TIMING
JF-Expert Member
- Apr 12, 2008
- 24,893
- 11,290
This is exactly what is happening now, tunasikia shule hazina mashimo ya vyoo na hao wanakijiji na mabwana afya wa wilaya wanaruhusu watoto wanakwenda shule bila vyoo. Wakati hao hao watu wana pesa za kuzuia vipindupindu, wanazipeleka wapi? utawakuta wanakwenda kwenye restaurants na kukusanya rushwa badala ya kwenda kuweka mikakati watoto wakapata vyoo.
Mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni. Kikwete kawawekea mashule, basi hata mashimo ya vyoo mnashindwa? hata madawati? hata nyumba za walimu? mpaka aje Kikwete kuwahamasisha?
Wabunge kazi yao kutafuta waandishi wa habari na kwenda nao kutoa handouts ili waonekane wanafanya la maana. Sijaona hata mmoja akiwakusanya wananchi na kuwa nao bega kwa bega katika mikakati ya kujitengenezea mashimo ya vyoo wala madawati wala nyumba za walimu, utasikia kapeleka bati alizopewa na barick jimboni kwake. What a way.
Hakuna hata mbunge mmoja anaekuja na mkakati wa kusema ntazifanya shule zangu ziwe mfano wa kuigwa kwa kuwafanya wanachi wa jimbo langu waziendeshe kwa ufanisi mkubwa kabisa.
Kamanda you are very right
ila sasa mimi hili naligeuza kuwa baya la JK....
wewe ni rais, ukiamua wananchi wote watavaa uniform kwenda kazini na jumamosi watadeki barabara na mataulo!! Unafanya nini na hilo rungu ulilopewa??? unasafiri, unapunzika, unachekacheka, ukishaona pametulia unakuja mbio bila soni unaanza kusema "ile aisee, nilisaini kwa presha tu" au hawa jamaa balaa hawa, wamenichemsha kweli hadi nikaamua kwenda kusherehekea chama kule chini, au naskia kuna stafu kafiwa hapo chini, haijalishi ngoja na mimi niende msibani (bila kujua uwepo wako kwenye misiba mingine ni inconvenience kwa kila mtu, si ajabu hadi maiti yenyewe inapata shida kutokana na ulinzi na protocols
IF I HAD 24 HOURS, NINGEBEBA BAKORA YANGU NA KUHAKIKISHA WANANCHI, WATENDAJI, WANASIASA NA VIONGOZI WANATIMIZA WAJIBU... KWA SASA KILA MTU ANARELAX KWANI WANAJUA KIKINUKA, MKULU HUWA ANAPISHIA MBALI
Kwangu mimi mtu anayemchekea nyani na kuyavua mabua siwezi kumuita charming au mtu wa watu, ntasema huyo muuaji na ana lake jambo, killing while smilling!!