Umuhirindahu
JF-Expert Member
- Feb 2, 2014
- 349
- 168
you are very right !!!Yote ya nini?? Kama amediriki kuchepuka basi ni dhahiri hathamini penzi lako wala utu wako.
Maradhi mengi siku hizi ya nini kuleteana vifo mapema. Mwenye asili yake haachi. Leo ka cheat na X kesho ata cheat na Y yote akijua adhabu itakuwa kununiwa na yeye atajinyong'onyesha na wewe utasamehe.
Pale ulipogundua kacheat ndipo palipaswa pawe ukomo wa ndoa yenyewe. Mpaka wewe kujua inamaanisha aidha aliamini sana 'ujanja' wake ama alitambua kuwa wewe ni mpumbavu kwake.
Niamini hata mkisameheana hutomuangalia kwa mtazamo ule ule tena kabla ya kumkamata, daima atakuwa msaliti kwako hivyo adhabu ni yenu wote.