Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Kinachoingoza Tanzania ni nini? Je ni Katibaya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania au Katiba za Vyama vya Siasa na hasa Chama Tawala CCM?
Je Watanzania waliopewa majukumu na dhamana ya kuingoza Serikali yetu, utii wao ni kwa Chama cha Siasa walicho na mapenzi yao au Katiba ya Jamhuri ya Tanzania inayotoa mwongozo na mamlaka yote waliyonayo?
Imebidi kufikia hapa na kujiuliza swali hili na ni lazima tuzichambue katiba hizi, ili tujue mipaka ipo wapi, mapungufu yapo wapi, Utata uko wapi na ni nani mwenye Mamlaka na Haki kudai na kutenda kazi kwa mujibu wa Mwongozo upi?
Kwa kuwa Vyama vya Upinzani; CHADEMA, UDP, TLP, NCCR, CUF na wengne bado hawajaonja Utamu wa Madaraka na Utawala, nitaangalia mwingiliano wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya CCM.
Kifupi, katika hili, hakuna la kipi kilitangulia, ama kuku au yai, kilichotangulia na chenye Mamaka ya juu ni Katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania na si Katiba ya CCM au Ilani ya CCM hata kama CCM ndio chama Tawala na kimepewa dhamana na mamlaka ya kuongoza Tanzania.
Ila, jinsi Katiba hizi zilivyoundwa, na makusudi mazima yanayoonekana kama uzao wa makusudi au upungufu, Katiba ya Tanzania na watendaji wa Serikali ya Tanzania, huelekea kumezwa na kulazimishwa kufanya mambo kutokana na Katiba za Vyama vya Kisiasa.
Kwa mujibu wa Marekebisho ya Katiba ya Tanzania ya mwaka 1992, Utawala wa Chama Kimoja na Chama hicho kujumuishwa ndani ya Katiba ulikoma. Lakini, Udhaifu wa Sheria hii na Katiba ni Upendeleo maalum, uliopewa CCM kwa kuruhusiwa kuendelea na shughuli zake kama Chama bila kupita Usajili na masharti kama vyama vingine vilivyopaswa.
Sheria ya kuunda vyama vingi inasema na kueleza haya katika Kipengele cha nne
Halafu Katiba ya Tanzania inasema hivi
Sehemu ya 8 ya Katiba inazungumza kwa uwazi kuhusu yafuatayo (mkazo ni wangu)
Kisha ile sehemu ninayoipenda kuliko zote hufuata katika kipengele cha 27 cha Katiba ya Jamhui
Nikiruka sehemu zingine na kwenda kwenye Urais, Katiba ya Tanzania inasema hivi kuhusu Urais na Mamlaka ya Serikali ya Jamhuri wa Muungano
Katiba ya Tanzania inasema hivi kuhusu kiti cha Urais kuwa wazi na Uchaguzi wa Urais
Sifa za mtu kuchaguliwa kuwa Rais ni
Sasa nikihamia kwenye Katiba ya CCM ya mwaka 2007, nitaanza mkutano mkuu katika vipengele hivi
NEC baadhi ya majukumu yake ni haya
Hivyo mtaona mkorogano ulioko ndani ya Katiba ya nchi ambao hutoa nguvu na mamlaka kwa Serikali, lakini CCM nayo ina ubavu wake na nguvu ambazo zinaweza kuleta mgongano na katiba ya Jamhuri hasa la mwanachama wa CCM kuvuliwa uanachama baada ya NEC kuamua.
Kilichotokea Dodoma majuzi, je walengwa walikuwa ni Sitta na "Wapiganaji" wenzake, au walioleta vitisho hivi vya kutimuana Uanachama walikuwa wakipima Upepo ili kujua kama malengo yao ya Mapinduzi bila kumwaga damu yanaweza kufanikiwa bila kushirikisha ngazi na hatua za Kiserikali?
Je Watanzania waliopewa majukumu na dhamana ya kuingoza Serikali yetu, utii wao ni kwa Chama cha Siasa walicho na mapenzi yao au Katiba ya Jamhuri ya Tanzania inayotoa mwongozo na mamlaka yote waliyonayo?
Imebidi kufikia hapa na kujiuliza swali hili na ni lazima tuzichambue katiba hizi, ili tujue mipaka ipo wapi, mapungufu yapo wapi, Utata uko wapi na ni nani mwenye Mamlaka na Haki kudai na kutenda kazi kwa mujibu wa Mwongozo upi?
Kwa kuwa Vyama vya Upinzani; CHADEMA, UDP, TLP, NCCR, CUF na wengne bado hawajaonja Utamu wa Madaraka na Utawala, nitaangalia mwingiliano wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya CCM.
Kifupi, katika hili, hakuna la kipi kilitangulia, ama kuku au yai, kilichotangulia na chenye Mamaka ya juu ni Katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania na si Katiba ya CCM au Ilani ya CCM hata kama CCM ndio chama Tawala na kimepewa dhamana na mamlaka ya kuongoza Tanzania.
Ila, jinsi Katiba hizi zilivyoundwa, na makusudi mazima yanayoonekana kama uzao wa makusudi au upungufu, Katiba ya Tanzania na watendaji wa Serikali ya Tanzania, huelekea kumezwa na kulazimishwa kufanya mambo kutokana na Katiba za Vyama vya Kisiasa.
Kwa mujibu wa Marekebisho ya Katiba ya Tanzania ya mwaka 1992, Utawala wa Chama Kimoja na Chama hicho kujumuishwa ndani ya Katiba ulikoma. Lakini, Udhaifu wa Sheria hii na Katiba ni Upendeleo maalum, uliopewa CCM kwa kuruhusiwa kuendelea na shughuli zake kama Chama bila kupita Usajili na masharti kama vyama vingine vilivyopaswa.
Sheria ya kuunda vyama vingi inasema na kueleza haya katika Kipengele cha nne
4. Ibara ya 2 ya Katiba inafanyiwa madadiliko katika ibara ndogo (2) kwa kufuta maneno "uliowekwa au kukubaliwa na Chama" na kuweka badala yake "uliowekwa na sheria au kwa mujibuwa sheria iliyotungwa na Bunge"
Halafu Katiba ya Tanzania inasema hivi
3.-(1) Jamhuri ya Muungano ni nchi ya kidemokrasia na ya kijamaa, yenye kufuata mfumo wa vyama vingi vya siasa.
(2) Mambo yote yahusuyo uandikishaji na uendeshaji wa vyama vya siasa nchini yatasimamiwa kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii na ya sheria iliyotungwa na Bunge kwa ajili hiyo.
Sehemu ya nne ya Katiba ya Jamhuri inasema wazi ni nani mwenye Mamlaka
4.-(1) Shughuli zote za Mamlaka ya Nchi katika Jamhuri ya Muungano zitatekelezwa na kudhibitiwa na vyombo viwili vyenye mamlaka ya utendaji, vyombo viwili vyenye mamlaka ya kutekeleza utoaji haki, na pia vyombo viwili vyenye mamlaka ya kutunga sheria na kusimamia utekelezaji wa shughuli za umma.
(2) Vyombo vyenye mamlaka ya utendaji vitakuwa ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, vyombo vyenye mamlaka ya kutekeleza utoaji haki vitakuwa ni Idara ya Mahakama ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Idara ya Mahakama ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, na vyombo vyenye mamlaka ya kutunga sheria na
kusimamia utekelezaji wa shughuli za umma vitakuwa ni Bunge na Baraza la Wawakilishi.
Sehemu ya 8 ya Katiba inazungumza kwa uwazi kuhusu yafuatayo (mkazo ni wangu)
8.-(1) Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Nchi inayofuata misingi ya demokrasia na haki ya kijamii, na kwa hiyo -
(a) wananchi ndio msingi wa mamlaka yote, na Serikali itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa wananchi kwa mujibu wa Katiba hii;
(b) lengo kuu la serikali litakuwa ni ustawi wa wananchi;
(c) Serikali itawajibika kwa wananchi;
(d) wananchi watashiriki katika shughuli za Serikali yao wa mujibu wa masharti ya Katiba hii.
Kisha ile sehemu ninayoipenda kuliko zote hufuata katika kipengele cha 27 cha Katiba ya Jamhui
27.-(1) Kila mtu ana wajibu wa kulinda mali asilia ya Jamhuri ya Muungano, mali ya Mamlaka ya Nchi na mali yote inayomilikiwa kwa pamoja na wananchi, na pia kuiheshimu mali ya mtu mwingine.watu ambao ndio waamuzi wa hali ya baadaye ya taifa lao.
(2) Watu wote watatakiwa na sheria kutunza vizuri mali ya
mamlaka ya nchi na ya pamoja, kupiga vita aina zote za uharibifu
na ubadhilifu, na kuendesha uchumi wa taifa kwa makini kama
Nikiruka sehemu zingine na kwenda kwenye Urais, Katiba ya Tanzania inasema hivi kuhusu Urais na Mamlaka ya Serikali ya Jamhuri wa Muungano
34.-(1) Kutakuwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano ambayo itakuwa na mamlaka juu ya mambo yote ya Muungano katika Jamhuri ya Muungano, na pia juu ya mambo mengine yote yahusuyo Tanzania Bara.
(2) Mamlaka ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano yatahusu utekelezaji na hifadhi ya Katiba hii na pia mambo mengineyo yote ambayo Bunge lina mamlaka ya kuyatungia sheria.
Katiba ya Tanzania inasema hivi kuhusu kiti cha Urais kuwa wazi na Uchaguzi wa Urais
(c) baada ya Rais kupoteza sifa za kushika nafasi madaraka ya kuchaguliwa;
Sifa za mtu kuchaguliwa kuwa Rais ni
39.-(1) Mtu hatastahili kuchaguliwa kushika kiti cha Rais wa
Jamhuri ya Muungano isipokuwa tu kama-
(a) ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya Muungano kwa mujibu wa Sheria ya Uraia.
(b) ametimiza umri wa miaka arobaini;
(c) ni mwanachama, na mgombea aliyependekezwa na
chama cha siasa;
(d) anazo sifa za kumwezesha kuwa Mbunge au Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi,
(e) katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya Uchaguzi Mkuu hajawahi kutiwa hatiani katika Mahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepa kulipa kodi yoyote ya Serikali.
Sasa nikihamia kwenye Katiba ya CCM ya mwaka 2007, nitaanza mkutano mkuu katika vipengele hivi
(5) Unapofika wakati wa uchaguzi, Mkutano Mkuu wa CCM wa Taifa utashughulikia mambo yafuatayo:-
(a) Kuwachagua Mwenyekiti wa CCM na Makamu wa Mwenyekiti wa CCM.
(b) Kuchagua jina moja la Mwanachama atakayesimama katika uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
NEC baadhi ya majukumu yake ni haya
(8) Kudumisha uangalizi juu ya vitendo vya Wanachama na Viongozi wa CCM na endapo itadhihirika kwamba tabia na mwenendo wa Mwanachama fulani vinamwondolea sifa za Uanachama au Uongozi itakuwa na uwezo wa kumwachisha au kumfukuza Uanachama au Uongozi alio nao. Kuhusu mtu aliyeachishwa au kufukuzwa Uanachama, Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa ndiyo itakayokuwa na uwezo wa mwisho wa kumrudishia Uanachama wake kwa mujibu wa Katiba, endapo itaridhika kuwa amejirekebisha.
(13) Unapofika wakati wa Uchaguzi, Halmashauri Kuu ya CCM ya TaifaMkuu wa CCM wa Taifa.
itashughulikia mambo yafuatayo:-
(a) Kuteua jina la Mwanachama atakayesimama katika uchaguzi wa
Mwenyekiti wa CCM, na majina mawili ya Wanachama watakaosimama
katika uchaguzi wa Makamu wa Mwenyekiti wa CCM.
(b) Kupendekeza kwa Mkutano Mkuu wa CCM wa Taifa majina
yasiyozidi matatu ya Wanachama wanaogombea nafasi ya Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuyawasilisha mbele ya Mkutano
(c) Kuchagua jina moja la Mwanachama atakayesimama katika uchaguzi wa Rais wa Zanzibar.(21) Kumsimamisha Mwenyekiti wa CCM au Makamu Mwenyekiti wa CCM iwapo mwenendo na utendaji wake wa kazi vinamwondolea sifa za uongozi. Hata hivyo Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa itafikisha mapendekezo yake mbele ya Mkutano Mkuu wa CCM wa Taifa kwauamuzi wa mwisho.
(22) Kumwachisha au kumfukuza Uongozi kiongozi yeyote ambaye uteuzi wake wa mwisho ulifanywa na Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa.
Hivyo mtaona mkorogano ulioko ndani ya Katiba ya nchi ambao hutoa nguvu na mamlaka kwa Serikali, lakini CCM nayo ina ubavu wake na nguvu ambazo zinaweza kuleta mgongano na katiba ya Jamhuri hasa la mwanachama wa CCM kuvuliwa uanachama baada ya NEC kuamua.
Kilichotokea Dodoma majuzi, je walengwa walikuwa ni Sitta na "Wapiganaji" wenzake, au walioleta vitisho hivi vya kutimuana Uanachama walikuwa wakipima Upepo ili kujua kama malengo yao ya Mapinduzi bila kumwaga damu yanaweza kufanikiwa bila kushirikisha ngazi na hatua za Kiserikali?