Greatest Of All Time
JF-Expert Member
- Jan 1, 2017
- 20,722
- 45,128
Tukiwa tunaeleka derby ya kariakoo hapo kesho, sio mbaya tukakumbusha baadhi ya vituko, mikasa na visa vilivyowahi kutokea huko nyuma. Leo tuikumbuke mechi iliyowafanya Yanga (Gongowazi) kuchapa bakora na kupelekea kufukuza karibia wachezaji wake.
July 2, 1994 katika dimba la Uhuru, Dar Es Salaam. Kulifanyika mchezo kati ya Simba dhidi ya Yanga.
Ikumbukwe, Yanga alikuwa bingwa mtetezi wa Kombe la Klabu bingwa Afrika Mashariki (Sasa Kagame Cup)
walitwaa kombe hilo nchini Uganda mwaka mmoja uliopita. Yanga alikuwa na kikosi kizuri sana. Lakini pia katika mechi ya mzunguko wa kwanza, Yanga aliifunga Simba 2-0. Hivyo Simba waliingia kama underdog.
Kuelekea mechi ya derby, Yanga wakaanza kuvutana wenyewe kwa wenyewe. Kulikuwa na Yanga asili chini ya Marehemu Mzee Mengi na matajiri akina Gulamali na Yanga kampuni chini ya mwenyekiti Mpondela.
Katika maandalizi ya mechi hiyo, Timu ya Yanga ikatekwa na kundi la Yanga asili na kufichwa Kibaha mkoani Pwani. Hali iliyompelekea aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Augustine Liyatonga Mrema kutoa tamko Wachezaji warejeshwe Dar Es Salaam. Kweli siku ya 3 wakarejeshwa.
July 2, ikafika, uwanja ukiwa umefurika, mechi ikapigwa, mapema tu kipindi cha kwanza Costantine Kimanda na George Magere Masatu wanazifungia timu zao na kufanya matokeo kuwa 1-1 wakati wa mapumziko.
Kipindi cha pili, kukatokea mauaji ya sharubela, Mnyama mkubwa mwituni, Simba Sc akaonyesha ukubwa wake, wakaisasambua Yanga bila hiyana.
Magoli ya Athumani China, Madaraka Selemani na Dua Said yakaizamisha Yanga jumla ya 4-1.
Mashabiki wa Yanga wakakasirika, wakatoka mapema uwanjani moja kwa moja mpaka klabuni Jangwani.
Kulikuwa na tuhuma za wachezaji wa Yanga kuhujumu mechi hiyo, basi hapo ndipo Yanga walipotembezeana bakora mpaka kuitana gongowazi. Yaani mwenye fimbo, gongo, mti angeweza kuitumia kama silaha ili kuadhibu waliohujumu iwe kiongozi, mwanachama au mchezaji.
Baada ya kipigo hiko, Yanga aliwafukuza karibia wachezaji 18 wa kikosi cha kwanza na kubakiza wachezaji nane tu akiwemo beki nguli Costantine Kimanda (aliyepo Ubeleshi kwasasa)
Baadhi ya wachezaji, waliofukuzwa ambao walikuwa mastaa ni pamoja na Said Mwamba Kizota, Steven Nemes, Edibily Jonas Lunyamila nk.
Yanga wakapandisha wachezaji wa kikosi B ili kuziba nafasi za waliofukuzwa, baadhi ya waliopandishwa ni pamoja na Anwar Awadh, Maalim Saleh, Nonda Shaban Papii.
July 2, 1994 katika dimba la Uhuru, Dar Es Salaam. Kulifanyika mchezo kati ya Simba dhidi ya Yanga.
Ikumbukwe, Yanga alikuwa bingwa mtetezi wa Kombe la Klabu bingwa Afrika Mashariki (Sasa Kagame Cup)
walitwaa kombe hilo nchini Uganda mwaka mmoja uliopita. Yanga alikuwa na kikosi kizuri sana. Lakini pia katika mechi ya mzunguko wa kwanza, Yanga aliifunga Simba 2-0. Hivyo Simba waliingia kama underdog.
Kuelekea mechi ya derby, Yanga wakaanza kuvutana wenyewe kwa wenyewe. Kulikuwa na Yanga asili chini ya Marehemu Mzee Mengi na matajiri akina Gulamali na Yanga kampuni chini ya mwenyekiti Mpondela.
Katika maandalizi ya mechi hiyo, Timu ya Yanga ikatekwa na kundi la Yanga asili na kufichwa Kibaha mkoani Pwani. Hali iliyompelekea aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Augustine Liyatonga Mrema kutoa tamko Wachezaji warejeshwe Dar Es Salaam. Kweli siku ya 3 wakarejeshwa.
July 2, ikafika, uwanja ukiwa umefurika, mechi ikapigwa, mapema tu kipindi cha kwanza Costantine Kimanda na George Magere Masatu wanazifungia timu zao na kufanya matokeo kuwa 1-1 wakati wa mapumziko.
Kipindi cha pili, kukatokea mauaji ya sharubela, Mnyama mkubwa mwituni, Simba Sc akaonyesha ukubwa wake, wakaisasambua Yanga bila hiyana.
Magoli ya Athumani China, Madaraka Selemani na Dua Said yakaizamisha Yanga jumla ya 4-1.
Mashabiki wa Yanga wakakasirika, wakatoka mapema uwanjani moja kwa moja mpaka klabuni Jangwani.
Kulikuwa na tuhuma za wachezaji wa Yanga kuhujumu mechi hiyo, basi hapo ndipo Yanga walipotembezeana bakora mpaka kuitana gongowazi. Yaani mwenye fimbo, gongo, mti angeweza kuitumia kama silaha ili kuadhibu waliohujumu iwe kiongozi, mwanachama au mchezaji.
Baada ya kipigo hiko, Yanga aliwafukuza karibia wachezaji 18 wa kikosi cha kwanza na kubakiza wachezaji nane tu akiwemo beki nguli Costantine Kimanda (aliyepo Ubeleshi kwasasa)
Baadhi ya wachezaji, waliofukuzwa ambao walikuwa mastaa ni pamoja na Said Mwamba Kizota, Steven Nemes, Edibily Jonas Lunyamila nk.
Yanga wakapandisha wachezaji wa kikosi B ili kuziba nafasi za waliofukuzwa, baadhi ya waliopandishwa ni pamoja na Anwar Awadh, Maalim Saleh, Nonda Shaban Papii.