Michelle Obama: Ndoa haina usawa wa 50/50, lazima mmoja akubali kujitoa

MALCOM LUMUMBA

JF-Expert Member
Jul 26, 2012
20,897
63,784
Huyu ni mke wa Rais Mstaafu Barrack Obama!

Huyu ni mwanamke mweusi aliyewahi kushika nafasi kubwa zaidi kisiasa hapa duniani, THE FIRST LADY OF USA. Lakini, pia ni msomi ambaye alibahatika kusoma vyuo vikubwa duniani kama Harvard University na Princeton.

Ukimsikiliza kwenye mahojiano yake haya kuhusu maisha yake ya familia hasa ndoa na malezi, utafahamu fika kwamba huyu mama ana kitu cha ziada ambacho kizazi cha leo hatuna. Kwenye ndoa kasema kuna wakati utakuwa unafanya zaidi kuliko mwenzako, na kama hutakuwa makini unaweza kukata tamaa na kuacha ndoa. Lile la 50/50 huwa haliji ghafla tu kama ambavyo wengi tunajarajia.

Amesema kazi kwa mwanamke ni muhimu sana, lakini pia ni lazima mtu ajifunze kuweka uwiano baina ya maisha na kazi yake binafsi. Haya utayapata vizuri kuanzia dakika ya tano (5) uzuri ni kwamba, mahojiano hayo yamewekea vipande hivyo unaweza kuangalia ambacho amekisema.



Baada ya kumsikiliza, nisema tu kwamba mimi siyo shabiki wa Michelle lakini, ukweli ni kwamba Raisi Obama alihitaji mwanamke mwenye hulka na akili kama Michelle ili aweze kufika pale alipofika. Huyu mama ana kitu cha ziada, ndiyo maana hata MUNGU akamfanya kuwa FLOTUS.

She's ethical, humble, emotional stable and matured: Simply Phenomenal.....
 
Kibongo bongo wewe ukijitoa, mwenzako ndiyo anajitoa ufahamu kabisa🤣🤣.
Tatizo siyo bongo mkuu, duniani kote ukipata LIFE PARTNER ambaye hajielewi lazima utakumbana na matatizo. Japo, lazima tuseme ukweli ambao vijana wengi wa leo hasahasa wanawake hatupendi kuusikia ni kwamba hata kama utapata mtu sahihi, ndoa imejaa changamoto kibao hivyo ni lazima ujifunze kuwa mvumilivu.

Sasa kama huyu mama anasema yeye mwenyewe alihisi kabisa kuna wakati anafanya 70% huku Obama akiwa anafanya 30%, lakini bado akaendelea mbele. Nadhani kuna somo kubwa la kujifunza hapa mkuu.
 
Tatizo siyo bongo mkuu, duniani kote ukipata LIFE PARTNER ambaye hajielewi lazima utakumbana na matatizo. Japo, lazima tuseme ukweli ambao vijana wengi wa leo hasahasa wanawake hatupendi kuusikia ni kwamba hata kama utapata mtu sahihi, ndoa imejaa changamoto kibao hivyo ni lazima ujifunze kuwa mvumilivu.

Sasa kama huyu mama anasema yeye mwenyewe alihisi kabisa kuna wakati anafanya 70% huku Obama akiwa anafanya 30%, lakini bado akaendelea mbele. Nadhani kuna somo kubwa la kujifunza hapa mkuu.
Huyu nae Michelle anasema nn? 70% zipi hizo? Za kukaa kwa sofa na kutazama CNN?
 
Tatizo siyo bongo mkuu, duniani kote ukipata LIFE PARTNER ambaye hajielewi lazima utakumbana na matatizo. Japo, lazima tuseme ukweli ambao vijana wengi wa leo hasahasa wanawake hatupendi kuusikia ni kwamba hata kama utapata mtu sahihi, ndoa imejaa changamoto kibao hivyo ni lazima ujifunze kuwa mvumilivu.

Sasa kama huyu mama anasema yeye mwenyewe alihisi kabisa kuna wakati anafanya 70% huku Obama akiwa anafanya 30%, lakini bado akaendelea mbele. Nadhani kuna somo kubwa la kujifunza hapa mkuu.
Mwanamke wa kibongo ikifikia mahala ambapo anafanya 70% wewe uko 30% huo huo ndio unakuwa mwanzo wa dharau na kebehi hata kama awali mume alikuwa akifanya 100% mwenyewe, mpasuko wa familia unaanzaga humo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom