mhhh! BAADA YA CUF ,SASA CHADEMA

zamwamwa

Member
Jun 16, 2011
46
10
Wakuu,
Ndo tabu ya kujenga demokrasia kwenye nchi masikini kama Tanzania, sio kazi rahisi hasa mafanikio yakishaanza kuonekana au kupata mafanikio kidogo sana, taasisi zinazoijenga demokrasia hasa vyama vya siasa husambaratika. Vikipona kusambaratika huushia kwenye migogoro isiyokuwa na kichwa wala miguu na hivyo vyama husika hudumaa>

Nchini tumeshuhudia kudumaa kwa NCCR-Mageuzi, TLP na sasa CUF inakoelekea SIO KUFA kama wengi wanavyotabiri isipokuwa KUDUMAA baada ya wanachama wengi wenye tija kwa chama kukihama na kuanzisha vyama vingine au kujiunga na vyama vingine.

Tafiti ndani na nje ya nchi zinaonyesha kuwa mara nyingi vyama hivi hudumazwa na migogoro ya ndani ya Chama ambayo huibuka mara tu baada ya kuanza kupata mafanikio kidogo katika harakati zao (mifano mizuri kwa hapa nchini ni NCCR-Mageuzi na TLP na sasa CUF).

Sioni namna ambayo Chadema wanakwepa shimo hili, either sioni juhudi zozote za kumulika na kuliona shimo hili zinazofanywa na Chadema,chama ambacho kiukweli kingeweza kutegemewa kuwa Chama mbadala au mshindani wa dhati wa CCM.

Najua kwa asili ya JF iliyojinyonyoa manyoya nitatukanwa na kubezwa lakini, hoja yangu hii nitaitunza na nitaileta hapa siku mambo yakiana kwenda kama nnavyo au tunavyoyaona wachambuzi wa mambo ya sayansi ya siasa.
 
kuna wimbo unasema mwombee adui yako aishi miaka mingi aweze kuona mafanikio yako.mahubiri ya kushidwa tushayazoea nakumbuka nilpokuwa najoin mech engneer watu walinivunja moyo nitadisko wapi wewe nimemaliza chuo bila hata supu
 
Wakuu,
Ndo tabu ya kujenga demokrasia kwenye nchi masikini kama Tanzania, sio kazi rahisi hasa mafanikio yakishaanza kuonekana au kupata mafanikio kidogo sana, taasisi zinazoijenga demokrasia hasa vyama vya siasa husambaratika. Vikipona kusambaratika huushia kwenye migogoro isiyokuwa na kichwa wala miguu na hivyo vyama husika hudumaa>

Nchini tumeshuhudia kudumaa kwa NCCR-Mageuzi, TLP na sasa CUF inakoelekea SIO KUFA kama wengi wanavyotabiri isipokuwa KUDUMAA baada ya wanachama wengi wenye tija kwa chama kukihama na kuanzisha vyama vingine au kujiunga na vyama vingine.

Tafiti ndani na nje ya nchi zinaonyesha kuwa mara nyingi vyama hivi hudumazwa na migogoro ya ndani ya Chama ambayo huibuka mara tu baada ya kuanza kupata mafanikio kidogo katika harakati zao (mifano mizuri kwa hapa nchini ni NCCR-Mageuzi na TLP na sasa CUF).

Sioni namna ambayo Chadema wanakwepa shimo hili, either sioni juhudi zozote za kumulika na kuliona shimo hili zinazofanywa na Chadema,chama ambacho kiukweli kingeweza kutegemewa kuwa Chama mbadala au mshindani wa dhati wa CCM.

Najua kwa asili ya JF iliyojinyonyoa manyoya nitatukanwa na kubezwa lakini, hoja yangu hii nitaitunza na nitaileta hapa siku mambo yakiana kwenda kama nnavyo au tunavyoyaona wachambuzi wa mambo ya sayansi ya siasa.

Unachosema ni sawa kabisa.Wewe kweli ni mpenzi wa demokrasia. Huo ni wosia mzito ulioutoa. Chadema waufanyie kazi. Sijui kama wanasoma posting za JF. CCM inasimama kwa vile kuna mkono kwenda kinywani, na sio mapenzi ya dhati. Chadema mnaweza kujenga msingi wa mapenzi ya kweli kwa sababu hamna dola sasa. Watu wnaipenda chadema kwa siasa safi na uongozi bora. Umenena jambo kubwa sana. Bravo!!!!!
 
Mimi pamoja na kuipenda Chadema lakini naamini mtoa mada yupo correct kabisa kabisa. Mara nyingi ubadhirifu, ubaguzi kwa misingi yote ya ubaguzi, ubabe na kukosekana uwazi vinapotokea na kushamiri kwenye chama kuna kundi linalojitokeza linaloachwa 'yatima' sasa kwakuwa CCM wana vyombo vya kumonitor external and internal progress ya vyama hivi kwao ni rahisi kuwa notified na kuweka mkakati wa kipropaganda na mamluki kukiua chama husika. So ni kweli inawezekana baada ya cuf ikafata chdm
 
Umejitahidi sana kueleza lakini napata taabu kidogo kwani hujaeleza nini unanakiona kwa mbali kama kingesababisha CHADEMA kudumaa japo kwa mifano tu

Kwa hapa unacho sema ni utabiri utokanao na unajimu au ramri aidha unapenda kuwa siku moja itokee hivyo na unaombea itokee hivyo ndiyo kisa cha kutunza kumbukumbu hii
Ungelikuwa msaada mzuri sana kwa CHADEMA kama ungelikuwa unaeleza wazi matatizo yaliyopo ndani ya chama ili kijirekebishe

tatizo matatizo au migogoro mnayo unda ni ya kufikirika tu mfano UKABIRA, UKANDA na sasa UDINI vyote hivi mna prove failure

Labda niseme wazi kuwa CHADEMA ni chama mbadala wa CCM ushahidi hata wewe unao practically na theoretically hata kama majina yanabadilika from CUF to ADC lakini bado CHADEMA inakubalika tu na ndiyo mkombozi wa kweli
 
Wakuu,
Ndo tabu ya kujenga demokrasia kwenye nchi masikini kama Tanzania, sio kazi rahisi hasa mafanikio yakishaanza kuonekana au kupata mafanikio kidogo sana, taasisi zinazoijenga demokrasia hasa vyama vya siasa husambaratika. Vikipona kusambaratika huushia kwenye migogoro isiyokuwa na kichwa wala miguu na hivyo vyama husika hudumaa>

Nchini tumeshuhudia kudumaa kwa NCCR-Mageuzi, TLP na sasa CUF inakoelekea SIO KUFA kama wengi wanavyotabiri isipokuwa KUDUMAA baada ya wanachama wengi wenye tija kwa chama kukihama na kuanzisha vyama vingine au kujiunga na vyama vingine.

Tafiti ndani na nje ya nchi zinaonyesha kuwa mara nyingi vyama hivi hudumazwa na migogoro ya ndani ya Chama ambayo huibuka mara tu baada ya kuanza kupata mafanikio kidogo katika harakati zao (mifano mizuri kwa hapa nchini ni NCCR-Mageuzi na TLP na sasa CUF).

Sioni namna ambayo Chadema wanakwepa shimo hili, either sioni juhudi zozote za kumulika na kuliona shimo hili zinazofanywa na Chadema,chama ambacho kiukweli kingeweza kutegemewa kuwa Chama mbadala au mshindani wa dhati wa CCM.

Najua kwa asili ya JF iliyojinyonyoa manyoya nitatukanwa na kubezwa lakini, hoja yangu hii nitaitunza na nitaileta hapa siku mambo yakiana kwenda kama nnavyo au tunavyoyaona wachambuzi wa mambo ya sayansi ya siasa.

Unaandika utumbo lakini unajua bila heading kuweka neno CDM hakuna atakayeifungua thread yako
 
CDM iko chini ya uongozi imara sana kwa sasa, we bakia na ndoto yako lakini CDM kumeguka sio leo.

After all CDM kwa sasa inaMEGA wengine. Tumeona aliyejiengua ubunge wa CCM Meru alimegukia CDM na hata makundi ya CCM yanayogombea madaraka yatamegukia CDM. Kumbuka hata akina Sitta walikuwa na option ya kuhamia CDM au kuunda CCJ but roho za usaliti na unafiki zikawazidi

Unayetamani CDM kumeguka utasubiri sana, sawa na Fisi kumfuata nyuma nyuma mlevi akidhania mikono ya mlevi itadondoka. CDM ina MEGA CCM
 
Umejitahidi sana kueleza lakini napata taabu kidogo kwani hujaeleza nini unanakiona kwa mbali kama kingesababisha CHADEMA kudumaa japo kwa mifano tu

Kwa hapa unacho sema ni utabiri utokanao na unajimu au ramri aidha unapenda kuwa siku moja itokee hivyo na unaombea itokee hivyo ndiyo kisa cha kutunza kumbukumbu hii
Ungelikuwa msaada mzuri sana kwa CHADEMA kama ungelikuwa unaeleza wazi matatizo yaliyopo ndani ya chama ili kijirekebishe

tatizo matatizo au migogoro mnayo unda ni ya kufikirika tu mfano UKABIRA, UKANDA na sasa UDINI vyote hivi mna prove failure

Labda niseme wazi kuwa CHADEMA ni chama mbadala wa CCM ushahidi hata wewe unao practically na theoretically hata kama majina yanabadilika from CUF to ADC lakini bado CHADEMA inakubalika tu na ndiyo mkombozi wa kweli

Mkuu usijisumbue huyu ni kibaraka namba moja wa Magamba
 
CDM iko chini ya uongozi imara sana kwa sasa, we bakia na ndoto yako lakini CDM kumeguka sio leo.

After all CDM kwa sasa inaMEGA wengine. Tumeona aliyejiengua ubunge wa CCM Meru alimegukia CDM na hata makundi ya CCM yanayogombea madaraka yatamegukia CDM. Kumbuka hata akina Sitta walikuwa na option ya kuhamia CDM au kuunda CCJ but roho za usaliti na unafiki zikawazidi

Unayetamani CDM kumeguka utasubiri sana, sawa na Fisi kumfuata nyuma nyuma mlevi akidhania mikono ya mlevi itadondoka. CDM ina MEGA CCM

Safi sana mkuu wangu.Umempa live huyu magamba asiye na haya
 
Mimi pamoja na kuipenda Chadema lakini naamini mtoa mada yupo correct kabisa kabisa. Mara nyingi ubadhirifu, ubaguzi kwa misingi yote ya ubaguzi, ubabe na kukosekana uwazi vinapotokea na kushamiri kwenye chama kuna kundi linalojitokeza linaloachwa 'yatima' sasa kwakuwa CCM wana vyombo vya kumonitor external and internal progress ya vyama hivi kwao ni rahisi kuwa notified na kuweka mkakati wa kipropaganda na mamluki kukiua chama husika. So ni kweli inawezekana baada ya cuf ikafata chdm

Nimetafakari kwa kina na nikagundua kumbe kweli yawezekana yakatukumba kama yaliyo wakumba CUF! Kwani inabidi CDM wawe makini katika kupokea mamluki na kuwapa nyazifa na dhamana kubwa ndani ya chama kabla ya kuwachunguza kiundani! Mfano mzuri ni yule jamaa aliyejitoa CCM baada ya kukosa kura kwenye kinyang'anyilo cha kura za maoni kule Arumeru Mashariki na hatimae akakimbilia CHADEMA na papo kwa papo akavuta fomu ya kuombe kuteuliwa kugombea ubunge! Mungu saidia kapata kura 8 je angepata kushinda kwenye kura za maoni si angetuuza?
CHADEMA TAFAKALI CHUKUA HATUA!.........
 
CDM iko chini ya uongozi imara sana kwa sasa, we bakia na ndoto yako lakini CDM kumeguka sio leo.

After all CDM kwa sasa inaMEGA wengine. Tumeona aliyejiengua ubunge wa CCM Meru alimegukia CDM na hata makundi ya CCM yanayogombea madaraka yatamegukia CDM. Kumbuka hata akina Sitta walikuwa na option ya kuhamia CDM au kuunda CCJ but roho za usaliti na unafiki zikawazidi

Unayetamani CDM kumeguka utasubiri sana, sawa na Fisi kumfuata nyuma nyuma mlevi akidhania mikono ya mlevi itadondoka. CDM ina MEGA CCM
Sina nyongeza ktk hili ila sioni kitufe cha ''THANKS''
 
Mimi siyo mpenzi wala mwanachama wa chama cha siasa lakini kwa namna ninavyofuatilia siasa ya multiparty CDM hakitakufa jaribu kuangalia trend yake na utamaduni wa chama ni tofauti na vyama hivyo vingine kwa mfano NCCRM Mrema kakipotezea mwelekeo na waliobakia wakazidi kukosa mwelekeo hivo zile weakness za Mrema zikahamishiwa TLP ukizingatia TLP hakikuwa chama chenye nguvu kama NCCRM.after all mimi naamini CHADEMA kina potential people na viongozi wako makini ikiwa ni pamoja na kufanyia kazi maoni haya tunayowapa
 
Aisee hiyo ni cra p takatifu
ukweli hata uufiche kwenye mazingira magumu vipi! still ukitoka utakuwa ukweli tu. ni kweli tunapata mafanikio. Na kupata baadhi ya majimbo kwenye miji mikubwa kama Arusha ,Mbeya Dar,K'njaro na Mwanza ni hatua nzuri na ya kujivunia. watu wa mazingira haya wana access huduma nyingi za msingi kama Hospital,Umeme,shule kwa kujipimia uwezo wenyewe. Mtoa mada ni mtu anayeitakia CDM mafanikio. Wenzetu CCM wana Dola na wana fedha za kurubuni wapinzani wao. nadhani usingeita thread hii ****. huenda ikawa we ni miongoni mwa wale kuzoea vya kunyonga. Mafanikio haya ya CDM yamejengwa na watu waliopitia tabu nyingi sana mpaka kukifikisha chama hapa. Hivyo ipo haja liibuke kundi lingine la Viongozi na wanachama wa CDM tunaotakiwa kulinda mafanikio haya na kuhakikisha chama kinatoka kwenye intercities na kushuka kwenye Rural areas ili pasiwepo na matatizo ya wizi wa kura zetu wakati huu tunapoelekea kuchukua Tanzania yetu baada ya kumtoa mkoloni CCM
 
Fungua macho nyanyua kichwa angalia mbali tatizo watu mnaitizama cdm kwa kumwangalia Mbowe na Slaa behind kuna vichwa vingi na makini sana tunamimini kuliko hata hao wawili nlowataja hapo na si watu wa kujionyesha bali wanakaa na kufikiria ni jinsi gani ya kuwasaidia watanzania niwataje kwa uchache
Prof Baregu
Prof Safari
Dr Kitila
Mzee wetu Mtei
Unaweza ukaongeza list.....
 
Mbona hamtaki kuona migogoro CCM,halafu haya mafundisho ya kushindwa ,woga,kufa ,kupotea ,kukata tamaa...yanatolewa wapi??wacha kuleta hisia zako binafsi za kushindwashindwa!
 
Umejitahidi sana kueleza lakini napata taabu kidogo kwani hujaeleza nini unanakiona kwa mbali kama kingesababisha CHADEMA kudumaa japo kwa mifano tu

Kwa hapa unacho sema ni utabiri utokanao na unajimu au ramri aidha unapenda kuwa siku moja itokee hivyo na unaombea itokee hivyo ndiyo kisa cha kutunza kumbukumbu hii
Ungelikuwa msaada mzuri sana kwa CHADEMA kama ungelikuwa unaeleza wazi matatizo yaliyopo ndani ya chama ili kijirekebishe

tatizo matatizo au migogoro mnayo unda ni ya kufikirika tu mfano UKABIRA, UKANDA na sasa UDINI vyote hivi mna prove failure

Labda niseme wazi kuwa CHADEMA ni chama mbadala wa CCM ushahidi hata wewe unao practically na theoretically hata kama majina yanabadilika from CUF to ADC lakini bado CHADEMA inakubalika tu na ndiyo mkombozi wa kweli

Wewe una mapenzi yasiyoona ukweli. Kinachonyemelea /kinachotokea kwa vyama vingine CDM is not an exception, ila wanaweza wakazuia kwa vile wameona mifano kwa wengine. Siyo kuwa anaombea itokee, anaipenda chadema ndio maana anaonyesha shimo isitumbukie!
 
Back
Top Bottom