Mke anataka watoto zaidi

Mwambie huyo mama asome gazeti la Mwananchi la leo -tarehe 22-2-2011, ukurasa wa 20. Kuna habari inasema WATAALAMU: DUNIA HAITAKALIKA IFIKAPO 2050.... Inaelezea madhara ya hususani nchi zinazoendelea kuongezeka kwa idadi ya watu na its implication to msosi, land implication, mazingira - climate change. Hivyo mwambie azae tu ila ajue....... ajiandae... japo of course by that time watakua washakua watu wazima......
 
Walee hao watatu tu!!Hiyo pesa ya kulea zaidi waweke akiba....siku mambo yakiwa mabaya hamna mtu atakae walelea watoto wanne na kuwapa maisha mazuri!!
 
umebahatika kupata mke kama uyo...sisi wengine kuzaa mwingine ni mbite, hadi ugomvi...sijui anaona panauma? mimi ningekubaliwa na mwenye kuzaa, ningeomba Mungu anipe watoto hata kumi na mbili, tena wa kiume ili ukoo uongezeke...lakini mke wangu, anaitaji kubembelezwa sana ili mwingine azaliwe...mara ohh anasingizia kulea kugumu, mara uchumi tukiwa na wengi utatetereka...sababu kibao...ningekuwa mchakachuaji ningesha enda kutafuta kama kumi hivi nje, lakini ni zambi si unajua tena.
 
high mortality rate ni mojawapo ya sababu inayowafanya waafrika wazae watoto wengi sasa jifanyeni kuzaa kimoja halafu ki.......
 
Ana watoto wa tatu mmoja std 3 wapili std1 watatu kindergarten. Anataka watoto zaidi kwani anadai haoni sababu ya kuwa na watoto wachache. Jamaa anasema mwanzoni alidhani ni utani lakini sasa hivi hii topic imekuwa too much. Kaniomba msaada ili ndoa yao iendelee kuwa na amani, kwani ana mpenda sana mke wake. Mimi nilipongea naye kiundani sana, lakini Nimeileta huku ili mnipe mawazo yenu.

...Tayari wana watoto watatu,...

Mke haoni sababu ya kuwa na watoto wachache.
Wangapi ni wachache kwake?

('huenda') Mume haoni sababu ya kuwa na watoto wengi.
Wangapi ni wengi kwake?

Wakishamaliza "PA-GA-ZI-JU-TO", wakubaliane namba muafaka kwao wote wawili
kulingana na uwezo wao kimaisha.
 
Asanteni wakuu kwa mawazo yenu. Mmenipa mwanga mkubwa saana wa kulishughulikia hili. First step na print hizi inputs zenu zote 2copies nawapelekea. Naongeza na ushauri wangu kidogo.. naamini itakuwa na impact fulani kwao.. na watafanya uamuzi ambao kila mmoja ataridhika Thanks alot
 
Asanteni wakuu kwa mawazo yenu. Mmenipa mwanga mkubwa saana wa kulishughulikia hili. First step na print hizi inputs zenu zote 2copies nawapelekea. Naongeza na ushauri wangu kidogo.. naamini itakuwa na impact fulani kwao.. na watafanya uamuzi ambao kila mmoja ataridhika Thanks alot

Nilidhani hili la mtizamo wa ukubwa wa familia linapaswa kuongelewa kabla ya ndoa yenyewe....kwangu mimi hii ni tofauti ya kimsingi ambayo ingefanya ndoa isiwepo!
 
Nilidhani hili la mtizamo wa ukubwa wa familia linapaswa kuongelewa kabla ya ndoa yenyewe....kwangu mimi hii ni tofauti ya kimsingi ambayo ingefanya ndoa isiwepo!

Misimamo mkuu, mambo yakiwa mazuri au mabaya watu wanabadilika. watu wanakua Controlled by environment..
 
Back
Top Bottom