MDAHALO: M4C, Hatima ni Mageuzi au Mapinduzi?

Kwa maoni yangu M4C inapaswa kuja na Package ya mageuzi ya kiujumla kwa watanzania kutokana na kwamba mapokeo yake na wananchi yamekuwa makubwa kupita kiasi, Kwa utafiti wangu mdogo nimeona walinzi wa M4C ni wananchi kwa uwingi na ujumla wao, nimeona wengi wamekuwa watetezi wakuu wa Chadema na hawapendi waguswe kwa namna yeyote kwa namna nyingine kama chama wameweza kushawishi jamii iweze kuwaonea huruma na kuwaamini katika yale wanayooamini kama dira ya mageuzi.

Kwa sasa unaweza ukasoma saikolojia ya wananchi ukaona kwamba wanachotaka ni kwamba CCM isiwepo madarakani na ukiuliza sababu wengi watakwambia wamechoka hawataki hata kusikia, ni hii hali unaweza kuithibitisha kwa jinsi wananchi wanavyokataa kupokea maneno, hotuba au maelezo, taarifa kutoka kwa watu wanaoonekana wako upande wa CCM, yaani wananchi hawaamini tena mfumo wa aina yeyote wa kiuongozi wa CCM iwe kiutawala au kiserikali au kichama unaweza kuyathibitisha haya ka njia mbalimbali ukisikiliza mawazo ya wananchi kwa mfano wanaposhiriki kwenye vipindi vya redio,televisioni,midahalo,makongamano unaona kabisa roho na nafsi zao zimegeuka na hawana tena mapenzi na CCM.

Sasa basi nikija kwenye mjadala kama M4C inaelekeza Mageuzi au Mapinduzi mimi kwa nafsi yangu naona ni mageuzi kwa sababu wametumia njia ya ushawishi,uwepo,na ukaribu na wananchi kutia hamasa kwenye vichwa vya wananchi na kuwaaaminisha wananchi kwamba CCM imefikia kikomo cha uwezo wa utawala,lakini ni lile la kufanya mambo kwa kushirikisha wananchi na kuwapa imani kwamba mwananchi yuko juu ya watawala,hili limepelekea kuongeza nguvu ya wananchi kujiamini na kujua kwamba wanaweza kudai haki zao.

Sasa ni juu ya CCM kupambana na kuweza kuweka misingi imara ya chama chao,kuondoa makundi ikitokea hata ikishindwa isije ikawa kama vyama vingine vya ukombo bali kibaki kujipanga na kurudi madarakani tena .
 
PILI, Je: Umma wa Tanzania Una Kiu Ya Mabadiliko Ya Aina Gani Baina ya MAGEUZI NA MAPINDUZI?

Nafikiri swali hili la pili is the key question. Hayo maswali mengine depend on this one. Ni vigumu kwa Mtanzania wa kawaida kujua tofauti kati ya mageuzi na mapinduzi kama hana kiu ya either of them or both. Kwa sasa sidhani kama Watanzania wengi wana kiu ya mabadiliko. Hawana mpango wowote wa kufanya mageuzi au mapinduzi kwa sababu wengi wanaona matatizo yanayowakabili ni sehemu ya maisha yao. Wameishi na haya matatizo kwa muda mrefu sana kiasi cha kuona kuwa ni sehemu ya maisha yao.

Hata hiyo, wako wachache kama wewe ambao wameelimika kidogo na kugundua kuwa Mtanzania anaweza kuwa na maisha bora zaidi haya aliyonayo. Lakini baada ya kugundua hivyo, wanajikuta wanasikitika tuu jinsi hali ilivyo. They
are sad, but not angry with their bad lives. Na kama alivyosema Malcolm X, watu wakiwa na masikitiko hawafanyi chochote. Wanalialia tuu na hali zao mbaya. Wakipatwa na hasira ndiyo wanakuwa na urge ya kutaka mabadiliko.

Kwa kujibu swali lako basi, umma wa Tanzania hauna kiu ya mabadiliko aidha ya mageuzi au mapinduzi kwa sababu umma huu hauna hata hiyo kiu. They aren't ready for any sort of change yet. Haya tunayoona sasa ni kelele tuu za masikitiko ya hali mbaya iliyopo. Majority of Tanzanians are simply sad. They aren't angry yet na ndio maana tunalalama tuu.


Tumekubali matatizo yanayotukabili kuwa part ya maisha yetu. Matokeo yake tumeishia kulalamika tuu bila kuchukua concrete action to eradicate the problems. Angalia hiyo picha hapo chini na jaribu kujiuliza kama inafikia hatua ya Watanzania kama hao kuyakubali matatizo kuwa part ya maisha. There is nothing you can do about it mpaka wenyewe wapatwe na hasira kuwa we don't deserve this anymore. Wapo pia wengi tuu wanaonufaika na hali iliyopo sasa.

30e4_46bb.jpg


Kama nilivyowahi kuandika huko nyuma kwenye thread ya Masanilo on mapinduzi yaja Tanzania Watanzania wengi hata hapa hapa JF wanaamini kuwa there is nothing they can do about the problems they are facing. So, they have left them to God to fix their problems. Ndiyo maana hata kwenye hii M4C unasikia wanasema sijui "wao wana pesa sisi tuna Mungu." Kila changes wanategemea miujiza ya Mungu. Hata wakati wa Mapinduzi ya Tunisia na Misri watu hapa walikuwa wanamwomba Mungu yatokee pia Tanzania wakati wao wako baa wanakunywa.

Then, jaribu kupitia blogs za Wakenya. They don't mention God in their comments, unless ni issue ya kidini. They don't depend on God to fix their problems. Kama Wakenya walikuwa wanamtegemea Mungu hata hiyo katiba mpya wasingeipata. Mungu atakupa mwongozo tuu wa kutatua matatizo yako. Lakini for us, we just sit there praying for God to fix our little problems bila hata kuchukua effort yoyote.
The LORD will give strength - prosperity in our secular affairs, success in our enterprises and his blessing upon our fields and cattle. But if you don't have enterprises, fields and cattle, then there will be no blessing. The LORD cannot bless for nothing.

Kuna watu hapa huwa wanasema kuwa adui namba moja kwa Tanzania ni CCM. Kwamba
CCM ndio liability kwa taifa. Realistically, that is not the case. Watanzania wote kwa ujumla ndio liability kwa faifa. That is the naked truth. Hata ukireplace CCM na kuweka CUF, Chadema, NCCR Mageuzi etc, we will still face the same problems, unless and until sisi Watanzania wenyewe tubadilike. Kama hujaoga mwezi, ukivaa nguo mpya bado utanuka tuu!

Many Tanzanians believe that "things have fallen apart" and that "It is no Longer at Ease" like it used to be. But they're doing nothing because they strongly believe "A Man of the People" or God will come around and rescue them. There are also those who believe that "The Beautiful Ones are not yet Born", kwa hiyo wanasubiri mpaka wazuri wazaliwe kwanza ili walete changes. Lakini naamini kabisa the majority of Tanzanians are afraid of "The Petals of Bloods" ndiyo maana tunasizitiza amani na utulivu. We're afraid to face "The Trial of Dedan Kimathi". As a result, hatuna hata kiu ya mabadiliko au mapinduzi.
 
Mkuu Pasco, Nashukuru sana kwa mchango wako mzuri.

Tangu uhuru mpaka hapa tulipofikia, CCM ndio imetifikisha hapa, na hapa ndio mwisho wa uwezo wa CCM!, nikimaanisha "CCM CAN NOT DO ANYTHING MORE THAT WHAT IT CAN"!, kwa maana hiyo ninamaanisha ili taifa liweze kusonga mbele, CHANGES are innevatible, unless tunaendelea kukubali kupiga mark time hapa tulipo!
Nakubaliana na proverb kwamba: “A Man Can Do No More Than What He Can” pamoja na application yako Ki- CCM. Lakini Je, na wewe unakubaliana na Mimi kwamba “CCM Does What It Can”, and Chadema Can Do What CCM Will”?
…. kwa maana hiyo ninamaanisha ili taifa liweze kusonga mbele, CHANGES are innevatible, unless tunaendelea kukubali kupiga mark time hapa tulipo!

Nakubaliana na wewe kwamba Changes are INEVITABLE, ndio maana vuguvugu la M4C kwa mtazamo wangu lazima litazamwe kwa umakini sana kwani linaweza kuzaa mabadiliko ya aina mbalimbali, mengine ambayo pengine hayakutegemewa lakini yote itategemeana na maamuzi ya UMMA juu ya aina ya Mabadiliko wanayotaka na Mbinu sahihi za kuwafikisha huko. Kwa mtazamo wangu, M4C ni amsha amsha ili wananchi wajue nini kinaendelea katika maisha yanayowazunguka huku ikiamini kwamba Once wakitambua hilo, Aina ya Mabadiliko Na Mbinu sahihi za mabadiliko, yatabaki kuwa Chaguo lao UMMA wenyewe. Ndio maana napenda kusisitiza tena kwamba kwenye mdahalo huu, sina maana kwamba Chadema inataka kuleta mapinduzi ingawa kama tunakubaliana na Aristotle kwamba “Mzazi wa Mapinduzi ni Ufukara na Uhalifu”, na pia kama maneno ya Mwalimu Nyerere kuhusu nchi kufikia hatua kama VOLCANO inayochemka, yanatuingia vizuri, basi tusije shangaa kuona siku moja M4C inageuzwa na UMMA kuwa daraja la kuleta mabadiliko “Very Radical”.

CCM inayo nafasi ya ku proove kwa umma wa Watanzania kuwa bado inao uwezo wa kuleta reforms kwa njia ya change for the better, ikiwa na something in the hand to show kuwa I did, this, I did that, such that if elected again, I can do this and that!. "a bird in the hand, woth two in the bush"!. Yaani kwa CCM "moja shika sii kumi nenda rudi"!. CCM ndio huyo ndege mmoja, anacho cha kuonyesha!, Chadema haina kitu cha kuonyesha isipokuwa ahadi kuwa nikipewa nchi, nitafanya hili na kile!, but with nothing to show, hivyo CCM hapa ndio yenye advantage!.
Chadema nayo kwa upande wake, kupitia M4C, inao mtihani mgumu, wa kuwa convince Watanzania kuwa kwa kipindi cha miaka 50, CCM imeshindwa kuondoa wale maadui wetu watatu wa ujinga, umasikini na maradhi, on top of that, imeongeza maadui wengine wawili, rushwa na ufisadi, hivyo CCM hata ikipewa miaka 100 mingine ya kuendelea kutawala, haitaweza kubadili chochote kwa sababu hapo ilipofika, ndio mwisho wa uwezo wake!. "CCM CAN DO NO MORE THAN WHAT IT CAN"!.

Nakubaliana na wewe kwamba CCM ina advantage kwa sababu inaa mambo mengi ambayo inaweza yaweka mezani na kuwaambia wananchi kwamba tumefanya hiki na kile huku Chadema wakiwa hawana kitu. Nadhani huu ni ujumbe muhimu kwa Chadema na wanaufahamu vizuri lakini hawaufanyii kazi ipasavyo. Chadema inatakiwa waanze kutumia studies na research zilizojaa chungu nzima za wataalam mbali mbali wa ndani na nje ya nchi zinazoelezea kwa ufasaha juu ya nini kifanyike kutokomeza umaskini Tanzania. Vile vile Chadema pia ni muhimu waunde idara ya utafiti na takwimu ili isimamie kazi hii kwa ufasaha. Vinginevyo kutegemea Ilani zinazotengenezwa Board Room kwa wiki moja haisaidii kitu, ndio maana ilani za kila chaguzi zinapishana. Vinginevyo umaskini wa wananchi upo persistent for 50 years – same enemies wa Maendeleo – Ujinga, Maradhi, Umaskini, hivyo ideas to resolve this predicament ought to be consistent, sio flip flaps kila chaguzi kupitia Ilani. This is where research comes handy.

Kitu kingine muhimu pia ni kwa Chadema waanze kutumia M4C kama “FACT FINDING MISSION”, kama vile Mwalimu alivyofanya katika ziara zake vijijini mara tu baada ya uhuru - alipomuachia Kawawa uongozi wa nchi; Aliyoyasikia na kuyakuta huko vijijini yalichangia sana kuanzishwa kwa sera ya Ujamaa; Chadema waendelee kutumia M4C kuamsha wananchi ili waelewe mazingira yao na haki zao za kisiasa, kiuchumi na kijamii, lakini pia watumie fursa hiyo kutambulisha potential candidate (s) wa 2015 kwani muda wa kutembeza mgombea hautatosha;

Lakini muhimu zaidi, ni suala la ‘Fact Finding Mission’, na wawe wanarudi kila mara kwenye drawing board na kuchanganya uhalisia wa mambo on the ground na tafiti nyingine mbalimbali kuhusu hali za maisha ya wananchi mkoa kwa mkoa/kanda kwa kanda, na mapendekezo mbali mbali ya wataalam jinsi gani umaskini unaweza punguzwa iin PRACTICE, kwani mawazo haya Watawala wengi chini ya CCM wanayapuuza; Chadema wakifanya haya na wakirudi kwenye Kampeni na kuuza sera zao na mipango yao mbadala, wata connect vizuri sana na UMMA, kwani Umma utagundua kwamba kumbe Chadema wanajua matatizo yetu na wana mapendekezo mengi ya kitaalam ambayo yamejaribiwa kwenye jamii zinazofanana na sisi huko Latin America au South Asia, na majaribio haya yamezaa matunda huko;

2010 Taanzania ikiwa na population ya watu milioni 40, eligible voters were 25 milions. Waliojindikisha ni 20 milions. Waliopiga kura ni 8 milions, walioichagua CCM ni 6 milions!. Ukisoma website ya CCM, wanajitapa wana wanachama milioni 6!, hivyo CCM ilichaguliwa na wale wana CCM milioni 6 suppose wote walijiandikisha na kupiga kura!. 2015 tutakuwa milioni 50, eligible voters milioni 30!. Nimewashauri Chadema, kuwa M4C iachane kabisa na CCM!, ijikite kuzitafuta zile kura milioni 20 ambazo CCM haiwezi kuzivuna ili tupate mabadiliko kwa njia ya amani kupitia ballot box!.

Upo sahihi katika hili; Mdau mwenzetu Mkandara pia aliwahi jadili suala hili vizuri sana pale alipohimiza kwamba Operesheni ya Vua Gamba Vaa Gwanda ina mapungufu kwani inalenga wanachama wa CCM, badala ya Wapiga Kura. Na mimi naomba niongezee kwamba:

Chadema inatakiwa kufahamu kwamba watanzania wengi zaidi (voters) bado wapo in the ‘swing’ column in terms of kuunga mkono between Chadema na CCM, kwani jumla ya wanachama HAI wa vyama vyote vya siasa kumi na tisa (19) Tanzania sidhani kama inafika hata milioni kumi. Tukirudi kwenye hoja ya Mkandara, nakubaliana nae kwani - wanachama wa CCM ni kama milioni saba, wakati wapiga kura kwa mujibu wa database ya 2010 wapo milioni kumi na nane. Hii ina maana kwamba katika Operesheni Vua Gamba, Vaa Gwanda, Chadema inalenga less than one third ya wapiga kura Tanzania i.e. about 27% - kwani inalenga wanachama wa CCM zaidi au pengine inaamini kwamba hakuna Wapiga Kura huru wengi, badala yake ni lazima mpiga kura kwanza awe na mapenzi na CCM hata kama sio mwanachama wakati hii si kweli kwani kwa Tanzania ya leo, Utambulisho wa Watanzania wengi kwanza ni Wapiga Kura, suala la uanachama wa vyama vya siasa ni secondary;

Kwa mwenendo wa demographics za sasa Tanzania, haitakuwa ajabu wapiga kura mwaka 2015 wakafikia hata milioni 22. Pia ni dhahiri kwamba by 2015, wanachama wa CCM watapungua pengine kufikia milioni tano, nne or less kutokana na ukweli kwamba CCM inazidi kupoteza mvuto kadri siku za kuelekea 2015 zinavyozidi kuyoyoma. Sasa tuseme kwamba wanachama hawa wa CCM by 2015 wapungue kufikia milioni nne kati ya jumla ya watanzania wapiga kura tuseme milioni 22, ina maana Vua Gamba, Vaa Gwanda itakuwa inalenga only 18% ya wapiga kura kuelekea mwaka 2015.

Tuseme Chadema manages to secure wapiga kura wake wa uchaguzi mkuu uliopita (2010) i.e about 2.5 million; na tuseme kwamba Chadema inafanikiwa kuvuna 25% ya wanachama wa CCM ambao tusema watabakia Milioni nne (2015) ambao ni sawa na wanachama milioni moja; na tuseme Chadema inafanikiwa kuongeza wanachama wengine milioni mbili kutoka katika column ya independent voters katika kipindi hiki cha miaka mitatu heading towards 2015, ina maana Chadema itaingia 2015 ikiwa na supporters wa uhakika between 5 and 6 million. Je Kura hizi zinatosha? HAPANA. Idadi hii itakuwa ni less than one third ya wapiga kura wa 2015 i.e only 27%. Je, ikitokea CCM ikaweka mgombea 2015 ambae ataleta mvuto kwa wapiga kura kama ilivyotokea 2005, Chadema itavuka? HAPANA.

Hata CCM ikiweka mgombea mwenye mvuto wa wastani tu, ili mradi UMMA umeshalisikia jina lake, kwa kanuni ya mshindi ni mshindi, CCM kupata ushindi wa 50.1% dhidi ya Chadema 49.9% ni kitu kirahisi sana, hivyo CCM kuwa mshindi wa kiti cha Urais 2015. Ushindi wa Chadema sana sana, May Be (MAY BE), itakuwa ni kualikwa na CCM kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa kutokana na godo performance huko majimboni, suala ambalo litakuwa ni msiba kwa Chadema Kisiasa kwani Chadema wameshalitolea msimamo suala hili – rejea ndoa baina ya CUF na CCM 2010 Zanzibar. Mbaya zaidi ni jeraha linaloweza kutokea kwenye demokrasia yetu – kwamba Chadema wakikataa Serikali ya Umoja wa Kitaifa, Propaganda dhidi ya Chadema kwamba kimekataa ridhaa ya 49.9% ya wananchi itakuwa ni mzigo mkubwa sana kwa Chadema kisiasa; Hii ni changamoto kubwa sana kwa Chadema, na inaingia katika hoja yako kwamba – Njia kwa Chadema 2015 ni Nyeupe lakini HAWAJAJIPANGA.

Zile singles za "list of Shame", ufisadi, rushwa, etc, by 2015, zitakuwa zimeisha shuka kwenye chart ya top of the pops. 2015 Wanzania wanahitaji hit single za Tukiichagua Chadema, tutapata nini tofauti na hiki tunachopewa na CCM, concentrations isiwe just change and replace CCM with Chadema, bali lets replace CCM with Chadema because CCM imeshindwa kufanya ABCD kwa sababu ya sera zake mbovu (failed policies),ABCD na Chadema wao wakiingia, watafanya ABCD kwa kutumia policies ABCD na resources from ABCD!.

Nakubaliana na wewe katika hili ingawa kila ninaposema kwamba Suala la Ufisadi ni suala la Mpito, tafsiri inayotolewa ni mbaya. Lakini naomba hapa nipingane na wewe – pale ulipowahi kusema kwamba Hoja ya Ufisadi sio Hoja ya Kuwakomboa Watanzania; Mimi nadhani ni hoja ya kuwakomboa watanzania lakini isijitegemee na badala yake izungumziwe katika mazingira uliyoainisha hapo juu in blue.

Kwa mliongalia mjadala wa jana US, sisi pia tutatamani kuwapima vagombea wetu kwa utaratibu huu, na tuweke mecchanisim lazima wagombea washiriki debate, sio options bali a compulsory ili kuwapima, tupate kiongozi bora na sio bora kiongozi!.

Nilitazama debate na Obama didn’t perform well, lakini huo ni mjadala mwingine. Suala la msingi hapa ni umuhimu wa midahalo katika kampeni/chaguzi zetu; Kwa sababu fulani fulani, CCM ni waoga wa midahalo, na hii ni weakness kubwa sana ambayo itakuja kuimaliza CCM mchana kweupe. Tatizo la CCM ni kwamba wameamua kuingia Siasa za ushindani “Defensively”, wakati wakiamua kujipanga vizuri kuna ya ku ‘Attack’ kihoja (sio kiviroja). Suala la midahalo kukataliwa na chama lipo hata katika chaguzi za ndani - kuteua wagombea ubunge na udiwani, midahalo au mijadala inayohusu uwezo, mapugufu, na mitazamo ya wagombea haipewi nafasi kwa hoja kwamba Wote Mle ni wana CCM hivyo wakianza kutofautiana, upinzani utapata hoja za kutumia majukwaani. CCM sio chama kinachoheshimu mawazo huru na demokrasia kama wengi wanavyofikiri, na ndio maana kuelekea 2015, kinajijengea mazingira ya kuwa Chama cha WAFU.

Mwisho mkuu Pasco, nashukuru kwa kunipa compliment kuhusu michango yangu yenye value ya shilingi laki Tano; Serioudly, kama una sehemu ambazo unajua wanapenda mijadala kama hii, na nikienda kuzungumza watanilipa hizo hela, nitashukuru kwani itakuwa ni jasho langu (sio ufisadi au ujanja ujanja wa kihujuma), lakini muhimu zaidi yaliyomo yatalenga zaidi maslahi kwa umma/taifa, sio wagombea fulani fulani au chama fulani fulani.
 
Wewe ni msomi mzuri na umechambua mambo kishule zaidi lakini hizi zote ni ngonjera na hadithi za watawala wetu na mfumo fikilika. Tunataka watu wapya wenye mtizamo mpya utakaotufanya siku moja tuione tena Tanzania aliyoiacha Mjamaa halisi Nyerere.
Kwa maana hii, Mageuzi yaliyoingia Tanzania miaka 26 iliyopita (1986), ambayo literally yalitupa kwenye jalala Sera ua Ujamaa chini ya Mwalimu, Ni mageuzi ambayo hayana manufaa kwa wananchi, na ndio maana Chama kinachoyatekeleza mageuzi haya (CCM), kinazidi kupoteza Credibility na Legitimacy ya UMMA;

Ni vigumu kuwaaminisha wataTanzania wa leo kuwa kuna eti Mageuzi ya Kisiasa , kiuchumi na Kijamii yanafanyika wakati kila kukicha ni afadhali ya JANA.
Hii ina maana kwamba Watanzania wengi wala hawana ufahamu kwamba nchi imekuwa katika aina mbalimbali ya mageuzi kama nilivyojadili, kuboresha hali zao za maisha; hili ni kosa la nani i.e. Umma kutofahamu kuhusu mageuzi yanayotekelezwa na Serikali ya CCM kwa manufaa yao, miaka 26 sasa?

Time will tell CCM ni lazima IFE kwa faida ya Umoja na Amani ya watanzania, kwani bila hivyo pengo lililopo la walionacho na wasionanacho linazidi kupanuaka na hakuna dalili za kuzibwa.
Tanzania ni zaidi ya CCM. Itawezekana tu bila CCM.

Hii ni hoja ya Kimapinduzi zaidi kuliko Mageuzi, na unayoyazungumza hapa niliyajadili kwa kina kwenye original post yangu, pale nilipoainisha masuala makuu manne ambayo yamenipa hamasa kuja na mdahalo huu;
 
Tatizo si kwamba tu mfumo unaosimamiwa na CCM umeoza bali pia watu wanaosimamia mfumo huo nao pia HAWAAMINIKI!! Watanzania wamefikia hatua ya kutokuwaamini wanasiasa wote ndiyo maana wanasema "sasa ni zamu ya wengine kula" kwa nini watanzania hao hao hawasemi "sasa ni wakati wa wengine kujenga nchi yetu?"
 
Mkuu Mchambuzi,

Watanzania ni wavumilivu na wapole sana kiasi cha wakati mwingine tunaona kama tunajinyima wenyewe haki zetu za msingi tunazozifahamu kabisa!
Hii ndio volcano Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere anaizungumzia:

["To be sure, you few Waswahili, do you really expect to rule Tanzanians through coercion, When there is no hope, and then expect that they will sit quiet in peace? Peace is born of hope, when hope is gone, there will be social upheavals. I'd be surprised if these Tanzanians refuse to Rebel, why? When the majorities don't have any hope you are building a volcano. It is bound to erupt one day. Unless these people are fools (wapumbavu). Many in these countries are fools, to accept being ruled just like that. To be oppressed just like that when they have the force in numbers, they are fools (wapumbavu). So Tanzanians would be fools (wapumbavu), ****** (mazuzu), if they continue to accept to be oppressed by minority in their own country. Why?"].

M4C imeleta hamasa sana kwa kuongeza kiu ya mabadiliko lakini bado wananchi hawajui baada ya hayo mabadiliko nini kitafanyika tofauti na sasa! je kwa mfano tutatengeneza mafisadi wapya?

Kwa mtazamo wako, Umma una kiu ya mabadiliko ya aina gani?

M4C nafikiri usiwe wimbo wa kuitoa CCM madarakani tu bali tuambiwe nini kitafanyika baada ya hayo mabadiliko! Mwanadamu anakawaida ya kupigania kitu kinachompa assurance ya better future akifanikisha,je nini mkakati wa CDM wakishaingia ikulu(wasisubiri ilani ya uchaguzi tu).
Hili ni moja ya mapungufu makubwa ya Chadema kuelekea 2015; Kuna kila dalili kwamba wakienda Ikulu wataenda kuendeleza Mageuzi yanayotekelezwa na CCM sasahivi chini ya uangalizi wa World Bank na IMF; Tofauti pengine ya CCM na Chadema Ikulu itakuwa ni UFANISI KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA ZILE ZILE.

Mfano tunataka watuhumiwa wote wa ufisadi wakamatwe na kushtakiwa regardless ya cheo alichokuwa nacho,CDM hawako wazi moja kwa moja kwenye hili ingawa ndio wapiga kelele wakuu wa ufisadi.

Ndio maana kuna baadhi ya watu wanajenga hoja kwamba Suala la Ufisadi kwa Chadema is just a "SALES GIMMICK";
 
Haijalishi nikichaa vichaa makahaba washirikina ndio wanao tuongoza kuendelea nasafari ya kuulinda na kuurejesha UTU wa mtanzania iwe ni KWA MAGEUZI YA KISIASA AU MAPINDUZI lakini muhimu kwa watanzania wengi hasa wanao ikubali na kushirikiana CHADEMA nikuing'oa CCM kwanza na kuandika katiba upya itakayo leta SEREKALI YA WATU NDANI YA WATU NANCHI YAO mingineyo yatajipanga baada ya CCM kukabidhi mamlaka kwa UUMA!...Usually

When people are sad they don't do anything they just CRY over their condition but when they gel Angry they bring about a change" (MALCOLM X)

Kwa mtazamo wa Mwanafalsafa Aristotle, mabadiliko ya katiba ni Mapinduzi. Aristotle anasema kwamba, kuna aina mbili za mapinduzi, na kwa zote, the common denominator ni mabadiliko ya Kikatiba:


  • Kwanza ni mabadiliko ya katiba/kuanza upya kabisa;
  • Pili ni marekebisho ya katiba iliyopo;

Kusema ukweli sijamuelewa vizuri, lakini nazidi kumsoma na nitarejea juu ya hili zaidi mara nitakapo pata ufahamu zaidi;
 
Kwa mtazamo wangu siyo umaskini unaowafanya watanzania waichukie CCM bali utekelezaji wa sera na haki.
watanzania wengi tulitegemea wala rushwa na wahujumu uchumi wakubwa wangepelekwa mahakamani na kuchukuliwa hatua bila kujali nyadhifa zao, lakini leo tumeona yule tuliyempa jukumu la kuwaadabisha wale wa chini yake anawatetea kwa lugha za huyu hajapokea rushwa bali alipewa takrima.

Haiingii akilini hata kwa ambaye hajaenda shule wanasiasa wenye skendo bado wanaendelea kupeta na kupewa nyadhifa za juu.Na hilo ndilo linalokera kuliko yote ndio maana watanzani tuliowengi tunaichukia CCM.

Kwa mtazamo huu, wewe ni MWANAMAGEUZI - Unaamini katika Mageuzi yanayoendelea kwa miaka 26 sasa, tatizo ni utekelezaji, hivyo Chadema ikiingia Ikulu, itaenda kutekeleza Mageuzi yale yale ya CCM lakini kwa ufanisi zaidi ili kuimarisha Uwajibikaji, Kuziba Mianya ya Rushwa, Kuboresha huduma za jamii kwa wananchi, kuthibiti ufujaji wa fedha za walipa kodi n.k, mambo ambayo yapo wazi chini ya Mageuzi ya Sekta ya Utumisha wa UMMA na Mageuzi Ya Sekta ya Usimamizi wa Fedha za Umma, lakini tatizo lililopo ni kasi na ufanisi katika utekelezaji chini ya CCM;
 
Liwalo na liwe weka ccm pembeni kwanza halafu ndio tutaweza kujadili.tunataka tz a kiaje?
 
Mkuu EMT,

Nashukuru sana kwa mchango wako, na kama kawaida, ujumbe wako huwa unaingia vyema sana. Na kwa kweli picha uliyoweka hapa is "Worth One Million Words" kuelezea unachojaribu kujadili katika mdahalo huu; Kwa hili suala la watanzania kuchukulia matatizo waliyonayo kuwa ni sehemu yao ya maisha naunga mkono hoja.

Mtazamo wako kwamba ‘Swali Langu la Pili' Ndio Key Question' – nimependa mtazamo huo, na nakubaliana na wewe; Nadhani Suala la msingi hapa unalojaribu kulieleza ni Kwamba - Watanzania Wapo Katika Hali ya Kutojitambua, na ili waweze kujitambua, ni muhimu kwanza wapitiea Mapinduzi ya Fikra, halafu, ndio mabadiliko mengine yafuate; Je nipo sahihi kwa hili? Kama nipo sahihi, ni wajibu wa nani kuwasaidia wajitambue/wapitie MAPINDUZI YA FIKRA?

Hata hiyo, wako wachache kama wewe ambao wameelimika kidogo na kugundua kuwa Mtanzania anaweza kuwa na maisha bora zaidi haya aliyonayo. Lakini baada ya kugundua hivyo, wanajikuta wanasikitika tuu jinsi hali ilivyo. They are sad, but not angry with their bad lives. Na kama alivyosema Malcolm X, watu wakiwa na masikitiko hawafanyi chochote. Wanalialia tuu na hali zao mbaya. Wakipatwa na hasira ndiyo wanakuwa na urge ya kutaka mabadiliko.
Kwa kujibu swali lako basi, umma wa Tanzania hauna kiu ya mabadiliko aidha ya mageuzi au mapinduzi kwa sababu umma huu hauna hata hiyo kiu. They aren't ready for any sort of change yet. Haya tunayoona sasa ni kelele tuu za masikitiko ya hali mbaya iliyopo. Majority of Tanzanians are simply sad. They aren't angry yet na ndio maana tunalalama tuu.
Tumekubali matatizo yanayotukabili kuwa part ya maisha yetu. Matokeo yake tumeishia kulalamika tuu bila kuchukua concrete action to eradicate the problems. Angalia hiyo picha hapo chini na jaribu kujiuliza kama inafikia hatua ya Watanzania kama hao kuyakubali matatizo kuwa part ya maisha. There is nothing you can do about it mpaka wenyewe wapatwe na hasira kuwa we don't deserve this anymore. Wapo pia wengi tuu wanaonufaika na hali iliyopo sasa.

Kwa hoja hizi, mwitikio mkubwa wa UMMA kwa M4C tunao uona sasa hautoshi kuelezea Kiu au Nia waliyokuwa nayo watanzania katika kuleta mabadiliko yenye manufaa kwa maisha yao; Na Badala yake, mikusanyiko hii ni sawa na ile ya Misiba ambayo watu wanaenda kujumuika na wenzao kwa uchungu mkubwa kuomboleza tatizo linalowakabili, na baada ya maombolezo ya siku kadhaa kialaiki, taratibu akili uanza kuhamia kwenye matukio mengine, na siku chache baada ya kutawanyika, wanarejea katika hali za maisha yao ya awali, na siku zinasonga mbele. Je katika hili, pia nipo sahihi? Kama nipo sahihi, kwa mtazamo wako, Hali hii itaendelea Mpaka lini na nani anafaidika na hali hii in the Long Run – Chadema au CCM? Again – Long Run.
 
Last edited by a moderator:
Tatizo si kwamba tu mfumo unaosimamiwa na CCM umeoza bali pia watu wanaosimamia mfumo huo nao pia HAWAAMINIKI!! Watanzania wamefikia hatua ya kutokuwaamini wanasiasa wote ndiyo maana wanasema "sasa ni zamu ya wengine kula" kwa nini watanzania hao hao hawasemi "sasa ni wakati wa wengine kujenga nchi yetu?"

RENOVATION ya MFUMO uliopo ni MAGEUZI na tumekuwa katika hili kwa miaka 26 sasa, tukianza na renovation ya uchumi mwaka 1986 baada ya Nyerere kung'atuka; Hoja yako haiweki wazi iwapo suluhisho ni Renovation ya Mfumo au Ujio wa mfumo mpya;
 
Mada ni nzuri sana na inatakiwa umakini katika kuijadili!

Niliposoma kichwa cha uzi huu nikapatwa na swali moja ambalo kwa bahati njema mtoa mada amelijibu vema kabisa. Swali lililonijia lilikuwa ni je, mtoa mada amefafanua maana ya maneno mageuzi na mapinduzi...! Nikakuta ndani yamefafanuliwa.

Sasa bila kuharibu utamu wa mada, kwa muono wangu mageuzi yote muhimu naamini yameshafanyika na bado hali yetu tulio wengi bado haina matumaini ya kuiona kesho yenye neema ambayo ndiyo umekuwa wimbo wa siasa iliyo katika madaraka ya nchi hii. Kwa hali hiyo basi pengine naamini kinachotakiwa sasa ni mapinduzi katika eneo moja tu...! Nalo ni usimamizi wa mifumo iliyowekwa katika kusimamia sekta mbali mbali za kijamii, kiuchumi, kielimu, na nyinginezo nyingi ambazo wadau mnaweza kuongeza hapa.

Nitatoa mfano mmoja tu ili wengine waendeleze kwa mifano mingine......

Katika budget ya mwaka huu wa fedha tuliambiwa serikali imejipanga, inafanya mchakato, n.k. ili kuboresha na kufufua miundombinu ya reli nchini! Lakini jiulize kweli tunalenga kufufua reli wakati tunaondoa ushuru wa magari makubwa ya mizigo hadi kufikia asilimia 0?? Unadhani hawa wenye uwezo wa kuagiza malori makubwa-makubwa ya mizigo ni akina nani kama si hawa hawa wenye madaraka ya nchi hii? Na je, wakiagiza malori unadhani yatafanya kazi gani ikiwa reli itafufuka na kufanya kazi kwa ufanisi? Katikati ya maswali haya ambayo hujapata majibu yake..., jiulize la mwisho ambalo ni Je, unadhani hawa wakubwa wenye uwezo kuaingiza vichwa kuanzia 50 vya kukokota matela ya mizigo kwa wakati mmoja watakaa na kufurahia ufanisi katika sekta ya usafiri kwa njia ya reli nchini??

Ndio maana nchi inakuwa na mipango mizuri ambayo inayotekelezeka kwa vitendo lakini hawataki kuitekeleza kwa kuwa itafunga ulaji wao na kinachotokea nchi nyingine huja na kuchukua mipango yetu mizuri iliyo katika makabati ya serikali na kwenda kuitekeleza kwao na wanapiga hatua kadhaa mbele wakati sisi waasisi wa mipango hiyo tukibaki pale pale kama si kurudi nyuma!!

TUNAHITAJI MAPINDUZI KATIKA KUSIMAMIA NA KUENDESHA MAGEUZI YANAYOENDELEA....... NA HILI HALIWEZI KUFANYWA NA SAME LEVEL OF THINKING THAT CREATED ALL THESE PROBLEMS WE ARE IN!
 
Kwa maoni yangu M4C inapaswa kuja na Package ya mageuzi ya kiujumla kwa watanzania kutokana na kwamba mapokeo yake na wananchi yamekuwa makubwa kupita kiasi, Kwa utafiti wangu mdogo nimeona walinzi wa M4C ni wananchi kwa uwingi na ujumla wao,nimeona wengi wamekuwa watetezi wakuu wa Chadema na hawapendi waguswe kwa namna yeyote kwa namna nyingine kama chama wameweza kushawishi jamii iweze kuwaonea huruma na kuwaamini katika yale wanayooamini kama dira ya mageuzi

Walinzi wa M4C ni wananchi - hii ni hoja yenye mashiko kwani UMMA ndio wenye maamuzi juu ya mbinu na aina ya mabadiliko wanayotaka; Lakini je, katika suala hili la Ulinzi - Wananchi ni walinzi wa imani na itikadi ipi in the context of M4C?

Kwa sasa unaweza ukasoma saikolojia ya wananchi ukaona kwamba wanachotaka ni kwamba CCM isiwepo madarakani na ukiuliza sababu wengi watakwambia wamechoka hawataki hata kusikia,ni hii hali unaweza kuithibitisha kwa jinsi wananchi wanavyokataa kupokea maneno,hotuba au maelezo,taarifa kutoka kwa watu wanaoonekana wako upande wa CCM,yaani wananchi hawaamini tena mfumo wa aina yeyote wa kiuongozi wa CCM iwe kiutawala au kiserikali au kichama unaweza kuyathibitisha haya ka njia mbalimbali ukisikiliza mawazo ya wananchi kwa mfano wanaposhiriki kwenye vipindi vya redio,televisioni,midahalo,makongamano unaona kabisa roho na nafsi zao zimegeuka na hawana tena mapenzi na CCM.

Ndio maana CCM ikianguka 2015 sidhani kama itaweza tena kurudi madarakani, hasa iwapo Chadema ita hijack Reforms za sasa chini ya Serikali ya CCM zinazosimamiwa na WorldBank na IMF na kuzitengenezea itikadi, dira na mikakati ya muda mfupi, wa kati na mrefu; bila ya kufanya hivyo, CCM itarudi madarakani 2020; Suala muhimu hapa ni kwamba - kutokana na Ombwe la Kiitikadi linalovikabili vyama vyote vya siasa Tanzania (pamoja na CCM), itakuwa ni vigumu sana kwa CCM kurudi madarakani iwapo Chadema itaenda Ikulu kutekeleza yale yale ya CCM ya sasa (rejea mjadala wangu wa aina ya mageuzi tanzania), lakini kwa ufanisi zaidi; Lakini je, iwapo Chadema itashindwa kuing'oa CCM madarakani 2015, hasa in the context of saikolojia ya UMMA iyenye mkao ulioujadili hapo juu, nini kitafuatia? Rejea post Number 37 ya M-mbabe pia...

Sasa basi nikija kwenye mjadala kama M4C inaelekeza Mageuzi au Mapinduzi mimi kwa nafsi yangu naona ni mageuzi kwa sababu wametumia njia ya ushawishi,uwepo,na ukaribu na wananchi kutia hamasa kwenye vichwa vya wananchi na kuwaaaminisha wananchi kwamba CCM imefikia kikomo cha uwezo wa utawala,lakini ni lile la kufanya mambo kwa kushirikisha wananchi na kuwapa imani kwamba mwananchi yuko juu ya watawala,hili limepelekea kuongeza nguvu ya wananchi kujiamini na kujua kwamba wanaweza kudai haki zao

Ni tafsiri juu ya kikomo ndio iliyochangia hamasa ya kuja na mdahalo huu; Kikomo kwa maana ya kwamba wananchi wengi wanapendelea CCM ikajipange na kuwa chama cha upinzani au Kikomo kwa maana ya kwamba CCM izikwe kabisa katika medani za siasa Tanzania?

Sasa ni juu ya CCM kupambana na kuweza kuweka misingi imara ya chama chao,kuondoa makundi ikitokea hata ikishindwa isije ikawa kama vyama vingine vya ukombo bali kibaki kujipanga na kurudi madarakani tena .
Kuna kila dalili kwamba hili CCM imeshashindwa, sana sana 2015 chama kitakuja na Sales Gimmick za kuweka Kijana au Mwanamke.
 
Mkuu Mchambuzi,
............Nimewashauri Chadema, kuwa M4C iachane kabisa na CCM!, ijikite kuzitafuta zile kura milioni 20 ambazo CCM haiwezi kuzivuna ili tupate mabadiliko kwa njia ya amani kupitia ballot box!.

pasco, mbona mabadiliko mwaka 2010 hayakupatikana pamoja na chadema kushinda kiti cha urais kupitia ballot box? that's the irony!

nadhani the issue is..je, umma umejiandaaje come 2015 endapo haki yao watakayoipata kihalali kupitia ballot box itapokwa kama iliyotokea 2010?

i think this is one of the pertinent questions being asked, albeit by inference, by mchambuzi.
 
Zile sare za Chadema, zimekaa kimapinduzi zaidi zikiashiria shari kuliko heri!, as days go by, tutawashauri, watumie kitambaa chepesi zaidi kuashiria amani zaidi, kuliko kuendelea na zile khaki nzito kama kombati kuashiria wako vitani!.

Huwa unanifurahisha kwa maoni yako lakini maoni yako mara nyingi sana lazima kuwe na statement inayotoa picha harisi ya namna unavyoichukia chadema. Hivi kwanini usiyaangalie yale magwanda ya Chadema kwa mtazamo wa kwamba chadema wameshona sare zao kwa kitambaa kigumu kwasababu hawana uwezo kama CCM hivyo wanataka zidumu zaidi?
 
Mkuu karug,

Nashukuru kwa mchango wako mzuri; Niseme tu kwamba umeleta dhana mpya and very stimulating to the thoughts i.e:
"TUNAHITAJI MAPINDUZI KATIKA KUSIMAMIA NA KUENDESHA MAGEUZI YANAYOENDELEA".

Unaweza kufafanua kidogo hili mkuu – hasa iwapo inawezekana Kuleta Mapinduzi katika Mageuzi Yaliyopo bila ya kuathiri mfumo wa utawala uliopo, na vile vile mahusiano katika umiliki wa njia za uzalishaji na umiliki wa mali?

Hoja yako kwamba:

"…LAKINI HILI HALIWEZI KUFANYWA NA SAME LEVEL OF THINKING THAT CREATED ALL THESE PROBLEMS WE ARE IN!"

Je, Same Level of thinking unayomaanisha hapa ni ya kimfumo au kisera? Kwani kama ni ya kimfumo – on a Renovation Basis, hizo ni fikra za kimageuzi zaidi, lakini kama ni kimfumo – based on a Complete Overhaul ya mfumo uliopo, fikra hizi ni za kimapinduzi zaidi; Au unaposema …Haliwezi Kufanywa na Same level of thinking that created all these problems that wera are in – Unalitazama Ki-sera zaidi?

Naunga mkono hoja yako juu ya Bajeti na umhimu wake katika kutatua matatizo yanayokabili wananchi; Lakini suala hili lipo chini ya Mageuzi Ya Usimamizi wa Fedha Za Umma, na CCM na serikali yake imekuwa inatekeleza mageuzi haya kwa kipindi kirefu sasa, tatizo pengine ni ufanisi katika utekelezaji wa Mageuzi haya; Vinginevyo moja ya vilio vya wananchi walio wengi ni Suala la bajeti kutokidhi Mahitaji Yao, hasa kwa mujibu wa Vipaumbele vya wananchi wenyewe;

Baada ya sera za - Structural Adjustment Policies (SAPs) chini ya World Bank na IMF zilizoingia 1986 to replace Ujamaa kushindwa kuleta mabadiliko as promised, Criticisms mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi kwamba by mid 1990s sera hizi zilipelekea wananchi walio wengi kuwa worse off kuliko enzi za Ujamaa, World Bank na IMF walikuja na sera mbadala ambazo waliziita Poverty Reduction Strategic Papers (PRSPs), na hizi ndio zilizaa Mkukuta, pamoja na Debt Cancelations; Lakini at the core of these policies, ilikuwa ni A Participatory Approach to Budgeting – ambapo Serikali ilipewa msamaha wa madeni na wahisani lakini kwa masharti kwamba iende kwa wananchi na kusikiliza nini wanataka ziwe priorities zao, kisha hela za msamaha wa madeni ziende kujibu matakwa husika ya wananchi; Kilichotokea ni Uchwara wa Serikali ya CCM katika kutekeleza hilo and many studies zimeweka suala hili wazi;
 
Last edited by a moderator:
Chadema wanapozungumzia (M4C) wana maanisha nini? M4C inasimama badala ya movement for Change ina maana kubwa.

Mabadiliko kama mabadiliko yana maana na dhana kubwa mno ambayo inahitaji umakini kujadili kwa kina.

Dhana ya M4C ya chadema sijaielewa kabisa. Ndio maana mimi naiita "movement for power" na hii M4C ni kivuli tu cha kufikia malengo yao ambayo kwa uhakika sio yenye malengo ya kuleta mabadiliko katika nchi yetu.

Msuguano uliopo sasa hivi kati ya CCM na Chadema ni msuguano wa kugombea madaraka na hauna chochote cha kufanya kwa mabadiliko ya umma. Ni uchu ule ule wa madaraka unawaongoza viongozi wengi wa Afrika hadi kuleta machafuko katika nchi zao. Sioni tumaini lolote kwa watu wa Taifa hili litakaloletwa na watu wa vyama hivyo hata kidogo.

Tunahitaji uongozi na mwelekeo, hatujui tunapoelekea kama Taifa. Tunahitaji uongozi. Taifa hili halitopata mabadiliko yeyote pasipo uongozi. Tunahitaji kuondoka kutoka hapa tulipo. Hatuwezi kuondoka hapa tulipo pasipo Order. Na order huletwa na kiongozi madhubuti. Anayejua nini nachotaka kufanya na wapi anataka kulipeleka Taifa. Kiongozi atakayeleta umoja wa Taifa na kuonyesha dira na mwongozo. kiongozi atakayeaminika kwa wanachi kwa maneno na matendo. Atakayeonyesha mfano kwa vizazi vijavyo. Kwamba hii ni njia ambayo kama Taifa tunapaswa kupita, kwasasa mapito yetu kama Taifa hayajulikani. Kwasasa siioni baadae yetu itakuwaje hakuna tumaini la baadae na haijulikani Taifa hili litakuwaje, hakuna tumaini.

Tumaini la vizazi vyetu liko gizani kutokana na kukosa uongozi. Sisi kama taifa tunapaswa kukusanya nguvu na kukua. Lengo la Taifa lolote ni utawala na uongozi wa dunia hatujawa Taifa ili tuwe wa mwisho au tutawaliwe daima. Ni lazima tukue kama Taifa na tuonyeshe uwezo wetu na hili litafanikiwa kama tukiwa wenye nia moja.

Tunahitaji kiongozi atakayeleta tumaini na mwelekeo katika Taifa letu, tumaini ambalo limeondoka miongoni mwa mamilioni ya watu wa Taifa hili. Umoja wetu ndio msingi wa kukua na kuendelea kwa Taifa hili. Hatuwezi kukua kama kila mtu atajiangalia mwenyewe na kuacha yale ambayo yametuunganisha kama Taifa. Tutaendelea haraka zaidi na kwa kasi kama tutakuwa wamoja na kila mmoja wetu kama atajitolea kwa moyo wake wote kulijenga Taifa hili na kulipenda. Kitu ambacho kimetuunganisha sisi ni Taifa letu na ni lazima tulijenge na tuwe na mapenzi nalo.

Hatuwezi kuendelea kama tutakandamizana wenyewe kwa wenyewe tabaka moja likijiona bora zaidi ya jingine. Tutaendelea kama tutaheshimiana kama watu wa Taifa moja na wenye nia na dhamira moja ya kulijenga Taifa hili hadi kufikia kilele chake cha maendeleo na ukuaji.

Taifa limekosa uongozi ni Taifa la watu walalamikaji hakuna anayeonyesha uongozi kwa kile kinachopaswa kufanywa kama Taifa. Watu wetu lazima wajue Taifa lao linaelekea wapi na ni nini wanaamini kama TAIFA.

Taifa letu liko katika mgawanyiko mkubwa na kutoridhika kwa watu wake juu ya mwelekeo na baadae ya Taifa. Tunahitaji tumaini hili linyanyuke. Tumaini hili ambalo wazee wetu waliopigania uhuru katika Afrika waliokuwa nalo, kuiona Afrika ikijitegemea na kuwa huru. Hili ni tumaini ambalo lazima liwepo mioyoni mwetu wote na ni lazima lifanikishwe kwa kufanya kazi kwa bidii na maarifa.

Hatutaweza pasipokuwa na uongozi wenye maono, pasipo uongozi imara Afrika itaendelea kudumaa na kuwa tegemezi Daima. Lakini Afrika na Tanzania inahitaji kukua. Hii ni changamoto ambayo tunayo na inahitaji jitihada zisizofifia ili kuikamilisha ndoto yetu ya kuwa huru na watu wanaojitegemea. Sidhani pasipo umoja tunaweza kufaniisha hili. Tunahitaji viongozi wasio wabinafsi ili Afrika na Tanzania ikue. Tunahitaji viongozi wasio tetereka katika dhamira zao kuifanya Tanzania na Afrika kuwa huru na zenye kujitegemea. Hii ni vita na ni lazima ipiganwe.

Tunachangamoto katika taasisi zetu ambazo ndizo mashine katika maendeleo yetu kama Taifa. Kuna kutoridhika na kukosa uzalendo miongoni mwa wasomi wa Taifa hili. Matatizo katika mifumo yetu ya elimu na Afya. Ambayo imepelekea migogoro ya mara kwa mara baina ya serikali na watumishi hawa wa umma.

Ni dhahiri lazima tufahamu kwamba sisi sote lazima tuwe na dhamira moja ya kulijenga Taifa hili na hatutaweza kulijenga Taifa hili pasipo juhudi za pamoja na kujitolea kwa upande wa serikali na kwa upande wa watumishi wa UMMA. Serikali inawajibika kuwapelekea nyenzo na kila msaada ambao utasaidia watumishi wa umma kufanikisha kazi yao ya kutumikia umma. Lakini watumishi wa umma wanawajibika kufanya kazi kwa bidii na kwa nidhamu kutumikia watu wa Taifa lao na kuwa na mapenzi kwa Taifa lao. Hatutaweza kulisukuma gurudumu la Taifa hili pasipo jitijada za pamoja na dhamira ya pamoja.

Lazima tutengeneze serikali ya watu ambayo raia na viongozi wao watakuwa pamoja katika jitihada zao za ujenzi wa Taifa lao, kwa manufaa yao na sio kikundi kidogo cha watu au chama. Hili ni TAIFA ambalo nalihitaji ambalo kila mtu anachangia katika maendeleo ya Taifa lake kwa moyo mmoja na kujitolea, kila mtu akitambuliwa kutokana na mchango wake na kuheshimiwa. hili ndilo Taifa ninalohitaji.

Taifa ambalo litamwezesha mtu kukua na kukuza kipaji chake. Taifa la watu huru na wanaofuata na kuheshimu sheria zilizo tungwa kwa misingi ya Haki. Haya ndio mabadiliko ninayoyahitaji na hii ndio "M4C INAYOHITAJIKA KUWEPO" Kubadili mitazamo ya watu kutoka katika ubinafsi kuja katika utaifa ili tujenge Taifa hili kwa moyo mmoja na kujitolea. Hatutaweza kubadili taifa hili kama hatutakuwa wamoja. Badiliko ya kweli ni kubadili fikra na mitazamo ya watu kuhusu Taifa lao, na watakapo fikiria chanya kuhusu Taifa lao hapo ndipo mabadiliko yatakapo tokea. Ya kwamba tuna uwezo wa kukua na tunauwezo wa kuendelea na kuwa kama Taifa lolote kubwa haya ndio matumaini yangu.

Watu wa Taifa hili wanahitaji kukua, wanahitaji kuona Taifa lao likinyanyuka na kuendelea, wanahitaji kuona Taifa lao likiwa Imara wamechoshwa na udhaifu. We will only achieve this if we have strong leadership. We can move as the Nation, we can be strong and independent. We have that potential.

Tuna mapambano mawili kuwaondoa viongozi mafisadi wote nchini mwetu lakini tunawajibu wa kulijenga na kuliendeleza Taifa hili kwa moyo wetu wote bila kubakiza kitu. Mapambano yetu sio kuondoa ufisadi tu bali kujenga nchi. Kujenga jamii zetu na kuleta ustaarabu. Kuleta umoja wa kitaifa na Wajibu. Tunaweza kuondoa chama kimoja tukikiingiza chama kingine cha kifisadi na nchi yetu ikaendelea kuwa palepale. Kinachojalisha ni mawazo mapya yatakayokuja na kubadilisha dira na mwelekeo wa Taifa hili kama upepo wa kisulisuli. Kuleta uzalendo na uwajibikaji katika Taifa.

Mabadiliko ya kweli katika Taifa hili yatakuja kutoka katika mabadiliko ya Fikra na Chama. Kwakuwa chama kinaweza kuwa Reformed kwa kubadili mitazamo yake na mwelekeo wake kinapoona kinakosea, wanapobadilika wanaweza kubadili dira na mwelekeo wa nchi.

Chadema na movement for Change ni propaganda tu. Wanaweza kuingia madarakani lakini maisha ya watu yakaendelea kuwa duni na yasiyo na matumaini. Sioni tofauti kati Ya CCM na CHADEMA katika mawazo yao na jinsi wanavyoendesha siasa zao. Hawawezi kulikomboa Taifa hili wala kuleta matumaini kwa waliokata tamaa. M4C is the movement for power. We are going to replace one tyranny with the Other. Uhuru wa kweli na maendeleo bado ni mgumu kwa aina za siasa ninazoziona.

The only true revolution is by changing the way people are thinking, by implementing new ideology and new values. We can not develop by the same thinking and the same values, we must change how we think. Watu wetu lazima waelewe hili tunalijenga Taifa letu kwa mawazo yetu, ubora wa mawazo yetu ndio ubora wa Taifa letu. Tunahitaji kiongozi atakayeleta mawazo mapya, mwenye akili na maono.

Lengo la kiongozi yeyote yule makini ni kuleta watu pamoja ili kujenga Taifa lao kwa manufaa yao kwa pamoja. Binadamu amepata maendeleo makubwa pale tu walipoanza kuishi pamoja na kuundwa serikali zao kwa manufaa yao. Hatujaunda serikali kusudi itawale na kunyima haki raia. Siasa ni chombo pekee chenye uwezo wa kukusanya watu kwa kushawishi juu ya faida ya pamoja tutakayoipata kama tutafanya jambo fulani kwa faida ya sasa na ya baadae ya taifa. Ni Siasa iliyokusanya watu na kuwa mataifa. Watu walishawishika kuunda mataifa kwasababu ya faida ya pamoja itakayopatikana kutokana na mtu kuishi katika Taifa. Siasa ikiwa chanzo cha vurugu na mgawanyiko katika Taifa hupoteza maana yake. Viongozi wenye uchu ambao hawafikiria chochote zaidi ya faida ya kipindi kifupi na sio baadae yetu na baadae ya vizazi vyetu.

Tuna kitu kimoja cha kufanya na kilichotuunganisha. Ni Taifa hili. Ni Tanzania. Naweza kukuita ndugu yangu kwakuwa tunaishi Taifa moja. Taifa hili likizama wote tunazama. Baadae ya Taifa hili inatutegemea sisi hakuna atakayejenga baadae yetu zaidi yetu. Kitu pekee ninachotaka kukiona ni kuliona Taifa hili likinyanyuka na likichukua nafasi yake katika Dunia. Hili ni tumaini ambalo kila mmoja wetu lazima awe nalo na kila mtu atakaye kabidhiwa mamlaka ya uraisi lazima awe nalo, kuwanyanyua watu wetu kutoka hapa tulipo. Sio ubinafsi na wala sio maslahi ya Chama bali dhamira yetu ya kulifanya Taifa hili liwe kubwa iliyozama ndani ya mioyo yetu. Ni lazima tuamini hivi ama sivyo hatutafanikiwa. Ni lazima tuamini tunauwezo wa kuwa Taifa kubwa kama Mataifa mengine na tutie jitihada kwa kufanikisha hilo.

Tumekuwa Taifa kutoka katoka katika makabila, koo na familia. Tumeunda kitu kimoja. Nguvu yetu itategemea sana umoja wetu pasipo kuangalia tofauti zetu za kikabila wala kidini ila dhamira yetu ya pamoja ya kujenga Taifa imara kwa vizazi vingi Vijavyo.

Mabadiliko ya kweli yatakayo likomboa Taifa hili ni mabadiliko ya fikra na mitazamo ya Watu. Tukifanikiwa kubadilisha mitazamo ya watu. Tutafanikiwa kubadilisha tabia na mabadiliko ya kimatendo tutarudi katika Taifa letu na kulitumikia kwa pamoja kwa maslahi ya wote.

Ni lazima tuangalie upya dhamira zetu kwa Taifa hili. Na tuwe wa kweli wa nafsi. Tujenge undugu wa watu wa Taifa moja. Tufikiri na kuamua mambo kutokana na fikra sahihi. Taifa hili litajengwa na busara na maono yetu.

Swali langu kwa "Chadema movement for Change" what change the wan't to bring in our country? Kuibadilisha CCM na kuwaweka wao madarakani? Watanzania wanahitaji zaidi ya hilo. Wanahitaji heshima na maendeleo ya Taifa lao. Wanatakiwa kutushawishi ni aina ya Taifa gani wanataka kulijenga. Tunu gani wanataka kuziweka kwenye Taifa letu na mwelekeo wao ni upi kama Chadema ni nini wanaamini? Wataleta matumaini gani kwa Tanzania? Tumeona katika Afrika vyama vingi vilikuja kama wakombozi wa wananchi lakini viliishia kuwa vyama visivyo kuwa na dira na vya kifisadi.Kwasababu waliongozwa na uchu ul ule sawasawa na wa watu walioko madarakani. Watanzania awahitaji ku replace tyranny with another Tyranny wanahitaji uhuru na maendeleo.

kitu Tanzania inachohitaji ni programmu itayobadili mitazamo na fikra za watu wetu juu ya nchi yetu. Kuingiza mioyoni mwa watu roho ya kulitumikia Taifa na uzalendo kwakuwa bila vitu hivi viwili Taifa haliwezi kusonga mbele. Bila umoja kamwe hatutaweza kusonga mbele. Lakini TAIFA hili linahitaji kukua na kusonga mbele katika umoja wetu. Naamini kabisa kama tukiwa wamoja na tukiwa determined kuliondoa Taifa hapa lilipo tunaweza.

Najua watu wa Tanzania wako katika Great distress na wamepoteza matumaini. Wengi wao wanajihisi sio sehemu ya Taifa hili. Tuna tatzio ni sawa na Chama kilichopo cha CCM ambacho kwa hakika hakina uhalali wa kuendelea kuwepo kutokana na ufisadi na kushindwa kuliongoza Taifa hili. Lakini pia vyama vyetu vya kisiasa vingi haviko imara kuleta mabadiliko ambayo tunahitaji ya kifikra, Wame focus mno katika kuitoa CCM madarakani bila kutayarisha programmu mbadala kwaajili ya kuleta mabadiliko kwa watu wa Taifa hili.

Chama chochote kitakacholeta mabadiliko katika Taifa hili ni kile ambacho kina maadili ndani yake. viongozi wake wana discipline na wanaheshimiana. Chenye ideology inayoeleweka na inayosambazwa kwa wananchi ili waijue na wajue chama chao kikiingia madarakani kitawafanyia nini. Kisicho okota okota ovyo viongozi wa kugombea katika majimbo bali kuwatayarisha katika maadili na discipline ya hali ya juu. Chenye Viongozi wanaoheshimu familia na majirani. Chenye watu wanaopenda jamii na kujitolea kujenga jamii.

Maendeleo ya kweli kwa jamii yeyote ile ni transformation ya roho, akili, mwili na mali, bila ya vitu vyote hivyo kukamilika binadamu hajakamilika kimaendeleo. Kwahiyo maendeleo ya binadamu sio ya mali tu lakini ya vile anavyofikiri, roho yake na ubora wa afya yake. Katika Taifa hli tunahitaji Order na bila order tunatambua taifa lolote halitoweza kuendelea. Na order hii itakuwepo tu kwa kuwa na viongozi wanaoheshimiwa na jamii. Utii huu wa jamii kwa kiongozi wao utakuja tu viongozi pale watakapojiheshimu na kuwa wa kweli na kuangalia mienendo yao ya kimaadili. Tunahitaji kiongozi atakayesema na watu kumsikiliza na kuhimiza utii wa sheria.

Tunawalea watoto wetu bila kufahamu haki zao na wajibu wao kwa Taifa kama Raia.

kila raia ana haki na wajibu kwa Taifa lake. Wajibu huu lazima uwe ndani kabisa ya kila mmoja wetu. Kwasababu sisi sote kama Taifa tumeungana kwa sababu ya lengo fulani, kuna sehemu tunahitaji kufika kwa pamoja, ni lazima tuwe na dira. Dira hii itapatikana kwa viongozi wenye maono. Kwahiyo kuwa wamoja ni muhimu. Hatuwezi kugawanyika kama Taifa tukafikiri tutafika popote hakuna. Those who are sincere in their hearts and speaks truth will bring direction to this Nation. Hatutaweza kuleta dira katika Taifa hili kwa propaganda na uongo. Sisi ni watu wamoja na muelekeo wetu ni mmoja. Hatutaweza kuleta ukombozi wa Taifa hili kwa style hii tunayoenda nayo.

Kwahiyo nina wasiwasi na Vuguvugu hili ambalo vijana wengi wanaliamini litabadili maisha yao. Ukweli ni kwamba vijana wa Taifa hili kwanza ni lazima wabadili tabia zao na kuwa watu wa kufikiri zaidi na watu wa kulipenda Taifa hili kiukweli. Wawe raia wanaowajibika kwa Taifa lao na wenye maadili. Kwasababu wao pekee ndio wenye uwezo wa kubadili mwelekeo wa Taifa hili kama wana fikra sahihi na kama ni wamoja na wazalendo. Kuna tatizo la kimaadili miongoni mwa vijana hili i lazima tulisema na baadae ya Taifa lolote inategemea sana vijana wao wamewaandaaje. Hii ni kazi ya wazazi katika familia na shule. Kwahiyo ni lazima tuangalie upya uundaji wa kijana wa Taifa katika fikra sahihi ili tupate raia bora.

Tunaweza kubadili CCM na kuwaweka CHADEMA ili kubadili chama tu. Lakini bila programmu sahihi na watu sahihi ili kubadili fikra za watu wa Taifa hili , Taifa letu litaendelea kubaki palepale bila kupiga hatua yeyote kubwa. Kwasababu bila Order katika jamii Taifa lolote halitoweza kupiga hatua. Na order hii inaenda deep mpaka ngazi ya familia. Ni jinsi gani tunaendesha familia zetu katika misingi ya adabu? Je tuna akina baba wawajibikaji wanaoweza kutawala familia zao katika misingi bora? Taifa huundwa katika ngazi ya familia. Ubora wa Taifa lolote hutegemea ubora wa familia. Lakini familia haiishi peke yake kuna majirani na mahusiano yakiwa mazuri katika ngazi hiyo ni hatua moja kubwa ya kuwa na mahusiano mazuri ya kitu kilichokikubwa zaidi ambacho ni Taifa. Bila mahusiano haya kama Taifa hatutapiga hatua. Kwahiyo Taifa letu linahitaji Social reformation, political reformation na economic reformation. Lakini kitu muhimu zaidi ni mahusiano yetu kama Taifa na kama mtu mmoja mmoja. Tukifikia hatua hii tutakuwa tayari kumpigania mtanzania mwenzetu hata mmoja atakapopata matatizo katika mataifa mengine. Ni lazima tupendane kama Taifa na kama mtu mmojammoja.

Mwisho Taifa hili linahitaji busara. Ni kiongozi mwenye busara na maono tu, atakayeweza kuliongoza taifa hili na kulitoa hapa lilipo. Atakayeunganisha vipande vilivyopo ili vifanye kazi kwa ufanisi na kutoa mazao. Tuna watu wa fani tofauti na vipaji tofauti lakini hatujafanikiwa kwasababu tumekosa kiongozi atayeunganisha vipande hivyo ili viweze kufanya kazi kwa ufanisi. We are not a well productive society kwasababu tumekosa a Leader. Ambaye kila mtu ata m admire na kumsikiliza because of ''intellegent, wisdom and Virtue''
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom