Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,478
- 39,997
Hotuba ya Kikwete:
Hotuba ya Mkullo:
Hotuba ya Kikwete:
Hotuba ya Mkullo:
Hotuba ya Kikwete:
Hotuba ya Mkullo:
Hotuba ya Kikwete:
Hotuba ya Mkullo:
Hotuba ya Kikwete:
Hotuba ya Mkullo:
Swali:
Mifano hiyo inatosha kusema mtu kadesa?
Jumla ya misaada na mikopo ya bajeti (GBS) katika kipindi cha Julai 2008 hadi Machi 2009 ilikuwa TSh milioni 869,563 ambazo ni asilimia 107 ya makadirio ya TSh milioni 812,113 zinazotegemewa kwenye bajeti ya mwaka 2008/09.
Hotuba ya Mkullo:
Mheshimiwa Spika, jumla ya misaada na mikopo ya bajeti
(General Budget Support - GBS) katika kipindi cha Julai 2008 hadi
Machi, 2009 ilikuwa shilingi milioni 869,563 ambazo ni sawa na
asilimia 115 ya makadirio ya shilingi milioni 757,722 katika kipindi
hicho.
Hotuba ya Kikwete:
Hii inatokana na baadhi ya wafadhili kutoa fedha zaidi ya walizoahidi kwenye bajeti na kushuka kwa thamani ya shilingi ya Tanzania dhidi ya dola ya Marekani.
Hotuba ya Mkullo:
Hii inatokana na baadhi ya Wahisani kutoa misaada na mikopo
zaidi ya makadirio ya awali, pamoja na kushuka kwa thamani ya
sarafu yetu dhidi ya Dola ya Kimarekani ikilinganishwa na makadirio
ya awali.
Hotuba ya Kikwete:
Hata hivyo, misaada na mikopo kwa ajili ya miradi ya maendeleo (ikijumuisha Mfuko wa Basket) kwa kipindi cha Julai 2008 hadi Machi 2009 ilifikia TSh milioni 866,412 sawa na asilimia 56 tu ya makadirio kwa mwaka 2008/09.
Hotuba ya Mkullo:
Aidha, misaada na mikopo kwa ajili ya miradi ya maendeleo
(ikijumuisha Mifuko ya Kisekta - Basket Funds) kwa kipindi cha Julai
2008 hadi Machi 2009 ilifikia shilingi milioni 867,564 sawa na asilimia
59 ya makadirio kwa mwaka 2008/09.
Hotuba ya Kikwete:
Tathmini ya mwelekeo wa bajeti kwa miezi tisa ya mwaka 2008/09 inaonyesha kuwa malengo ya sera za mapato hayatafikiwa kama ilivyopangwa.
Hotuba ya Mkullo:
Mheshimiwa Spika, tathmini ya mwenendo wa bajeti kwa
miezi tisa ya mwaka 2008/09 inaonesha kuwa malengo ya sera za
mapato hayatofikiwa kama ilivyopangwa.
Hotuba ya Kikwete:
Mapato ya ndani yanategemewa kufikia TSh milioni 4,248,858 ikiwa ni asilimia 10 chini ya lengo la TSh milioni 4,728,595.
Hotuba ya Mkullo:
Mapato ya ndani yanategemewa kufikia shilingi milioni 4,248,858 (trilioni 4.2) ikiwa ni asilimia 90 ya lengo la shilingi milioni 4,728,595 (trilioni 4.7).
Swali:
Mifano hiyo inatosha kusema mtu kadesa?