sulphadoxine
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 2,257
- 645
WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe, amewataka viongozi wa dini kuwa macho na wanasiasa wanaotumia nyumba za ibada, kujisafisha kwa jamii ili kulinda maslahi yao binafsi.
Membe aliyasema hayo juzi mjini Mtwara katika hafla fupi ya kuliombea Taifa, iliyoandaliwa na Mbunge wa Mtwara Mjini, Asnein Murji na kuwakutanisha viongozi mbalimbali wa dini za Kiislamu na Kikristu.
Alisema amani ya taifa imo shakani na kwamba kama viongozi wa kidini wataruhusu nyumba za ibada kuwa kimbilio la wanasiasa na wao kutumika katika kuwasafisha, hali hiyo inaweza kusababisha mgawanyiko katika jamii.
Alisisitiza kuwa kama viongozi hao wataruhusu hali hiyo, watakuwa wanaligawa taifa kwa sababu kila muumini atamfuata mwanasiasa wa mrengo wake.
"Viongozi wa dini msipokuwa makini mtaliingiza taifa katika Machafuko, hakuna chama chochote cha siasa kinachoweza kuvuruga amani yetu, ila ninyi viongozi wa dini mkiamua mnaweza kuvuruga amani yetu,"alisema Membe.
"Kuweni macho na wanasiasa wanaokimbilia kwenu,msikubali kutumiwa kwa kulinda maslahi ya wanasiasa, fanyeni kazi zenu za kuwajenga waumini wenu kwa mujibu wa mafundisho ya imani zenu, mkiruhusu kutumiwa na wanasiasa amani ya nchi mtaivuruga," alisisitiza.
Alisema ni jambo la faraja kuona viongozi wa dini wanakutana na kuliombea taifa bila kujali tofauti za itikadi zao na kwamba ushirikiano huo unapaswa kuendelezwa kwa kutoruhusu kugawanywa na wanasiasa.
Membe ambaye pia ni Mbunge wa Mtama, mkoani Lindi aliwataka wakazi wa mikoa ya kusini kuhakikisha kuwa wanakuwa na haki miliki ya ardhi ili kujihami dhidi ya uporaji unaoweza kujitokeza wakati mikoa hiyo itakapofunguka kiuchumi.
"Upajikanaji wa gesi mkoani Mtwara ni jambo ambalo litaifanya Mtwara na hata Lindi kuwa sehemu ya mapinduzi ya kiuchumi,shauri wangu wa bure kwenu ni kuhakikisha kuwa mnakuwa na haki miliki ya ardhi, vinginevyo mtaporwa ardhi yenu," alishauri.
Aliwataka maofisa ardhi katika mikoa hiyo, kuongeza kasi ya kupima viwanja na kuwapatia wananchi haki miliki.
Kwa upande wake, Murji, alisema lengo la hafla hiyo ni kuliombea taifa ili liondokane na matatizo.
Alisema hatua hiyo pia inalenga katika kuwawezesha viongozi wa dini kukutana na
kubadilishana mawazo.
"Nimeona ni heri kwetu kukutana viongozi wote wa dini na kuliombea Taifa ili liepukane na changamoto mbalimbali zinazolikabili, lakini pia ni vizuri kama viongozi wa dini watazingatia ushauri uliotolewa na Waziri Membe ili kunusuru uvunjifu wa amani' alisema Murji
Membe aliyasema hayo juzi mjini Mtwara katika hafla fupi ya kuliombea Taifa, iliyoandaliwa na Mbunge wa Mtwara Mjini, Asnein Murji na kuwakutanisha viongozi mbalimbali wa dini za Kiislamu na Kikristu.
Alisema amani ya taifa imo shakani na kwamba kama viongozi wa kidini wataruhusu nyumba za ibada kuwa kimbilio la wanasiasa na wao kutumika katika kuwasafisha, hali hiyo inaweza kusababisha mgawanyiko katika jamii.
Alisisitiza kuwa kama viongozi hao wataruhusu hali hiyo, watakuwa wanaligawa taifa kwa sababu kila muumini atamfuata mwanasiasa wa mrengo wake.
"Viongozi wa dini msipokuwa makini mtaliingiza taifa katika Machafuko, hakuna chama chochote cha siasa kinachoweza kuvuruga amani yetu, ila ninyi viongozi wa dini mkiamua mnaweza kuvuruga amani yetu,"alisema Membe.
"Kuweni macho na wanasiasa wanaokimbilia kwenu,msikubali kutumiwa kwa kulinda maslahi ya wanasiasa, fanyeni kazi zenu za kuwajenga waumini wenu kwa mujibu wa mafundisho ya imani zenu, mkiruhusu kutumiwa na wanasiasa amani ya nchi mtaivuruga," alisisitiza.
Alisema ni jambo la faraja kuona viongozi wa dini wanakutana na kuliombea taifa bila kujali tofauti za itikadi zao na kwamba ushirikiano huo unapaswa kuendelezwa kwa kutoruhusu kugawanywa na wanasiasa.
Membe ambaye pia ni Mbunge wa Mtama, mkoani Lindi aliwataka wakazi wa mikoa ya kusini kuhakikisha kuwa wanakuwa na haki miliki ya ardhi ili kujihami dhidi ya uporaji unaoweza kujitokeza wakati mikoa hiyo itakapofunguka kiuchumi.
"Upajikanaji wa gesi mkoani Mtwara ni jambo ambalo litaifanya Mtwara na hata Lindi kuwa sehemu ya mapinduzi ya kiuchumi,shauri wangu wa bure kwenu ni kuhakikisha kuwa mnakuwa na haki miliki ya ardhi, vinginevyo mtaporwa ardhi yenu," alishauri.
Aliwataka maofisa ardhi katika mikoa hiyo, kuongeza kasi ya kupima viwanja na kuwapatia wananchi haki miliki.
Kwa upande wake, Murji, alisema lengo la hafla hiyo ni kuliombea taifa ili liondokane na matatizo.
Alisema hatua hiyo pia inalenga katika kuwawezesha viongozi wa dini kukutana na
kubadilishana mawazo.
"Nimeona ni heri kwetu kukutana viongozi wote wa dini na kuliombea Taifa ili liepukane na changamoto mbalimbali zinazolikabili, lakini pia ni vizuri kama viongozi wa dini watazingatia ushauri uliotolewa na Waziri Membe ili kunusuru uvunjifu wa amani' alisema Murji