Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,405
SEHEMU YA KWANZA: UTANGULIZI
Ingawa huu ni mdahalo, kuna mambo kadhaa muhimu ambayo yanahitaji kuwekwa sawa ili kuepuka upotoshwaji wa hoja. Hivyo nitaomba uvumilivu kidogo. Taifa lipo ndani ya mjadala kali juu ya UMMA WA WATANZANIA NA KIU YA MABADILIKO. Ni dhahiri kwamba mjadala huu umezidi kupanda joto baada ya ujio wa M4C.
Suala la UMMA WA TANZANIA Kuwa na kiu ya mabadiliko halina mjadala tena, badala yake, mjadala sasa ni juu ya AINA ya Mabadiliko ambayo Umma unayahitaji, kuelekea 2015. Kwa mujibu wa wanafalsafa na wanazuoni mbalimbali, Mabadiliko katika taifa hutokea kwa njia kuu mbili ambazo ni: MAGEUZI au MAPINDUZI. Swali linalofuata ni je:
UMMA wa Tanzania Leo Una Kiu ya Mabadiliko ya Aina Gani?
Ni matumaini yangu kwamba Mdahalo huu utatupatia mwanga zaidi juu ya swali hili muhimu. Yafuatayo ni mambo makuu manne yaliyonipa hamasa ya kuja na mdahalo huu:
1. Kwanza, hisia inazidi kujengeka ndani ya jamii kwamba tunavyozidi kuelekea 2015, REACTION YA ‘DOLA' kwa M4C inazidi kuwa Counter – Revolutionary, kama vile tayari vuguvugu la mapinduzi limeanza Tanzania – kwa mfano rejea sakata la Mwangosi, na Mauaji ya Songea, Arusha na Morogoro; Hii imepelekea wananchi wengi kuwa na hisia kwamba kwa mwendo huu, hatima ya M4C inaweza kuwa ni "MAPINDUZI", kutegemeana na jinsi mwitikio wa UMMA kwa M4C, utavyoendelea kujengeka kuelekea 2015.
2. Pili, ni kauli za viongozi kadhaa wa Chadema dhidi ya mfumo wa utawala wa CCM na Serikali yake pamoja na mapungufu na madhaifu mengi yaliyopo yanayopelekea madhara kadhaa kwa watanzania walio wengi. Baadhi ya kauli za viongozi wa Chadema zinazidi kutoa hamasa kwa UMMA kwamba Mabadiliko ya Kweli yatapatikana iwapo CCM sio tu kwamba itaondolewa madarakani lakini pia iwapo CCM itazikwa moja kwa moja kwenye "Political Graveyard ya Tanzania". Kwa mfano, ni kawaida kusikia wananchi wengi wakinena kwamba: Bila ya kuiondoa CCM 2015 na kuizika moja kwa moja, Ukombozi kwa Watanzania itaendelea kuwa ni ndoto. Wananchi wanaojenga hoja kwamba CCM iendelee kuwepo baada ya 2015 pia wapo, lakini wengi ni wanachama wa CCM, sio Wapiga kura huru.
3. Tatu, ni mtazamo wa ‘elites' in Tanzania – hii ni sehemu ya watanzania (wa nje na ndani ya nchi) ambayo ina "enjoy Superior intellectual, Social & Economic Status" kutokana na viwango vyao vya elimu, exposure, access to wealth n.k.; Wengi ya Watanzania wa tabaka hili wana mtazamo wa ‘KIMAPINDUZI' kuliko ‘KIMAGEUZI' – kwa maana ya kwamba, hawaizungumzii CCM kama chama cha upinzani kitarajiwa bali Chama marehemu kitarajiwa. Ikumbukwe kwamba katika taifa lolote maskini kama Tanzania, tabaka hili lina ‘influence' kubwa sana kwenye jamii, hasa ikizingatiwa kwamba sehemu kubwa ya jamii yetu ni predominantly POOR & IGNORANT/maskini na wajinga;
4. Na Nne, ni UMMA kwa ujumla: Sehemu kubwa ya UMMA inayounga mkono M4C kwa sasa ipo katika State of Confusion, hasa katika kubaini malengo na hatima ya M4C kwa ujumla wake. Wengi wanajiuliza: Juu ya hatima ya M4C; na juu ya mbinu zinazohitajika kuleta mabadiliko, hasa ikizingatiwa kwamba Tanzania imekuwa katika mageuzi ya aina mbalimbali yenye lengo la kuboresha maisha ya wananchi, tangia mwaka 1986, huku wananchi wengi wakiendelea kulalamika kwamba hawaoni faida ya maana ya mageuzi haya;
Wanafalsafa,Mageuzi na Mapinduzi:
Viongozi Wetu na Umuhimu wa Mabadiliko Tanzania:
["To be sure, you few Waswahili, do you really expect to rule Tanzanians through coercion, When there is no hope, and then expect that they will sit quiet in peace? Peace is born of hope, when hope is gone, there will be social upheavals. I'd be surprised if these Tanzanians refuse to Rebel, why? When the majorities don't have any hope you are building a volcano. It is bound to erupt one day. Unless these people are fools (wapumbavu). Many in these countries are fools, to accept being ruled just like that. To be oppressed just like that when they have the force in numbers, they are fools (wapumbavu). So Tanzanians would be fools (wapumbavu), ****** (mazuzu), if they continue to accept to be oppressed by minority in their own country. Why?"].
"…Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nimesimama hapa kuomba trust, lazima tu-build trust. Popote pale nilipopita, nimekuta mahali ambapo kuna trust. Kama hakuna trust; kama sasa hivi we cannot do a permanent election.
Uchaguzi ulishaisha na tunatekeleza Ilani ya CCM. Kwa hiyo, lazima tu-build trust, tuko kwenye nyumba moja. Kama kifo au vurugu; wengine mnasemasema vurugu lakini vurugu tunasema ni ultimate revere. Mbele ya vurugu we are all equal. Ikitokea vurugu hapa kila mtu anabeba
sanduku anakimbia bila kujali ulikuwa opposition au kwenye Serikali kila mtu ni mkimbizi. Kwa hiyo, tusifike hapo na wote hapa ndani ya nyumba hii bila kujali upo chama gani we are all reformers.
Mheshimiwa Naibu Spika, asubuhi katika kuchangia alizungumzia about revolution. Yes, agrarian revolutions, that's what makes revolutions. If you fail agrarian reform a revolution is guaranteed. Yaani ukishindwa kumiliki ardhi, utapata mapinduzi kwa sababu ya ardhi. Katika hili Mheshimiwa Tundu Lissu amesema kama ilivyo. Lakini ukiwa ndani ya nyumba hii ya Bunge wewe si revolutionary, wewe ni reformer. Ndiyo maana tuko Bungeni. Hakuna revolutionary hapa. Sisi ni reformers, tuko hapa tunajaribu kuweka mambo yawe mazuri. Tunachangiana mawazo, tuna-add value."
******
SEHEMU YA PILI: MAANA YA MAGEUZI
Mageuzi ni mabadiliko yenye nia ya kuboresha mfumo uliopo, lengo kuu ikiwa ni kurekebisha mfumo ambao hautendei HAKI Raia, kurekebisha mfumo usiojibu kikamilifu mahitaji ya wananchi (umma), na kuondokana matumizi mabaya ya MADARAKA na RASILIMALI za Umma.
Muhimu:
MAGEUZI NCHINI TANZANIA
Tanzania imekuwa katika mageuzi makuu ya aine NNE, yenye lengo la kuboresha maisha ya wananchi, BILA YA KUONDOA MFUMO ULIOPO – Soko Huria, Ubepari, pamoja na mahusiano katika uzalishaji na umiliki wa mali ndani ya jamii.
1. MAGEUZI YA KIUCHUMI
Kwanza ni mageuzi ya kiuchumi. Haya yalianza Mwaka 1986 chini ya usimamizi wa Benki ya Dunia na Mfuko wa Kimataifa wa Fedha baada makubaliano baina ya serikali na taasisi hizi kwamba Sera ya Ujamaa na Kujitegemea ilikuwa inaligharimu taifa na wananchi kiuchumi. Mageuzi haya yalilenga na bado yanalenga kurekebisha the "MACRO ECONOMIC FUNDAMENTALS", hasa maeneo katika maeneo yafuatayo:
Muhimu:
2. MAGEUZI YA KISIASA
Pili ni mageuzi ya KISIASA. Mageuzi ya KISIASA yaliingia Tanzania miaka ya mwanzo ya tisini baada ya tume ya Nyalali kumaliza kazi yake ya kutathmini hali ya demokrasia nchini. Katika ripoti yake, Tume ya Nyalali ilikuja na mapendekezo mbalimbali yaliyopelekea kurudishwa tena kwa DEMOKRASIA YA MFUMO WA VYAMA VINGI, huku pia ikipendekeza mambo mengine muhimu yenye kulenga kuboresha Demokrasia Tanzania kama vile Mabadiliko ya Katiba ya nchi (1977) ambayo kwa kiasi kikubwa bado yalikuwa yanaipa CCM hatamu, kuimarisha Utawala wa sheria, Kutenganisha wa mihimili ya dola n.k.
3. MAGEUZI YA SEKTA YA UTUMISHI WA UMMA
Tatu ni mageuzi ya Sekta ya UMMA. Kazi ya Sekta hii ni kuhudumia Jamii. Hapa ndipo uhusiano baina ya Serikali na UMMA upo ‘established'. Kwa kawaida, watumishi wote wa umma huajiriwa kwa mujibu wa sheria na kanuni za ajira, lakini muhimu zaidi, kwa kuzingatia sifa walizonazo na katika mazingira ya ushindani; Utumishi wa UMMA hau usishi majeshi yetu ya ulinzi na usalama ingawa hata katika majeshi yetu kuna raia wachache wenye ajira kama watumishi wa UMMA. Sekta muhimu katika utumishi wa UMMA ni pamoja na zile za Elimu, Afya, Uhamiaji, Kilimo, Mifugo, Maji, Miundombinu, Ardhi, Benki Kuu, Mamlaka ya Kodi (TRA), n.k.
Lengo kuu la kuleta Mageuzi YA SEKTA YA UTUMISHI WA UMMA ni kuboresha maisha ya wananchi kwa njia kama vile:
Ili kufanikiwa katika haya, Mageuzi haya pia hulenga:
4. MAGEUZI KATIKA USIMAMIZI WA FEDHA ZA UMMA
Na Nne ni mageuzi katika Sekta ya Usimamizi wa Fedha za Umma. Mageuzi haya yanaenda sambamba na yale ya sekta ya utumishi wa UMMA, lakini haya hulenga zaidi:
Ina aminiwa kwamba Mageuzi haya yatapelekea mambo makuu matatu: KWANZA, kuimarisha The ‘Macro Economic Fundamentals' tulizokwisha ziona; PILI, Serikali itaweza kutoa huduma bora zaidi za jamii na kwa ufanisi zaidi; na TATU, maisha ya wananchi yataboreshwa, hivyo umaskini kupungua;
SEHEMU YA TATU: DHANA YA MAPINDUZI
Dhana ya mapinduzi inaweza kuangaliwa kwa njia mbalimbali. Nitajaribu kuijadili katika mazingira ambayo yenye uhusiano wa moja kwa moja na mdahalo huu;
MAANA YA MAPINDUZI
Kwa kifupi, Mapinduzi ni mabadiliko makubwa katika mpangilio na uendeshaji wa maisha ndani ya jamii husika. Mara nyingi mapinduzi hupelekea mabadiliko makubwa ya mfumo mzima wa mahusiano ya jamii, kisiasa, kiuchumi, na mara nyingine kiutamaduni. Mapinduzi hutofautiana kwa:
Kuna aina nyingi za mapinduzi, lakini nitajadili zaidi mapinduzi ya kisiasa na mapinduzi ya kijamii:
MUHIMU
2. Mapinduzi ya Kijamii: Hii ni aina ya pili ya Mapinduzi ambayo huwa na madhara makubwa zaidi katika jamii husika na huwa ya aina mbili kuu:
Lengo kuu katika Mapinduzi haya ya Kijamii ni kupangua ‘completely' mfumo uliopo, hasa mahusiano ya uzalishaji na umiliki wa mali, tofauti na mapinduzi ya Kisiasa kama tulivyoona kwamba mara nyingi huacha masuala haya kama yalivyovyo; Mara nyingi, mapinduzi ya Kijamii hubadilisha mfumo mzima wa maisha na mahusiano ya raia kiuchumi, kisiasa, kijamii, kiutamaduni n.k. Mfano mzuri ni mapinduzi ya Russia ya 1917 na yale ya Cuba mid 20[SUP]th[/SUP] century ambayo yalikuwa Marxist in nature, hence very radical – kwani yalilenga kuondoa mfumo wa kibepari na ku - install mfumo wa kijamii/kikomunisti;
Muhimu:
Kuna mapinduzi mengine ya aina mbili ambayo hayana uhusiano wa moja kwa moja na mdahalo wetu, pengine indirectly, nayo ni:
Tukijereaa kwenye Mdahalo wetu, focus yetu zaidi ipo kwenye mapinduzi ya Kisiasa na Ya Kijamii, ambapo tumeona kwamba Three Key Themes ndio hujenga dhana ya Mapinduzi:
Na pengine ni sahihi kusema kwamba M4C inabeba elements za hizi three themes ingawa haina maana kwamba M4C inalenga Mapinduzi. Vinginevyo mapinduzi huwa yanayohusisha MOVEMENTS na hulenga zaidi kubadili ‘the socio-political institutions' kwa sababu hizi institutions ndio zinazotunga sheria na kusimamia utendaji wa taasisi nyingine zote zinazogusa maisha ya kila siku ya wananchi, kwa mfano Usalama wa raia, ustawi wa maisha ya wananchi n.k. Kuna kila dalili kwamba M4C inalenga hilo, au angalau UMMA unavutiwa na M4C kutokana na hili, ingawa again, haina maana kwamba lengo kuu la M4C ni Mapinduzi.
SEHEMU YA NNE: UFUNGUZI WA MDAHALO
Baada ya kuweka mdahalo huu katika Muktadha Sahihi (Right Context) na Kujaribu kujenga Hadidu Rejea (terms of reference), yafuatayo ni masuala muhimu ya kujadili:
KWANZA, Je: Umma wa Tanzania Una Ufahamu Gani Juu ya Tofauti Hizi Baina ya MAGEUZI NA MAPINDUZI?
PILI, Je: Umma wa Tanzania Una Kiu Ya Mabadiliko Ya Aina Gani Baina ya MAGEUZI NA MAPINDUZI?
TATU, Je: Viongozi wanaoendesha "Mass Movements" wana lengo gani – kuboresha Mageuzi (Reforms) ambazo Serikali ya CCM imekuwa inazitekeleza kwa miaka 26 sasa chini ya usimamizi wa IMF na World Bank au Viongozi wanaoendesha hizi "Mass Movements" wanalenga mbali zaidi ya Mageuzi?
NNE, Je: CCM ina nafasi gani katika kipindi hiki kuelekea 2015 kujenga imani mbele ya UMMA kwamba njia sahihi ya kuelekea kwenye mabadiliko ya kweli kwa wananchi – more economic, social & political justice [kwa pamoja], ni kwa wananchi kuendelea kuiamini serikali ya CCM 2015 na kuwa wavumilivu kwamba CCM itaendeleza MAGEUZI (Reforms) katika sekta za Uchumi, Siasa, Utumishi wa Umma na Usimamizi wa Fedha za Umma, na hatimaye to deliver the promise of: MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA?
Ingawa huu ni mdahalo, kuna mambo kadhaa muhimu ambayo yanahitaji kuwekwa sawa ili kuepuka upotoshwaji wa hoja. Hivyo nitaomba uvumilivu kidogo. Taifa lipo ndani ya mjadala kali juu ya UMMA WA WATANZANIA NA KIU YA MABADILIKO. Ni dhahiri kwamba mjadala huu umezidi kupanda joto baada ya ujio wa M4C.
Suala la UMMA WA TANZANIA Kuwa na kiu ya mabadiliko halina mjadala tena, badala yake, mjadala sasa ni juu ya AINA ya Mabadiliko ambayo Umma unayahitaji, kuelekea 2015. Kwa mujibu wa wanafalsafa na wanazuoni mbalimbali, Mabadiliko katika taifa hutokea kwa njia kuu mbili ambazo ni: MAGEUZI au MAPINDUZI. Swali linalofuata ni je:
UMMA wa Tanzania Leo Una Kiu ya Mabadiliko ya Aina Gani?
Ni matumaini yangu kwamba Mdahalo huu utatupatia mwanga zaidi juu ya swali hili muhimu. Yafuatayo ni mambo makuu manne yaliyonipa hamasa ya kuja na mdahalo huu:
1. Kwanza, hisia inazidi kujengeka ndani ya jamii kwamba tunavyozidi kuelekea 2015, REACTION YA ‘DOLA' kwa M4C inazidi kuwa Counter – Revolutionary, kama vile tayari vuguvugu la mapinduzi limeanza Tanzania – kwa mfano rejea sakata la Mwangosi, na Mauaji ya Songea, Arusha na Morogoro; Hii imepelekea wananchi wengi kuwa na hisia kwamba kwa mwendo huu, hatima ya M4C inaweza kuwa ni "MAPINDUZI", kutegemeana na jinsi mwitikio wa UMMA kwa M4C, utavyoendelea kujengeka kuelekea 2015.
2. Pili, ni kauli za viongozi kadhaa wa Chadema dhidi ya mfumo wa utawala wa CCM na Serikali yake pamoja na mapungufu na madhaifu mengi yaliyopo yanayopelekea madhara kadhaa kwa watanzania walio wengi. Baadhi ya kauli za viongozi wa Chadema zinazidi kutoa hamasa kwa UMMA kwamba Mabadiliko ya Kweli yatapatikana iwapo CCM sio tu kwamba itaondolewa madarakani lakini pia iwapo CCM itazikwa moja kwa moja kwenye "Political Graveyard ya Tanzania". Kwa mfano, ni kawaida kusikia wananchi wengi wakinena kwamba: Bila ya kuiondoa CCM 2015 na kuizika moja kwa moja, Ukombozi kwa Watanzania itaendelea kuwa ni ndoto. Wananchi wanaojenga hoja kwamba CCM iendelee kuwepo baada ya 2015 pia wapo, lakini wengi ni wanachama wa CCM, sio Wapiga kura huru.
3. Tatu, ni mtazamo wa ‘elites' in Tanzania – hii ni sehemu ya watanzania (wa nje na ndani ya nchi) ambayo ina "enjoy Superior intellectual, Social & Economic Status" kutokana na viwango vyao vya elimu, exposure, access to wealth n.k.; Wengi ya Watanzania wa tabaka hili wana mtazamo wa ‘KIMAPINDUZI' kuliko ‘KIMAGEUZI' – kwa maana ya kwamba, hawaizungumzii CCM kama chama cha upinzani kitarajiwa bali Chama marehemu kitarajiwa. Ikumbukwe kwamba katika taifa lolote maskini kama Tanzania, tabaka hili lina ‘influence' kubwa sana kwenye jamii, hasa ikizingatiwa kwamba sehemu kubwa ya jamii yetu ni predominantly POOR & IGNORANT/maskini na wajinga;
4. Na Nne, ni UMMA kwa ujumla: Sehemu kubwa ya UMMA inayounga mkono M4C kwa sasa ipo katika State of Confusion, hasa katika kubaini malengo na hatima ya M4C kwa ujumla wake. Wengi wanajiuliza: Juu ya hatima ya M4C; na juu ya mbinu zinazohitajika kuleta mabadiliko, hasa ikizingatiwa kwamba Tanzania imekuwa katika mageuzi ya aina mbalimbali yenye lengo la kuboresha maisha ya wananchi, tangia mwaka 1986, huku wananchi wengi wakiendelea kulalamika kwamba hawaoni faida ya maana ya mageuzi haya;
Wanafalsafa,Mageuzi na Mapinduzi:
- ARISTOTLE:
- ISAIAH BERLIN:
Viongozi Wetu na Umuhimu wa Mabadiliko Tanzania:
- MWALIMU NYERERE [in Shivji, Issa: Critical Elements of a New Democratic Consensus in Africa, 2000]:
["To be sure, you few Waswahili, do you really expect to rule Tanzanians through coercion, When there is no hope, and then expect that they will sit quiet in peace? Peace is born of hope, when hope is gone, there will be social upheavals. I'd be surprised if these Tanzanians refuse to Rebel, why? When the majorities don't have any hope you are building a volcano. It is bound to erupt one day. Unless these people are fools (wapumbavu). Many in these countries are fools, to accept being ruled just like that. To be oppressed just like that when they have the force in numbers, they are fools (wapumbavu). So Tanzanians would be fools (wapumbavu), ****** (mazuzu), if they continue to accept to be oppressed by minority in their own country. Why?"].
- PROFESSOR ANNA TIBAIJUKA [Hansard Julai 12, 2012, akijibu hoja za wabunge].
"…Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nimesimama hapa kuomba trust, lazima tu-build trust. Popote pale nilipopita, nimekuta mahali ambapo kuna trust. Kama hakuna trust; kama sasa hivi we cannot do a permanent election.
Uchaguzi ulishaisha na tunatekeleza Ilani ya CCM. Kwa hiyo, lazima tu-build trust, tuko kwenye nyumba moja. Kama kifo au vurugu; wengine mnasemasema vurugu lakini vurugu tunasema ni ultimate revere. Mbele ya vurugu we are all equal. Ikitokea vurugu hapa kila mtu anabeba
sanduku anakimbia bila kujali ulikuwa opposition au kwenye Serikali kila mtu ni mkimbizi. Kwa hiyo, tusifike hapo na wote hapa ndani ya nyumba hii bila kujali upo chama gani we are all reformers.
Mheshimiwa Naibu Spika, asubuhi katika kuchangia alizungumzia about revolution. Yes, agrarian revolutions, that's what makes revolutions. If you fail agrarian reform a revolution is guaranteed. Yaani ukishindwa kumiliki ardhi, utapata mapinduzi kwa sababu ya ardhi. Katika hili Mheshimiwa Tundu Lissu amesema kama ilivyo. Lakini ukiwa ndani ya nyumba hii ya Bunge wewe si revolutionary, wewe ni reformer. Ndiyo maana tuko Bungeni. Hakuna revolutionary hapa. Sisi ni reformers, tuko hapa tunajaribu kuweka mambo yawe mazuri. Tunachangiana mawazo, tuna-add value."
******
SEHEMU YA PILI: MAANA YA MAGEUZI
Mageuzi ni mabadiliko yenye nia ya kuboresha mfumo uliopo, lengo kuu ikiwa ni kurekebisha mfumo ambao hautendei HAKI Raia, kurekebisha mfumo usiojibu kikamilifu mahitaji ya wananchi (umma), na kuondokana matumizi mabaya ya MADARAKA na RASILIMALI za Umma.
Muhimu:
- Tofauti na Mapinduzi, Mageuzi YANALENGA KUBORESHA MFUMO ULIOPO, SIO KUONDOA MFUMO ULIOPO.
MAGEUZI NCHINI TANZANIA
Tanzania imekuwa katika mageuzi makuu ya aine NNE, yenye lengo la kuboresha maisha ya wananchi, BILA YA KUONDOA MFUMO ULIOPO – Soko Huria, Ubepari, pamoja na mahusiano katika uzalishaji na umiliki wa mali ndani ya jamii.
1. MAGEUZI YA KIUCHUMI
Kwanza ni mageuzi ya kiuchumi. Haya yalianza Mwaka 1986 chini ya usimamizi wa Benki ya Dunia na Mfuko wa Kimataifa wa Fedha baada makubaliano baina ya serikali na taasisi hizi kwamba Sera ya Ujamaa na Kujitegemea ilikuwa inaligharimu taifa na wananchi kiuchumi. Mageuzi haya yalilenga na bado yanalenga kurekebisha the "MACRO ECONOMIC FUNDAMENTALS", hasa maeneo katika maeneo yafuatayo:
- Kukuza pato la Taifa; Kuongeza kasi ya kukua kwa uchumi; Kudhibiti deni la umma/Taifa; Kurekebisha riba katika taasisi za kifedha ili ziendane na nguvu ya soko; Kudhibiti mfumuko wa bei; Kuboresha biashara ya ndani na nje ya nchi; Kuboresha uzalishaji wa Sekta mbalimbali muhimu kwa uchumi wa taifa; Kuboresha mazingira ya Uwekezaji ili kuvutia mitaji toka ndani na kutoka nje ya nchi; & Kuimarisha Akiba ya taifa, n.k.
Muhimu:
- Chini ya Mageuzi haya ya KIUCHUMI, lengo kuu ni kuboresha hali za maisha ya watanzania kwa imani kwamba kazi hii inaweza kufanikiwa zaidi chini ya mfumo wa UBEPARI & SOKO HURIA, Kuliko Mfumo wa UJAMAA.
2. MAGEUZI YA KISIASA
Pili ni mageuzi ya KISIASA. Mageuzi ya KISIASA yaliingia Tanzania miaka ya mwanzo ya tisini baada ya tume ya Nyalali kumaliza kazi yake ya kutathmini hali ya demokrasia nchini. Katika ripoti yake, Tume ya Nyalali ilikuja na mapendekezo mbalimbali yaliyopelekea kurudishwa tena kwa DEMOKRASIA YA MFUMO WA VYAMA VINGI, huku pia ikipendekeza mambo mengine muhimu yenye kulenga kuboresha Demokrasia Tanzania kama vile Mabadiliko ya Katiba ya nchi (1977) ambayo kwa kiasi kikubwa bado yalikuwa yanaipa CCM hatamu, kuimarisha Utawala wa sheria, Kutenganisha wa mihimili ya dola n.k.
3. MAGEUZI YA SEKTA YA UTUMISHI WA UMMA
Tatu ni mageuzi ya Sekta ya UMMA. Kazi ya Sekta hii ni kuhudumia Jamii. Hapa ndipo uhusiano baina ya Serikali na UMMA upo ‘established'. Kwa kawaida, watumishi wote wa umma huajiriwa kwa mujibu wa sheria na kanuni za ajira, lakini muhimu zaidi, kwa kuzingatia sifa walizonazo na katika mazingira ya ushindani; Utumishi wa UMMA hau usishi majeshi yetu ya ulinzi na usalama ingawa hata katika majeshi yetu kuna raia wachache wenye ajira kama watumishi wa UMMA. Sekta muhimu katika utumishi wa UMMA ni pamoja na zile za Elimu, Afya, Uhamiaji, Kilimo, Mifugo, Maji, Miundombinu, Ardhi, Benki Kuu, Mamlaka ya Kodi (TRA), n.k.
Lengo kuu la kuleta Mageuzi YA SEKTA YA UTUMISHI WA UMMA ni kuboresha maisha ya wananchi kwa njia kama vile:
- Kuongeza efficiency (ufanisi) katika utoaji huduma za jamii; Kuongeza effectiveness katika utoaji wa huduma za jamii; Kujenga dhana ya professionalism katika utoaji wa huduma za jamii; Kujenga dhana ya uwajibikaji, n.k.
Ili kufanikiwa katika haya, Mageuzi haya pia hulenga:
- Kupunguza mianya ya rushwa; Kuboresha usimamizi wa rasilimali watu; Kuboresha mishahara ya watumishi wa umma kama njia ya kuwaongezea motisha kiutendaji; Kujenga mazingira ya transparency (uwazi); Kujenga nidhamu, hasa ya matumizi ya fedha za walipa kodi (fiscal discipline), n.k.
4. MAGEUZI KATIKA USIMAMIZI WA FEDHA ZA UMMA
Na Nne ni mageuzi katika Sekta ya Usimamizi wa Fedha za Umma. Mageuzi haya yanaenda sambamba na yale ya sekta ya utumishi wa UMMA, lakini haya hulenga zaidi:
- Kuimarisha mfumo wa fedha za umma ili kuzidisha uwazi (transparency), kuimarisha uwajibikaji, kuboresha ‘responsiveness' ya "MATUMIZI YA UMMA" dhidi ya "MAHITAJI YA UMMA"; kuthibiti ufujaji wa fedha za umma; Kuimarisha uwajibikaji; kuboresha mchakato wa maandalizi wa bajeti za serikali; Kuboresha maandalizi ya sera yaendane na mahitaji ya UMMA; Kuboresha Mfumo wa fedha serikalini/Integrated Financial Management Systems; Kuhimiza matumizi ya TEKNOHAMA katika kuboresha maamuzi ya ki-sera na pia katika utoaji wa huduma za jamii (e.g. e-government/e-governance); Kuimarisha mapato ya serikali; Kusimamia na kuthibiti manunuzi ya umma; Kusimamia na kuthibiti deni la umma n.k;
Ina aminiwa kwamba Mageuzi haya yatapelekea mambo makuu matatu: KWANZA, kuimarisha The ‘Macro Economic Fundamentals' tulizokwisha ziona; PILI, Serikali itaweza kutoa huduma bora zaidi za jamii na kwa ufanisi zaidi; na TATU, maisha ya wananchi yataboreshwa, hivyo umaskini kupungua;
SEHEMU YA TATU: DHANA YA MAPINDUZI
Dhana ya mapinduzi inaweza kuangaliwa kwa njia mbalimbali. Nitajaribu kuijadili katika mazingira ambayo yenye uhusiano wa moja kwa moja na mdahalo huu;
MAANA YA MAPINDUZI
Kwa kifupi, Mapinduzi ni mabadiliko makubwa katika mpangilio na uendeshaji wa maisha ndani ya jamii husika. Mara nyingi mapinduzi hupelekea mabadiliko makubwa ya mfumo mzima wa mahusiano ya jamii, kisiasa, kiuchumi, na mara nyingine kiutamaduni. Mapinduzi hutofautiana kwa:
- Mbinu;
- Muda/Duration kufanikisha mapinduzi; na
- Msukumo/hamasa, mfano kiitikadi n.k;
Kuna aina nyingi za mapinduzi, lakini nitajadili zaidi mapinduzi ya kisiasa na mapinduzi ya kijamii:
- Mapinduzi ya Kisiasa: Haya yanalenga kuondoa kwa nguvu (nje ya utaratibu wa KIKATIBA) serikali iliyopo madarakani pamoja na mfumo mzima wa dola; Lengo kuu la mapindizu ya kisiasa huwa ni kuondokana na utawala wa kidikteka, utawala usioheshimu Demokrasia na haki za raia, utawala wa kifisadi unaonufaisha wachache na kuumiza walio wengi, n.k. Mara nyingi mapinduzi ya kisiasa uambatana na machafuko na umwagaji mkubwa wa damu;
MUHIMU
- Mara nyingi, Mapinduzi ya KISIASA hulenga tu kuondoa serikali iliyopo madarakani pamoja na mfumo mzima wa dola LAKINI HAYAGUSI mahusiano yaliyopo ndani ya jamii, hasa katika uzalishaji na umiliki wa mali; Mfano mzuri wa mapinduzi ya namna hii ni yale ya Ufaransa (1789) na mengine mengi, ambapo dola iliyopo madarakani uangushwa lakini mahusiano katika Uzalishaji na Umiliki wa mali hubaki kama yalivyo;
2. Mapinduzi ya Kijamii: Hii ni aina ya pili ya Mapinduzi ambayo huwa na madhara makubwa zaidi katika jamii husika na huwa ya aina mbili kuu:
- Kwanza – ni Yale ambayo ni BOTTOM – UP - yanaendeshwa zaidi na nguvu ya UMMA (tofauti na yale ambayo ni more 'top – down'). Mfano mzuri ni mapinduzi yaliyotokea Afrika ya Kaskazini hivi karibuni.
- Pili ni yale ambayo ni TOP – BOTTOM – yanayoongozwa zaidi na certain personalities, na mara nyingi a vanguard party, kama vile Chama cha kikomunisti.
Lengo kuu katika Mapinduzi haya ya Kijamii ni kupangua ‘completely' mfumo uliopo, hasa mahusiano ya uzalishaji na umiliki wa mali, tofauti na mapinduzi ya Kisiasa kama tulivyoona kwamba mara nyingi huacha masuala haya kama yalivyovyo; Mara nyingi, mapinduzi ya Kijamii hubadilisha mfumo mzima wa maisha na mahusiano ya raia kiuchumi, kisiasa, kijamii, kiutamaduni n.k. Mfano mzuri ni mapinduzi ya Russia ya 1917 na yale ya Cuba mid 20[SUP]th[/SUP] century ambayo yalikuwa Marxist in nature, hence very radical – kwani yalilenga kuondoa mfumo wa kibepari na ku - install mfumo wa kijamii/kikomunisti;
Muhimu:
- Pamoja na kwamba Mapinduzi ya aina hii hubadilisha mfumo mzima wa kijamii na kiuchumi, hasa mahusiano katika uzalishaji na umiliki wa mali, bado haina maana kwamba walio wengi (kwa mfano WAKULIMA NA WAFANYAKAZI), ndio wanakuwa wamiliki wapya moja kwa moja wa mali na njia kuu za uchumi, badala yake, uthibiti na usimamizi wa uzalishaji na usambazaji mali na mitaji huenda kwa to the new "ELITE", wanaojificha nyuma ya chama cha KIKOMUNISTI au Serikali ya Kijeshi.
Kuna mapinduzi mengine ya aina mbili ambayo hayana uhusiano wa moja kwa moja na mdahalo wetu, pengine indirectly, nayo ni:
- Mapinduzi yenye Orientation ya KIDINI ambayo hutokea zaidi kwenye jamii ambazo aina fulani ya dini ndio predominant; na
- Mapinduzi yasiokuwa na uhusiano wa moja kwa moja wa kisiasa au kijamii lakini yenye madhara kwenye jamii husika, pengine kulika mapinduzi mengine tuliyokwisha jadili, kwa mfano mapinduzi ya Kilimo, Mapinduzi ya Viwanda n.k.
Tukijereaa kwenye Mdahalo wetu, focus yetu zaidi ipo kwenye mapinduzi ya Kisiasa na Ya Kijamii, ambapo tumeona kwamba Three Key Themes ndio hujenga dhana ya Mapinduzi:
- Mobilization of the Mass
- Movement of the Mass
- Regime Change
Na pengine ni sahihi kusema kwamba M4C inabeba elements za hizi three themes ingawa haina maana kwamba M4C inalenga Mapinduzi. Vinginevyo mapinduzi huwa yanayohusisha MOVEMENTS na hulenga zaidi kubadili ‘the socio-political institutions' kwa sababu hizi institutions ndio zinazotunga sheria na kusimamia utendaji wa taasisi nyingine zote zinazogusa maisha ya kila siku ya wananchi, kwa mfano Usalama wa raia, ustawi wa maisha ya wananchi n.k. Kuna kila dalili kwamba M4C inalenga hilo, au angalau UMMA unavutiwa na M4C kutokana na hili, ingawa again, haina maana kwamba lengo kuu la M4C ni Mapinduzi.
SEHEMU YA NNE: UFUNGUZI WA MDAHALO
Baada ya kuweka mdahalo huu katika Muktadha Sahihi (Right Context) na Kujaribu kujenga Hadidu Rejea (terms of reference), yafuatayo ni masuala muhimu ya kujadili:
KWANZA, Je: Umma wa Tanzania Una Ufahamu Gani Juu ya Tofauti Hizi Baina ya MAGEUZI NA MAPINDUZI?
PILI, Je: Umma wa Tanzania Una Kiu Ya Mabadiliko Ya Aina Gani Baina ya MAGEUZI NA MAPINDUZI?
TATU, Je: Viongozi wanaoendesha "Mass Movements" wana lengo gani – kuboresha Mageuzi (Reforms) ambazo Serikali ya CCM imekuwa inazitekeleza kwa miaka 26 sasa chini ya usimamizi wa IMF na World Bank au Viongozi wanaoendesha hizi "Mass Movements" wanalenga mbali zaidi ya Mageuzi?
NNE, Je: CCM ina nafasi gani katika kipindi hiki kuelekea 2015 kujenga imani mbele ya UMMA kwamba njia sahihi ya kuelekea kwenye mabadiliko ya kweli kwa wananchi – more economic, social & political justice [kwa pamoja], ni kwa wananchi kuendelea kuiamini serikali ya CCM 2015 na kuwa wavumilivu kwamba CCM itaendeleza MAGEUZI (Reforms) katika sekta za Uchumi, Siasa, Utumishi wa Umma na Usimamizi wa Fedha za Umma, na hatimaye to deliver the promise of: MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA?