Mh. Livingstone Lusinde Under Microscope?

Maji Marefu:
Chama Cha Mapinduzi, CCM Regional Economic Secretary 2008

Chama Cha Mapinduzi, CCM Economic Secretary, Korogwe rural 2007

Lusinde:
Chama Cha Mapinduzi, CCM Secretary, Tarime 2007 na kuna wakati alikuwa eti ACCOUNTANT

Kwa mwendo huu CCM itawezaje kuwa na dira ya kuongoza taifa kama hawa LY's wanapewa majukumu yanayohitaji taaluma??????? Hawa CCM na watanzania hatuko serious kabsaaaaaaa!!!!!!!
 
Sidhani kama Lusinde ndiye yuko under microscope. Otherwise, utakuwa una-narrow tatizo na kufanya solution isipatikane. Tatizo hapa ni Watanzania wenyewe. Kama walikuwa tayari kuwa pale kusikiliza na kushangilia kwa yale waliokuwa wanayasikia, basi wao ndio wanatakiwa kuwa under microscope. Labda na wale waliomchagua pia. Kumbuka Lusinde ni mwakilishi wa watu na possibly ata-reflect waliomchagua.

Kama hao Watanzania wangekataa kusikiliza matusi, angeyasemea wapi? Ndio maana hata chama chake kinaweza kisimchukulie hatua zozote kwa sababu kinajua wazi walio na tatizo ni akina nani.

Kwa hiyo, badala yake, hotuba yake ya matusi ingekufanya binafsi upende kujua kwa undani baadhi ya mambo ya msingi kuhusu Watanzania waliokuwa wanamsikiliza na kumshangilia kama:

1. Wanazo akili timamu kweli?
2. Kama hawana akili sheria inasemaje kwa mtu asiye na akili?
3. Kama wanazo kwa nini walishangilia matusi yale?
4. Je historia yao ikoje?
5. Malezi yao yalikuwaje?
6. Na mengine ambayo wadau mtapenda kuongezea.

Hakika mzee. Wanaopaswa kuwa under scrutiny ni hao watu waliokua wakishangilia matusi na maneno ya kiuwendawizimu yaliyokuwa yakitoka mdomoni mwa Livingstone Lusinde!!

Lakika licha ya hivyo, bado kuna haja ya kumtathmini huyu mtu; kwani hayuko kawaida. Tathmini hii pia inapaswa kufika hadi kwenye chama alichopo huyu mtu; nacho hakipo kawaida. Haiwezekani, mtu kama huyo aendelee kuwepo kwenye kikundi cha watu wenye kuwa na mtazamo na itikadi zinazoshabihiana!!

Inasikitisha kwa kweli kuwa na hayo makundi matatu ambayo yanapaswa kuwa under microscope.
 
Tanzania Tanzania
Nakupenda kwa moyo wote
Nchi yangu Tanzania
Jina lako ni tamu sana
Nilalapo nakuota wewe
Niamkapo ni heri mama wee
Tanzania Tanzania
Nakupenda kwa moyo wote
 
Hakika mzee. Wanaopaswa kuwa under scrutiny ni hao watu waliokua wakishangilia matusi na maneno ya kiuwendawizimu yaliyokuwa yakitoka mdomoni mwa Livingstone Lusinde!!

Lakika licha ya hivyo, bado kuna haja ya kumtathmini huyu mtu; kwani hayuko kawaida. Tathmini hii pia inapaswa kufika hadi kwenye chama alichopo huyu mtu; nacho hakipo kawaida. Haiwezekani, mtu kama huyo aendelee kuwepo kwenye kikundi cha watu wenye kuwa na mtazamo na itikadi zinazoshabihiana!!

Inasikitisha kwa kweli kuwa na hayo makundi matatu ambayo yanapaswa kuwa under microscope.


Mkuu, ukipewa Leseni ya Piki Piki au ya gari dogo huwezi ukaendesha Semi Trella unless uwe una kipaji cha ajabu sana na umakini wa hali ya juu.

Lusinde Elimu yake ni darasa la saba, hicho ndicho tunachojua mpaka sasa unless kama kuna mtu ana data zaidi.

Sasa kama kweli elimu yake ni darasa la saba, piga picha uwezo wa walio wengi walioishia darasa hilo katika kuchanganua mambo. Kisha piga picha sasa kapewa Semi Trella ya kuingia bungeni na kupiga Kampeni na kutunga sheria na kutumikia kamati za Bunge. Ni nini unachotegemea?

WYSIWYG . . .
 
Halafu jamaa yeye ndiyo "mshamba kweli" eti anauliza mtoto akizaliwa kwenye basi au ndege anakua raia wa wapi?!!!
With morons like these as our leaders this country will never go forward.
 
Mkuu, ukipewa Leseni ya Piki Piki au ya gari dogo huwezi ukaendesha Semi Trella unless uwe una kipaji cha ajabu sana na umakini wa hali ya juu.

Lusinde Elimu yake ni darasa la saba, hicho ndicho tunachojua mpaka sasa unless kama kuna mtu ana data zaidi.

Sasa kama kweli elimu yake ni darasa la saba, piga picha uwezo wa walio wengi walioishia darasa hilo katika kuchanganua mambo. Kisha piga picha sasa kapewa Semi Trella ya kuingia bungeni na kupiga Kampeni na kutunga sheria na kutumikia kamati za Bunge. Ni nini unachotegemea?

WYSIWYG . . .

Sawa. Lakini kama alivyosema mzee EMT, hili suala lazima tuliangalie kwa mapana zaidi.
Ni kweli Lusinde ana matatizo ya akili (kwa kutumia reference ya hiyo hotuba); lakini mimi bado naendelea kuamini wenye matatizo zaidi ni hao watu waliokuwa wakimshangilia na kumtaka aendelee kuporomosha matusi!! Kwa maana kwa watu wenye utashi na uelewa, wasingeweza kuvumilia kusikiliza maneno machafu kama yale!!

Yaani ni sawa na mtu anayeoga mtoni, kisha "chizi" akaja kukwapua nguo zake, kisha mtu huyo akaanza kumkimbiza "chizi" yule, akiwa "mtupu". Sasa hapa tutamlaumu "chizi" tu bila ya kumshangaa na huyo mtu anayemkimbiza "chizi" akiwa mtupu?! Namaanisha kwamba, pamoja na kumsema Lusinde, lakini "audience" yake kwa siku hiyo haiwezi kuachwa kusemwa pia. Kwani walikua na haki na uwezo wa "ku-walk" out na kumwacha huyo "chizi" akimbie na nguo!!
 
Sawa. Lakini kama alivyosema mzee EMT, hili suala lazima tuliangalie kwa mapana zaidi.
Ni kweli Lusinde ana matatizo ya akili (kwa kutumia reference ya hiyo hotuba); lakini mimi bado naendelea kuamini wenye matatizo zaidi ni hao watu waliokuwa wakimshangilia na kumtaka aendelee kuporomosha matusi!! Kwa maana kwa watu wenye utashi na uelewa, wasingeweza kuvumilia kusikiliza maneno machafu kama yale!!

Yaani ni sawa na mtu anayeoga mtoni, kisha "chizi" akaja kukwapua nguo zake, kisha mtu huyo akaanza kumkimbiza "chizi" yule, akiwa "mtupu". Sasa hapa tutamlaumu "chizi" tu bila ya kumshangaa na huyo mtu anayemkimbiza "chizi" akiwa mtupu?! Namaanisha kwamba, pamoja na kumsema Lusinde, lakini "audience" yake kwa siku hiyo haiwezi kuachwa kusemwa pia. Kwani walikua na haki na uwezo wa ku-walk out na kumwacha huyo "chizi" akimbie na nguo!!

Kamanda Nzi, mimi sina tatizo la arguments zako au EMT, hili jambo lina wigo mpana zaidi kama tutalifanyia upembuzi. Kama tukiamua kuwa focused zaidi tatizo hili si la wanaomsikiliza tu, bali ni mfumo mzima wa kuchagua viongozi. Kama Lusinde hii ndo tabia yake halisi na style yake ya leadership basi hakupaswa afike hapa alipom ukienda mbele zaidi utagundua pamoja na mfumo mbaya wa uchaguzi, kuna suala zima la kihistoria, elimu nk.

Na ukienda kwa mapana zaidi ukaangalia mfumo wote wa kiutendaji serikalini na siasa za maji taka ndani ya vyama, utagundua hata mimi na wewe tuna matatizo, ni mangapi tumetukanwa na viongozi direct au indirect lakini tumekaa kimya kama kondoo na kuona sawa tu? vingapi tumenyanyaswa? Tumepuuzwa? Tumeonewa, Tumedharauliwa? nk?

Hata kama suluhu ni katiba mpya kwa namna moja au nyingine, lakini bado suala zima la uongozi bora bado liko palelepale. Hilo nalo linaendana sambamba na attitude za watu na Elimu kwa ujumla. It is a Viscous Cycle hata sijui tutaanzia wapi . . . . The reason why I hate to be a Politician . . . may be I can, but only If I can be a President ili nisiwekewe kiwingu na yetote, then I know only what guts I have and the love for my country.

If you cant be a better and a Patriotic Politician, better not be one! Nawapongeza Wanasiasa wote ambao katika mfumo mbovu wa siasa tulionao sasa hivi wanasimama kidete kutetea maslahi ya nchi na umma kwa uzalendo wa hali ya juu. Though, I am not sure how many we have maana pia kuwa Opportunist si kuwa Mzalendo!
 
Mkuu, ukipewa Leseni ya Piki Piki au ya gari dogo huwezi ukaendesha Semi Trella unless uwe una kipaji cha ajabu sana na umakini wa hali ya juu.

Lusinde Elimu yake ni darasa la saba, hicho ndicho tunachojua mpaka sasa unless kama kuna mtu ana data zaidi.

Sasa kama kweli elimu yake ni darasa la saba, piga picha uwezo wa walio wengi walioishia darasa hilo katika kuchanganua mambo. Kisha piga picha sasa kapewa Semi Trella ya kuingia bungeni na kupiga Kampeni na kutunga sheria na kutumikia kamati za Bunge. Ni nini unachotegemea?

WYSIWYG . . .

Mkuu, watu wengi huwa tunadhani kuwa usomi ndio kipimo cha mtu mwenye hekima na busara. Ni kweli mtu msomi licha ya kuheshimika katika jamii lakini pia anatumika kama mshauri katika masuala mbalimbali yakiwemo ya kitaaalamu au hata ya kijamii, pale itakapohitajika ushauri katika kupata suluhu iwapo kutatokea kusigishana katika jamii.

Lakini vidato pekee haviwezi kupambanua kiwango cha busara na hekima alizo nazo mtu. Na hii inatokana na jinsi wasomi wetu walivyofinyangwa kuanzia katika malezi mpaka huko mashuleni. Kama elimu ndiyo kipimo cha hekima na busara ni dhahiri kabisa leo kusingekuwepo na ufisadi na ubadhirifu ambayo hufanywa na wasomi wanaotegemewa. Kama elimu ndiyo kipimo cha hekima na busara ni dhahiri kabisa Halima Mdee asingesema kwenye mkutano wa hadhara kuwa Wassira ana sura mbaya kama ya sokwe mtu.

Kwa hiyo, Lusinde hakuhitaji kuwa msomi ili asimwage yale matusi. Alichohitaji ni hekima na busara tuu. Naamini kabisa mtu aliyeishia darasa la saba ana uwezo wa kuwa na hekima na busara ya kutoongea matusi ya aina ile hadharani tena kwenye mkutano wa kampeni za kisiasa.
 

Kamanda Nzi, mimi sina tatizo la arguments zako au EMT, hili jambo lina wigo mpana zaidi kama tutalifanyia upembuzi. Kama tukiamua kuwa focused zaidi tatizo hili si la wanaomsikiliza tu, bali ni mfumo mzima wa kuchagua viongozi. Kama Lusinde hii ndo tabia yake halisi na style yake ya leadership basi hakupaswa afike hapa alipom ukienda mbele zaidi utagundua pamoja na mfumo mbaya wa uchaguzi, kuna suala zima la kihistoria, elimu nk.

Na ukienda kwa mapana zaidi ukaangalia mfumo wote wa kiutendaji serikalini na siasa za maji taka ndani ya vyama, utagundua hata mimi na wewe tuna matatizo, ni mangapi tumetukanwa na viongozi direct au indirect lakini tumekaa kimya kama kondoo na kuona sawa tu? vingapi tumenyanyaswa? Tumepuuzwa? Tumeonewa, Tumedharauliwa? nk?

Hata kama suluhu ni katiba mpya kwa namna moja au nyingine, lakini bado suala zima la uongozi bora bado liko palelepale. Hilo nalo linaendana sambamba na attitude za watu na Elimu kwa ujumla. It is a Viscous Cycle hata sijui tutaanzia wapi . . . . The reason why I hate to be a Politician . . . may be I can, but only If I can be a President ili nisiwekewe kiwingu na yetote, then I know only what guts I have and the love for my country.

If you cant be a better and a Patriotic Politician, better not be one! Nawapongeza Wanasiasa wote ambao katika mfumo mbovu wa siasa tulionao sasa hivi wanasimama kidete kutetea maslahi ya nchi na umma kwa uzalendo wa hali ya juu. Though, I am not sure how many we have maana pia kuwa Opportunist si kuwa Mzalendo!

Nimekupata mzee.

Inasikitisha na inauma kwamba sisi sote tuna matatizo; mbaya zaidi tumekubali kuishi na kuzoea na matatizo, kama tusemavyo wasukuma; "ndoho tabu". Hii ya ndoho tabu ndiyo imelifikisha taifa letu hapa lilipo.
Hakika ni vicious cycle ambayo tumefungwa na mpaka sasa bado hajutafikiria (au kukubali) namna ya kujitoa katika mzunguko huo!!
 
WanaJF

Nadhani wengi tumepata bahati ya kusikia Mh. Livingstone Lusinde akimwaga Sera za CCM kule Arumeru Mashariki katika moja ya mikutano ya Kampeni ya CCM. Ni wazi kuwa katika kampeni vijembe vya hapa na pale kwa vyama pinzani haviwezi kukosekana. Hata hivyo vijembe vinapogeuka consinstently kuwa matusi tena mbele ya kadamnasi ya watu wakiwepo watoto wadogo wa shule, ni wazi kuwa mhusika anakuwa amevuka na kuvunja maadili ya ustaarabu wa kawaida wa Watanzania.

Hotuba yake ya matusi imenifanya binafsi nipende kujua kwa undani baadhi ya mambo ya msingi kuhusu Mh. Lusinde kama:


  1. Mh. Livingstone Lusinde anazo akili timamu kweli?
  2. Kama hana akili Katiba inasemaje kwa mtu asiye na akili kuwa kiongozi?
  3. Kama anazo kwa nini aliporomosha matusi yale?
  4. Je historia yake ikoje?
  5. Malezi yake yalikuwaje?
  6. Na mengine ambayo wadau mtapenda kuongezea.

Wakati tukiendelea kumweka mh. Lusinde katika Microscope, naomba pia tuendelee kukusanya kumbukumbu zake za kila namna kuridhisha hasa ni mtu wa namna gani.


Mkuu, mimi binafsi ningependa kujua BUNGE linatakiwa kuchua hatua gani pale Mbunge wake anapofanya mambo kama haya mbele ya jamii. Mbunge yeyote akipita mtaani, anaheshimka kwa hadhi yake ya kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, bila kujali anatoka Chama gani. Hata wanapopata matatizo huchukuliwa kama Wabunge wa Bunge la Jamhuri.

Sasa ktk hili la bwana Lusinde, ni Lazima Bunge liwajibike, na kama Bunge litakuwa kimya ktk hili, au kanuni zake hazimgusi mbunge anapokuwa ktk shughuri zake za Kisiasa za chama chake, basi Bunge letu litakuwa na kanuni zisizojitosheleza. Itafika kipindi tutakuwa na wabunge wengi kama lusinde, sijui tutegemee sheria za namna gani zitatungwa na Bunge hilo. Nasubiri kusikia kauli ya ofisi za Bunge.
 
si kweli. kuna wajasiriamali wengi wenye mafanikio na ni darasa la saba.

Mkuu,
ukipewa Leseni ya Piki Piki au ya gari dogo huwezi ukaendesha Semi
Trella unless uwe una kipaji cha ajabu sana na umakini wa hali ya juu.
Lusinde Elimu yake ni darasa la saba, hicho ndicho tunachojua mpaka
sasa unless kama kuna mtu ana data zaidi.
Sasa kama kweli elimu yake ni darasa la saba, piga picha uwezo wa walio
wengi walioishia darasa hilo katika kuchanganua mambo. Kisha piga picha
sasa kapewa Semi Trella ya kuingia bungeni na kupiga Kampeni na kutunga
sheria na kutumikia kamati za Bunge. Ni nini unachotegemea?
WYSIWYG . . .
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Nimeona video ile na kushangaa kuwa walikuwa wapo watoto wadogo wengi sana kuliko watu wazima, na baadhi ya watoto walikuwa wakifunika midomo yao kuonyesha mashangao kwa yale waliyokuwa wanasikia kutoka jukwaani.
 
Wakati nasoma thread yenye hotuba yake, nilidhan ni masikhara ya mtoa maada! Daaaah! Naogopa kuamini, kwani ni aibu kubwa kwa mtu mzima! Au anavuta bangi??
 
Mkuu, mie siyo GAY hadi nianze KUMJUA huyu Lusinde. Haya mambo ya Adam akamjua Mkewe...... Mie na Mwanaume ni kama maji na mto. Pia hii kusema atanibajaji, wee umejulia wapi? Alishakubajaji hadi ukajua jamaa ndiyo tabia zake?

Soma ujumbe wangu wa chini labda utanielewa.
Wewe nawe ukilaza kweli,unataka kusema wewe unamjua sana Lusinde? haya ngoja akubajaji mwenzio
 
Superman,

Naona kwa heshima yako basi nitaelezea hicho kilichokuwa kimejificha ndani ya huo uandishi wangu ingawa kama Mwandishi, nitakuwa ninafanya makosa kuweka maana yangu. Inabidi uwaache wenyewe wafikirie kidogo.

Baadhi ya wana JF wamenielewa na kwa kunisoma katikati ya mistari. Nawashukuru kwa hilo na siku nyingine ukiona nimeandika kitu kichwa chini miguu juu, basi kipindue juu chini na utanielewa.

Nafahamu kuwa Lusinde ni Mkristo haswaa kwa kuangalia jina na kuwa Dodoma, Waislaam ni wachache sana na haswa kwa Wagogo ukiacha Warangi ambao wengi ni Waislaam.

Kumekuwepo Tabia za akina Malaria Sugu, Topical, FF, Ritz na wengine wengi ambao huwa wakali sana kila kiongozi Muislaam akishambuliwa au kutukanwa kwa upuuzi wake au Ufisadi. Huwa wanakuja kwa nguvu zote kulalamika kuwa Wakristo wanamshambulia Muislaam huyo kwa sababu ya dini yake ila angelikuwa Mkristo, basi wala wasingelimgusa.

Ndipo nikataka kuonyesha kuwa, LUSINDE kaboronga, na Wakristo wamemuweka Kikaangoni. Watu hawakujali sana dini ya mtu ila waliangalia tu upuuzi alioufanya.

Lengo langu lilikuwa kuwaambia hao Waislaam wachache wasiotaka kukosolewa na kukimbilia kujitetea kama Weusi wa USA/UK nk ambao wakiguswa tu hata kama wana makosa, analalamika kuwa ameguswa kwa sababu yeye ni MWEUSI.

Kwa Waislaam wote ambao huwa Wanamkoma Nyani giledi bila kuangalia dini yake, hao mbona wamenielewa tu na wamejua lengo langu? Ila ninashangaa watu wanakuja na mapovu meengi kuonyesha wao ndiyo wanapigana wakati kila mtu anapita kivyake ili muradi wote lengi letu ni moja.

Mie ni wale NATANGULIZA TAIFA zaidi ya Chama. Mungu Ibariki Tanzania.
Haaaa haaa Mzee wa Sikonge leo umenifurahisha sana. Isije ikawa umetekwa na Malaria Sugu . . .

Livingstone Joseph Lusinge inawezekana akawa ni Mwislamu maana jina si lazima liwe ni hatimiliki au liashirie dini fulani.

Lakini kwa matusi haya yenye harufu mbaya ya kama CHOO CHA CITY najua hata Waislamu tutamkana.
 
kuna mtu kasema lusinde ni member humu,nakataa,huyu kilaza hajui hata kushika mouse!
 
baada ya miaka ishirini ndo effects zake zitadhihirika kwa wengi.

Kama Baba yao ndio huyo,nawaonea huruma.Nashauri watafutiwe mlezi,maana kila watakapo kosea,itaonekana sio kosa lao,ni kosa la malezi ya Baba yao.
Lusinde umewaharibia future watoto wako.

What you have done ina kuhukumu na kuula ukoo wako ndani na nje ya CCM kwa zaidi ya miaka 100
 
Back
Top Bottom