Mlinzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Kaboom

JF-Expert Member
Nov 6, 2011
10,828
14,976
mlinzi.jpg

Mlinzi wa Rais wa Tanzania huwa anachaguliwa na rais mwenyewe au kuna utaratibu mwingine unatumika kumpata?

Je, Mlinzi huyu anakuwa na likizo? Kama hana likizo, Je, Anapataje muda wa kujamiiana (Socialize) na jamii inayomzunguka pamoja na masuala ya kifamilia?

Sijui unamananisha nini unaposema mlinzi wa Rais. Kama unamananisha yule Ofisa wa jeshi mwenye sare ambaye unamananisha siku zote huwa nyuma ya Rais basi yule siyo mlinzi.

Yule ni ADC ambaye shughuli yake ni kuwa karibu na Rais kwa mambo mbalimbali ya kijamii na kazi kwa Rais.

ADC anaweza kuwa kazi yake ni kubeba speech kwa Rais, kumsaidia kwa mambo mengine kama kuangalia kiti kimekaaje na kadhalika na kadhalika.

Kwa upande mwingine ADC ni symbolic gesture ya madaraka ya Rais. Na ukumbuke sio marais wote wana Ma-ADC. Ukichunguza kwa makini utaona si rais kumuona ADC kwa Rais wa Marekani.

Kwa upande wa walinzi wa kiukweli ni kuwa wao hawavai sare. Walinzi hao wako wengi ingawa ni kweli yuko mmoja au wawili ambao siku zote ndiye yuko karibu na Rais. Mlinzi huyo aliye karibu na Rais hawezi kuchaguliwa na Rais.

Kikosi cha ulinzi cha Rais ndicho kinamteua mlinzi huyo kutokana na vigezo mbalimbali of course vikiwemo vya ukakamavu, ujuzi wa mafunzo ya mapambano kama karate, loyalty kwa system na kwa rais, muonekane wake na kadhalika na kadhalika.

Sidhani kama Rais anaweza kuwa na mkono katika uteuzi wake ingawa inawezekana pengine baada ya muda Rais anaweza akasema kuwa abadilishiwe mlinzi kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za majungu na kadhalika.

ADC huteuliwa na Jeshi lakini inawezekana pengine Rais akawa na 'ushawishi' katika uteuzi wake. Hapa neno 'ushawishi' liko kwenye mabano kwa makusudi.

Inamananisha vikundi mbalimbali katika jamii ambavyo viko karibu na Rais vinaweza vikapenyeza jina la ADC. Lakini kwa nchi zinazozingatia mfumo mzuri wa utendaji wa kazi na kuacha pembeni masuala ya ubabaishaji si rahisi kwa ADC kuteuliwa kiushikaji.Kuhusu hali ikoje kwa Tanzania mimi sijui. Tafuteni wenyewe uteuzi unakuwaje.
 
Duh! hii nayo elimu nzuri. Watakuja wajuzi wa mambo haya aatujuze. Tena ngoja nii'subscribe topic hii.

Nijuavyo mimi(na naamini ni sahihi,watakuja kunikosoa wajuzi zaid), nikwamba, MLINZI huyo huchaguliwa na Rais kwani anapaswa kuwa anayejuana naye au mtu wa karibu sana mfano shemeji, mdogowake, ukoo wake na mengine kama hayo.

Nimeyasema hayo nikirejea hisia zangu kwamba, ni lazima nimchukue mtu ambaye ana'fall ktk categories hizo for my benefits.

Kwa upande mwingine, unaweza ukakuta mtu huyu anachaguliwa na system kwa maana ya Jopo au Kikosi cha ulinzi wa Rais.

Ni hayo tu.
 
Duh! hii nayo elimu nzuri. Watakuja wajuzi wa mambo haya aatujuze. Tena ngoja nii'subscribe topic hii.

Nijuavyo mimi(na naamini ni sahihi,watakuja kunikosoa wajuzi zaid), nikwamba, MLINZI huyo huchaguliwa na Rais kwani anapaswa kuwa anayejuana naye au mtu wa karibu sana mfano shemeji, mdogowake, ukoo wake na mengine kama hayo.

Nimeyasema hayo nikirejea hisia zangu kwamba, ni lazima nimchukue mtu ambaye ana'fall ktk categories hizo for my benefits.

Kwa upande mwingine, unaweza ukakuta mtu huyu anachaguliwa na system kwa maana ya Jopo au Kikosi cha ulinzi wa Rais.

Ni hayo tu.

Mkuu upo utaratibu wa kumpata msaidizi wa rais, lakini mara nyingi kwenye huo mchakato rais mwenyewe anahusishwa,mfano mpambe anaweza akaanza na rais mpaka anamaliza nae mihula yote miwili mfano mkapa,,,,,aliyeanza na kikwete alimpandisha cheo na kuwa gen,,,ikabidi abadiliswe, na huyo nikama msaidizi wanaomlinda rais ni wanausalama waliobobea na wako well trained na wanabeba silaha tena nzito sio raisi raia kuona hizo silaha,,,,,kutegemea na eneo rais alipo,,,na taarifa za inteligensia za wakati huo wanaweza wakawa wengi na hawavaagi uniform sana sana suti nyeusi au rangi nyingine,,,na wanasaidiwa na polisi ffu amao na wenyewe wana mafunzo maalum

mpambe wa rais sio lazima awe ni ndugu yake,,na anakuwaga na mapumziko kama ratiba ya boss wake ilivyo
 
Humu kweli na uwazi hakuna kupepesa macho
unapo kosea kukosolewa Dakika zero tuu hongereni
Ila turudi ktk hiyo Mada watu tujue mengi
 
yule jamaa sio mmoja , huwa wapo zaidi ya mmoja , na yule sio bodyguard bali ni mpambe tu.. jaribu kuangalia picha tofauti za mheshimiwa raisi , utaona kwamba yule jamaa huwa anakuwa tofauti

mpambe wa rais ni mmoja tu,aliyekuwepo awali alipandishwa cheo kuwa brigedia gen hivyo amerudi jeshini........wanaobadilika ni walinzi maana ni kundi la watu wengi kdg
 
Mimi wanaojiita wazee wa jf! na wanadai wakati huo walijadili mambo ya maana naomba wanijibu maswali yangu.

1, kwanza waniletee hizo link za maana ambazo zilipositiwa mwaka 2006 hadi 2011.

2, majadiliano yao mazuri yalisaidia nini? bona wao wezi wamaescrow walichanguliwa 2005 na 2010.

3, katika uchumi mbona nchi yetu ni masikini tu, pamoja na majadiliano yao mazuri?.
 
Mimi wanaojiita wazee wa jf! na wanadai wakati huo walijadili mambo ya maana naomba wanijibu maswali yangu.

1, kwanza waniletee hizo link za maana ambazo zilipositiwa mwaka 2006 hadi 2011.

2, majadiliano yao mazuri yalisaidia nini? bona wao wezi wamaescrow walichanguliwa 2005 na 2010.

3, katika uchumi mbona nchi yetu ni masikini tu, pamoja na majadiliano yao mazuri?.

Mkuu tayari upo nje ya mada! mtuhumiwa ameshaachiwa kwa dhamana! soma comment zote halafu uanzishe uzi wako!
 
mpambe wa rais ni mmoja tu,aliyekuwepo awali alipandishwa cheo kuwa brigedia gen hivyo amerudi jeshini........wanaobadilika ni walinzi maana ni kundi la watu wengi kdg

Haiwezekani akawa mmoja. Inamaana yeye haumwi? Hana dharura? Au akiwa na dharura ndio raisi siku hiyo atakuwa hana mpambe? Raisi ndio mmoja , ila wengine wote wanabadilika.. Nitajitahidi kukuletea picha
 
Safi sana...huwa napenda wanavofanya kazi zao kumlinda raisi mfano walinzi wa OBAMA makini sana....ila nafikiri msaidizi wa raisi yaani boardguard yaani anayevaa uniform na mara nyingi anakaa nyuma ya raisi huwa ni mmoja mda wote mpaka atakapostaafu au kupandishwa cheo mfano mzuri ni kikwete alipoanza uraisi alikua na mwingine na sasa ni mwingine...
 
Haiwezekani akawa mmoja. Inamaana yeye haumwi? Hana dharura? Au akiwa na dharura ndio raisi siku hiyo atakuwa hana mpambe? Raisi ndio mmoja , ila wengine wote wanabadilika.. Nitajitahidi kukuletea picha

Aisee........mi huwa najua ni yule yule..........na mbona huwa wanafanana.......?......kuna maumbo maalum........?
 
Aisee........mi huwa najua ni yule yule..........na mbona huwa wanafanana.......?......kuna maumbo maalum........?

Hapana huwa unaona wanafanana tu kwa sababu haukuzingatia sana na pia labda kwa sababu ya nguo wanazovaa labda.

Kuhusu maumbo ni lazima uwe na umbo flani , huwezi kuwa mpambe na ukawa andunje..

Nitawaletea picha zao zinazotofautiana.
 
Back
Top Bottom