Salaam, Shalom!!!
Jana, CHADEMA ilikuwa na mkutano wa hadhara na Maneno hayo ameyasema Nabii Lema akiwa Tunduma.
Niliwahi kuandika thread iliyosema,
WAKOMA wageuka mashujaa na kuikomboa nchi- Rabbon.
Kwa ufupi kisa cha wakoma 4 kulikuwa hivi.
Israeli ilipata habari juu ya maadui kuizingira Israel,
Israeli iliamuru Malango ya mji yafungwe Ili kujilinda.
Palikuwa na wakoma 4 ambao walikuwa wametengwa sababu ya ugonjwa wao,
Kwa kuwa njaa ilikuwa Kali sana mjini sababu Malango yalikuwa yamefungwa hakuna chakula kuingia Wala Kutoka. Njaa ilizidi sana, ikafikia time watu walianza kununua mavi ya njiwa na kuyala.
wakoma wakasemezana kwamba, ndugu zetu waisraeli wamejifungia hawatusaidii nasi tunakaribia kufa Kwa njaa.
Kuliko kufa Kwa njaa, ni kheri twende kuomba chakula katika kambi ya Washami.
Wakituua sawa maana tukikaa hapa tutakufa vile vile Kwa njaa. Wakituacha hai yote kheri.
Mungu alionao ujasiri wa wakoma 4, na walipoanza kutembea kuelekea kambi ya Washami maadui wa Israeli, Mungu aliwasikilizisha Washami sauti ya hatua zao na zilisikika kama kishindo kikubwa cha majeshi mengi.
Washami walikimbia wakiamini Israeli imekodi majeshi kuja kuwashambulia, walitimua mbio na kuacha Kila kitu.
wakoma 4 walipofika kambi ya Washami, walishangaa kuona hakuna mtu ila vyakula ,silaha nk nk vipo, na walishangaa zaidi kukuta mavazi ya wanajeshi Washami waliotimua mbio wa mnyama!!
Walipokula na kuteka Mali, pesa na Dhahabu, walirudi kuwaarifu wanajeshi wa Israel waliojifungia Kwa woga Ili watoke kuteka nyara.
Tangu siku Ile, wakoma 4 waliandikwa ktk historia ya mashujaa hadi leo.
Nabii Lema asema, wananchi tuige mfano wa wakoma 4, Mungu atatusaidia.
Kuelekea November, tuungane na Manabii wetu Slaa, Mwabukusi, Madeleka, Mdude, Lissu katika kudai TUME HURU ya UCHAGUZI na KATIBA mpya kabla ya Uchaguzi wowote.
Na maandamano hayo ni ya Amani bila kubeba silaha yoyote, maandamano yanayoruhusiwa kikatiba.
Aluta continua.
Jana, CHADEMA ilikuwa na mkutano wa hadhara na Maneno hayo ameyasema Nabii Lema akiwa Tunduma.
Niliwahi kuandika thread iliyosema,
WAKOMA wageuka mashujaa na kuikomboa nchi- Rabbon.
Kwa ufupi kisa cha wakoma 4 kulikuwa hivi.
Israeli ilipata habari juu ya maadui kuizingira Israel,
Israeli iliamuru Malango ya mji yafungwe Ili kujilinda.
Palikuwa na wakoma 4 ambao walikuwa wametengwa sababu ya ugonjwa wao,
Kwa kuwa njaa ilikuwa Kali sana mjini sababu Malango yalikuwa yamefungwa hakuna chakula kuingia Wala Kutoka. Njaa ilizidi sana, ikafikia time watu walianza kununua mavi ya njiwa na kuyala.
wakoma wakasemezana kwamba, ndugu zetu waisraeli wamejifungia hawatusaidii nasi tunakaribia kufa Kwa njaa.
Kuliko kufa Kwa njaa, ni kheri twende kuomba chakula katika kambi ya Washami.
Wakituua sawa maana tukikaa hapa tutakufa vile vile Kwa njaa. Wakituacha hai yote kheri.
Mungu alionao ujasiri wa wakoma 4, na walipoanza kutembea kuelekea kambi ya Washami maadui wa Israeli, Mungu aliwasikilizisha Washami sauti ya hatua zao na zilisikika kama kishindo kikubwa cha majeshi mengi.
Washami walikimbia wakiamini Israeli imekodi majeshi kuja kuwashambulia, walitimua mbio na kuacha Kila kitu.
wakoma 4 walipofika kambi ya Washami, walishangaa kuona hakuna mtu ila vyakula ,silaha nk nk vipo, na walishangaa zaidi kukuta mavazi ya wanajeshi Washami waliotimua mbio wa mnyama!!
Walipokula na kuteka Mali, pesa na Dhahabu, walirudi kuwaarifu wanajeshi wa Israel waliojifungia Kwa woga Ili watoke kuteka nyara.
Tangu siku Ile, wakoma 4 waliandikwa ktk historia ya mashujaa hadi leo.
Nabii Lema asema, wananchi tuige mfano wa wakoma 4, Mungu atatusaidia.
Kuelekea November, tuungane na Manabii wetu Slaa, Mwabukusi, Madeleka, Mdude, Lissu katika kudai TUME HURU ya UCHAGUZI na KATIBA mpya kabla ya Uchaguzi wowote.
Na maandamano hayo ni ya Amani bila kubeba silaha yoyote, maandamano yanayoruhusiwa kikatiba.
Aluta continua.