Wakuu,
Ndo tabu ya kujenga demokrasia kwenye nchi masikini kama Tanzania, sio kazi rahisi hasa mafanikio yakishaanza kuonekana au kupata mafanikio kidogo sana, taasisi zinazoijenga demokrasia hasa vyama vya siasa husambaratika. Vikipona kusambaratika huushia kwenye migogoro isiyokuwa na kichwa wala miguu na hivyo vyama husika hudumaa>
Nchini tumeshuhudia kudumaa kwa NCCR-Mageuzi, TLP na sasa CUF inakoelekea SIO KUFA kama wengi wanavyotabiri isipokuwa KUDUMAA baada ya wanachama wengi wenye tija kwa chama kukihama na kuanzisha vyama vingine au kujiunga na vyama vingine.
Tafiti ndani na nje ya nchi zinaonyesha kuwa mara nyingi vyama hivi hudumazwa na migogoro ya ndani ya Chama ambayo huibuka mara tu baada ya kuanza kupata mafanikio kidogo katika harakati zao (mifano mizuri kwa hapa nchini ni NCCR-Mageuzi na TLP na sasa CUF).
Sioni namna ambayo Chadema wanakwepa shimo hili, either sioni juhudi zozote za kumulika na kuliona shimo hili zinazofanywa na Chadema,chama ambacho kiukweli kingeweza kutegemewa kuwa Chama mbadala au mshindani wa dhati wa CCM.
Najua kwa asili ya JF iliyojinyonyoa manyoya nitatukanwa na kubezwa lakini, hoja yangu hii nitaitunza na nitaileta hapa siku mambo yakiana kwenda kama nnavyo au tunavyoyaona wachambuzi wa mambo ya sayansi ya siasa.
Ndo tabu ya kujenga demokrasia kwenye nchi masikini kama Tanzania, sio kazi rahisi hasa mafanikio yakishaanza kuonekana au kupata mafanikio kidogo sana, taasisi zinazoijenga demokrasia hasa vyama vya siasa husambaratika. Vikipona kusambaratika huushia kwenye migogoro isiyokuwa na kichwa wala miguu na hivyo vyama husika hudumaa>
Nchini tumeshuhudia kudumaa kwa NCCR-Mageuzi, TLP na sasa CUF inakoelekea SIO KUFA kama wengi wanavyotabiri isipokuwa KUDUMAA baada ya wanachama wengi wenye tija kwa chama kukihama na kuanzisha vyama vingine au kujiunga na vyama vingine.
Tafiti ndani na nje ya nchi zinaonyesha kuwa mara nyingi vyama hivi hudumazwa na migogoro ya ndani ya Chama ambayo huibuka mara tu baada ya kuanza kupata mafanikio kidogo katika harakati zao (mifano mizuri kwa hapa nchini ni NCCR-Mageuzi na TLP na sasa CUF).
Sioni namna ambayo Chadema wanakwepa shimo hili, either sioni juhudi zozote za kumulika na kuliona shimo hili zinazofanywa na Chadema,chama ambacho kiukweli kingeweza kutegemewa kuwa Chama mbadala au mshindani wa dhati wa CCM.
Najua kwa asili ya JF iliyojinyonyoa manyoya nitatukanwa na kubezwa lakini, hoja yangu hii nitaitunza na nitaileta hapa siku mambo yakiana kwenda kama nnavyo au tunavyoyaona wachambuzi wa mambo ya sayansi ya siasa.