Kamukhm
JF-Expert Member
- Aug 30, 2015
- 2,799
- 4,195
Natanguliza salamu za dhati kwako Mh. Waziri
Pili, niwasalimu waatalamu wa Ardhi nchi nzima wanao kusaidia kufikia azma ya majukumu yako ulio aminiwa na Taifa kuyasimamia na kuyaongoza.
Waraka huu ni mahususi kwa taaluma ya mipangomiji ambayo ni moja ya nyenzo muhimu katika kutekeleza majukum yako Mh. Waziri.
Mh. Waziri; siku chache zilizopita umekuwa ukifanya ziara maeneo mbalimbali kwa lengo la kutatua migogoro na kuona namna bora ya kuisimamia sekta hii nyeti ya ardhi kuiepusha na migogoro
Mh. Waziri; moja ya ziara yako imegusia sana kuhusu ujenzi au uwepo wa vituo vya mafuta katika miji hususan Dar es salaam.
Mh. Waziri; mara kadhaa nimeshuhudia maelekezo yako yakielekeza hatua mbalimbali zichukuliwe ndani ya sekta ya mipangomiji. Moja ya hatua ulio elekeza ni kumsimamisha kazi Mkurugenzi anaesimamia mipangomiji na maendeleo ya makazi ngazi ya wizara. Hoja yako iliyokusuma kufanya hivyo ni kuhusu waraka unaotumika katika kuidhinisha ujenzi wa vituo vya mafuta jambo ambalo siku chache zilizopita lilijitokeza Katika maeneo ya Mikocheni na bado lawama zako na hatua unazozichukua umezielekeza katika kitengo cha mipangomiji manispaa ya Kinondoni
Mh. Waziri; sina shaka na weredi wako katika medani za kisheria pamoja na utashi wako binafsi katika kufuatilia mambo ya kijamii
Mh. Waziri; kwa wataalamu wa mipangomiji Kinondoni umewakaripia kwa kusema kwamba hawawashiriki Wenye ardhi yao ambao kwa maelezo yako watu hao ni Waheshimiwa madiwani.
Mh. Waziri; naomba nikukumbushe kwamba kwa mujibu wa sheria ya Ardhi No. 4 (1999) ikisomeka pamoja na marekebisho yake inaeleza bayana kwamba Ardhi ya Tanzania ina milikiwa na wananchi na Rais ni mdhamana wa hilo. Hata hivyo pamoja na kwamba ardhi inamilikiwa na wananchi lakin hawana idhini ya kuitumia moja kwa moja bila kibali cha mdhamana ambaye ni Rais, na kibali hicho cha matumizi hutolewa na mamlaka za upangaji zilizo kasimishiwa wadhifa huo kwa niaba ya Rais
Mh. Waziri moja ya kaul yako umeeleza kwamba wataalamu wasiamue kupanga matumizi ya ardhi bila kuwahusisha madiwani na ukaenda mbali ukasema. Naomba kunukuu ......."waacheni Wakae Waheshimiwa Madiwani waamue wenyewe kupanga mji wao au kuharibu mji wao...."
Mh. Waziri; kauli hii inakwenda kuididimiza taaluma ya upangajimiji, miji yetu imeharibika kutokana na ardhi kuamuliwa na wanasiasa wasio na weredi na masuala ya ardhi hususan katka kupangilia matumizi na kukidhi haja ya watumiaji ardhi.
Ni wazi kwamba kwa kauli hiyo ni sawa na kusema hakuna haja ya kuwepo wataalamu na badala yake wakae wawakilishi wa wananchi wajipangie wenyewe mahitaji ya matumizi katika ardhi yao jambo ambalo linakwenda kuharibu mionekano ya miji yetu, inakwenda kudidimiza mipangilio ya miji lakin pia sura ya nchi inakwenda kusiginwa kupitia kaul hii.
Mh. Waziri; nipende pia kukupa taarifa kwamba sekta ya ardhi tangu mwaka 2016 imeandamwa na matamko tofauti ya viongozi waandamizi, matamko ambayo yameleta shida kubwa sana katika usimamizi wa maendelezo ya makazi nchini
Moja ya shida hizo ni kuwa na muundo mbovu wa maamuzi na kiutendaji katika idara zote za Ardhi na maendeleo ya makazi, watumishi wa idara hizo pia kuandamwa na mazingira magumu kiutendaji na kupekelea kukosa moral ya kazi.
Mh. Waziri; kwa hakika kabisa bila kuwa na muundo bora wa utendaji katika wizara yako, unayo isimamia madudu yataongezeka, maamuzi ya kiutendaji katika Halmashauri yatafubaa, kwa sasa ni jambo la kawaida kuikuta ofisi ya aradhi haina umeme wala printer au photocopy machine, ofisi za ardhi hazina hata kabati au shelf la kutunzia kumbukumbu watumishi hawana bajet ya kutekeleza majukum yao
Mh. Waziri; watangulizi wako katika wizara yako kuna jambo walilifanya huenda ni kwa nia njema lakin linahitaji maboresho makubwa sana, mambo hayo ni muundo, utoaji wa matamko kwa njia ya Waraka, maelekezo yasio tekelezeka.
Mh. Waziri; nilikusikusikia ukisema kwamba watumishi wa ardhi wakatae maelekezo ya Waziri wao kwa kuwa si alie waajiri, unasahau kwamba kwa sasa watumishi hao hawapo tena TAMISEM bali unao hapo ofisin kwako na muajiri ni Katibu mkuu wako maana yake chombo cha kinidhamu ambacho ni muajiri ni Waziri, mtumishi anawezaje kukataa maelekezo ya waziri au kuhoji maelekezo ya mwajiri wake??
Mh. Waziri; nia yako ni njema sana katika kuisimamia wizara pamoja na kuiratibu ili ikupe matokeo utakayo lakin bila kuondoa changamoto za kimuundo ya mikocheni utayakuta maeneo mengi nchini. Wataalamu wa mipangomiji si sehem ya CMT hawaingii katika kamati tendaji huu mfumo utaumiza hii sekta
Mh. Waziri; kwa heshima kubwa sana nikusihi kufanya marekebisho ya kimuundo katika wizara yako. Punguza urasimu katika idara hizi na buni mfumo tendaji utakao saidia kuratibu matumizi ya ardhi ili hayo ya Mikocheni yasijitokeze tena, migogoro ya utumiaji ardhi ipungue na kila Mtanzania apate stahiki sahihi ya kutumia Ardhi ya nchi yake.
Mh. Waziri; mimi nikiwa kama Mtanzania na mwenye kuipenda sekta ya ardhi naomba nikushauri yafuatayo;-
1. Boresha mfumo kimuundo wa wizara yako
2. Ondoa kauli ya kuwaachia madiwani kupanga au kuharibu mji wao
3. Peleka wataalam wa mipangomiji ngazi ya kata kusaidia kudhibiti ukuaji holela wa miji na makazi
4. Unda tume ikusaidie kuchunguza chanzo cha ujenzi holela wa vituo vya mafuta na katika muda ambao tume itakuwa kazin sitisheni utoaji wa vibal vipya na majibu ya tume yalete mapendekezo ya namna bora ya kujenga vituo vya mafuta mijin
5. Tengeneza kamati shauri katika ofisi yako itumie kama chombo chako cha kiintelijensia, kamati hiyo iwe na wataalam wa ardhi pekee yaani mipangomiji, Afisa ardhi, Mpima ardhi na mthamini mali na ardhi. Kamati hii iwe na watu wenye wered wa hali ya juu sana na wanao weza kukueleza ukwel bila kujal ni uchungu au utamu wake
6. Ikikupendeza simamisha kwanza ziara zako na kutana na wataalam wa ardhi wakueleze changamoto zao kiutendaji pamoja na wadau wengine ili kwa pamoja mtoke na njia mahususi ya kushughulikia migogoro ya ardhi na udhibiti wa maendelezo ya ardhi nchini
Mh. Waziri; nikuombe radhi pale nilipo tumia neno lisilo kuvutia machoni mwako lakin kwa sababu ile ile ya nia njema ya kutekeleza Ilani ya CCM na kudumisha maelekezo ya Rais wetu mpendwa ya kuitaka sekta hii iwe na mchango katika maendeleo ya Taifa letu
Wasalam
Na
Ismal Chingwele
(Dip.CE, Bsc. URP, Msc. PPM, Msc. CEM)
Land Development Consultant-East Africa
Pili, niwasalimu waatalamu wa Ardhi nchi nzima wanao kusaidia kufikia azma ya majukumu yako ulio aminiwa na Taifa kuyasimamia na kuyaongoza.
Waraka huu ni mahususi kwa taaluma ya mipangomiji ambayo ni moja ya nyenzo muhimu katika kutekeleza majukum yako Mh. Waziri.
Mh. Waziri; siku chache zilizopita umekuwa ukifanya ziara maeneo mbalimbali kwa lengo la kutatua migogoro na kuona namna bora ya kuisimamia sekta hii nyeti ya ardhi kuiepusha na migogoro
Mh. Waziri; moja ya ziara yako imegusia sana kuhusu ujenzi au uwepo wa vituo vya mafuta katika miji hususan Dar es salaam.
Mh. Waziri; mara kadhaa nimeshuhudia maelekezo yako yakielekeza hatua mbalimbali zichukuliwe ndani ya sekta ya mipangomiji. Moja ya hatua ulio elekeza ni kumsimamisha kazi Mkurugenzi anaesimamia mipangomiji na maendeleo ya makazi ngazi ya wizara. Hoja yako iliyokusuma kufanya hivyo ni kuhusu waraka unaotumika katika kuidhinisha ujenzi wa vituo vya mafuta jambo ambalo siku chache zilizopita lilijitokeza Katika maeneo ya Mikocheni na bado lawama zako na hatua unazozichukua umezielekeza katika kitengo cha mipangomiji manispaa ya Kinondoni
Mh. Waziri; sina shaka na weredi wako katika medani za kisheria pamoja na utashi wako binafsi katika kufuatilia mambo ya kijamii
Mh. Waziri; kwa wataalamu wa mipangomiji Kinondoni umewakaripia kwa kusema kwamba hawawashiriki Wenye ardhi yao ambao kwa maelezo yako watu hao ni Waheshimiwa madiwani.
Mh. Waziri; naomba nikukumbushe kwamba kwa mujibu wa sheria ya Ardhi No. 4 (1999) ikisomeka pamoja na marekebisho yake inaeleza bayana kwamba Ardhi ya Tanzania ina milikiwa na wananchi na Rais ni mdhamana wa hilo. Hata hivyo pamoja na kwamba ardhi inamilikiwa na wananchi lakin hawana idhini ya kuitumia moja kwa moja bila kibali cha mdhamana ambaye ni Rais, na kibali hicho cha matumizi hutolewa na mamlaka za upangaji zilizo kasimishiwa wadhifa huo kwa niaba ya Rais
Mh. Waziri moja ya kaul yako umeeleza kwamba wataalamu wasiamue kupanga matumizi ya ardhi bila kuwahusisha madiwani na ukaenda mbali ukasema. Naomba kunukuu ......."waacheni Wakae Waheshimiwa Madiwani waamue wenyewe kupanga mji wao au kuharibu mji wao...."
Mh. Waziri; kauli hii inakwenda kuididimiza taaluma ya upangajimiji, miji yetu imeharibika kutokana na ardhi kuamuliwa na wanasiasa wasio na weredi na masuala ya ardhi hususan katka kupangilia matumizi na kukidhi haja ya watumiaji ardhi.
Ni wazi kwamba kwa kauli hiyo ni sawa na kusema hakuna haja ya kuwepo wataalamu na badala yake wakae wawakilishi wa wananchi wajipangie wenyewe mahitaji ya matumizi katika ardhi yao jambo ambalo linakwenda kuharibu mionekano ya miji yetu, inakwenda kudidimiza mipangilio ya miji lakin pia sura ya nchi inakwenda kusiginwa kupitia kaul hii.
Mh. Waziri; nipende pia kukupa taarifa kwamba sekta ya ardhi tangu mwaka 2016 imeandamwa na matamko tofauti ya viongozi waandamizi, matamko ambayo yameleta shida kubwa sana katika usimamizi wa maendelezo ya makazi nchini
Moja ya shida hizo ni kuwa na muundo mbovu wa maamuzi na kiutendaji katika idara zote za Ardhi na maendeleo ya makazi, watumishi wa idara hizo pia kuandamwa na mazingira magumu kiutendaji na kupekelea kukosa moral ya kazi.
Mh. Waziri; kwa hakika kabisa bila kuwa na muundo bora wa utendaji katika wizara yako, unayo isimamia madudu yataongezeka, maamuzi ya kiutendaji katika Halmashauri yatafubaa, kwa sasa ni jambo la kawaida kuikuta ofisi ya aradhi haina umeme wala printer au photocopy machine, ofisi za ardhi hazina hata kabati au shelf la kutunzia kumbukumbu watumishi hawana bajet ya kutekeleza majukum yao
Mh. Waziri; watangulizi wako katika wizara yako kuna jambo walilifanya huenda ni kwa nia njema lakin linahitaji maboresho makubwa sana, mambo hayo ni muundo, utoaji wa matamko kwa njia ya Waraka, maelekezo yasio tekelezeka.
Mh. Waziri; nilikusikusikia ukisema kwamba watumishi wa ardhi wakatae maelekezo ya Waziri wao kwa kuwa si alie waajiri, unasahau kwamba kwa sasa watumishi hao hawapo tena TAMISEM bali unao hapo ofisin kwako na muajiri ni Katibu mkuu wako maana yake chombo cha kinidhamu ambacho ni muajiri ni Waziri, mtumishi anawezaje kukataa maelekezo ya waziri au kuhoji maelekezo ya mwajiri wake??
Mh. Waziri; nia yako ni njema sana katika kuisimamia wizara pamoja na kuiratibu ili ikupe matokeo utakayo lakin bila kuondoa changamoto za kimuundo ya mikocheni utayakuta maeneo mengi nchini. Wataalamu wa mipangomiji si sehem ya CMT hawaingii katika kamati tendaji huu mfumo utaumiza hii sekta
Mh. Waziri; kwa heshima kubwa sana nikusihi kufanya marekebisho ya kimuundo katika wizara yako. Punguza urasimu katika idara hizi na buni mfumo tendaji utakao saidia kuratibu matumizi ya ardhi ili hayo ya Mikocheni yasijitokeze tena, migogoro ya utumiaji ardhi ipungue na kila Mtanzania apate stahiki sahihi ya kutumia Ardhi ya nchi yake.
Mh. Waziri; mimi nikiwa kama Mtanzania na mwenye kuipenda sekta ya ardhi naomba nikushauri yafuatayo;-
1. Boresha mfumo kimuundo wa wizara yako
2. Ondoa kauli ya kuwaachia madiwani kupanga au kuharibu mji wao
3. Peleka wataalam wa mipangomiji ngazi ya kata kusaidia kudhibiti ukuaji holela wa miji na makazi
4. Unda tume ikusaidie kuchunguza chanzo cha ujenzi holela wa vituo vya mafuta na katika muda ambao tume itakuwa kazin sitisheni utoaji wa vibal vipya na majibu ya tume yalete mapendekezo ya namna bora ya kujenga vituo vya mafuta mijin
5. Tengeneza kamati shauri katika ofisi yako itumie kama chombo chako cha kiintelijensia, kamati hiyo iwe na wataalam wa ardhi pekee yaani mipangomiji, Afisa ardhi, Mpima ardhi na mthamini mali na ardhi. Kamati hii iwe na watu wenye wered wa hali ya juu sana na wanao weza kukueleza ukwel bila kujal ni uchungu au utamu wake
6. Ikikupendeza simamisha kwanza ziara zako na kutana na wataalam wa ardhi wakueleze changamoto zao kiutendaji pamoja na wadau wengine ili kwa pamoja mtoke na njia mahususi ya kushughulikia migogoro ya ardhi na udhibiti wa maendelezo ya ardhi nchini
Mh. Waziri; nikuombe radhi pale nilipo tumia neno lisilo kuvutia machoni mwako lakin kwa sababu ile ile ya nia njema ya kutekeleza Ilani ya CCM na kudumisha maelekezo ya Rais wetu mpendwa ya kuitaka sekta hii iwe na mchango katika maendeleo ya Taifa letu
Wasalam
Na
Ismal Chingwele
(Dip.CE, Bsc. URP, Msc. PPM, Msc. CEM)
Land Development Consultant-East Africa