Mfungo mtukufu na kufungulia radio kwa sauti ya juu

Mhache

JF-Expert Member
Jun 20, 2008
345
24
Huu ni mwezi mtukufu kwa waumini wa dini ya Kiislamu. Mimi na mmoja wa wapenda dini. Dini ni njia ya kumcha Mungu au kumcha unayemwamini. Mimi ni mkazi wa Manzese Uzuri. Sifa mojawapo ya eneo hili ni msongamano wa nyumba ka utitiri wa sisimizi. Mlango wa nyumba yako unatazamana na wa jirani, si ajabu hata milango ya vyoo vinaangaliana.

Kero ninayoipata ni ndugu zetu hawa wakati huu wa mfungo kuweka mikanda ya dini yao na kufungulia redio kwa sauti ya juu hasa wakati wa jioni. Inakuwa ni kero kwetu kwani sisi wengine inabidi tuzime viredio vyetu vya mkulima tusikilize mikanda yao ambayo wakati mwingine tunashindwa kuielewa. Kwani hatuna mafundisho ya dini hiyo.

Ninajiuliza nifanye nini? Au nikae kimya nisubiri fadhila kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
 
Huu ni mwezi mtukufu kwa waumini wa dini ya Kiislamu. Mimi na mmoja wa wapenda dini. Dini ni njia ya kumcha Mungu au kumcha unayemwamini. Mimi ni mkazi wa Manzese Uzuri. Sifa mojawapo ya eneo hili ni msongamano wa nyumba ka utitiri wa sisimizi. Mlango wa nyumba yako unatazamana na wa jirani, si ajabu hata milango ya vyoo vinaangaliana.

Kero ninayoipata ni ndugu zetu hawa wakati huu wa mfungo kuweka mikanda ya dini yao na kufungulia redio kwa sauti ya juu hasa wakati wa jioni. Inakuwa ni kero kwetu kwani sisi wengine inabidi tuzime viredio vyetu vya mkulima tusikilize mikanda yao ambayo wakati mwingine tunashindwa kuielewa. Kwani hatuna mafundisho ya dini hiyo.

Ninajiuliza nifanye nini? Au nikae kimya nisubiri fadhila kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Pole ndugu yangu kwa madhira yanayo kukuta kutoka kwa hao jirani zako. Usiwe mnyonge ndugu yangu, chukuwa hatua za kiistaarabu, nenda kwa jirani yako anayekusumbuwa na mfahamishe kuwa anacho kisikiliza ni kitu kizuri sana kwa imani yake, ila anapaswa kuzingatia kuwa kuna majirani wanakerekwa na huo usikilizaji wake wa sauti kubwa. Na anacho kifanya ni Ithrafu na anapata dhambi kwani Uislam hautaki kuwaudhi majirani na yeye anakuudhi wewe uliye jirani yake mwema.

Uislam unasisitiza sana kuwafanyia wema wazazi wawili, kuunga undugu, kuwafanyia wema jirani, kumsaidia anayehitaji, kulea yatima, kuwa na moyo msafi usio na husda, wala chuki, kuwa na tabia njema, na mengi mengineyo yote yaliyo mema.

Sasa huyo jirani yako anaonyesha kasahau hayo, nawe ukiwa ni mmoja wa majirani zake ni jukumu lako kumkumbusha, kwani utulivu ni moja ya haki zako za msingi. Usikubali mtu wa imani yeyote haichukuwe haki yako.
 
article-0-028523B500000578-29_233x423.jpg
 
Back
Top Bottom