duuuuuh!wana cdm mnapenda vibaya.
Tafadhali tufafanulie maana ya hilo neno nililoliwekea rangi nyekundu, sijawahi kulisikia na Kiswahili ni kipana.
Mijitu mingine bwana nawahi mahakamani mtu kashapigwa chini safari hakuna posho wala mshahara
kudadeki kama zamani tuu full njaaa na ilemela tumekata rufaa nahbari zilizopo Hihness atapigwa chini
chezea cc
Hali ya mambo ni nzuri watu hawana munkari kama ilivyotarajiwa hasa wale wa Chadema ndio wengi na wanaonyesha wana matumaini ya Ushindi,
Hukumui haijaanza kusomwa tunaelezwa itaanza mida ya saa 3 hivi,
Polisi kwa mida hii sio wengi sana kwa hesabu hawafiki 50. Kwa ujumla hali ni ya amani kabisa!
Tutawajuza hatua kwa hatua moja kwa moja toka ukumbini!
Updates:
- Basi aina ya coaster lililobeba mashabiki wa chadema ndio linaingia huku likishangiliwa na watu kwa alama ya vidole viwili alimaarufu Amani na Upendo!
- Naaaaam vijana wakazi (FFU) ndio wanaingia kwenye eneo la tukio wakiwa wamevalia kikazi yani kama Baghdad lakini wapo kwa usalama tu hakuna dalili ya vurugu yoyote hali ni yaamani tu!
- Kuna mabishano ya hapa na pale kati ya wananchi na wahudumu wa mahakama, watu wanalalamika kuwa mbona mda unakwenda na hawaruhusiwi kuingia mahakamani! Lakini wamefanikiwa kuwasihii na wananchi wametuliza munkali
- Tunaendelea kusubiri mda ufike tuanze kufuatilia kesi hii!
- Naaaaam tumeshaingia ukumbini tayari kuanza usikilizaji wa kesi hii uendelee! Tumeambiwa tuzime simu lakini MIMI sitazima mwanzo mwisho!
- Tunasubiri jaji aingie na jopo la mawakili wa pande zote wapo tayari!
UPDATES:
Kuna kichekesho kimejitokeza hapa, yani wakati wakuingia ukumbini kuna mbinu iliyotumika na mashabiki wa CDM kuwabana mlangoni wale wa Magamba na wakashindwa kupata siti kilichofuata ni afande kuwatoa nje, wakati wakitolewa nje kuna kuna mwanachadema mashuhuri akaingia ukumbini afande akataka kumuunganisha na wanachadema kutoka nje, unaambiwa ukumbi umelipuka na kusema huyo siti ipoo!
Naaaaaaaaaaam Mh Mnyika ndio anaingia ukumbini anashangiliwa kwa makofi na Pipooooooozi Pawaaaaaaaaaaaaaa!
Updates:
Wakili wa Mnyika ndugu Mbogolo ndio anaingia anasalimiana na mnyika waapiga picha wanaendelea kupiga picha!
Sasa kilichobaki ni kumsubiri jaji tu aingie ukumbini!
Updates:
Jambo la kufurahisha ktk kesi hii nikuwa Mh Mnyika na Hawa Ng'umbi wamekaa pamoja na wanapiga stori kweli, hata alipotokea afisa usalama akataka kuwatenganisha mnyika amemwambia haina tatizo watu pipoooooooooooz!
UPDATES:
M/Kiti wa CHADEMA na Kiongozi wa Upinzani Bungeni Mh Freeman Mbowe aka Sauti ya Zege ndio anaingia anashangiliwa ile mbaya pipooooooozi
UPDATES: Mpaka dakika hii saa nne kamili bado Jaji haja ingia ukumbini, tunaendelea kumsubiri!
UPDATES:
Naaaam jaji ameingia na hukumu inaanza rasmi,
Kwa watanzania wanaopenda maendeleo ya taifa hili john ameonesha ana upeo mkubwa sana bungeni, kusingekuwepo siasa mbovu za kuangaria uchama kwa pamoja tumeona bungeni john aliomba miongozo mingi pia aliomba marekebisho kwenye miswada mbalimbali kuliko mbunge yeyote.
aiseee.....kazi ipo hapo........mkuu usisumbue kichwa kutafsiri...wewe subiri ukuiona cdm wanashangili update.....Jaji anaomba radhi kuwa ataisoma hukumu kwa lugha ya kitumwa! Twendeleeee!
Wakiamuru kuzima simu, tafadhali yako usiizime, kuna mamilioni ya watu huku nje unatufanya tujione kama truko ndani ya mahakamaHaahaa ondoa shaka mkuu pamoja sana!
Dah! Wanasoma kwa kingereza wakuu ni nooma