Mishahara ya wafanyakazi wa serikali iko wapi mwezi huu?

Tikerra

JF-Expert Member
Sep 3, 2008
1,702
146
Leo ni tarehe 30 July 2009,na hakuna dalili yeyote kwamba wafanyakazi wa serikali watapata mishahara yao.Mitaani tunasikia wafanyakazi wa serikali kuu wakiilalamikia serikali yao katika kiwango cha kutisha sana.

Tunacho hoji ni kwamba inakuwaje maagiza ya Rais yanakiukwa bila hata wafanyakazi husika kupewa taarifa yeyote?Itakumbukwa kwamba Rais alishaagiza ifikapo tarehe 23 ya kila mwezi wafanyakazi wawe wameshapata mishahara yao.Akaongeza kwamba kama itakuwa lazima kucheweshewa mishahara yao,basi isizidi tarehe 25 ya kila mwezi.

Ikumbukwe kwamba mishahara ya wafanyakazi wa serikali ni midogo mno,na kwa sababu hiyo wengi wao hawana njia nyingine yeyote ya kujipatia kipato.Kwahiyo wakicheleweshewa mishahara athari ina kuwa kubwa sana kwa wao wenyewe na wale wote wanao wategemea.

Tunaiomba serikali iwe makini zaidi katika swala hili ili kuwaepushia wafanyakazi usumbufu usio wa lazima.Tunaelewa fika kwamba kuna uzembe katika swala hili,kwa hiyo wale wote wanaochelewesha mishahara aidha kwa makusudi au kwa uzembe,wachukuliwe hatua kali za kinidhamu zinazostahili.

Mungu wabariki wafanyakazi wa Tanzania na naomba uwape nguvu ya kuendelea mbele hata katika mazingira yao magumu.
 
Leo ni tarehe 30 July 2009,na hakuna dalili yeyote kwamba wafanyakazi wa serikali watapata mishahara yao.Mitaani tunasikia wafanyakazi wa serikali kuu wakiilalamikia serikali yao katika kiwango cha kutisha sana.

Tunacho hoji ni kwamba inakuwaje maagiza ya Rais yanakiukwa bila hata wafanyakazi husika kupewa taarifa yeyote?Itakumbukwa kwamba Rais alishaagiza ifikapo tarehe 23 ya kila mwezi wafanyakazi wawe wameshapata mishahara yao.Akaongeza kwamba kama itakuwa lazima kucheweshewa mishahara yao,basi isizidi tarehe 25 ya kila mwezi.

Ikumbukwe kwamba mishahara ya wafanyakazi wa serikali ni midogo mno,na kwa sababu hiyo wengi wao hawana njia nyingine yeyote ya kujipatia kipato.Kwahiyo wakicheleweshewa mishahara athari ina kuwa kubwa sana kwa wao wenyewe na wale wote wanao wategemea.

Tunaiomba serikali iwe makini zaidi katika swala hili ili kuwaepushia wafanyakazi usumbufu usio wa lazima.Tunaelewa fika kwamba kuna uzembe katika swala hili,kwa hiyo wale wote wanaochelewesha mishahara aidha kwa makusudi au kwa uzembe,wachukuliwe hatua kali za kinidhamu zinazostahili.

Mungu wabariki wafanyakazi wa Tanzania na naomba uwape nguvu ya kuendelea mbele hata katika mazingira yao magumu.

Amen!
 
Na iwe kama ulivyoomba!
Lakini ni wazi kwamba kuna uzembe mkubwa sana mahali!
Kuna watu wanataka wajulikane kwamba wao ndo wao, na bila wao, hakuna linalowezekana!
Anyway, siku zao zinahesabika!
 
Siwaelewi wahasibu wa sector mbalimbali a serikali, hawa haswa ndio wenye shida kubwa! wanapenda kuonekana miungu watu, na ukiwaambia ukweli tu basi ni visa mtindo mmoja. unaweza kukaa miezi miwili huna mshahara, unaambiwa kuna tatizo hazina, sijui jia lako limekosewa wakati wa kulipeleka hazina.

lakini hilo ni moja tu, maboss wa hawa wahasibu nao hawafanyi chochote kuhakikisha wanawawajibisha. Na wahasibu wanafahamu hilo.

Hivi huu ndo utendaji utakaolipeleka taifa letu kule tutakapo?
 
Jamani ina maana hamjanote tu mbona karibia kila July huwa ni hivi? Si ndo mwisho sijui mwanzo wa mwaka wa fedha? huwa kuna mahesabu yao wanafanyaga (wajuzi watujuze).

Kosa huwa hawatutaarifu ili watu tujipange vizuri
 
Kila mwaka mwezi wa 7 wafanyakazi wa serikali mshahara huchelewa kutoka
 
Kila mwaka mwezi wa 7 wafanyakazi wa serikali mshahara huchelewa kutoka

Kwanini?

Bajeti ya Mshahara ya Wafanyakazi wa Serikali hupangwa hadi Juni? Au kuna jambo gani linalosababisha hii hali?

Wanaofahamu tafadhali (MwanaJ1) tunaomba sababu ya hii "trend"
 
Belo,

Hiyo "Avanta" vipi? Tevez keshahamia Man City. Au na wewe umebadilisha TIMU?
 
Kwanini?

Bajeti ya Mshahara ya Wafanyakazi wa Serikali hupangwa hadi Juni? Au kuna jambo gani linalosababisha hii hali?

Wanaofahamu tafadhali (MwanaJ1) tunaomba sababu ya hii "trend"

Kuna marekebisho hufanywa kwenye mishahara ya wafanyakazi wa serikali kila mwezi wa saba. Kwa kuwa ndio mwaka mpya wa fedha wafanyakazi huongezewa ngazi ndogo ya mshahara mfano toka TGA D1 kwenda TGS D2 na ndio maana mishahara inachelewa kwa ajili ya marekebisho hayo
 
Re: Mishahara ya wafanyakazi wa serikali iko wapi mwezi huu?

Quote:


Poleni sana




Kwani wewe unajiweka wapi, maana mfanyakazi akipata mshahara ndipo na mfanyabiashra anapata wateja, au wewe fisadi?

Hakika mimi nilisha ondoka huko Tanzania nipo ughaibuni ndio maana nawapa pole wenzangu.
 
Hakika mimi nilisha ondoka huko Tanzania nipo ughaibuni ndio maana nawapa pole wenzangu.

Mkuu matatizo hayakimbiwi, yanafanyiwa kazi!!! kaka, dada, wadogo zako n.k. bado watapata tabu hii tunayopata sisi..
 
wafanyakazi wa serikali si wanadai wao hawatumii mishahara wanakula poshos tu? au waongo? au ni wachache tuu?
 
Jamani mishahara huchelewa mwezi huu ni kwa sababu ya transition toka mwaka mmoja wa fedha kwenda mwingine.Ingawa kuna uzembe nao huwa unachangia kama wa kuongeza siku bze mishahara si inajulikana.
Unaweza kuta signatories wako bado Dodoma still wanajipongeza!!Hi ndio Tz bwana no hurry kabsaaa ukiwa na haraka nenda ulaya.
Businessmen wanalalamika mzunguko wa fedha umepwaya!!!!!!!!
 
...Itakumbukwa kwamba Rais alishaagiza ifikapo tarehe 23 ya kila mwezi wafanyakazi wawe wameshapata mishahara yao....
Hivi mshahara ukitolewa tarehe 23 hadi 23 mwezi ufuatao, NA ukitolewa tarehe 30 hadi 30 mwezi ufuatao, interval si inabaki ile ile ya mwezi mmoja? Wakati mwingine hizo ni kauli za kisiasa tu kuwapumbaza watu kwamba Serikali inawajali watumishi wake kwa kutoa mishahara mapema, wakati suala la msingi si kuwahi kutoa, bali kuongeza mishahara, kupunguza makato na kudhibiti mfumuko wa bei za bidhaa ili hela wanayoipata ifanye mambo makubwa yanayoonekana dhahiri.
 
Mkuu matatizo hayakimbiwi, yanafanyiwa kazi!!! kaka, dada, wadogo zako n.k. bado watapata tabu hii tunayopata sisi..

Limbani,

Sijakimbia matatizo bali nimarudi kwenye asli yangu.
 
wafanyakazi wa serikali si wanadai wao hawatumii mishahara wanakula poshos tu? au waongo? au ni wachache tuu?
wapo kweli wale wanaokula posho, tena posho inakuwa maradufu kwa mshahara. Hata mishahara yao kweli baadhi hawatumii. Ila kumbuka kuna wale wanaosubiri mshahara mwezi hadi mwezi ndio wapate kula yao na mahitaji mengine hao posho hawana. Hivyo ni wachache tu wapatao posho.
 
Mbona juzi tu ulikuwa unaripoti live matukio ya sherehe za Mwaka Kogwa huko Zanzibar ?
__________________
.

Labda ubainishe nilikuwa na ripoti wapi matukio hayo ya mwaka kogwa?
 
Back
Top Bottom