Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,143
- 18,774
Siku kadhaa zilizopita, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alitoa agizo kwamba kutokana na meneja wa Tanroads wa Morogoro Godwin Andalwisye kufanya uzembe wa kutoyafanyia ukaguzi madaraja ya barabara ya Morogoro hadi Dodoma na kusababisha uvunjikaji wa daraja, basi aondolewe mara moja Morogoro na kurudishwa wizarani kupangiwa kazi nyingine. Wazirir Mkuu alikasirishwa na kitendo hicho kwa kuwa fedha za kufanyia ukaguzi zilikuwapo na alibainisha kwamba daraja hilo lingefanyiwa ukaguzi lisingevunjika.
Aliporudi Morogoro kuangalia maendeleo ya kazi, Waziri Mkuu ameshangaa kukuta meneja wa Tanroads Morogoro bado hajaondolewa. Alikerwa na hilo na kuuliza kwa nini meneja huyo bado hajaondolewa licha ya agizo lake. Kwa kujiamini kabisa, Mfugale alimjibu Waziri Mkuu kwamba "Andalwisye ni mmoja wa mainjinia wachache wenye utaalamu wa ujenzi wa madaraja, kwa hiyo huduma yake bado inahitajika hapa. Wewe ulitoa agizo na mimi ndio mtekelezaji, lakini bado tunahitaji utaalamu wake".
Ukweli ni kwamba si kweli kwamba Tanzania hatuna mainjinia wa kutosha wa ujenzi wa madaraja. Wapo wengi sana. Na tangu lini amri ya Waziri Mkuu inapingwa kwa sababu anaetuhumiwa anaonekana bado anahitajika? Watumishi wangapi wanaondolewa kwa amri toka juu licha ya utumishi wao kuhitajika?
Waziri Mkuu ni kiongozi anamuwakilisha Raisi kiutendaji. Je Raisi Magufuli anaweza kutoa amri na mteule wa chini akaikiuka kwa kuwa mtu aliyetumbuliwa bado anahitajika?
Katika hali ya kawaida Mfugale anatakiwa kuwajibishwa. Kufuata protokali, alitakiwa akamuombe Waziri Mkuu Majaliwa kwamba huyo Meneja wa Morogoro abaki kwa sasa - kitu tunaita "no surprise" katika mambo ya utawala. Kitendo alichofanya Mfugale ni kumdhalilisha Waziri Mkuu na Waziri wake wa Ujenzi.
Kwani kulikuwa na ubaya gani kwa Mfugale kuteua meneja mpya wa Tanroads Mororgoro na kumpeleka Andalwisye kwenye site kama mtaalamu tu kutoka Wizarani kama ni kweli anahitajika kiasi hicho? Kwani hilo daraja ni lazima lijengwe Andalwisye akiwa ndio meneja wa Tanroads Morogoro?
Sasa suala la kujiuliza ni kwamba Mfugale ametoa wapi ujasiri wa kumvimbia Waziri Mkuu na hata Waziri wake wa Ujenzi? Mengi sana yamesemwa kuhusu uhusiano wa Magufuli na Mfugale kuhusiana na miradi ya barabara wakati Magufuli ni waziri wa ujenzi. Watu hawakushangazwa na flyover ya Tazara kupewa jina la Mfugale.
Je, hilo ndilo linalomfanya Mfugale aone kwamba yuko "untouchable" na Waziri Mkuu Majaliwa na anaweza kumvimbia? Tangu lini amri ya Waziri Mkuu inakuwa "overruled" na mtu kama Mfugale ambaye kimadaraka yuko chini ya Waziri wa Ujenzi? Kumbuka amri hii ilitolewa na Majaliwa kwa Waziri wa Ujenzi, kwa hiyo kimsingi, Mfugale amemvimbia Waziri wake wa Ujenzi pamoja na Waziri Mkuu.
Source:
Majaliwa ahoji aliyemhamisha kuendelea na kazi
PM aghast to find manager he transferred still at work
Uzembe wa TANROADS sijaanza kuuandika leo. Ukweli ni kwamba mimi nachukia watu wazembe, wawe TANROADS au Polisi au hata serikali. Ajali nyingi Tanzania naona zinatokea kwa uzembe tu wa TANROADS, pamoja na hili suala la daraja. Angalia hii thread ya 31 Dec 2019.
Ajali iliyoua watu 6 Dodoma: Wanaopaswa kukamatwa na kuwekwa ndani ni Mfugale na Meneja wa Dodoma wa TANROADS Dodoma, sio dereva wa lori
Aliporudi Morogoro kuangalia maendeleo ya kazi, Waziri Mkuu ameshangaa kukuta meneja wa Tanroads Morogoro bado hajaondolewa. Alikerwa na hilo na kuuliza kwa nini meneja huyo bado hajaondolewa licha ya agizo lake. Kwa kujiamini kabisa, Mfugale alimjibu Waziri Mkuu kwamba "Andalwisye ni mmoja wa mainjinia wachache wenye utaalamu wa ujenzi wa madaraja, kwa hiyo huduma yake bado inahitajika hapa. Wewe ulitoa agizo na mimi ndio mtekelezaji, lakini bado tunahitaji utaalamu wake".
Ukweli ni kwamba si kweli kwamba Tanzania hatuna mainjinia wa kutosha wa ujenzi wa madaraja. Wapo wengi sana. Na tangu lini amri ya Waziri Mkuu inapingwa kwa sababu anaetuhumiwa anaonekana bado anahitajika? Watumishi wangapi wanaondolewa kwa amri toka juu licha ya utumishi wao kuhitajika?
Waziri Mkuu ni kiongozi anamuwakilisha Raisi kiutendaji. Je Raisi Magufuli anaweza kutoa amri na mteule wa chini akaikiuka kwa kuwa mtu aliyetumbuliwa bado anahitajika?
Katika hali ya kawaida Mfugale anatakiwa kuwajibishwa. Kufuata protokali, alitakiwa akamuombe Waziri Mkuu Majaliwa kwamba huyo Meneja wa Morogoro abaki kwa sasa - kitu tunaita "no surprise" katika mambo ya utawala. Kitendo alichofanya Mfugale ni kumdhalilisha Waziri Mkuu na Waziri wake wa Ujenzi.
Kwani kulikuwa na ubaya gani kwa Mfugale kuteua meneja mpya wa Tanroads Mororgoro na kumpeleka Andalwisye kwenye site kama mtaalamu tu kutoka Wizarani kama ni kweli anahitajika kiasi hicho? Kwani hilo daraja ni lazima lijengwe Andalwisye akiwa ndio meneja wa Tanroads Morogoro?
Sasa suala la kujiuliza ni kwamba Mfugale ametoa wapi ujasiri wa kumvimbia Waziri Mkuu na hata Waziri wake wa Ujenzi? Mengi sana yamesemwa kuhusu uhusiano wa Magufuli na Mfugale kuhusiana na miradi ya barabara wakati Magufuli ni waziri wa ujenzi. Watu hawakushangazwa na flyover ya Tazara kupewa jina la Mfugale.
Je, hilo ndilo linalomfanya Mfugale aone kwamba yuko "untouchable" na Waziri Mkuu Majaliwa na anaweza kumvimbia? Tangu lini amri ya Waziri Mkuu inakuwa "overruled" na mtu kama Mfugale ambaye kimadaraka yuko chini ya Waziri wa Ujenzi? Kumbuka amri hii ilitolewa na Majaliwa kwa Waziri wa Ujenzi, kwa hiyo kimsingi, Mfugale amemvimbia Waziri wake wa Ujenzi pamoja na Waziri Mkuu.
Source:
Majaliwa ahoji aliyemhamisha kuendelea na kazi
PM aghast to find manager he transferred still at work
Uzembe wa TANROADS sijaanza kuuandika leo. Ukweli ni kwamba mimi nachukia watu wazembe, wawe TANROADS au Polisi au hata serikali. Ajali nyingi Tanzania naona zinatokea kwa uzembe tu wa TANROADS, pamoja na hili suala la daraja. Angalia hii thread ya 31 Dec 2019.
Ajali iliyoua watu 6 Dodoma: Wanaopaswa kukamatwa na kuwekwa ndani ni Mfugale na Meneja wa Dodoma wa TANROADS Dodoma, sio dereva wa lori