Escaper
JF-Expert Member
- Nov 11, 2018
- 1,780
- 3,232
Na nyie ongezeni juhudi ya kupiga makofi na vigeregere huku wenzenu wakila teuzi kutoka mnapoita unyumbuni.Binafsi nawapongeza wale wote waliokuwa upinzani na kuteuliwa baada ya kujiunga CCM, na Sisi wafuasi wao ni Bora tufurahi Kwa wenzetu kupewa nafasi za kutumikia wananchi.
Hii ni nafasi ya wao kuonyesha kile walichokuwa wanapigania wakiwa nje kama wapinzani Kwa kuonyesha Kwa vitendo, kuna wengine wamepewa nafasi nzuri ambazo wanaweza kuleta tofauti kutokana na misimamo yao, mtu kama Prof. Mkumbo alikuwa muongeaji mzuri alipokuwa chadema na ATC wazalendo na sasa amepewa wizara ya maji kama katibu mkuu ambaye ni mtendaji mkuu wa wizara ni nafasi ya kuonyesha umahili wake wa kuwaletea maendeleo wananchi Kwa kuja na solutions za matatizo ya maji Kwa wananchi ili sasa tuamini Kwa kile wanachokisema na misimamo yao upinzani wakija kuongoza wanaweza kuja na solutions za matatizo ya wananchi ambazo CCM wameshindwa, naamini wengi mtasema hawawezi kufanya chochote Bali ni utekelezaji wa ilani ya CCM, lakini naamini ilani ya CCM na chadema zote ni nzuri na kama kiongozi ni mzuri anaweza kutekeleza regardless chama gani kinatawala.
Lakini pia hii kuteuliwa kutaonyesha umahili wa utendaji kazi wa hawa waliokuwa wanapiga kelele wakisema CCM inakosea kwenye utendaji kazi wake, maana kuongea ni kitu kingine lakini pia utendaji ni Jambo lingine.
Duniani hapa wapo watu wengi Sana walionyesha ni wazuri kwenye kuongea kama akina Zitto, Lissu lakini walipopewa madaraka walifeli Kwa sababu walifikilia kinadharia zaidi kuliko vitendo.
Mtatiro ukuu wa wilaya au mkoa ni madaraka ambayo unaweza kuonyesha umahiri katika utendaji wa kazi tunaomba utuonyeshe umahiri wako angalau Kwa sehemu ndogo uliyopewa kuongoza, kuna wakuu wa mikoa na wilaya ambao wameonyesha tofauti na jamii imewakubali kama Yule wa Simiyu na Arusha, ni vijana walioonyesha wanaweza kuleta mawazo tofauti kwenye serikali ya CCM.
Mtatiro karibu utuonyeshe uwezo wako wa kutumikia wananchi