Mdahalo Star Tv: Nape, Jussa na Marando

Ismail Jussa Ladhu akiongea katika mdahalo uliorusha na Star Tv amesema CCM ni kilichochoka hakifai tena kupewa nafasi ya kuongoza nchi kwa hata sasa wanainchi wanajionea chama hicho kuwa ombwe la uongozi.

Akiongea kwa kujiamini amesema chama hicho hakijui mpaka leo kinasimamia itikadi gani ujamaa au ubepari.

Akielezea chama cha CHADEMA amesema kuwa ni hatari kuwa na viongozi ambao hawatembei katika maneno yao ambapo alisema CDM wamesimama kupinga posho lakini wabunge wake wanachukua posho mf. shibuda, pia katibu mkuu Wilbrod Slaa alikuwa anapinga posho na mishahara ya wabunge kuwa mikubwa lakini leo ndio amewashinikiza cdm wamlipe mshahara wa mbunge.

Kwa kweli ameongea kwa ufasaha mkubwa na amewataka viongozi wenzake kuacha malumbano na matokeo yake tujenge nchi ili tuwaletee wanainchi maendeleo.

kusema kuwa ccm haifai kuongoza nchi jusa alikuwa na maana gani wakati naye pia ni kati ya hiyo serikali ambayo haifai kwahiyo hapa anadhiirisha hajui anachoongea kwani ameshajisahau kuwa naye ni sehemu ya serikali.

kuhusu swala la chadema kupinga posho lilikuwa ni swala la principal kukataa posho na waliweza kufikisha ujumbe wao na watanzania wote akiwemo maalim seif aliyewaunga mkono CDM tulisikia na kwa idadi yao ya wabunge hakuna cha ziada ambacho wangeweza kukifanya. wanaweza kususia posho lakini hiyo sio dawa kama ki sera bado posho itaendelea kutolewa cha msingi ni kubadilisha kabisa mfumo wa kulipana posho na siyo kususia kwani kususa tu hakubadilishi sheria.

kuhusu swala slaa sioni kama hoja ni mshahara kwani mzee anastahili kila senti anayolipwa na yeye ni mtu mmoja hana uwezo wa kuilazimisha kamati kuu imlipe pesa anayotaka yeye. slaa anastahili kila senti kwa maana bila yeye sidhani chama hiki kingefika hapo kilipo na wanachama wao
hasa ndio walipaswa kupiga kelele lakini kama wao wanaunga mkono mshahara huo wewe ni nani kutoka chama kingine kuja kuoji issue za CDM.
 
Ndugu mwanaJF katika ule mdahalo uliorushwa Star Tv kati ya Nape, Marando na Jussa ni nani hasa aliyekuvutia/aliyekugusa katika suala zima kujenga hoja na kuzipangua za pande pinzani?
 
kwa mchanganyiko huu, ambulance iwe jirani tu make kuna hatari miongoni mwa hawa kupata Pressure za ghafla pale watakapozidiwa kete/hoja na kukosa wa kuwashangilia! yetu macho na masikio kuona
 
tumeusikia mdahalo ulikuwa mzuri kweli nape mwanzo alichemka mwishoni alitulia na akajibu maswali vizuri jussa amekielezea vizuri chama chake cha cuf kweli ni mwanasiasa mzuri anajua kujenga hoja na kujibu maswali, tumeelewa uliberali wa cuf. marando mmmmmm
 
Je kwenye kesi ya Babu seya ambayo ni kubaka watoto, Marando ndiye alifanikiwa ile rufaa mpaka watoto wawili wakaachiwa na mahakama ya rufaa, sasa je hapa tutasema Marando anakumbatia ubakaji?

Hivi kumbe pamoja na kutetea majambazi wa fedha EPA pia anajishughulisha na hawa mashetani? Kwa kweli CDM inajichimbia kaburi na huyu mtetezi wa mafisadi.
 
Sasambua jamvini yaliyojiri wengine hatukuweza kupata uhondo huo kisa Ngeleja katufunga speed gavana.
 
kitu pekee ninachomsifu mh Nape ni ujasiri!
ujasiri wa kutetea Chama kilichozeeka na kujaa kila aina ya Uovu, leo ameamua kuyabeba yote ya chama chake na kuyatetea mbele ya Umma....kwa ccm ya leo hata Makamba senior hawezi kuitetea kwa muda wa masaa mawili bila kutukana watu, ukimleta Wassira atapigana tu.

Mh Jussa ana uelewa mzuri wa mambo ya siasa ila tatizo lake ni wivu kwa CDM, alikuwa anapotosha hoja za CDM kwa makusudi kabisa. Issue ya KIGOMA kwa mfano ni kwamba CDM na CCM waliongoza kwa zamu siyo kwa kujichanganya kama wao walivofanya(ccm miaka 2 na nusu na CDM kadhalika), Miafaka feki ya Arusha ambayo CDM inapinga na imepelekea kuwafukuza madiwani wake yeye anachukulia kama mfano wa kuongoza pamoja,why??halafu anasema mambo ya posho ni mepesi !!kweli??karibu trillion inaishia kwenye posho halafu anasema ni mepesi.!!!?

Mabere amejitahidi sana japo approach yake siyo ya kisiasa sana, yuko kisheria zaidi. Kwa maoni yangu hoja nyepesinyepesi za kina Nape na Jusa ilikuwa kuzijibu harakaharaka na kuwaacha wakijilamba midomo,hoja ya udini hakuipangua vizuri..,hoja ya serikali mseto aliipuuza,itikadi ya CDM hakuieleza vizuri alirukaruka kama NAPE(kama inawezekana ufafanuzi wa itikadi au mlengo uelezewe vizuri kupitia platform nyingine,ijulikane CDM inafuata usocialist,ucapitalist au Uliberal na uhusianishwe na matendo ya CDM).

Leo nimefurahia zaidi mdahalo,kulikuwa na utulivu na Mwakitwange amejitahidi kumiliki mdahalo kama kawaida yake.

Ushauri: Next mdahalo ujumuishe washiriki zaidi ya mmoja kutoka kila Chama ili kusaidiana kujibu hoja na pia tuwe na muda mrefu zaidi kama ITV wanavyofanya kwenye midahalo ya katiba. TV zetu zina muda mwingi kutuonyesha miziki ya uchiuchi na matamthiliya ya hovyohovyo ila mambo ya msingi kama haya wanabaaaaaaaaana! agriii agriiiii,napata hasira mie
 
Leo magwanda yamelowa yamekuwa mazito baada ya kukutana na vichwa vya siasa, badala ya kujadili hoja nzito za ukomavu katika kufanya maamuzi na hatima ya Shibuda na ushirikiano wa karibu na kiutendaji wa Marando na wizi wa EPA mnatufuta vitu vya kitoto...owkey ngoja tujadili huo utoto, tumemshuhudia Marando anajikuna sana kwenye masaburi hivi TUNDU LUSSU lake lipo salama kweli au?
 
Ngugu zangu kuna watu wanataka kupotosha wengine: Marando hajasema anatetea Mafisadi isipokua amejibu kwamba hao anaowatetea si Mafisadi isipokua majalada ya hao wezi ambao ndio walitakiwa washitakiwe nayo,kwa nyie mnaokumbuka ndugu zangu je si kuna kipindi Mh Raisi alisema wale wezi warudishe fedha na akawapa muda wa kuzirejesha baada walisamehewa kwa hyo ndio hawa Marando anasema ana Majalada yao kwa hyo watu wasipotoshe wengine hapa hyo kauli si sahihi.

Kweli ukipenda mtu hata chongo utaliita kengeza. Kwahiyo Marando hatetei mafisadi wa EPA mpaka pale mahakama itakapowatia hatiani ndio watakua mafisadi, yaani kwa hili unataka ile presumption ya innocense until proven guilty iapply. Sasa Dr W. Slaa na orodha yake ya Mwenge yanga wale watu walihukumiwa na mahakama gani? Mbona tunajichanganya. Au tunakua wanazi tu kwa vile ni wa chama fulani.

Marando kama anataka huo uwakili wa mafisadi asijipambanue kuwa anaupiga vita ufisadi. Halafu kesho yake anasimama upande wa defense.
Akaendelee na biashara ya uwakili ya kula pesa za mafisadi huko.
 
mnh ajabu sana bw jussa kuwapondelea mbali ccm ati wamechoka na hawana jipya kwanza wamekosa mwelekeo hvo wanahitaji kupumzishwa,ssa najiuliza mbna kule zenji hawa mabwana wamefunga ndoa?
 
daaah mkuu me mwenyewe alikua anaikeeeera anvolambalamba lipz zake huku anakula ulimi, sijui alikua ana njaa?
 
Hivi kumbe pamoja na kutetea majambazi wa fedha EPA pia anajishughulisha na hawa mashetani? Kwa kweli CDM inajichimbia kaburi na huyu mtetezi wa mafisadi.
Anaetetea majambazi ni Jakaya Kikwete, yeye ndio aliwasamehe wale majambazi waliorudisha pesa za EPA ili wasishitakiwe mahakamani.
 
Wakati wa mdahalo wa Star Tv, muda mwingi Nape alikuwa anakunjuakunjua mdomo utafikiri kuna kitu anatafuana.
Hii tabia anayo JK, si kawaida ya Nape lakini nafikiri kaiga kwa mkubwa wake JK.

Kwa kweli alikuwa ananikera. Utafikiri ndio amemaliza kula

Mada zingine hazipaswi kuingia humu,mfano mada ya kimajungumajungu kama hii inatafuta nini humu? Yaani kweli kwa akili zako tuanze kula unit kwa kujadili mdomo wa NAPE kweli? hebu usiwe mvivu wa kufikiri kama huna kitu cha kuweka tukijadili acha, sio kuleta mambo ya kipuuzi great thinkers tujadilli, au basi ungepeleka mada hii huko kwenye vituko sio hapa ambapo tunahitaji mijadala yenye afya yenye kuleta mstakabali mzuri wa taifa letu, kwakweli hata mimi umenikera sana, ni bora uwe msomaji tu sio kuanzisha topic za kitoto kama hii.
 
Aaah!!!! Hahahaaaa!! JADILINI ALIVYOWAPAKATIA LEO MAGWANDA TEPETEPE MNALOOO!!!! Kumbe ndo MAANA HUWA MNAMJADILI SANA HUMU KUMBE MNAJUA KIBOKO YENU

Nakuambia hawa dawa yao ni NAPE tu jeshi la mtu mmoja.
 
Leo magwanda yamelowa yamekuwa mazito baada ya kukutana na vichwa vya siasa, badala ya kujadili hoja nzito za ukomavu katika kufanya maamuzi na hatima ya Shibuda na ushirikiano wa karibu na kiutendaji wa Marando na wizi wa EPA mnatufuta vitu vya kitoto...owkey ngoja tujadili huo utoto, tumemshuhudia Marando anajikuna sana kwenye masaburi hivi TUNDU LUSSU lake lipo salama kweli au?
mlipiga kelele madiwani madiwani kwisha kazi, sasa shibuda, twawauliza lowasa, na chenge vipi?
 
Umeshindwa kuandika Ball position?
Teh teh teh teh, achana na hiyo lugha ni ngumu kwako.
Wewe jikite zaidi kwenye lugha yako ya Kichagga, ulisoma wapi shule ya kata ya Kishumundu
 
Nape:
Usimlaum mtoto wa kiongoz kuwa kiongoz kwa kuwa wametoka ktk familia za viongoz. Mlaumu kutokana na udhaifu wake.
Kuhusu shule za kata:
hakuna safar inayoanzia mia, ccm wameanza kwa kuwa amsha wananch kwa kuwajengea shule wakat cdm wanawaamsha kwa maandamano.
Amchana Marando kuwa ndiye anayesimamia kesi za wez wa Epa, je anaamin anachotenda, anasema huu n unafk!


Hili analosema Nape ni la kweli. Hata mimi hili jambo linanikera sana. Huwezi kusimamia vita thidi ya mafisadi halafu hapo hapo ukawatetee mahakamani. Hili ni kuwachanganya raia na hasa wapiga kura. Viongozi wa CDM mnapaswa kuliangalia.

Cha kumshukuru Mungu ni kwamba CDM kinaviongozi wengi wenye upeo na walio safi. Naamini ifikapo 2015 nitasherehekea kuizika CCM na kumsimika raisi wangu Dr Slaa.
 
Back
Top Bottom