Mkuu Ibrah,
Washiri ni viongozi wa kimila wa kabila la waMeru ni kama Olaigwanani wa kabila la waMaasai.Washiri wa kabila la waMeru wakitoa maagizo chini mti wa Mringaringa hata kama ni maagizo yanayovunja sheria yatatekelezwa sasa CCM wamebaini maji yapo shingoni wamekuja na mbinu ya kuwatumia washiri mnaweza kuona ni jambo la kijinga lakini nawahakikishia njia ya Moshi Arusha itakuwa haipitiki wengi hapa ni wakizazi cha dot com wengine tunakilometa za kutosha tuna uzoefu kama Tembo jike tuna kumbu kumbu nzuri ya mgogoro wa Meru dayosisi.
Kwahiyo, Washiri hao ni wanaCCM?Mkuu Ibrah,
Washiri ni viongozi wa kimila wa kabila la waMeru ni kama Olaigwanani wa kabila la waMaasai.Washiri wa kabila la waMeru wakitoa maagizo chini mti wa Mringaringa hata kama ni maagizo yanayovunja sheria yatatekelezwa sasa CCM wamebaini maji yapo shingoni wamekuja na mbinu ya kuwatumia washiri mnaweza kuona ni jambo la kijinga lakini nawahakikishia njia ya Moshi Arusha itakuwa haipitiki wengi hapa ni wakizazi cha dot com wengine tunakilometa za kutosha tuna uzoefu kama Tembo jike tuna kumbu kumbu nzuri ya mgogoro wa Meru dayosisi.
Noted!!!Na hasa kama Mzee wa siasa katili, Lowasa, atakuwa nyuma ya hawa WASHIRI kwa ajili ya mkwewe.
Wameru ni nuksi ! Hao jamaa wakitumika na magamba hapatatosha ! Watu ambao walikuwa na ujasiri wa kuwafukuza settlers enzi hizo !Who are those Washiris, do they have power to prohibit a prrson to get in Meru?
Tendwa ni mtu wa ajabu sana, yaani yeye anaishi Dar, Washiri Arusha, Lema Arusha. Hao Washiri wameshindwa kufikisha ujumbe Arusha hadi wamtume Tendwa !
Yaani CHADEMA nao wafanye kama CCM ilivyofanya kwa Nape kule Igunga? Sidhani kama hatua hii inahitajika ingawa nafahamu pia ipo chuki nyingine ya miaka mingi kati ya Wameru na Wachagga ambao wana-share hadi majina. Kuna watu walitaka Dr Slaa aende huko nadhani kwa kutowafahamu Wameru.
Tendwa anafanya kazi isiyo yake. Anajiandaa kwa 2015 akagombee kwao kwa tiketi ya CCM.
Kwahiyo, Washiri hao ni wanaCCM?
Turudi kwenye Hoja, usipindishe,
Tendwa anaona ni sahihi kwa mtu/kundi la watu kumtishia mtu mwingine tena kwa kusema damu itamwagika kwa sababu ya hisia ya kufikiri wametukanwa?
Kwa mujibu wa post nilizozisoma humu, ni kwamba, Lema alionyesha alama ya Vidole viwili (alama inayotumika na CHADEMA, na vyama vingine vya upinzani duniani) wakatuwa mazishi ya aliyekuwa mbunge wa Meru mashariki. Sijui mazingira yaliyopelekea kufanya hivyo. Lakini naamini kwamba hilo sio tusi kwa yeyote, labda ni tusi kwa wanaCCM.
Anyways. issue ni kwanini kiongozi wa calibre ya juu kabisa kama Tendwa, badala ya kuwaambia vyombo vya usalama walinde na kutoa ulinzi, yeye anasema Lema awaombe Washiri radhi au asiend Meru?
Mkuu kwa badinko lako, unataka kutuaminisha kwamba, Meru hakuna wafuasi wa vyama vingine ikiwamo CHADEMA?
Mbowe atakwenda kwenye kampeni hizi? Dr Slaa na Ukatoliki wake je? Siasa za AruMeru ni hasa. Tendwa naye anazidi kuwachafua CHADEMA.Mkuu WildCard,
WaMeru walikuwa na mgogoro wa makabila mawili waChagga na waArusha migogoro yote ni kwaajili ya maslahi.
WaChagga walikuwa wamewameza waMeru katika dayosisi ya kaskazini KKKT,miradi yote ya kanisa ilijengwa Kilimanjaro eg KCMC,Machame Hospital,Marangu Hospital na nk.WaMeru wakalilia dayosisi yao wakapewa baada ya vurugu kubwa na umwagaji wa damu ni A L Mrema aliyeweza kusuluhisha mgogo huo Mzee A H Mwinyi akamzawadi cheo cha naibu waziri mkuu.
WaArusha walikuwa wamewameza waMeru kisiasa zaidi kabla Arumeru haijagawanywa mara mbili Mashariki na magharibi waMeru hawakuwahi kutoa mbunge kila uchaguzi ukifanyika mbunge mwarusha lazima ashinde nadhani eneo lote la Meru kabla halijagawanywa idadi ya waArusha ni kubwa kuliko waMeru.
WaMeru sasa wana halmashauri yao,mbunge wao na Askofu wao,vyote hivi walivipata kwa kutumia nguvu kubwa kupita kiasi ni watu waliozoea harakati wakitaka jambo lao lazima litimie.Hili CCM wanalijua hili,Madereva wa daladala wanalijua hili ni shida sana kupata usafiri wa daladala kwenda eneo la USA na Tengeru kuanzia saa mbili usiku na kuendelea,ni hatari sana kuharibikiwa na gari muda wa usiku maeneo ya Tengeru,USA hadi kwa Mrefu.
Wana JF kitendo cha Msajili wa vyama vya siasa Jonn Tendwa kazungumza na Waandishi wa habari na kusema kuwa katika tathimini yake katika uchaguzi wa Arumeru Wazee wa kimila wamemwambia kuwa wanamwonya Lema asiende kwenye kampeni eti watamuuwa kauli hii imenisikitisha kama si kunishangaza kuwa Tanzania kuna tatizo gani?.
Hii bila kumumunya maneneo ni makakati wa ndani wa CCM wa kuandaa mazingira ya vurugu ili ikionekena CCM inashindwa waanzishe vurugu katika kampeni ili watu waumizwe waogope kwenda kupiga kura.
Hili naomba CHADEMA wajiandae mapema . Haingii akilini mtu wa heshima kama msajili wa vyama kuongelea vitu vya vurugu kutoka kwa watu wa kimila waabudu mizimu na wasiomjua Mungu. Nasema hakika haya mnayofanya laana ya Mungu na damu zitakazo mwagika bila hatia itakuwa juu yako na familia yako na vizazi vyako.
Mimi nadhani wazee hawa ilikuwa ni wakati wa kujenga Tanzania yenye amani zaidi kwa kuweka mazingiza ya watu kushindana kwa hoja na kwa amani ili ichi yetu ambayo imepata heshima kubwa iendelee kuwa nchi ya amani.
Tuachane na mawazo mgando kuwa ni lazima nyie muendelee kutawala na kutumia mbinu hata zisizofaa jamani tuamke watu wa aina ya Tendwa ni ukoma kwa Taifa.