamano la BAWACHA Siku ya Wanawake Duniani Machi 3, 2023; Rais Samia mgeni rasmi

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
Ni Asubuhi tulivu siku ya Jumatano tarehe 8 March ikiwa ni kilele Cha Siku ya Wanawake Duniani.

Macho na masikio ya Watanzania leo yanaelekezwa katika mji maarufu wa Moshi mkoani Kilimanjaro.

Chama kikuu Cha Chadema chenye wafuasi takribani Milioni 10 nchini kupitia Baraza lake la Wanawake Bawacha linafanya Kongamano kubwa la kuadhimisha siku hii ya Wanawake Kitaifa katika Ukumbi wa KURINGE.

Kinachovutia kwenye Kongamano hili la Bawacha mwaka huu ni mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ambaye atakuwa mgeni Rasmi kwenye Kongamano hilo.

Kukubali kwa Rais Samia Suluhu Hassan kuwa mgeni Rasmi kwenye Kongamano la Chadema kumevuta hisia za mamilioni ya Watanzania na hata Jamii ya Kimataifa.

Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe ndiye atakayekuwa mwenyeji wa Rais Samia na anatarajia kumpokea kuanzia saa 3 asubuhi.

Rais Samia kuhutubia Jukwaa moja na Chama kikuu Cha Upinzani Chadema kinaonyesha kilele Cha mafanikio ya Maridhiano ya kisiasa yaliyoasisiwa na Rais pamoja na Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe.

Rais Samia Suluhu Hassan amesikika mara kadhaa akitangaza hadharani kwamba wapinzani nchini siyo maadui wake tofauti na mtangulizi wake John Magufuli aliyejiapiza kuangamiza upinzani nchini na hatimaye kuuvuruga uchaguzi mkuu wa mwaka 2020

Mji wa Moshi ambao ni Kati ya ngome kuu za Chadema nchini umepambwa na bendera nyingi za chama hicho kikuu Cha Upinzani huku mazungumzo katika mikusanyiko mbalimbali ikiwa ni tukio hili la kihistoria.

Molemo Media tunatarajia kuwaletea mubashara matukio yote muhimu yatakayoendelea hapa ukumbini mjini Moshi kabla na wakati wa Kongamano hilo

Karibuni Sana

Mbowe Awasili Ukumbini
Mwenyekiti Freeman Mbowe anaingia hapa Ukumbini saa 5 kamili na kulakiwa kwa Shangwe kubwa hapa Ukumbini

Mwenyekiti Mbowe amewasili tayari kumlaki Mgeni Rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia Suluhu Awasili saa 5.10
Rais anawasili hapa kwenye viwanja vya Kuringe na kulakiwa kwa Shangwe kubwa na Wanawake wa Bawacha.Mwenyekiti Freeman Mbowe anamlaki na kumkaribisha kwa ajili ya tukio hili la kihistoria

Yanayoendelea Ukumbini
Zimeimbwa nyimbo tatu baada ya Rais kuingia Ukumbini umeanza wimbo wa Taifa, wimbo wa Afrika Mashariki na Wimbo wa Peoples Power

Viongozi wa dini wameongoza Dua ambao ni Askofu Mkuu wa KKKT na Sheikh wa mkoa wa Kilimanjaro

Zimefuata salaam za Bawacha mkoa zilizotolewa na Katibu wa Mkoa na pia Salam za mkoa kupitia mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu

Mbowe Ahutubia

Mwenyekiti Freeman Mbowe ameanza hotuba yake kwa kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kukubali mwaliko wa kuwa mgeni Rasmi kwenye Kongamano la Bawacha.

Mwenyekiti Mbowe ameeleza mbele ya Rais Samia kuhusu madhila mbalimbali ambayo wafuasi wa Upinzani waliyopitia katika awamu ya 5

Mbowe amemhakikishia Rais Samia kwamba Chadema itaendeleza Maridhiano kutokana na nia njema ya Rais.

Mwenyekiti Mbowe amemueleza Rais umuhimu wa Katiba Mpya na ulazima wa kuharakisha mchakato huo.

Mwenyekiti Mbowe amemalizia hotuba yake kwa kueleza kwa uchungu jinsi Serikali iliyopita kwa kushirikiana na waliokuwa Viongozi wa Bawacha kuhujumu chama hicho kwa kupeleka bungeni Wanawake 19 ambao hawakuwahi kuteuliwa na Chama hicho.Mbowe amesema katika hali ya kusikitisha Viongozi wa bunge nao walihusika na uharamia huo.Kiongozi huyo amemtaka Rais kutumia mamlaka yake kuwaondoa watu hao wanaojiita wabunge wa viti Maalum wasio na Chama kinyume kabisa na Katiba ya nchi.

Rais Samia Suluhu Hassan ahutubia Taifa

Rais Samia alipokaribishwa kuhutubia amewapongeza Sana akina mama wa Bawacha kwa kuandaa Kongamano kubwa na zuri linalovutia.

Pa Raia Samia amewashukuru Bawacha na Chadema kwa Ujumla kwa kumkaribisha kuwa mgeni Rasmi na kusema ni kitu ambacho hakutarajia

Rais Samia amesema ataendeleza maridhiano ya kisiasa kutokana na ukweli kwamba ndiyo njia pekee ya kuleta utengamano na kuleta Amani na utulivu nchini.

Rais Samia amesema mwanzoni hakueleweka ndani ya chama chake kutokana na kusimamia Maridhiano na hata Mpaka Sasa wapo wahafidhina wenye nia ya kukwamisha maridhiano

Kuhusu mchakato wa Katiba Mpya Rais Samia ameahidi siku siyo nyingi atatangaza kuundwa kwa Tume ya Rais itakayosimamia mchakato wa Katiba Mpya kwa mujibu wa Sheria.

Kuhusu wabunge wa viti Maalum waliopo bungeni kinyume na Katiba Rais Samia ameomba suala hilo liachwe mikononi mwa mahakama mpaka liishe kwa sababu itakuwa vigumu kwake kuingilia mhimili wa mahakama.

Mwisho Rais amemalizia kwa kuwashukuru tena Bawacha kwa heshima waliyompatia.
 
sisi washabiki wa vyama tunapaswa tutambue na tuelewe kuwa siasa sio uadui wala kuchukiana.

RAIS Dr. Samia ni Rais wa watanzania wote bila kujali unachama au huna
Hakika Rais anaonyesha demokrasia ya kweli kwa vitendo hivyo hatuna budi kufuata nyayo zake, haswa kwa viongozi wa vyama vya upinzani,
Ukionyeshwa wema tenda wema tuache unafiki.
 
Angekuwepo shwetaani wa afrika, ukumbi wangejazwa FFU wakiwa na mabom, mbwa, bunduki na washawasha.

lakn leo mama anaenda na kalamu na notibuku ili kuchukua changamoto za watanzania wenzake ambao ni wanachama wa chadema na anazitatua.

maRPC na OCDs watapeana mikono na makamanda wenzao wa heshima wa chadema badala ya kuwachota tanganyika jeki na kuwasukuma ndani.

MAMA TUNAOMBA MAOFISA WOTE WALIOKUWA WANATUMIWA NA SHETANI WA AFRIKA UWAKAMATE NA KUWASWEKA LUPANGO.
 
Haya maigizo ya SAA 100 bila katiba ya wananchi ya jaji Warioba ni Bure

SAA 100 akirudisha mchakato wa katiba mpya ya jaji warioba ndio nitamuona kweli yeye na CCM yake wamedhamilia kubadilika (maridhiano) zaidi ya hapo ni utapeli
 
Ikumbukwe kwamba katiba ya jaji warioba iliharibiwa na CCM kwa kutanguliza uchama, na SAA 100 anahusika sana kwa sababu alikuwa makamo mwenyekiti wa bunge la katiba
 
sisi washabiki wa vyama tunapaswa tutambue na tuelewe kuwa siasa sio uadui wala kuchukiana.

RAIS Dr. Samia ni Rais wa watanzania wote bila kujali unachama au huna
Hakika Rais anaonyesha demokrasia ya kweli kwa vitendo hivyo hatuna budi kufuata nyayo zake, haswa kwa viongozi wa vyama vya upinzani,
Ukionyeshwa wema tenda wema tuache unafiki.
Ndio imejulikana hivyo leo? Mbona enzi za Mkapa haikujulikana hivyo? Enzi za Kikwete naye hivyo hivyo? Enzi za Magufuli ndio kabisa aliwaona kama mashetani?

Tuache unafiki tatizo kuu la nchi hii wengine kuonekana kama third class since then ni CCM. Kauli na matendo yao yanadhihirisha hivyo pasi na shaka. Let's give Her Excellency the benefit of the doubt anyway!
 
Haya maigizo ya SAA 100 bila katiba ya wananchi ya jaji Warioba ni Bure

SAA 100 akirudisha mchakato wa katiba mpya ya jaji warioba ndio nitamuona kweli yeye na CCM yake wamedhamilia kubadilika (maridhiano) zaidi ya hapo ni utapeli
Umeongea kitu chenye nyama na afya ya milele, kama kweli wana nia njema katiba mpya ingeanza kwanza ili uwanja uwe sambamba kwa wote halafu maridhiano baadae, utafanyaje maridhiano huku mwenzio mgongoni kashika silaha ya kukuangamiza Kweli hapo utasema pana maridhiano?
 
Hayo ndio matokeo ya maridhiano, pale unapoambiwa na mwenzio siasa sio uadui, hapo mnaanza kukaribishana mpaka nyumbani, ajabu wanafiki wanataka hayo maridhiano yasihusishe ruzuku hata kama ipo kisheria, lakini yaguse pengine pote.
 
Ni Asubuhi tulivu siku ya Jumatano tarehe 8 March ikiwa ni kilele Cha Siku ya Wanawake Duniani.

Macho na masikio ya Watanzania leo yanaelekezwa katika mji maarufu wa Moshi mkoani Kilimanjaro.

Chama kikuu Cha Chadema chenye wafuasi takribani Milioni 10 nchini kupitia Baraza lake la Wanawake Bawacha linafanya Kongamano kubwa la kuadhimisha siku hii ya Wanawake Kitaifa katika Ukumbi wa KURINGE.

Kinachovutia kwenye Kongamano hili la Bawacha mwaka huu ni mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ambaye atakuwa mgeni Rasmi kwenye Kongamano hilo.

Kukubali kwa Rais Samia Suluhu Hassan kuwa mgeni Rasmi kwenye Kongamano la Chadema kumevuta hisia za mamilioni ya Watanzania na hata Jamii ya Kimataifa.

Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe ndiye atakayekuwa mwenyeji wa Rais Samia na anatarajia kumpokea kuanzia saa 3 asubuhi.

Rais Samia kuhutubia Jukwaa moja na Chama kikuu Cha Upinzani Chadema kinaonyesha kilele Cha mafanikio ya Maridhiano ya kisiasa yaliyoasisiwa na Rais pamoja na Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe.

Rais Samia Suluhu Hassan amesikika mara kadhaa akitangaza hadharani kwamba wapinzani nchini siyo maadui wake tofauti na mtangulizi wake John Magufuli aliyejiapiza kuangamiza upinzani nchini na hatimaye kuuvuruga uchaguzi mkuu wa mwaka 2020

Mji wa Moshi ambao ni Kati ya ngome kuu za Chadema nchini umepambwa na bendera nyingi za chama hicho kikuu Cha Upinzani huku mazungumzo katika mikusanyiko mbalimbali ikiwa ni tukio hili la kihistoria.

Molemo Media tunatarajia kuwaletea mubashara matukio yote muhimu yatakayoendelea hapa ukumbini mjini Moshi kabla na wakati wa Kongamano hilo

Karibuni Sana
Samia ningekuwa mume wake Leo ningempa staili zote,

Samia 5 tena!!!!!!
 
Hayo ndio matokeo ya maridhiano, pale unapoambiwa na mwenzio siasa sio uadui, hapo mnaanza kukaribishana mpaka nyumbani, ajabu wanafiki wanataka hayo maridhiano yasihusishe ruzuku hata kama ipo kisheria, lakini yaguse pengine pote.
Huyo ni Zitto na Sukuma Gang
Wana wivu na gubu hatari
 
IMG-20230308-WA0002.jpg
 
Haya maigizo ya SAA 100 bila katiba ya wananchi ya jaji Warioba ni Bure

SAA 100 akirudisha mchakato wa katiba mpya ya jaji warioba ndio nitamuona kweli yeye na CCM yake wamedhamilia kubadilika (maridhiano) zaidi ya hapo ni utapeli
Siyo mbaya Kwa hiki kidogo
 
Kukubali kwa Rais Samia Suluhu Hassan kuwa mgeni Rasmi kwenye Kongamano la Chadema kumevuta hisia za mamilioni ya Watanzania na hata Jamii ya Kimataifa.

Rais Samia kuhutubia Jukwaa moja na Chama kikuu Cha Upinzani Chadema kinaonyesha kilele Cha mafanikio ya Maridhiano ya kisiasa yaliyoasisiwa na Rais pamoja na Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe.

Karibuni Sana
Mkuu Molemo , asante kwa taarifa hii, leo macho na masikio yetu yote ni kwenye tukio hili.

P
 
sisi washabiki wa vyama tunapaswa tutambue na tuelewe kuwa siasa sio uadui wala kuchukiana.

RAIS Dr. Samia ni Rais wa watanzania wote bila kujali unachama au huna
Hakika Rais anaonyesha demokrasia ya kweli kwa vitendo hivyo hatuna budi kufuata nyayo zake, haswa kwa viongozi wa vyama vya upinzani,
Ukionyeshwa wema tenda wema tuache unafiki.

JPM aliharibu sana mtazamo wa kisiasa nchini, kwahilo alikosea sana.
 
Back
Top Bottom